Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Dada Mdogo FaizaFoxy (nasema hivyo kwa sababu nina uhakika mimi ni kaka yako mkubwa kiumri):-

1.Ni hivi karibuni nilikuwa Pakistan. Unapotua uwanja wa ndege Islamabad unakaribishwa na bango lisemalo "Welcome to the Islamic Republic of Pakistan". Lakini licha ya nchi hiyo kuwa ni ya mfumo wa kiislamu bado wanamuita kiongozi wa kwanza wa nchi hiyo, Muhammad Ali Jinah, Baba wa Taifa "Baba-e-Qaum (بابائے قو&#1605😉".

2. Na sio Pakistan peke yake kati ya nchi za kiislamu ambako viongozi wamepewa wadhifa wa Baba wa Taifa. Kwa mfano Uturuki, Mustafa Kemal Atatürk (Atatürk = Great Father of the Turks). Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan wa United Arab Emirates (والد الأمة = Waalid Alamat) na pia Ibn Saud of Saudi Arabia ( والد الأمة = Waalid Alam)

Kwa hiyo nadhani sio kila mada ni lazima uchangie kwa mtizamo wa kidini. Waswahili husema ujanja mwingi mbele giza!
Askari Kanzu,
Kwa Faiza na wengine wa aina yake kama nafasi ya Baba wa Taifa ingemwangukia Muislam mwenzao wala kusingekuwa na tatizo. UDINI ni ulevi zaidi ya bangi au gongo kwa kuwa hautoki kirahisi kichwani. Kila mara nawaambia watu Mungu mwenyewe hakuwa na hana DINI. Hawanielewi.
 
Neno baba haiamanishi ukatoliki. Mzazi wako wa kiume unamwitaje Baba au mkatoliki? Acha kupotosha umma wa kislam na kikristu.
 
Nyerere I salute him, haters wezi msio na uchungu na nchi hii ndo mnaleta vijimaneno vya kumkashifu Mwalimu, na hii tabia inazidi kukua kila m'k'were & co anapozidiwa majukumu
 
Mchambuzi,
Sasa kama mpo mnaoelewa kinachoendelea kwa kiwango kikubwa namna hii, kwa nini mko kimya? Hayo unayosema ni maelekezo toka nje watawala wetu wanayaorodhesha kama mafanikio kila uchao na wanataka tuamini hivo. Ingieni angalau Bungeni mpaze sauti huko zenye kuleta tija na mabadiliko ya maana.
Badala yake wasomi kama akina Zitto wanajielekeza kwenye mambo ya kuwapa umaarufu wa haraka kama posho. Bunge lijalo la January nadhani watajadili ndoa za jinsia moja!

Nashukuru sana kwa maoni yako; labda niseme tu kwamba mimi binafsi naamini kwamba mbali na ubunge au udiwani, zipo njia nyingi sana kwa mtu mwenye nia ya kweli kuelimisha watanzania au kwasaidia katika shughuli zao za maendeleo, hasa hasa ndugu zetu walio vijijini; kila siku tunakutana na vijana na kina mama mitaani waliokufa matumaini na kukata tamaa ya maisha, huko huko huwa tunakaa nao katika vijiwe vya bao, draft, tukinywa kashata na kahawa na kubadilishana mawazo, na ujumbe unafika vizuri tu, kuliko hata ule wa kupitia kwenye TV au Redio; wengi bado wana matumaini sana na Mwalimu ingawa hayupo nasi tena, lakini wanatambua hazina aliyotuachia, na hii inawapa sana ujasiri, imani, na matumaini makubwa kwamba ipo siku tutafika;
 
Hatujafanya jambo moja ambalo pia linamstahiki Mwalimu kama Baba wa Taifa hili pamoja na Mzee Karume kwa upande ule wapili:
-Picha kwenye maofisi ya UMMA na binafsi zibaki za Mwalimu tu huku bara na Karume Mzee kule Zanzibar.
-Kwenye noti zetu pia tuwabakize wazee hawa hadi tutakapopata kiongozi atakayeonesha analitumikia Taifa hili.
 
Ahsante sana Mkuu, hakuna mwingine kama Mwalimu Nyerere. Mwalimu alikuwa na mapungufu mengi kama binadammu/kiongozi lakini aliitumikia nchi yetu kwa moyo mmoja na kuipenda sana na pia kuwapenda Watanzania ukilinganisha na hao waliokuja baada yake akina Mwinyi, Mkapa na Kikwete ambao wote waliweka mbele matumbo yao na kudharau kiapo chao cha kuitumia nchi kwa moyo mmoja na kulinda maslahi ya nchi kwa hali yoyote ile.
 
