Nyerere alimkosea nini Mungu?

Duh...? Sijui hata mmesoma shule gani nyie watu,unao ushahidi wa mkataba kati ya Mandela na wazungu ili wamtoe jela kisha alinde mali zao? Weka ushahidi mkuu.
Tanzania wakati wa Nyerere ilikuwa kituo kikuu cha wanaharakati wa kusini na mwa Africa na Dunia pia,ndo maana hata Che Guevera alikuja kwa siri Dar akakaa karibia mwezi kabla hajauawa na majasusi wa CIA Bolivia.
Huwezi kumsifia Nyerere kisha ukawadharau kina Mandela waliokuwa frontline wakati Nyerere akila mayai ikulu,kitendo cha kumdharau Mandela shujaa wa Africa kinadhihirisha jinsi Elimu ya Tanzania ilivyokufa
Kama elimu ya Tanzania imekufa basi jua kuwa haikuwahi kuwa hai. Kubali kujifunza kwa wenzako, ninachojua mimi wewe hujui na chako sijui pia.
 
Kuna mtu alinisihi sana nisiwajibu ila uvumilivu unanishinda ,hapa umeandika na kuonyesha uwezo wako wote wa akili ,hongera kwa kuwa na uwezo huo wa akili
Kama ni mfuasi wa chama fulani na viongozi wako ni marafiki na watu weupe ujue kanunuliwa tayari! Mzungu sio mjinga eti akuweke ndani akutoe bure. Kama hujui kaa kimya usaidiwe.
 
mandela anapewa promo tu yaani kama kwenye mpira tunasema anabebwa nimejaribu kumsoma mzee mandela lakini bado sijaona maajabu aliyofanya zaidi ya quotes zake tamu
SAsa anza kupitia quotes za Nyerere, km zimewekwa asali vile, daaah!. RIP father of the nation (Nyerere)
 
Nyerere kaondoka Duniani akiwa kaacha heshima kubwa mno kimataifa.
Wanasiasa wa Tanzania wamekuwa hawaachi kumtaja huyu Mzee kila mara kwenye kampeni au hotuba zao.

Alimshauri rafiki yake mkubwa hayati Nicolai Cesesscue enzi za uhai wake akiwa Rais wa Romania aachie ngazi ili kulinda heshima yake ,Nicolai hakusikia matokeo akaja kuuawa kikatili yeye na mkewe.

Alimshauri Kaunda wa Zambia naye hakusikia, "mzee mwenzangu waachie Vijana ulinde heshima yako ".

Kaunda akapuuza ushauri wa Nyerere matokeo yake akaja kuondoka Kwa aibu ya kushindwa uchaguzi, badala ya kustaafu, yaani Rais wa kwanza wa nchi unagombea tena, what a shame?

Heshima ya Nyerere Kwa Africa inazidiwa na Mandela tu, ukimtoa Mandela hakuna Rais tena wa kufananishwa na Nyerere ktk bara la Africa.

Kwanza alikuwa akiaanza kuongea unatamani uendelee kumsikiliza tu muda wote hata Kama ulikuwa na stress Ukisikiliza hotuba za Nyerere stress zinapungua.

Ukombozi wa mataifa ya kusini mwa Africa huwezi kuujadili bila kumjadili Nyerere ambaye ndo alikuwa key point ya Ukombozi Huo.

Ni katika Kipindi cha Urais wake Tanzania iliheshimiwa na hata kuogopwa na mataifa makubwa Duniani.

Pamoja na matatizo ya hapa na pale, lakini enzi zake uchumi wa Tanzania ulikuwa juu, pesa ilikuwa na thamani kubwa, noti ya mwisho Kwa thamani kubwa ilikuwa noti ya sh 100.

Elimu ilikuwa juu, siyo kama leo hii ambapo hata kiswahili tu kinawapa shida hata wahitimu wa vyuo vikuu, neno "hela " wanatamka "ela" neno "halafu "wanatamka "alafu " eti hao ni university graduates, kwenye English ndo unaweza hata kulia Kwa namna wanavyoboronga.

Enzi zake hata intelligence ya nchi ilitisha, TISS ya Nyerere haikuwa tofauti na CIA hutaki kuamini acha.

Wakati wa vita vya Kagera, TISS ilimzunguka Idd Amin Spain, alikuwa ameagiza makombora ya kisasa yenye nguvu lakini akajikuta anayakosa na yakaangukia mikononi mwa Tanzania.

