Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Ndio maana kwanza nikakupa "link" waone Watanzania wengine wanasemaje kuhusu Nyerere ingawa wewe uling'anga'ania "magharibi" na halafu nikakupa "link" umsikilize mwenyewe anasema nini alipokubali kuwa yeye ni dikteta. Na halafu ndio nikakupa hao wa "magharibi" uliong'ang'ania, nilikuwa na maana yangu. Watu kama wewe nawaelewa sana tu, hamnipi shida.

Sasa chaguwa wewe unaloona linakufaa, anayosema FF, wanayosema Watanzania wengine, anayosema Mwenyewe Nyerere au wanayosema wa "magharibi" uliong'ang'ania kuhusu udikteta wa Nyerere. Unalo? Kumbuka, Sikisii!
Ni wapi "nimeng'ang'ania" magharibi, bi mdogo. Mbona unazidi kuchanganyikiwa?
 
Ukimchukia ndugu yako unaweza kumuunga mkono hata shetwani iwapo anazungumza lugha moja na wewe... Lakini kumbuka kuwa kazi unayofanya sasa ina malipo yake.... utalipwa! Nakutakia kazi njema na malipo yake pia uje ufurahie .... alamsiki...
Waswahili husema "mtoto umleavyo ndio akuavyo". Nadhani hivyo ndivyo alivyolelewa huyu bi mdogo FaizaFoxy. Yaani malezi ya chuki, uongo, unafiki na uzandiki!
 
Ji habari reeeefu halisomeki, wala sina muda wa kulisoma, kwa kifupi:

Kwanza kabisa mimi sikubaliani na hilo "baba" wa Taifa, huo ni ukatoliki na hutumika kanisani kuwaita wachungaji "baba", kumuita "papa" "baba" mtakatifu.

Hii nchi Nyerere aliikuta ina watu wa imani tofauti na ameondoka ametuwacha watu wa imani tofauti, kwanini mtubambikie vyeo vya kikatoliki na Kikristo? hamuoni kuwa huo ni "udini" wa wazi wazi?

Hakuna "baba" wa Taifa, huo ubaba alipewa na nani na kwa ridhaa ya nani? msitujaze ujinga

Hilo jina la baba wa taofa alijipa mwenyewe? sasa kwanini na wewe usimpe jina la kiislamu? Katoliki kuna baba wa taifa? Au ukipenda tupe tafsiri ya Father of nation. au dad of nation.
 
Huna swali ambalo hujajibiwa unatafuta pakutokea hupapati. Hapa ni "wrong number".
Tutakutana jukwaa la wakubwa tujadili ngono. Kwa sasa nimechoshwa na pumba zako za kujifanya wewe ni Mwislamu safi wakati hakuna ukweli wowote!
 
Nilikuwepo wakati wa nyerere, nilikuwa nimeshaanza shule na kuelewa. Na nilipiga kura wakati wa Mwinyi. Nakumbuka miaka ya sabini ilivyokuwa.
Tena Mwalimu Nyerere angekuwa ameshawataifisha watu kama kina RA zamani.
Nyerere wanted what was best for us.

Ila ngoja nikuache na chuki zako binafsi.
Be careful though: the hate in your heart will consume you too.

It is so sad that in this country we still have people worship a dead dictator ...But I have news for you guys , there is nothing and nothing at all that can clean his legacy.
Police brutality that we see today, is a result of his making...Mwenyezi Mungu, atamuonyesha nani hasa baba wa kweli.
 
It is so sad that in this country we still have people worship a dead dictator ...But I have news for you guys , there is nothing and nothing at all that can clean his legacy.
Police brutality that we see today, is a result of his making...Mwenyezi Mungu, atamuonyesha nani hasa baba wa kweli.

Na wewe unajiona great thinker, eh?
 
Baada ya kukupa aya za Qur'an, nimekushishia nondo kutoka biblia, tazama post #648 sasa wewe amuwa unaifata ipi? au kama unafata matamanio yako huko jukwaa la wakubwa hayo ni yako, mradi uwe umekidhi vigezo. Hapa ni JF na mimi ni FF aka selebriti namba moja JF. Bye.
Bi mdogo unaboa!
 
Mkandara
Inawezekana mnaongea kitu kimoja lakini kwa vipindi tofauti; wakati Mwl. Nyerere anachukua uongozi wa kuliongoza Taifa hili alifanya mabadiliko makubwa ya mwelekeo wa Taifa hili; na alipoachia madaraka viongozi waliofuatia nao waliamua kuendesha nchi kwa mitazamo yao; yapo mambo ya msingi lazima yafanyike ili Taifa liwe na hiyo sifa ya modern nation kuanzia uchumi, kisiasa, kiutamaduni na kidini; ukichulia maana ya modern nation; Tanzania ya wakati wa Mwl. Nyerere ileta maana halisi; hivi sasa Tanzania tunaelekea kwenye Fallen state.