Mchambuzi, nimekuvulia kofia. Kuna swali ningeomba yeyote mwenye kujua anisaidie: Kuna kazi fulani tulikuwa tunafanya wiki chache zilizopita, kuna point tulilazimika kupata kanda za taarifa za habari na magazeti ya miaka ya '70 na 80. Baada ya kumaliza navyo, nilitaka kupitia karibu kila kitu katika magazeti na taarifa hizo, pamoja na mengine mara kwa mara unasikia/soma kitu kama hiki...'Rais wa JMT amemstaafisha kwa manufaa ya umma aliyekuwa meneja/mkurugenzi wa .....' Je hii ina uhusiano wowote na hiyo inayosemwa kuwa walioharibu hawakuchukuliwa hatua?! Mzee mmoja ameniambia kuwa huko kustaafishwa kwa manufaa ya umma kuliwakumba wengi.

Mimi binafsi nilikuwa mdogo sana lakini nakumbuka kusikia taarifa kama hizo kwenye vyombo vya habari; wapo waliochukuliwa hatua, wengi tu, serikalini na hata Uraiani; lakini tusisahau kwamba Mwalimu alikuwa katika vita kubwa sana na mabepari wa humu ndani ambao walikuwa wanashirikiana na mabepari wa nje kuhujumu Ujamaa na hata kuyadhoofisha mashirika ya umma ili mradi sera za mwalimu zionekane ni failure ili to pave way for foreign capital kuja ku finance uchumi; hakuna biashara tamu kama ile ya kufanya na serikali,hata worldbank wanalijua hilo;

Vinginevyo umenikumbusha enzi zile ambapo Rais kufukuza, kuteua, au kuhamisha mtu kazi, hata wahusika walikuwa wanasikia redioni wakiwa mezani na familia zao wanakula chakula cha usiku, hapakuwa na leakage za ovyo ovyo za taarifa za serikali;
 
Wadau,
hivi ni kwanini Nyerere Foundation haipo effective katika makusudio yake pamoja na kwamba ina watu wazito na wasomi wengi tu mle? Hii ilitakiwa iwe moja ya top think tanks in this country to influence all major policies.................
 
FP
Ukitazama mantik nzima ya vijiji vya ujamaa iikuwa nzuri na inasimama mpaka leo. Lakini kuna baadhi ya maeneo kulingana na utaratibu wao maisha.( eg ufugaji 100%) hawakuwa na utamaduni wa settle. So hilo iuwa ni tatizo moja Lakini failure ya vijiji vya ujamaa sehemu chache haiwezi kufunika sucess ya vijiji vya ujamaaa sehemu kubwa ya Tanzania


Unapokuwa na uhaba wa resoruces (wich is always the case) lazima kuna kitu kifanyike (organisation) Sasa kama unalaumu vijiji vya ujamaa ebu fafanu ungefanya nini wakati cha tofauti japo kuweka shule mbili za primary kwenye jamii zilizotawanyika.

Mkuu Zing,

Nitakujibu kwa mfano. Kwanini Uchagani hasa nilipofika mie Marangu, mwika, Kibosho na Rombo kwa ujumla wana maendeleo sana (wamesoma, wana maji, wana umeme, wana barabara, wana mashule, wana majumba mazuri ya kulala in totality) lakini hamna vijiji vya ujamaa?

Ninge fanya vijiji vya ujamaa kulingana na mazingira. Isingekua swala la NGUVU. Ningeweka huduma kama ilivyo Kilimanjaro.

Ni hilo tu. Na kumbuka sipingi the concept napinga utekelezwaji wake.

Chunguza sana
 
Wadau,
hivi ni kwanini Nyerere Foundation haipo effective katika makusudio yake pamoja na kwamba ina watu wazito na wasomi wengi tu mle? Hii ilitakiwa iwe moja ya top think tanks in this country to influence all major policies.................

Kwasababu iliingia malumbano na chama tawala na kukosoa kwa uwazi sana.
 
Wadau,
hivi ni kwanini Nyerere Foundation haipo effective katika makusudio yake pamoja na kwamba ina watu wazito na wasomi wengi tu mle? Hii ilitakiwa iwe moja ya top think tanks in this country to influence all major policies.................
Ilijiingiza kwenye siasa za ndani ya CCM ikidhani kuna watu wanaiheshimu na kuisikiliza. Ikadhoofishwa kiaina tangu enzi za Mkapa. SAS alipojitokeza kupambana na WANAMTANDAO wakaimalizia kabisa.
 