Hatukuwa na silaha Kali Kama za Idd Amin, lakini tulikuwa na intelligence imara mno, hii ndo ilifanya tushinde vita bila msaada wa nchi yoyote, Idd Amin pamoja na kusaidiwa na Gaddafi bado tuliweza kumtwanga hadi akaikimbia Uganda.
Inahitaji Kitabu kuandika mambo mazito aliyofanya Nyerere.

Lakini alimkosea nini Mungu huyu mzee?
Mwandishi Munga Tehenani (RIP) aliandika Kitabu kiitwacho "Nyerere alikuwa mchawi ".
Kitabu hiki hakikukaa mitaani hata siku tatu kikawa kimepotea kimaajabu, ilikuwa ni kati ya mwaka 2001 au 2003.

Inadaiwa aliingia maagano na kuzimu na fimbo yake ndo ilikuwa muongozo wa mambo yake yote.

Maagano yoyote ya nguvu za giza humkasirisha Mungu na kukilaani kizazi cha mtu aliyeingia maagano hayo.

Mungu hulaani kuanzia watoto na hata vitukuu na vilembwe na hata kizazi cha nne.

Familia ya Rais Kennedy wa US aliyepigwa risasi mwaka 1963 imepukutika yote Kwa vifo vya ajali na kuuawa, hakuna alama yoyote ya Kennedy Marekani, yamebakia majina tu.

Nikiitazama Kwa jicho la tatu familia ya Nyerere haiko sawa, imefunikwa na giza nene, haing'ai, haionekani, it looks like Nyerere left no children to walk his ways,haya ni mambo ya Ulimwengu wa roho.

Hata ukuu wa wilaya tu imekuwa ishu? wanapata watu ambao wanaonea wivu wenzao wanaoinuliwa na Mungu, yaani mtu anataka ampangie hadi Mungu kwamba fulani anapaswa kuwa maarufu na mwingine hatakiwi.

Matendo yetu yawe mema au mabaya yana reflect maisha yetu ya baadaye.
Tuwe makini sana na tujae hofu ya Mungu .

cc:mshana jr

Makala ijayo:Dini ni Ugonjwa wa akili




Sent using Jamii Forums mobile app

Mmh nisitie neno ila wengine inaezekana kuzikwa wamezikwa kwa uchawi but hawafikii hata robo ya chembe kwa Mzee mi nakubali mzee alikuwa nondo mbona wapo wengi tu wapo kwenye maibada ya kuzimu na bado wanapelea na wengine wamerithisha koo zao mambo ya ajabu ajabu.

Nachohisi mzee aliwakuza watoto kimtindo wa enzi zile hakuwapa exposure tu kituu ambacho hata wazazi wa enzi hizi hawakifanyi kwa watoto wao unaeza kuta baba mfanya biashara mzuri akisepa tuu...biashara zinakufa haziendelei tena sababu hakuweza kupasisha kipaji kwa watoto.

Kwa hiyo concept yakusema mzee amelaanika eti kwakuwa kina nyereye hawapo sikubaliani.

WAPO WATU WENGI MAKOOO YAO YANARITHI USHETANI BADO WANADUNDA HAWAJALAANIKA HATA KIDOGO (kwa macho ya kibinadamu)

Nachofahamu ukoo wa nyerere hautaweza kuendana na ushetani uliopo sasa wizi, ubadhilifu, roho mbaya, ubinafsi ,upigaji dili, uonevu, kauli mbovu, vitisho ule ukoo hauwezi kabisa kuendana na uchafu uliopo sasa.

Ni kweli Mzee kwa level ya urasisi inaezekana alifanya mengi ambayo yalimlazimu kuyafanya akiwa kama kiongozi wa nchi sa zingine kuiumiza nafsi yake kwa kitu kibaya ili mambo yaende wanaoface challenge za uongozi wanaelewa.

Tuache utani kwa busara alizokuwa nazo mzee alijitahidi japo hata kuepusha bendera kutokuwa na marangi mekundu laana za damu ambazo tunaona wenzetu, kutwa rangi za damu kwenye bendera haziwaachi salama , halafu mtu unakuja tu kutamka laana kirahisi............Chunga sana.

