Binafsi suala la Baba wa Taifa hili Mwalimu Nyerere sio suala la kujadili na mtu.Wala siwezi kuhoji ubaba wake kwa kadiri ninavyoelewa yeye alishakuwa na yake ya kutenda, katika usimamizi wa jamii kwa nyakati zile na mazingira inalazimu kuhalalisha aina zote za mapungufu aliyopitia......
Tupo katikati ya nyakati hizi mgogoro wa kisiasa katika kujenga mustakabali wa Taifa letu, 2015 ni kipenga..!
Ni lazima turejeshe tafakari hapa juu ya aina za siasa katika vyama vinavyoamua muelekeo wetu, hasa katika kudaka pale alipoishia Baba wa Taifa.
Ni wazi kuwa CCM imeshashindwa!!
Vipi kuhusu CDM??
Ni vipi kinabeba ndoto ile ya Baba wa Taifa??
Uchumi wa mchanganyiko ni siasa za kimalaya/ siasa koko zisizo na sura ya kueleweka katika kusimamia maslahi ya masikini wa vijijini.
Ifike sehemu tuchore mstari uliowazi kwa chama chenye uelekeo wa kushika dora (CDM) juu ya tathmini mpya juu ya Itikadi na Mlengo wa kati haufai katika kulivusha taifa hili na kurudisha uchumi kwa UMMA.
Na hiyo ndio ilikuwa ndoto ya Baba wa Taifa.
JouneGwalu,
Asante sana kwa mchango wako. Hakika suala la baba wa taifa halina mjadala kama lengo ni kuhoji uhalali wake. Lakini kama nilivyokwisha sema, wenye hoja hii inaonekana kama vile nia yao (pengine sipo sahihi) wanataka kulivunja taifa ili kwa kutafuta visingizio kwamba kuna sehemu fulani ya jamii haikuwa sehemu ya ukombozi wa awali uliozaa baba wa taifa aliyepo, na kwamba matunda ya harakati zile yanaliwa na wachache, na walio wengi wanaonewa n..k; hoja hii inawezekana (pengine sipo sahihi) ili kuhamasisha walio wengi, na hivyo kuhalalisha mapinduzi ya umwagaji damu, na hatimaye wao kujitengenezea historia mpya, taifa jipya, na hatimaye baba mpya wa taifa lao. Ningependa kusahihishwa kama mtazamo wangu haupo sahihi juu ya hisia zangu juu ya nini haswa watu wa namna hii wanataka kuleta au wapi wanataka tupeleka.
Nakubaliana na wewe kwamba siasa za 2015 zina determine mengi sana, na inaonekana ndizo zina shape kwende huko; Mimi kama Mtanzania sijali nani atakuwa rais wa tano wa Tanzania, atokee dini ile au ile, atokeee mashariki, kusini, kaskazini, magharibi, unguja, pemba, kwangu mimi hilo sio suala la msingi, muhimu kwangu ni rais ambae atatuongoza bila ya kujali tofauti zetu, ataongoza kwa mujibu wa sheria na katiba, atatoa fursa na haki sawa kwa wananchi wite bila ya kujali dini, makabila, au jinsia zao;
Kuhusu CCM kushindwa kazi, ni sahihi kwani hakina dira - kwenye vitabu kinasema kina itikadi ya ujamaa na kujitegemea, kwenye vitendo, soko huria kiholela; Kuwa na mwongozo wa Chama ambao kushoto una azimio la arusha, na kulia azimio la zanzibar, ni kujichanganya; huku ndiko kukosa dira kama alivyotamka Marehemu Kolimba karibia miaka 20 iliyopita, na kuonekana mwehu; CCM haina dira wala mwelekeo kwa miaka 20 (tangia azimio la arusha), chama kinaongozwa kwa Ilani za chaguzi, pamoja na kanuni ambazo kwa kiasi kikubwa hazifuatwi, na pia taarifa za hali ya siasa nchini zinazozaa mikakati mizuri sana lakini hazifanyiwi kazi ipasavyo;
Chadema kina watu makini sana, hilo halina ubishi; kwa mtazamo wangu, hakuna kiongozi mwenye uwezo wa kujenga hoja katika CCM (wazee na vijana) kama Mnyika, Zitto, Lissu; nipo wazi kupingwa juu ya hilo;
Tatizo la CDM kwa mtazamo wangu ni kwamba, wakifanikiwa kupata uongozi wa nchi, wasipokuwa makini, watapoteza legitimacy yao haraka sana in the eyes of watanzania waliowachagua kwenda ikulu kutokana na mambo niliyoyaelezea hapo awali;