Wadau,
hivi ni kwanini Nyerere Foundation haipo effective katika makusudio yake pamoja na kwamba ina watu wazito na wasomi wengi tu mle? Hii ilitakiwa iwe moja ya top think tanks in this country to influence all major policies.................

Nilipata kuongea na mzee mmoja ambaye yuko konekted na NF akasema watawala wa sasa wanaiona taasisi hiyo kama anti-government kiasi kuwafanya baadhi yao kunywea.
Ukiangalia kwa sasa ni kama hawana ajenda ya msingi ukiondoa matamko ya hapa na pale.

Halafu kale kamjengo kao pale Shaban Robert ambako kiwanja walipewa na utawala ulopita waliambiwa kimjengo aina hiyo hakiruhusiwi mitaa ile maana ni karibu na jumba jeupe. Sasa usiulize ule mghorofa wa jirani na Ocean road hospitali uliruhusiwa na nani.

Kwa maoni yangu ulichokiandika kilipaswa kuwa kimefanywa na NF way back lakini seem wazee wamechoka kama chama kilivyochoka
 
Mimi binafsi nilikuwa mdogo sana lakini nakumbuka kusikia taarifa kama hizo kwenye vyombo vya habari; wapo waliochukuliwa hatua, wengi tu, serikalini na hata Uraiani; lakini tusisahau kwamba Mwalimu alikuwa katika vita kubwa sana na mabepari wa humu ndani ambao walikuwa wanashirikiana na mabepari wa nje kuhujumu Ujamaa na hata kuyadhoofisha mashirika ya umma ili mradi sera za mwalimu zionekane ni failure ili to pave way for foreign capital kuja ku finance uchumi; hakuna biashara tamu kama ile ya kufanya na serikali,hata worldbank wanalijua hilo;

Vinginevyo umenikumbusha enzi zile ambapo Rais kufukuza, kuteua, au kuhamisha mtu kazi, hata wahusika walikuwa wanasikia redioni wakiwa mezani na familia zao wanakula chakula cha usiku, hapakuwa na leakage za ovyo ovyo za taarifa za serikali;
Asante mkuu, Sasa kwa nini watu wanajaribu kudanganya kuwa JKN hakuwachukulia hatua wazembe?! Nina maswali zaidi ya nyongeza! Kenya kama ilivyo Tanganyika kuna maeneo hadi sasa
watu wanaliwa na simba, haya malalamiko kuwa watu walipelekwa maporini, walikuwa mijini wakaondolewa au ilikuwaje? Na tangu enzi waafrika wamejua kwa kiasi kikubwa kujikinga/kupambana na wanyama wakali, hawa 'wengi' walioliwa walitolewa dunia gani?! Kwa nini wakati wa ukoloni watu waliobahatika kusoma (tunaambiwa wengi walilazimika kutembea km nyingi sana kwenda shule) hawakuliwa na simba?! Ni nani alikuwa anaamua kijiji A kiwe eneo fulani ni Nyerere au watendaji wa ngazi za chini na je hawakuwashirikisha wananchi kuangalia faida na hasara za maeneo husika?
 
Kwa nini Nyerere alipora sekondari za Bukoba,Mbeya na Kilimanjaro na kuwasomesha wanafunzi wa Lindi,Mtwara na kwingineko???
Kwa nini Nyerere alituunganisha na Wazenji wavivu??????????

atakaye vunja muungano atakuwa shujaa wa Taifa
 
Mkuu Zing,

Nitakujibu kwa mfano. Kwanini Uchagani hasa nilipofika mie Marangu, mwika, Kibosho na Rombo kwa ujumla wana maendeleo sana (wamesoma, wana maji, wana umeme, wana barabara, wana mashule, wana majumba mazuri ya kulala in totality) lakini hamna vijiji vya ujamaa?

Ninge fanya vijiji vya ujamaa kulingana na mazingira. Isingekua swala la NGUVU. Ningeweka huduma kama ilivyo Kilimanjaro.

Ni hilo tu. Na kumbuka sipingi the concept napinga utekelezwaji wake.

Chunguza sana

Mkuu FP,

Hilo la kilimanjaro kutokuwa na vijiji vya ujamaa kuna mdau ameligusia bila shaka utakuwa umemuelewa. Na kwakuwa mpango wa vijiji vya ujamaa haukutekelezwa huko basi ni dhahiri kwamba pale palipoonekana pako vizuri kimiundombinu ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa jamii, serikali iliwaacha waendelee kuishi vivyo hivyo.

