bwana Mchambuzi wewe unasema mimi nakwepa hoja yako, mbona unakuwa msahaulifu mimi nasimamia ndani ya hoja yako ile ile, ulipotamka wazi tofauti kati ya heshima ya "baba wa Taifa " na "Raisi bora" ukasema wazi kwamba "Ubaba wa Taifa" ni jambo la kisheria, NIKAKUOMBA ULETE HIYO SHERIA ILI BASI TUPROVE KWAMBA MWALIMU NYERERE NI "BABA" WA TAIFA KWA MUJIBU WA SHERIA BADO HUJAILETA HAPA JAMVINI.
Sasa basi unaposema kwamba Bunge limeridhia Nyerere kuitwa baba wa Taifa kati ya mwaka 2003 na 2005, basi maana yake mwaka 2002 kurudi nyuma hakuwa baba wa Taifa, UNLESS OTHERWISE UBADIRISHE USEMI WAKO KWAMBA "UBABA" WA TAIFA NI HESHIMA YA KISHERIA.
NDIYO MAANA NI MUHIMU SANA UKATULETEA SHERIA INAYOMTAMBUA NYERERE KAMA BABA WA TAIFA, LA SIVYO HILI LITAENDELEA KUWA NI MAONI YA MTU MMOJA MMOJA.
sasa wewe unataka kujua maoni yangu kuhusu "Ubaba wa Taifa", maoni yangu ni haya yaafuatayo.
(1) WAASISI WOTE WA TAIFA LETU WENYE MCHANGO MZITO , KAMA NI WA KIUME BASI NI MABABA WA TAIFA, NA WA KIKE NI MAMA WA TAIFA.
(2) UBABA WA TAIFA SIYO LAZIMA UWE RAISI WA KWANZA, KUWA RAISI NI MGAWANYO WA KAZI TU, LAKINI MTU YEYOTE ALIYEFANYA JUHUDI KUBWA ZA KULINUFAISHA TAIFA ZIMA WAKATI ULE WA UASISI WA TAIFA LETU BASI NI BABA WA TAIFA, KWA MAANA HIYO MTU KAMA KAWAWA NA KARUME SENIOR NINAWAONA KAMA MABABA WA TAIFA.
(3) NYERERE NINAMUONA PIA KAMA BABA WA TAIFA
(4) MPAKA MIAKA TAKRIBAN 30 HIVI YA UCHANGA WA TAIFA, NACHUKULIA KAMA MWENDLEZO WA UASISI KWA HIYO MTU YEYOTE ATAKAYETUMIKIA TAIFA KWA UADILIFU MKUBWA NA KUWA KATIKA NAFASI YA MAAMUZI MAZITO YA UMMA NA KUFANYA VYEMA BASI NI BABA WA TAIFA, KWA MAANA HII NAMUONA SOKOINE KAMA BABA WA TAIFA, NAMUONA ALHAJI MWINYI KAMA BABA WA TAIFA.
KWA NINI NYERERE HAWEZI KUWA BABA WA TAIFA PEKE YAKE?
(1) TANZANIA IMEUNDWA NA NCHI MBILI HURU ZANZIBAR NA TANGANYIKA, NYERERE SI MUASISI PEKE YAKE, YUPO MZEE KARUME, KAMA HOJA NI UASISI WA TANZANIA BASI NDO AWE BABA WA TAIFA BASI NA MZEE KARUME ANASTAHILI AWE BABA WA TAIFA
(2) KAMA NI SUALA LA UTENDAJI KAZI KIPINDI CHA UTAWALA WAKE BASI TUMEONA KASORO NYINGI SANA ZA UTENDAJI WAKE WA KAZI SITAKI KUZIRUDIA( KUNA MADA MAALUM KABISA YA HILO HAPA JF).
