Hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba Bunge liliridhia Nyerere kuitwa BABA WA TAIFA, na ninaendelea kutafuta taarifa hizo niziweke humu. Suala hilo lilitamkwa bungeni between 2003 au 2005;
Kuhusu hoja kwamba MOD to freeze the discussion, nadhani unge shauriana nae wewe moja kwa moja kuafikiana au kutoafikiana juu ya hilo;
Vinginevyo, binafsi naona kuna mambo ya msingi mengi sana ambayo tunaweza kuyajadili, including wewe kuendelea kukwepa thread yangu that i addressed kwako na kwa faiza na wengine; angalau tuanze mjadala kwa kusema kwamba - kwavile mchambuzi hajaweka taarifa rasmi za bunge kuridhia Baba wa Taifa kuwa Nyerere, basi mimi GAMBA LA NYOKA simtambui Nyerere kama baba wa taifa; Naomba tamko lako rasmi tadhafali ili nijue unasimama wapi, kama ni suala la bunge, imani ya dini na neno baba, au mengine ambayo nimeshayaeleza ili wakati natafuta taarifa za bunge, mimi na wewe tuendeleze mjadala kwa hoja, na kama hauwezi endelea kutokana na suala la bunge, basi tamka hivyo na mimi na wewe tuishie hapo, na niendelee na wengine, unless MOD afunge thread kama unavyomshauri. Ni hayo tu kwa sasa;
bwana Mchambuzi wewe unasema mimi nakwepa hoja yako, mbona unakuwa msahaulifu mimi nasimamia ndani ya hoja yako ile ile, ulipotamka wazi tofauti kati ya heshima ya "baba wa Taifa " na "Raisi bora" ukasema wazi kwamba "Ubaba wa Taifa" ni jambo la kisheria, NIKAKUOMBA ULETE HIYO SHERIA ILI BASI TUPROVE KWAMBA MWALIMU NYERERE NI "BABA" WA TAIFA KWA MUJIBU WA SHERIA BADO HUJAILETA HAPA JAMVINI.
Sasa basi unaposema kwamba Bunge limeridhia Nyerere kuitwa baba wa Taifa kati ya mwaka 2003 na 2005, basi maana yake mwaka 2002 kurudi nyuma hakuwa baba wa Taifa, UNLESS OTHERWISE UBADIRISHE USEMI WAKO KWAMBA "UBABA" WA TAIFA NI HESHIMA YA KISHERIA.
NDIYO MAANA NI MUHIMU SANA UKATULETEA SHERIA INAYOMTAMBUA NYERERE KAMA BABA WA TAIFA, LA SIVYO HILI LITAENDELEA KUWA NI MAONI YA MTU MMOJA MMOJA.
sasa wewe unataka kujua maoni yangu kuhusu "Ubaba wa Taifa", maoni yangu ni haya yaafuatayo.
(1) WAASISI WOTE WA TAIFA LETU WENYE MCHANGO MZITO , KAMA NI WA KIUME BASI NI MABABA WA TAIFA, NA WA KIKE NI MAMA WA TAIFA.
(2) UBABA WA TAIFA SIYO LAZIMA UWE RAISI WA KWANZA, KUWA RAISI NI MGAWANYO WA KAZI TU, LAKINI MTU YEYOTE ALIYEFANYA JUHUDI KUBWA ZA KULINUFAISHA TAIFA ZIMA WAKATI ULE WA UASISI WA TAIFA LETU BASI NI BABA WA TAIFA, KWA MAANA HIYO MTU KAMA KAWAWA NA KARUME SENIOR NINAWAONA KAMA MABABA WA TAIFA.
(3) NYERERE NINAMUONA PIA KAMA BABA WA TAIFA
(4) MPAKA MIAKA TAKRIBAN 30 HIVI YA UCHANGA WA TAIFA, NACHUKULIA KAMA MWENDLEZO WA UASISI KWA HIYO MTU YEYOTE ATAKAYETUMIKIA TAIFA KWA UADILIFU MKUBWA NA KUWA KATIKA NAFASI YA MAAMUZI MAZITO YA UMMA NA KUFANYA VYEMA BASI NI BABA WA TAIFA, KWA MAANA HII NAMUONA SOKOINE KAMA BABA WA TAIFA, NAMUONA ALHAJI MWINYI KAMA BABA WA TAIFA.
KWA NINI NYERERE HAWEZI KUWA BABA WA TAIFA PEKE YAKE?
(1) TANZANIA IMEUNDWA NA NCHI MBILI HURU ZANZIBAR NA TANGANYIKA, NYERERE SI MUASISI PEKE YAKE, YUPO MZEE KARUME, KAMA HOJA NI UASISI WA TANZANIA BASI NDO AWE BABA WA TAIFA BASI NA MZEE KARUME ANASTAHILI AWE BABA WA TAIFA
(2) KAMA NI SUALA LA UTENDAJI KAZI KIPINDI CHA UTAWALA WAKE BASI TUMEONA KASORO NYINGI SANA ZA UTENDAJI WAKE WA KAZI SITAKI KUZIRUDIA( KUNA MADA MAALUM KABISA YA HILO HAPA JF).
(3) KAMA TUKIKUBALI KWAMBA ZANZIBAR WANA MTU WAO WANAYESTAHILI KUMUITA BABA WA TAIFA, BASI NYERERE HAWEZI KUWA BABA WA TAIFA PEKE YAKE MAANA TAYARI UPANDE MMOJA WA MUUNGANO TAYARI UNA MTU AMBAYE ASHAPEWA HESHIMA HIYO.
NI NINI TOFAUTI YANGU KATI YANGU MIMI NA WEWE?
(1) WEWE UNASEMA UBABA WA TAIFA NI JAMBO LA KISHERIA, MIMI NASEMA SIYO LA KISHERIA
(2) WEWE UNASEMA HESHIMA YA "UBABA" WA TAIFA NI YA MTU MMOJA TU, MIMI NINASEMA WENGI AMBAO NI WAASISI WA TAIFA WANASTAHILI HESHIMA HII.
TUENDELEE NA MJADALA