Ukitaka kuwatendea haki watanzania wenzako unapozungumzia maendeleo katika maeneo yaoi, unazungumzia kilimanjaro kuwa mbele kielimu, miundombinu, maji, umeme na nyumba nzuri, usisahau historia ya Tanganyika enzi za ukoloni. Utakubaliana nami kwamba wamisionari wa kikristo waliingia maeneo hayo mapema sana na wakawekeza kwa kujenga mashule na miundombinu mbalimbali.

Watoto wa kichaga wakapata nafasi ya kusoma na hivyo wakapata nafasi ya kuajiriwa na serikali ya kikoloni na hatimaye Tanganyika huru. Na kwakuwa walikuwa wamesoma vizuri bila shaka wakapata nafasi za kulitumikia taifa hili katika nafasi za ajira za serikali na mashirika ya umma, tena wakiwa wengi ukilinganisha na makabila mengine.

Katika mazingira hayo utaona kwamba walifanikiwa kujiletea maendeleo makubwa ya miundombinu, kielimu, kiuchumi, maji na makazi.
Kwa ujumla wake mpango wa vijiji vya ujamaa uliwasaidia wale wa jamii zilizokuwa zimetawanyika sana na watu wako mbali na huduma za msingi kama shule na hospitali.

Kwa mfano kwa mkoa wa Mara tulifaidika sana na mpango huo wa vijiji kwakuwa jamii zetu wengi ni wafugaji, wakulima na wavuvi. Huduma za afya na elimu zilikuwa zinapatikana kwa watu kutembea umbali mrefu sana kuzitafuta. Wazee wangu walikuwa wakitembea takribani kilometa 50 kuifikia hospitali lakini sasa tunatembea kilometa 5. Wazee wangu walikuwa wakitembea takribani kilometa 35 kuifikia shule, sisi tumetembea kilometa 4 kuifikia shule.

Kiujumla vijiji vya ujamaa vimetusaidia sana. Kuna wale wanaosema watu waliliwa na simba kwa sababu ya kupelekwa porini. Je wanafuatilia kuona ni wananchi wangapi bado wanaliwa na simba hadi leo hii tukiwa na miji mikubwa iliyojaa watu na miundombinu bora?
Nenda Doma-Mikumi hapo uone shughuli yake, nenda rombo huko, nenda lindi huko ruangwa, na maeneo mengine mengi vilio havijakwisha, simba wanaendelea kula watu!
 
Tofauti na Heshima ya Baba wa Taifa ambayoe inatambulika kisheria, heshima Rais Bora huwa ni maoni ya wananchi walio wengi ambayo hupitia mchakato wa tafiti/vipima joto mbali mbali zinazolenga kukusanya maoni ya wananchi.

Mchambuzi naomba Utusaidie Kidogo: Mwalimu Nyerere alipewa ubaba wa Taifa kwa sheria ipi ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania?.
 
Mkuu Zing,

Nitakujibu kwa mfano. Kwanini Uchagani hasa nilipofika mie Marangu, mwika, Kibosho na Rombo kwa ujumla wana maendeleo sana (wamesoma, wana maji, wana umeme, wana barabara, wana mashule, wana majumba mazuri ya kulala in totality) lakini hamna vijiji vya ujamaa?
Mkuu ukisoma historia vizuri utaona una baadhi ya sehemu ni kama walikuwa tayari wana vijijii vya vya ujamaa hata kabla havijaazishwa rasmi. Ardhi ni tatizo kilimanjaro hali hiyo ilisababisha watu wabanane sehemu moja yenye rutuba hata kabla zoezi halijaanza . So kuna maeneo zoezi la vijiji vya ujmaa ilikuwa rahisi kutokana na nature ya maisha ya watu na mazingira. Hata Mkoa kama kagera nadhani watu hawakuathirikia sana sababu utasona hitoria yao walikuwa wana mambo ya clan. na kilimo cha mazao kama ya ndizi ambayo ni ya mwaka mzima

Cha msingi elewa hakuna sera nzuri ambayo itamfanya kila mtu acheke. Vijiji vya ujamaa vilikuwa ni muhimu na lengo lake lilikuwa zuri

Ninge fanya vijiji vya ujamaa kulingana na mazingira. Isingekua swala la NGUVU. Ningeweka huduma kama ilivyo Kilimanjaro.
Unapotolea mfano wa kilimanjaro basi nisome pale juu na soma historia vizuri. Kuna mikoa na maneno na mazigira fulani watu walikuwa kama tayari wana vijiji vya ujamaa. Ni adjustmenet ndogo tu. Kama ni tatizo a vijiji vya ujamaa may be mikoa kama ( singida, dodom uliyotaja) lakini mkoa kama kagrea basi ni vijimatatizo kidogo sana vilijitokeza.