Chama
Gongo la Mboto DSM
Nakubaliana na wewe kabisa na hakika Mwalimu ndiye baba wa Taifa wasiokubaliana na hilo wameze wembe...Lakini Nyerere sii baba wa Taifa la kisasa maana Taifa la kisasa lilikuja mwaka 1992 baada ya kuacha kuvunja utawala wa chama kimoja, kufuta Azimio la Arusha na kuondoa miiko na maadili ya uongozi tulipoingia Azimio la Zanzibar. Nchi sii tena ya Wakulima na Wafanyakazi na no one is responsible or accountable - ni RUKSA - Hili ndilo Taifa la kisasa...
 
Unafikiri wote wanataifishika? kwani hao kina RA hawakuwepo wakati huo? uliza kama huelewi.

Ukimaliza uliza kisa cha LONRHO au Tiny Rowlands na Nyerere. Si wote wanataifishika, alijidai kumtaifisha Tiny Rowlands, mwenyewe akarudisha baada ya kuona mnhhhh hapa pagumu. Si kila mtu aliweza kumchezea anavyotaka. Alisema nikigeuka nyuma ntageuka jiwe, Tiny akamfanya alambe matapishi yake.

Hakuna chuki binafsi kuna ukweli tu hapa, kama una mbadala tueleze. Nyinyi ndio wale mna macho lakini hamuoni, mna masikio lakini hayasikii. Mmejazwa ujinga na mnaukubali bila kutazama upande mwingine, kwangu hilo ni NO.

Na kama huna hoja za kupingana na niliyoyasema bora ujinyamazie tu. Kwani nna uhakika huwezi kuufuta ukweli, ukweli upo na utazidi kuonekana kila siku zinavyokwenda. Sana sana utaanza FaizaFoxy hivi FaizaFoxy vile kama wenzio wengine. Si unawaona hapa?
Uzuri wako FaizaFoxy una Nyerere wako mwenyewe mbali na huyu tunaemfahamu. Endelea tu dada kutoa maoni yako kwa uhuru mpana kabisa wa JF. Tunaomfahamu Mwalimu hatuna tatizo nawe ati. Jana ulikwenda kuchangia TV IMANI?
 
YAHUSU: MAJIBU JUU YA HESHIMA KWA MWALIMU NYERERE KAMA BABA WA TAIFA, KUTAMBULIWA NA BUNGE

Naomba mniwie radhi kwa kuchukua muda kuwarudia juu ya hili, sababu kubwa ni kwamba ilinibidi pia nisubiri majibu ya email kutoka kwa historians (kutoka vyuo vya nje) kuhusu mtazamo wa juu ya Heshima inayoitwa "BABA WA TAIFA". Historians hawa ni raia wa: Marekani, Afrika Kusini, China na India. Nitaanza na utafiti wangu wa nje, halafu baadae Tanzania.

Niliwauliza these historians maswali makuu kama ifuatavyo:

I. Je, Suala la kiongozi kupewa heshima ya BABA WA TAIFA katika Taifa husika linahitaji kutambulikwa kisheria?

II. Je, heshima ya BABA WA TAIFA inaweza kutenguliwa?

MAELEZO YAO yamegawanyika katika maeneo makuu sita:

  1. Kwanza, suala la BABA WA TAIFA, sio lazima litambulike kisheria; nchi haina haja ya kuwa na sheria maalum; muhimu ni uwepo wa makubaliano, mapatano, au mwafaka miongoni mwa wengi; historia ya nchi husika ndiye mzazi wa tunu hiyo, na sio ugomvi, ushindani, au majadiliano yenye utata kitaifa, juu ya mtu huyo.
  2. Mbili, ni nchi chache sana duniani zenye heshima hii Kisheria. Viongozi kama NELSON MANDELA, MAHTMA GHANDI, na SUN YAT SEN wana heshima za kudumu kama BABA WA MATAIFA YA, ingawa hakuna sheria maalum inayowapa heshima hiyo.
  3. Tatu, heshima ya BABA WA TAIFA is not supposed to be controversial (ugomvi, ushindani, majadiliano yenye utata), kwani ni suala la LOGIC (la kimantiki), ilimradi kuna makubaliano, mapatano, au mwafaka miongoni mwa wengi katika jamii, kwa kufuata jadi na kuzingatia historia iliyopo.
  4. Nne, ikiwa Serikali husika (inayo ongozwa kidemokrasia) tayari inamtambua mtu Fulani kwa matamshi na maandishi, kwamba yeye ndiye BABA WA TAIFA, na heshima hii kupokelewa na wengi katika jamii, tunu hii haiwezi tena futwa au batilishwa, sana sana itatungiwa Sheria mbalimbali ili kuiongezea nguvu, huku juhudi kubwa ikielekezwa katika kutunza kumbukumbu juu ya kiongozi huyo, hasa vizazi vya baadae.
  5. Tano, iwapo Heshima ya BABA WA TAIFA kwa mhusika, inatumika rasmi ndani ya chombo cha kutunga sheria (BUNGE) la kidemokrasia, bila ya kupelekea ugomvi, ushindani, au majadiliano yenye utata, hata kama hakuna sheria maalum kumtambua mtu huyo kama BABA WA TAIFA, kwa vile Bunge ni Chombo Cha Kutunga Sheria, kuna MANTIKI, SIO UHALALI, juu ya hoja kwamba, BABA WA TAIFA anatambulika na BUNGE, kwa mujibu wa Sheria.
  6. Sita, ni msisitizo kwamba:
​Hakuna mantiki kwenye hoja kwamba Heshima BABA WA TAIFA ni halali iwapo tu he is conferred (ametunukiwa) by ACT OF PARLIAMENT (Muswada/Sheria ya Bunge). Kwani ili Heshima Hiyo itambulike kisheria kupitia ACT OF PARLIAMENT, ni lazima kwanza itanguliwe na heshima kwa njia ya JADI au DESTURI. Kwa maana nyingine, mtu huyo lazima awe na heshima hiyo as CUSTOMARILY CONFERRED/JADI/DESTURI; sheria hufuata baadae (iwapo kutakuwa na ulazima).

