Baba wa Taifa wa Zaire (DRC), Patrice Lumumba, ambae alifariki miaka michache sana baada ya kuikomboa Zaire, na ambae alikuwa mshirika mkubwa wa Nyerere, Je amelifanyia nini Taifa la Zaire kitakwimu mpaka aitwe baba wa taifa? Tusisahau kwamba aliuwawa kikatili na mabepari wa nje wakati anajaribu kufanya uchumi wa Zaire uwe wa wote kama Nyerere.
Mkuu Mchambuzi,
Tuweke rekodi sawa, DRC ilipata uhuru wake June 30, 1960 na Mwanamapinduzi Patrice E. Lumumba aliuawa January 17, 1961. Serikali yake nadhani ilidumu kwa miezi miwili na nusu [June 30 - September 14]. Kwa hiyo haikuwa miaka michache sana baada ya Uhuru, bali ilikuwa ni miezi miwili na nusu tu baada ya uhuru.
Dhambi ya baadhi ya wa-Congoman ya kumsaliti Lumumba inaendelea kuwatesa mpaka leo hii. Uroho wa madaraka na ubinafsi ndio ambavyo vinaendelea kututafuna Afrika mpaka leo. Tunataka kuendelea kugawana sehemu ili kila mmoja apate authority.
Mobutu Sese seko ambaye ni mmoja wa wasaliti wa Lumumba, mwaka 1966 alitambua rasmi mchango wa Lumumba wa kudai uhuru na kutaka kujenga DRC moja iliyoungana na siyo kila jimbo lijitawale kivyake. Baada ya hapo alianza kutumia kauli zile zile za Lumumba katika kuhamasisha watu ili aweze kupata support ya wananchi, lakini kwa bahati mbaya hakuweza kupata support ya kutosha na hivyo kuishia kutawala kimabavu na ndio maana wapinzani walikuwa wamesambaa kwenye nchi zote za jirani zinazoizunguka DRC.
Leo hii hapa Tanzania kuna watu wanabeza mchango wa Mwalimu Nyerere katika kudai uhuru na wakati huo huo wakitaka kupata support wanakuwa wa kwanza kutumia nukuu za Mwalimu ili kuhamasisha wa-Tanzania waweze kuwaona kwamba wana nia njema juu ya maisha yao na kumbe ni chui waliojivisha ngozi ya kondoo ili kuwa-fool wananchi.
Hata kwenye swala la ubora wa marais, bado ninampa consideration kubwa sana Mwalimu Nyerere. Marais waliofuata baada ya uongozi wa Nyerere, kama wao ndio wangekuwa ni viongozi wakati huo, nina hakika kwamba wangetuuza hata sisi wenyewe maana sijawahi kuona uongozi ambao umejaa ubinafsi na kujali maslahi yao wenyewe kama wa awamu ya Mkapa na JK. Kila wanachofanya wanaangalia kwanza hapa nita-gain nini, akishashikishwa chake ndipo anaanza kuja kwa nguvu na kufoka mpaka povu linamtoka. Kila siku nikikumbuka jinsi Mkapa alivyokuwa anatokwa na povu kutetea ununuzi wa radar na baadaye inakuja kugundulika kwamba ni "dili", na jinsi alivyowaingia NetGroup Solution kwa kutumia mtutu wa FFU na kumbe ni dili la shemeji yake na madudu mengine kibao.
Kosa la Mwalimu Nyerere ni moja, hakujua kuwa alikuwa amezungukwa mafisadi. Mkapa [Mr. Clean] ambaye tulijua ni chaguo la Mwalimu kumbe alikuwa ni fisadi aliyeficha makucha yake. Hawa akina Lowassa na JK ndo walikuwa vijana wa chama, wasomi waliotoka Mlimani na kwenda kukitumikia chama na walifundwa ipasavyo pale Chuo Kikuu Cha Chama Kivukoni. Alitakiwa kuzinduka mwaka 1992 alipowaambia kwamba upepo wa mageuzi unaokuja hamtasalimika, kubalini kuingia kwenye mfumo wa siasa za vyama vingi. Wapo waliombeza kwa kusema kwamba Mzee huyu amekula amemaliza, inafika zamu yetu ndo anakuja kutuambia habari za kukubali vyama vingi. In a way ilikuwa ni msaada mkubwa sana maana wangeingizwa ghafla na kwa nguvu, wasingeweza kupata nafasi ya kujiandaa yangewakuta yaliyomkuta Babu yangu Ken Kaunda.
Nyerere alikuwa yuko well informed kuliko hawa viongozi wetu wa siku hizi ambao hawasomi wanasubiri kupewa briefing then wanaanguka sahihi zao hata bila kusoma kilicho kwenye makaratasi aliyosaini. Viongozi wetu wa sasa wanachofikiria ni namna gani ya kuongeza utajiri wao na ndiyo maana wanashindwa kujenga hoja kutetea misimamo yao, wanaishia kusema hata Nyerere, Mwinyi na Mkapa walifanya hivyo. Je, kama wao walifanya hivyo kimakosa, ndo na Rais wa sasa anataka kutuingiza kwenye mkenge huo huo? Mazingira ya utawala wa Mwinyi, Nyerere na Mkapa, JK na kwa hiyo kati yao hakuna ambaye anatakiwa kumtumia mwenzake kama justification ya kufanya kitu fulani, unless kiwe ni kitu cha kikatiba. Na kama ni kitu cha kikatiba hakuna ambaye ata-question kwa kuwa Katiba inamlinda Rais kufanya kile anachokifanya.
Wapo waliomwita HAAMBILIKI, tatizo ni kwamba unapokuwa kiongozi kuna vitu ambavyo unasimamia na sidhani kama mtu akija na hoja tofauti unaweza kukubaliana naye kirahisi bila kukupa hoja yenye mashiko. Anakuja mshauri wa Uchumi anakushauri hiki, lakini ukikiangalia kwa makini unakuta kiko kinyume na kile unachokisimamia, ni ngumu sana kuweza kukubaliana nacho kirahisi. Kwa hiyo swala la kwamba alikuwa HAAMBILIKI au hakubaliani na washauri wake au wasaidizi wake, ni swala ambalo liko kwa kila binadam, ni sehemu ya mapungufu yetu kusimamia kile ambacho tunachokiamini.
Sasa yupi ambaye haambiliki kati ya hawa? Mkapa aliyetokwa na povu kununua radar? au JK aliyekubaliana na Lowassa kutuletea Richmond na Dowans na huku magazeti yakipiga kelele sana? Katika zama za utawala wa Mkapa na JK, information kuhusu mambo mbali mbali zimekuwa zikitoka na magazeti/wanaharakati wamekuwa mstari wa mbele kupiga kelele zao kwa nguvu zote, lakini kelele hizo hazikufika popote. Baada ya madudu kuwa wazi, JK anasema ajali ya kisiasa, Lowassa anasema Rais alijua kila kitu. JK anasema mwacheni mzee wetu apumzike, ebooo yaani afisadi mali ya walala hoi halafu aachwe apumzike then watu wanakuja kusema ni Rais Bora!