Ni hilo tu. Na kumbuka sipingi the concept napinga utekelezwaji wake.
Chunguza sana
Utekelezaji wake hauwezi kuwa sawa maeneo yote. Matatizo ya hapa na pale hayakwepeki.
 
a
Kamanda you have to all intents and purposes hammered the point home and it's only researching guys and those who view issues on the wide spectrum can argue in favour or against you. Umechokoza mada ambayo inajieleza na wale walioweka watu kumkejeli Mwalimu ili wafiche makosa yao watatafuta pahala pa kujificha. Lakini lili dhahili ni uwezo wa kufikiri ulivyokuwa mfupi maana waliwaandaa wawapigie debe ili waitwe marais bora na mababa wa taifa hili either ni vilaza au wabaguzi au uadilifu wao unatiliwa shaka.Hawawezi kushinda kwa hoja maana hata takwimu zao za kupika zinashindwa kuelezeka. Mada yako ni nzuri na imejibu hoja nyingi sana na inachokoza haja ya watanzania kujiangalia upyab kama taifa na kuacha ubinafsi. Inachochea haja ya kujisomea ili tuapte kujenga hoja za kisomi, hoja tafiti na hoja chokonozi kama hii ya kwako. Wito wangu usiachie hapo maana watakija watu wenye mawazo mgando na matusi na kejeli kumbe wao hata mistari miwili kama yako hawawezi kuandika.

Jingine nitoe ushauri kuwa vyama vyetu usivichananye kama ulivyoonyesha kuwa kama ilivyokuwa kwa CCM na CDM hivyohivyo. Watanzania tuliokuwa wengi unatujua maana hatufanyi tafiti na hatujisomei kiasi kwamba mataifa jirani yanatudharau. Siku moja nilikutana na jamaa ametokea Canada. Alikuwa anelekea mwanza akitokea Rwanda.Nilimuuliza kama yeye ambaye anafanya kazi kwenye shirika linashughulikia maendeleo ya Afrika ni kwanini Rwanda imeendele a na inazidi kuendelea ktk kipindi kifupi na hali imeathiriwa na vita. Alinijibu kuwa wale watu wako fucused na wamezuia rushwa. Akatoa mfano wa Rais wao anavyochuklia rushwa na wachache walioko madarakani kujilimbikizia mali. Alitoa mfano wa kuuza magari ya kifahari yaliyokuwa yanatumiwa na viongozi na kugawa ardhi kutoka kwa waliokuwa wamehodhi umiliki wa ardhi na kuwapa wasiokuwa na ardhi.Akasema hiyo sacrifical martdom ambayo viongozi wengi wa Afrika hawana na hasa Tanzania. Akasema amesikia watanzania wanaibeza Rwanda kuwa eti eneo lake ni dogo na ndio maana inaendelea. Akasema swala ni management sio eneo. Na hapaanaonyesha watanzania wanavyopenda short cut kwenye mambo muhimu. Hivyo basi nikuombe CCM-CDM au chama chochote iwe ni topic independent. Ila nikumbe uwatie moyo wananchama wa vyama hivi wenye uzalendo wa kweli wasife moyo. Sina shaka n uzalendo wa viongozi wa CDM hasa wa ngazi za juu ukiacha waliotumwa kama Shibuda. Hawa wanajitolea sana kwa manufaa ya taifa.Kwanza kwa taifa lenye hujuma kusimama hadharani ukawataja mafisadi wakiwemo viongozi wa juu sio mchezo.Halafu majimbo yalioongozwa na CDM ni mfano wa kuigwa kwa maendeleo ya watu kama shule, maji na afya.

Mwisho nami kama wewe Mwalimu ni Baba wa Taifa na bado ni Rais bora kwa vigezo vyako na vyangu
 
Mchambuzi - nimejaribu kusoma makala yako hapo juu. Kusemakweli umechambua mpaka mwisho. Mimi sina la kupunguza wa la kuongeza maana yamekalika. Yaani kama bado kuna mtu anayepinga Nyerere kuitwa BABA WA TAIFA basi huyo hana akili timamu. Ni wakumwacha jinsi alivyo maana pesa za mafisadi zinamlevya. Kwa niaba ya Watanganyika wote nakutumia shukrani nyingi sana kwa kazi nzuri uliyoifanya ya kuichambua mada hii kwa utaalam na ustadi uliotukuka! Mungu akubariki sana mchambuzi wetu!!!
 
Back
Top Bottom