Vinginevyo, heshima hiyo kuanzia na njia ya Sheria sio sahihi, iwapo nia ni kumpa mhusika heshima ya kudumu. Iwapo sheria itatangulia desturi, basi uwezekano wa kuitengua heshima hii siku za mbeleni utakuwa ni mkubwa. Mwana historia huyu akasisitiza pia kwamba, katika jamii yoyote, Heshima sio kitu cha sheria, bali jadi, vinginevyo heshima haitakuwa na maana, thereby not sustainable.



Historian mmoja akatoa maelezo kwamba heshima ya BABA WA TAIFA:

[…is conferred upon people who are exceptionally benevolent; who have rendered extraordinary services to the nations' Liberation and Unity; who are widely recognized in their society as compassionate and venerable men; and loyatly towards such individuals should not be confided within a certain political party, but instead, nation-wide in a non – partisan way; the incumbent should always and clearly act first and foremost in the interest of the nation, not his political party...]

This Historian pia amesema kwamba:

[…For a country like Tanzania (as it is often the case in most societies in Africa), customary law is often used along side common law and civil law; incase the incumbent becomes conferred by ACT OF PARLIAMENT, in order for this ACT to have a footing in the society concerned, customary law also has to be considered…]

Hapa katika suala la CIVIL LAW, COMMON LAW, CUSTOMARY LAW kwa kweli alinichanganya, kwani hakufafanua zaidi.

Historian mmoja pia aliniacha na Maswali matatu:

  • Je, loyalty ya BABA WA TAIFA lenu inaegemea zaidi on his political party, au dini Fulani au ethnic group fulani, au ni Loyatly kitaifa bila itikadi za chama, dini, au kabila?
  • Je, did he rise above his political party, in words and deeds?
  • Je those who doubt and disqualify Nyerere's key role in the liberalization and unification of such a diverse society, with results that are vivid, how do they build their argument?
Sikuyajibu maswali haya, nia yangu ikiwa ni kuyaacha yawe sehemu ya mjadala huu.Vinginevyo, mengi nilikwisha yaeleza kwenye hoja yangu ya msingi.

Pia kuna historian mmoja wa Marekani, Professor Emeritus, aligusia suala la Mwalimu na JFK na kusema kwamba serikali ya marekani chini ya Rais J.F.Kennedy (1963) ilimtambua Nyerere kama BABA WA TAIFA, kwa kufananisha juhudu zake na za George Washington. HILI NTALITOLEA USHAHIDI ALIONIPA BAADAE KIDOGO). Professor huyu akaenda mbali zaidi na kuelezea jinsi gani Nyerere alijijengea Heshima kwa mataifa makubwa kutokana na uwezo wake to lead the liberation struggle bila kuhamasishwa his followers kunyanyua silaha, pamoja na uwezo wake mkubwa wa kujenga hoja UN kudai uhuru wa nchi yake, kiasi cha kumpelekea kupata heshima kubwa sana duniani. Pia anasema kwamba, wakati wa Utawala wa Kennedy, Uongozi wa Marekani ulijiona upo sawa na wa Nyerere in the sense of kujitoa katika makucha ya ukoloni wa Mwingereza, huku pia ku advocate for peace, unity, and reconciliation katika jamii iliyokuwa very much diverse at that time.

Nadhani LOGICALITY OF MY ARGUMENT kuhusu Heshima ya BABA WA TAIFA Mwl NYERERE NA BUNGE, doent requires much explanation. Hata hivyo, nitazidi kuwasumbua na maelezo marefu hapa chini on how I came up with this logic, hususan Nyerere kutambulika kama BABA WA TAIFA na Bunge Kwa Mujibu wa Sheria. Hii ni muhimu kwa GAMBA LA NYOKA, Dada Faiza, na wengineo.