(3) KAMA TUKIKUBALI KWAMBA ZANZIBAR WANA MTU WAO WANAYESTAHILI KUMUITA BABA WA TAIFA, BASI NYERERE HAWEZI KUWA BABA WA TAIFA PEKE YAKE MAANA TAYARI UPANDE MMOJA WA MUUNGANO TAYARI UNA MTU AMBAYE ASHAPEWA HESHIMA HIYO.
Kwa haraka haraka, kwani sina mud asana, nadhani sasa nimekuelewa. Mbali ya wewe kusubiri nilete taarifa za bunge kuridhia heshima hii kwa Mwalimu, msimamo wako juu ya hii mada ni kama ifuatavyo:
a)Baba wa taifa sio lazima atokane na mchango wake kama kiongozi wa harakati za mapambano dhidi ya ukombozi au uhuru wa taifa husika; badala yake anaweza kuwa mtu mwingine yoyote ambae hata hakushiriki harakati hizo (mfano umemtaja Sokoine);
* Hili nilishalieleza kwenye my original post - kuhusu mchakato wa mtu kupitia before he's conferred with such a title; and this was based on the global view ambayo ni standard kwa nchi zote, na ndio maana kimataifa Mwalimu anatambulika hivyo; Kama hoja yako hapa ni kukataa kupangiwa views kama taifa (Tanzania) juu ya nani anastahili na nani hastahili na badala yake kila taifa liwe na vigezo vyake, huo ni mjadala mzuri, lakini hapa sio mahali pake; mjadala wa hapa ni je, wenzetu Afrika, Asia etc, wanatumai vigezo gani? Na nikaelezea kwamba kwa maana hiyo, hata sisi Nyerere ni Baba wa taifa; vinginevyo mjadala huu unaweza kwenda out of hand na tukaanza kuulizana kama Nyerere alikuwa na jeraha lolote la risasi Vis-a-Vis mwanaharakati mwenzake kupoteza mguu kabisa; the global view doesn't detail such; vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
b) Mtazamo wako wa pili: Nyerere sio Baba wa Taifa la Tanzania hata tukiamua kuiweka Zanzibar pembeni kwa dakika moja (nasema hivi kwa sababu umemtaja Sokoine);
* Hoja yako ya msingi hapa ni kwamba wapo watu wengine wanaostahili kupewa heshima hiyo kutokana na mchango wao katika taifa hili; hili nimeshalisema hapo juu na pia katika my original post; Otherwise kwa hoja hii, you are challenging the current global consensus on what establishes mtu kuitwa baba wa taifa; Mtazamo kwamba Sokoine, which means basi hata majina kama Msekwa, Msuya, kwamba wanastahili, can be very stimulating intellectually; ningependa kwa wakati mwingine kuingia katika mjadala huu kwani najua nitajifunza mengi; pia inaweza kuleta mabadiliko ya kifikra na kimtazamo kuhusu dhana nzima ya baba wa taifa, iwapo utalipanga in a good research context, and convince mabadiliko hayo kitaifa au hata kimataifa; Vinginevyo mpaka hilo litokee, mawazo yako nitaendelea kuyaheshimu juu ya Sokoine kustahili, lakini huku nikiendelea kuamini kwamba Mwalimu bado ni baba wa Baba wa taifa, kutokana na qualifications which have been already established in a global sense, hence emulated hapa kwetu;
vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
c) Mtazamo wako wa tatu ni kwamba Nyerere sio baba wa taifa hata katika mazingira ya Muungano (kwani umetoa hoja juu ya umuhimu wa Karume);
* Hili nilishalijibu katika hoja yangu ya msingi, ni kiasi cha wewe tu kurejea sehemu nayozungumzia Ubaba wa taifa na Muungano ambapo nilitoa mifano ya George Washington kama Muasisi wa Muungano wa Marekani uliokuwa na mataifa 16 tu (sio 50 ya leo); baadae muungano ukavunjika kwa miaka mitano, na uliporudi ukarudi na mataifa mengine mengi zaidi na kuzaa USA tofauti kabisa leo hii (50 states), na kwamba ingawa yote haya yalitokea akiwa hayupo, bado akapewa heshima hiyo; pia nikaeleza jinsi gani muungano wetu unachukua sura ile ile, mfano nikataja Tume ya Mark Bomani
vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
d) Mtazamo wako wa Nne ni kwamba Baba wa taifa sio lazima awe Rais wa kwanza wa Jamhuri huru;
* Hili nililielezea katika my original post kwamba sio lazima, ingawa mara nyingi waliendelea na hatua ya kuwa Marais wa kwanza wa Jamhuri huru husika; na kwamba kikubwa kuhusu baba wa taifa ni uongozi wake katika mapambano ya ukombozi kwa taifa husika; vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
e)Mtazamo wako wa tano ni kwamba hauna tatizo na neno BABA WA TAIFA kwa misingi ya dini;
* Hata kama ungekuwa na tatizo na hili, nilishalisemea kwamba naheshimu sana mtazamo huu kwani hakuna BABA katika Uislam. Nikashauri kwamba ni muhimu tufikie consensus on a term ambayo itakidhi mahitaji ya pande zote za jamii, as long as wana msimamo mmoja juu ya heshima hiyo kwa Nyerere; lakini kama hata katika hilo hakuna consensus, ofcurse kila mtu yupo huru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
f) Mtazamo wako wa sita/mchango wako tuseme, hautoi hisia zozote kwamba Tanzania tunahitaji mapinduzi mapya ili kumpata baba wa taifa;
* Hii inatokana na hoja yako kwamba wapo tayari watu wanaostahili kuitwa baba wa taifa, lakini sio Nyerere. Mjadala huu nao ni very stimulating kwani pia una challenge the current consensus kwamba baba wa taifa is inherent na harakati za ukombozi/uhuru; hili tumeshaliongelea hapo juu; vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
g) Mtazamo wako wa saba/mchango wako unatoa hisi kwamba Historia iliyopo ya taifa letu inatosha kutuzalia baba wa taifa mwingine kwa kutengua heshima wa baba wa taifa aliyepo, Nyerere ili apewe mtu mwingine ambae anastahili zaidi;
* Hii nayo ina challenge the current global consensus jinsi gani baba wa taifa anapatikana; ni hoja yenye mchanganyo sana, vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge utaratibu uliopo, na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
h) Mtazamo wako wa nane, Nyerere hastaili kuwa Baba wa taifa kutokana na mapungufu yake kiutendaji;
Hili nilishalizungumzia katika my original post nilipo ongelea mapungufu ya George Washington na wengine katika utawala wao; mfano, tofauti na Nyerere ambae angalau aliruhusu demokrasia ya chama kimoja, marekani haikuwa na chama chochote cha siasa chini ya baba wao wa taifa, George Washington; pia mchakato wa katiba mpya ya taifa la Marekani ulifanywa kwa njia zisizo za kidemokrasia kwani ilikuwa ni Washington na kikundi kidogo sana cha wanajeshi na wanasiasa; na katiba hiyo ilihusu mataifa 13 tu, na baadae wakati wa utawala wake, amendmentz zikafanywa kuruhusu mataifa mengine matatu; akafariki na katiba juu ya mataifa 16 (sio 50 ya leo) lakini bado akawa baba wa taifa; vinginevyo ofcourse una uhuru wa kuendelea to challenge vigezo vilivyopo kuhusu baba wataifa, san asana iwapo suala la utendaji liwe featured; na mpaka mabadiliko yatokee, tukubali kwamba kwa maoni ya wengi, kwa sasa JKN ndie baba wa taifa;
h) Na mtazamo wako wa tisa, Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzani, mbali na kutamka kutakuwa na Rais wa TZ na wa Zanzibar, haitambua heshima ya baba wa taifa.
Mimi sikusema chochote juu ya katiba, hapo unajichanganya, nimesema heshima hii inatambulika na bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania na kuomba unipe muda nije na taarifa kamili;
Nipo safarini mkoa kidogo lakini nina access ya internet from time to time, ntajitahidi kujibu hoja zako as much as I can;