Kwanza, lazima nikiri kwamba hoja yangu ya msingi kuhusu Heshima ya BABA WA TAIFA kutambulika kwa mujibu wa sheria, ilikuwa dominated zaidi na passion and feelings, with minimum facts, kwani sikueleza bayana sheria ipi inamtambua Mwalimu kama baba wa taifa. Mniwie radhi kwa hilo. All that being said, majibu ya wana historia hapo juu ni ishara kwamba, kwa mtu mzalendo wa taifa hili, hana haja ya kutumia akili ya ziada kuhoji facts, au kupitia utafiti unaohitaji a certain methodology kufikia conclusion kwamba Mwalimu Nyerere anatambulika na Bunge, kwa mujibu wa Sheria (tafadhali rejea jibu la NNE, TANO, na SITA la historian hapo juu).

Besidies, sote twafahamu kwamba Humans Are Not Creatures of Reason, BUT of Passion or Feelings. Lakini haina maana kwamba tafiti zangu zote huwa zinasukumwa na belief au opinion, hapana; I am always a good slave of reason, and hardly a master of belief or opinion, kama kwa hili la Mwalimu Nyerere, ambalo nipo tayari kubeba lawama. Vinginevyo, given majibu ya historians (Jibu namba 4, 5 na 6, hapo juu), I still believe kwamba hoja yangu ilikuwa, NOT ONLY REASONED BUT ALSO WAS BASED ON A REASONABLE JUDGEMENT.

Kwanini nadiriki kusema hivyo?

Mbali ya majibu ya historian hapo juu (jibu 4, 5, 6), sasa tuangalie mambo yaliyojiri katika kikao Cha 30 Cha Bunge, Mwaka 2004. Taarifa hii nimeipata kwenye Hansard.


  • KIPINDI CHA MASWALI NA MAJIBU BUNGENI, MWAKA 2004
Kikao cha 30, Tarehe 21 Julai, 2004, Mheshimiwa Eliachim Simpasa, aliuliza Swali juu ya matumizi ya Jina la Hayati Mwalimu J. K Nyerere, kama ifuatavyo kwa Waziri husika:

Kwa kuwa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere alifanya mambo mengi na makubwa na mema ndani na nje ya nchi kama vile kuwaunganisha Watanzania kujiona wamoja, kuweka misingi ya maendeleo kama shughuli za uchumi, elimu, afya, miundombinu lakini zaidi alikuwa Kiongozi Mashuhuri wa karne katika harakati za Ukombozi wa Afrika, kupinga unyanyasaji, ubaguzi, ukandamizaji wa aina yoyote popote duniani na hivyo kujijengea umaarufu ndani na nje ya Taifa letu, Je:

  • Isingekuwa jambo la busara na la hekima kuhakikisha kuwa Jina hilo (Nyerere) linatajwa kila siku ndani na nje ya nchi kwa kuvipa jina lake vitu kama Dar es Salaam International Airport ikaitwa Nyerere International Airport (NIA) na University of Dar es Salaam kuitwa Nyerere University?
Waziri Husika Alijibu:

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Eliachim Simpasa, Mbunge wa Mbozi Magharibi kama ifuatavyo:-

· Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi wakati nikijibu Swali Na. 259 la Mheshimiwa Faida Mohammed Bakar, Mbunge wa Wawi kuwa, kutunza kumbukumbu za nchi hususan za Waasisi wa Taifa ni jambo la msingi.

· Kwasasa Serikali inaandaa utaratibu wa Sheria utakaojenga mazingira ya kuwa na utamaduni wa kudumu wa kuthamini, kutunza na kudhibiti kumbukumbu za Viongozi wetu Wakuu wa Kitaifa ili kuhakikisha kuwa hazina waliyonayo viongozi wetu hawa haipotei na inakuwepo kwa ajili ya vizazi vijavyo. Mapendekezo ya Mheshimiwa Eliachim Simpasa, ni mazuri na Serikali imeyapokea na itayawasilisha kwa wadau mbalimbali likiwemo Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kupitia Muswada na kutunga Sheria. (Makofi).

· Mheshimiwa Spika, moja ya mambo ambayo Muswada utazingatia ni matumizi ya Jina la Baba wa Taifa. Muswada huu utaweka utaratibu wa matumizi sahihi ya majina ya Waasisi wa Taifa letu kwa kuhakikisha kwamba, majina yao hayatumiki kibiashara, hayadhalilishwi na hadhi yao haipotei. (Makofi).]


  • KIKAO CHA BUNGE MWAKA 2005 KILICHOPITISHA MNMA ACT, 2005
Taarifa hii niliisikia/ona kwa macho yangu kwenye luninga.

Baada ya majibu katika kikao cha 30 (Mwaka 2004) juu ya msimamo wa serikali huo juu ya matumizi ya jina la baba wa taifa, mwaka uliofuatia (2005), suala hili likajitokeza tena katika Bunge, wakati huu kupitia muswada wa Kuanzishwa kwa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa mujibu wa Sheria.

Katika kikao chiki, Hoja za serikali, hoja za wabunge, pamoja na majibu ya serikali, yalizidi kujenga, sio kubomoa, maandalizi ya utaratibu wa kumpa Mwalimu Nyerere Heshima kama BABA WA TAIFA, kama iliyvoahidiwa na serikali, katika kikao cha mwaka mmoja kabla (rejea kikao cha 30, Julai 31 2004).
Wakati waziri husika anawasilisha "The Mwalimu Nyerere Memorial Academy Act, 2005", alitamka yafuatayo, ndani ya chombo cha kutunga sheria, chenye wabunge wa pande zote mbili za muungano, na kutoka vyama mbalimbali vya Siasa (pia oanisha hili na jibu namba 4 & 5 la historians pale juu):

[…Mheshimiwa Spika, Serikali imeidhinisha uamuzi wa kubadili jina la Chuo cha Sayansi Kijamii Kivukoni ili sasa kiitwe Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kumuenzi Mwalimu Nyerere kama Baba wa Taifa Letu. Nia ni kuendelea na utekelezaji wa serikali wa kuendeleza mambo yote ambayo Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, aliyasimamia wakati wa uhai wake kwa maslahi ya Taifa. (MAKOFI).

[..…Chuo hiki pia kitakuwa na tawi lake Zanzibar, kwa mujibu wa Sheria (MAKOFI).]


  • MKUTANO WA ISHIRINI, KIKAO CHA NANE, TAREHE 16 JUNI, 2005
KIPINDI CHA MASWALI NA MAJIBU

MHE MBARUK K. MWANDORO aliuliza:

Kwa kuwa utumishi wa Hayati Mwalimu J. K. Nyerere hauna mfano katika taifa letu, Afrika na Ulimwenguni kote na kwa kuwa, njia mojawapo ya kuwaenzi watu wenye sifa kama hizo ni kuhakikisha kuwa majina yao yanawekwa kwenye kumbukumbu za vitu vikubwa ili majina yao yaendelee kukumbukwa:-

  • Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kubadilisha jina la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Dar es Salaam kuwa Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (Nyerere International Airport) au Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwa, The Mwalimu Nyerere University ili jina hili liendelee kutajwa kwenye Taasisi kubwa kama hizo kuliko kulitumia jina hili kwa vitu vidogo vidogo ambavyo havijulikani sana Kimataifa?]
Waziri Husika alijibu:-

  • Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwandoto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa utumishi Hayati J. K. Nyerere hauna mfano katika Taifa letu, Afrika na Ulimwenguni kote na kuwa moja ya njia nzuri za kuenzi watu wenye sifa kama za Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume, ni kutumia majina yao kwenye kumbukumbu za vitu…..]

  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mapendekezo ya kumuenzi Baba wa Taifa yaliyotolewa na Mheshimiwa Simpasa, Wizara na Taasisi husika katika kutimiza azma hiyo zimechukua jitihada za awali. Ni mategemeo yetu kuwa wahusika ambao ni sekta ya uchukuzi na elimu sawia watazingatia ushauri huo wakati wanatafakari namna ya kumuenzi Baba wa Taifa na Ofisi yangu itatoa ushirikiano wake. (Makofi)……….]
​

MKUTANO KUMI NA TATU, TAREHE 31 OKTOBA, 2008

KIPINDI CHA MASWALI NA MAJIBU: Makumbusho ya Taifa ya Mwalimu J. K. Nyerere

MH. ROSEMARY K. KIRIGINI Aliuliza:-

Kwa kuwa, Makumbusho ya Kitaifa ya Mwalimu J. K. Nyrerere yaliyoko kwenye kijiji cha butiama yalifunguliwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Fredrick T. Sumaye hapo tarehe 2 Julai, 1999 kwa lengo la kutafiti, kuhifadhi, kutoa elimu kwa Umma na kutunza Kumbukumbu za ki-historia za Baba wa Taifa na za Taifa kwa ujumla; na kwa kuwa Makumbusho hayo yamekuwa kichocheo cha Utalii wa ndani ambao unachangia paoto la ndani la Serikali lakini yako katika hali mbaya ya ukosefu wa fedha, watumishi wachache n a uhaba wa nyumba za kuishi watumishi:-

(a)Je, Serikali haioni umuhimu wa kuyaboresha Makumbusho hayo ili yawe ya kisasa kwa kuongeza na kuanisha maeneo ya Kumbukukmbu za kihistoria za Baba wa Taifa, kuboresha mazingira yake, kujenga nyumba za watumishi wake na kuweka urafiki kwa ajili ya watalii?

(b)Je, Serikali haioni kwamba ni muhimu Makumbusho hayo yakawekwa chini ya Serikali kuu ili itengwe fungu maalum la Bajeti ya Serikali na kuondoa ile dhana ya kueleweka kuwa Makumbusho hayo ni Shirika la Umma na pia iweze kufanya shughuli zake kwa ufanisi mkubwa kwani shughuli zake zinafanana na zile za Makumbusho yote hapa nchini?

Waziri Husika alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Rosemary Kirigini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Serikali kupitia Shirika la Makumbusho ya Taifa, linaendelea na mchakato wa kuongeza na kuanisha maeneo ya kumbukumbu za historia ya Baba wa Taifa kama moja ya majukumu yake. Katika kuboresha mazingira yake, kiasi cha shilingi milioni sitini (60,000,000/=) kimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa gari jipya ili kurahisisha utendaji wa kazi katika makumbukusho hiyo. Aidha bajeti kwa ajili ya makumbusho ya Mwalimu J. K. Nyerere imeongezeka katika kipindi cha miaka minne (4) kutoka Tsh. 14,561,580 mwaka 20005/2006 hadi Tsh. 123,624,202.40 mwaka 2008/2009.


  • John F. Kennedy na BABA WA TAIFA:
​

Wadau, ni jambo lisilo na mjadala kwamba hakuna Rais wa Tanzania (pengine Afrika nzima) alie wahi kupewa heshima kubwa katika ziara/mapokezi nchini Marekani, marufu kama ‘free world', kama aliyopewa Mwalimu Nyerere wakati wa JKF (1963). Nimepewa link ya video na historian mmoja inayoonyesha jinsi gani MAREKANi ilimpa heshima Mwalimu Nyerere kutokana na mchango wake kulikomboa Taifa. Katika dunia ya leo, pengine ni Mandela pekee ndiye anaweza pokewa vile, vinginevyo heshima kama hii sana sana wanapata viongozi wa G8, na baadhi ya nchi za OECD.

This video is dedicated to wale wote humu JF, wenye kumheshimu Mwalimu katika nafasi aliyonayo kama BABA WA TAIFA (au kwa heshima equivalent to BABA, ilimradi haiwanyimi haki kutokana na imani zao za dini au mila), THIS VIDEO CLIP IS FOR YOU.

Kwa wengine wote, GAMBA LA NYOKA, NAS DAZ, Dada FF, TOPICAL, BARUBARU na wengineo, mna haki ya kutompa heshima Mwalimu kama BABA WA TAIFA, kama heshima inavyosimama sasa (bila mabadiliko). Lakini Ndugu zangu, iwapo video clip ya Mwalimu na JFK haikugusi kwa namna moja au nyingine, na pengine kupelekea machozi kukulenga kwa furaha na kujisikia kama shujaa kuwa Mtanzania (ingawa sio lazima), kutokana na heshima aliyotujengea Mwalimu, na kumuheshimu kwa kazi aliyoifanya kwa ajili ya taifa hili, hakika mna haki zote kumkebehi, lakini huo ni ushahidi tosha kwamba kwa kweli we have fundamental differences in this country – kuhusu tumetoka wapi, tupo wapi , na tunaenda wapi.

Video hii ni kwa wale wanaothamini kazi ya Mwalimu kutuunganisha kuikomboa nchi yetu bila migawanyiko ya dini, kabila, rangi, au jinsia, na kutuongoza tuishi kama taifa huru kwa amani, umoja, na mshikamano bila ya kujali tofauti zetu, na kutubakisha kazi moja tu sasa ya: KUJIKOMBOA KIUCHUMI.

Kwa wale wanaopingana na hilo, hakika, haki ni yenu. Kwa video hiyo ya Mwalimu na JFK, gonga hapa Nyerere's Official Visit to US 1963 - YouTube

Nawasilisha.
 
kwanza, lazima nikiri kwamba hoja yangu ya msingi kuhusu heshima ya baba wa taifa kutambulika kwa mujibu wa sheria, ilikuwa dominated zaidi na passion and feelings, with minimum facts, kwani sikueleza bayana sheria ipi inamtambua mwalimu kama baba wa taifa. Mniwie radhi kwa hilo. All that being said, majibu ya wana historia hapo juu ni ishara kwamba, kwa mtu mzalendo wa taifa hili, hana haja ya kutumia akili ya ziada kuhoji facts, au kupitia utafiti unaohitaji a certain methodology kufikia conclusion kwamba mwalimu nyerere anatambulika na bunge, kwa mujibu wa sheria (tafadhali rejea jibu la nne, tano, na sita la historian hapo juu).

bwana mchambuzi, kwanza naomba nikupongeze kwa kuwa muungwana, kwa kukiri pale ulipokosea, hivi ndivyo kijiwe chetu cha jf kinavyotakiwa kiwe!. Ni vyema next time ukaja na facts badala ya passion na emotion, wengi tunamkubali mwalimu lakini tunataka ifahamike wazi kwamba historia ya tanzania nyuma yake wapo watu wengi na wala siyo one man show.

Hata hivyo, kutamkwa kwa jina "baba" wa taifa ndani ya bunge bila kipingamizi haimaanishi nguvu ya kisheria ya jina hilo, au jambo hilo!. Bungeni kuna taratibu mbalimbali za kufuata ili kulipa jambo nguvu za kikanuni/kisheria.

Kwa mantiki hiyo basi, nasema kwamba tanzania tuna "mababa"/ mama wa taifa wengi, mwalimu akiwa mmojawapo, wengine miongoni mwao ni kama mzee karume, kawawa, wale 17 aliowataja jk, na wale waadilifu waliofanya kazi ya kusimika misingi ya taifa letu kama sokoine etc.

Hawa ndiyo founding fathers/ fathers of the nation.
 
bwana mchambuzi, kwanza naomba nikupongeze kwa kuwa muungwana, kwa kukiri pale ulipokosea, hivi ndivyo kijiwe chetu cha jf kinavyotakiwa kiwe!. Ni vyema next time ukaja na facts badala ya passion na emotion, wengi tunamkubali mwalimu lakini tunataka ifahamike wazi kwamba historia ya tanzania nyuma yake wapo watu wengi na wala siyo one man show.

Hata hivyo, kutamkwa kwa jina "baba" wa taifa ndani ya bunge bila kipingamizi haimaanishi nguvu ya kisheria ya jina hilo, au jambo hilo!. Bungeni kuna taratibu mbalimbali za kufuata ili kulipa jambo nguvu za kikanuni/kisheria.

Kwa mantiki hiyo basi, nasema kwamba tanzania tuna "mababa"/ mama wa taifa wengi, mwalimu akiwa mmojawapo, wengine miongoni mwao ni kama mzee karume, kawawa, wale 17 aliowataja jk, na wale waadilifu waliofanya kazi ya kusimika misingi ya taifa letu kama sokoine etc.

Hawa ndiyo founding fathers/ fathers of the nation.

Kwa mtazamo wangu, hadi ifikie hatua hiyo - yani, kuwaita hao baba na mama wa taifa hili, what ever has been conferred on Mwalimu ambacho kwa kweli hakijaamsha hisia nchini za kupingana na hilo, should stand as it is; lakini umuhimu wa kuwatambua hao wengine upo, na kama kuna watu watakaochagua kufanya hivyo kwa kuanzisha mjadala wa kitaifa, basi iwe hivyo, vinginevyo wale watu kumi na 17 ni founders wa TANU after TAA, in 1954, ambao mafanikio ya organization hayo since its inception yalitegemea sana influence ya Mwalimu. Nitawasilisha hilo baadae kidogo based on how history was being written as it happened miaka ile, sio historia iliyoandikwa sasahivi bali reactions, na vurugu zote za serikali ya kikoloni, na jinsi gani baadhi ya wenzake mwalimu (wale 17) walivyokuwa wanasubiri maamuzi ya Mwalimu n.k.

Vinginevyo ningependa sana kujua kwa mtazamo wako, Nyerere angekuwa baba wa taifa peke yake under what factors, and what specific factors make you believe he shares hiyo heshima na wengine uliowataja;
 
Hata hivyo, kutamkwa kwa jina "baba" wa taifa ndani ya bunge bila kipingamizi haimaanishi nguvu ya kisheria ya jina hilo, au jambo hilo!. Bungeni kuna taratibu mbalimbali za kufuata ili kulipa jambo nguvu za kikanuni/kisheria.

Nimelielezea hili - kwamba mwaka 2004, serikali iliahidi kuweka utaratibu unaousema; then ilipofika mwaka 2005, utaratibu huo ukaanza kwa kuanzisha chuo cha kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, kama hatua za kumuenzi Mwalimu kama baba wa taifa; vikao vilivyofuatia ikawa ni ahadi zaidi juu ya jinsi gani taratibu hizo zitafuata;

isitoshe, je, kwanini Chuo cha Kumkukumbu Cha Mwalimu Nyerere kipitishwe chini ya sheria maalum, unlike vyuo vingine kama Agha Khan, Tumaini n.k ambavyo ile sheria ya kuruhusu participation ya taasisi nje ya serikali ilitosha kukianzisha MNMA?
 
bwana mchambuzi, kwanza naomba nikupongeze kwa kuwa muungwana, kwa kukiri pale ulipokosea, hivi ndivyo kijiwe chetu cha jf kinavyotakiwa kiwe!. Ni vyema next time ukaja na facts badala ya passion na emotion, wengi tunamkubali mwalimu lakini tunataka ifahamike wazi kwamba historia ya tanzania nyuma yake wapo watu wengi na wala siyo one man show.

Hata hivyo, kutamkwa kwa jina "baba" wa taifa ndani ya bunge bila kipingamizi haimaanishi nguvu ya kisheria ya jina hilo, au jambo hilo!. Bungeni kuna taratibu mbalimbali za kufuata ili kulipa jambo nguvu za kikanuni/kisheria.

Kwa mantiki hiyo basi, nasema kwamba tanzania tuna "mababa"/ mama wa taifa wengi, mwalimu akiwa mmojawapo, wengine miongoni mwao ni kama mzee karume, kawawa, wale 17 aliowataja jk, na wale waadilifu waliofanya kazi ya kusimika misingi ya taifa letu kama sokoine etc.

Hawa ndiyo founding fathers/ fathers of the nation.
Public Holidays Act.

Nyerere Day, pia ipo kwenye employent Ordinance na Bank of Tanzania Act.... Bank days huwa zipo internationally recognized. Nyerere Day is internationally and Nationally recognized by law.

So his legacy as the Father of the Nation is legally recognized by those acts.
 
Baada ya kukupa aya za Qur'an, nimekushishia nondo kutoka biblia, tazama post #648 sasa wewe amuwa unaifata ipi? au kama unafata matamanio yako huko jukwaa la wakubwa hayo ni yako, mradi uwe umekidhi vigezo. Hapa ni JF na mimi ni FF aka selebriti namba moja JF. Bye.

Kama ambavyo dini imekukataza kumwita mtu mwingine DINI hiyo hiyo ndiyo inayotukataza kuitana majina ya dhihaka yasiyo na mantiki ndani ya dini yetu; inakuwaje wewe unatulazimisha kukuita FOXY jina ambalo limekaa kikahba zaidi? Sasa hiyo ni tafsiri kutoka Sura Al-Hujurat 49 :11; na kama unataka nikuwekee aya zote 49:11&12; zinafuatana na hata ulipoweka tafsiri ya 49:12 uliiona aya 11 mbona hukuiweka? Wewe si mkweli hata ndani ya nafsi yako; nakiri tasfiri ya kwanzan ilikuwa nakosa la uchapishaji kwenye namba ya aya, lakini ukweli aya ya Mwenyezi Mungu yenye kukataza majina ya namna yako kama FOXY yapo ndani ya Sura Al Hujurat.

Sahih International
O you who have believed, let not a people ridicule [another] people; perhaps they may be better than them; nor let women ridicule [other] women; perhaps they may be better than them. And do not insult one another and do not call each other by [offensive] nicknames. Wretched is the name of disobedience after [one's] faith. And whoever does not repent - then it is those who are the wrongdoers.

Swahili
Enyi mlio amini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao, wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao. Huenda hao wakawa bora kuliko wao. Wala msivunjiane hishima, wala msiitane kwa majina ya kejeli. Ni uovu kutumia jina baya baada ya kwisha amini. Na wasio tubu, hao ndio wenye kudhulumu.
 
Hili la baba wa taifa tuachane nao wanopinga wakameze wembe... turudi kwenye mada yetu.
Ndugu zetu mnaomkejeli Mwalimu, hoja zenu kwamba Ujamaa umetupotezea muda, Je wenzetu hapo juu wameutumiaje muda huo? Je, hii haitoshi kuwaonyesha kwamba kuna mdudu hapa ambae ni common kwetu sote ambae anatufana, bila ya kujali Ujamaa au Soko Huru? Ndio maana Mwalimu anabakia kuwa Rais Bora wa Tanzania mbali ya kuwa baba wa taifa kwa sababu alithubutu kujaribu geuza madudu haya, kwa kulipa taifa letu a self determination chini ya Ujamaa na Kujitegemea. Kilichomshinda Mwalimu ni uchanga wan chi kuweza kuzalisha kwa wingi na wakati huo huo kutimiza ahadi za uhuru – ajira kwa wote, huduma bora kwa wote. Angalau alishindwa lakini hakuwasaliti na ahadi zake za wakati wa uhuru. Mbali ya hili na pia utekelezaji mbaya wa sera, sababu za kushindwa pia ni kutokana na unduminakwili wa baadhi ya watendaji wake ambao walikuwa wanashirikiana na mabepari wa nje, na hatimaye kumshinda nguvu. Nyerere bado ni Rais bora kutokana na ukweli kwamba alishindwa kwa sababu za maadui (ukiachilia utekelezaji mbovu wa sera); Bado Nyerere ni Rais bora kwani hata nchi za nje zilimpa heshima ya kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kusini – South Commision, hata baada ya Ujamaa kushindwa, kwa kutambua kwamba ana uwezo wa kuziletea nchi zote maskini mwongozo wa jinsi gani ya kupambana na mfumo wa uchumi wa kimataifa usio wa haki.
Kipande hiki nimekipenda sana na hakika nitachangia kwa wale wasiojua mahesabu ili wapate kujua kama kweli tulishindwa ama kulichangiwa sababu nyingine kabisa..

Nitawapa mfano mdogo sana:-
- Kuanzia mwaka 1972 hadi 1982, Tanzania tulikuwa na mashamba ya Kahawa Hectares 126,000 zikizalisha kahawa wastani wa tani 46,000kila mwaka - yields about 390 kgs per hectare...
- Na sasa hivi tuna hectares za kilimo cha kahawa zaidi ya 300,000 tunazalisha kahawa kwa wastani wa tani 60,000 kwa mwaka - yields about 320 kgs per hectare...

Sasa waungwana kweli unaweza kusema leo hii tumeendelea kwa sababu tu leo hii Kahawa imepanda bei wakati uzalishaji ndio kama mnavyoona hapo juu.
Hivi kweli mama mpika vitumbua alokuwa akiuza vitumbua 1,000 kwa siku mwaka jana kwa bei ya Tsh 500 ana nafuu zaidi mwaka huu kwa sababu anauza vitumbua 600 kwa bei ya Tsh 1000? kwa sababu tu kuna watu wanatazama pato la mauzo kutoka laki 5 ya mwaka jana kwenda laki 7 mwaka huu bila kuzingatia sababu nyinginezo ikiwa ni pamoja na hata gharama za huyo mama ktk matumizi na kupoteza wateja 300!...

Naomba wasomi wa uchumi mnielimishe..
 
Back
Top Bottom