Wakati huohuo kuna wabongo leo hii wanatoa kafara za basi yenye watu mia na zaidi ili tu yeye awe tajiri na bado familia inapeta, please tuwe serious mtu usiamke tu na mawazo uliyotoa kwenye astral nightmare.................kama upo kwenye asral experience please rudi uongee vitu vya duniani

Kama ungetaka kuwaona watoto wa nyerere kwenye nafasi kipindi hiki ni kama tu BABA YAO MWLIMU ANGEWARITHISHA MAMBO YA AJABU wangeweza tu, sababu wangekuwa wapigaji, watoa rushwa, wababe, wauza ngada na wakorofi na uhakika kwa tabia hizo wasingekosa nafasi unazotaka wawe.............

Kama ni conspiracy please ipeleke ulaya italipa (sababu wana wivu na weusi wenye akili sana).........hapa bongo utafeli.......

USIMTUKANE FATHER OF THE NATION KIRAHISIRAHISI...................

NIISHIE HAPO;

Cc: Wadau JF
 
Mmh nisitie neno ila wengine inaezekana kuzikwa wamezikwa kwa uchawi but hawafikii hata robo ya chembe kwa Mzee mi nakubali mzee alikuwa nondo mbona wapo wengi tu wapo kwenye maibada ya kuzimu na bado wanapelea na wengine wamerithisha koo zao mambo ya ajabu ajabu.

Nachohisi mzee aliwakuza watoto kimtindo wa enzi zile hakuwapa exposure tu kituu ambacho hata wazazi wa enzi hizi hawakifanyi kwa watoto wao unaeza kuta baba mfanya biashara mzuri akisepa tuu...biashara zinakufa haziendelei tena sababu hakuweza kupasisha kipaji kwa watoto.

Kwa hiyo concept yakusema mzee amelaanika eti kwakuwa kina nyereye hawapo sikubaliani.

WAPO WATU WENGI MAKOOO YAO YANARITHI USHETANI BADO WANADUNDA HAWAJALAANIKA HATA KIDOGO (kwa macho ya kibinadamu)

Nachofahamu ukoo wa nyerere hautaweza kuendana na ushetani uliopo sasa wizi, ubadhilifu, roho mbaya, ubinafsi ,upigaji dili, uonevu, kauli mbovu, vitisho ule ukoo hauwezi kabisa kuendana na uchafu uliopo sasa.

Ni kweli Mzee kwa level ya urasisi inaezekana alifanya mengi ambayo yalimlazimu kuyafanya akiwa kama kiongozi wa nchi sa zingine kuiumiza nafsi yake kwa kitu kibaya ili mambo yaende wanaoface challenge za uongozi wanaelewa.

Tuache utani kwa busara alizokuwa nazo mzee alijitahidi japo hata kuepusha bendera kutokuwa na marangi mekundu laana za damu ambazo tunaona wenzetu, kutwa rangi za damu kwenye bendera haziwaachi salama , halafu mtu unakuja tu kutamka laana kirahisi............Chunga sana.

Wakati huohuo kuna wabongo leo hii wanatoa kafara za basi yenye watu mia na zaidi ili tu yeye awe tajiri na bado familia inapeta, please tuwe serious mtu usiamke tu na mawazo uliyotoa kwenye astral nightmare.................kama upo kwenye asral experience please rudi uongee vitu vya duniani

Kama ungetaka kuwaona watoto wa nyerere kwenye nafasi kipindi hiki ni kama tu BABA YAO MWLIMU ANGEWARITHISHA MAMBO YA AJABU wangeweza tu, sababu wangekuwa wapigaji, watoa rushwa, wababe, wauza ngada na wakorofi na uhakika kwa tabia hizo wasingekosa nafasi unazotaka wawe.............

Kama ni conspiracy please ipeleke ulaya italipa (sababu wana wivu na weusi wenye akili sana).........hapa bongo utafeli.......

USIMTUKANE FATHER OF THE NATION KIRAHISIRAHISI...................

NIISHIE HAPO;

Cc: Wadau JF
Punguza mahaba,mfano angalia tz ilivyo sasa, huu ni uzao wake yeye na tz itazidi kulaanika kwa sbb yake yeye.
 
Punguza mahaba,mfano angalia tz ilivyo sasa, huu ni uzao wake yeye na tz itazidi kulaanika kwa sbb yake yeye.
uzao ni wanae aliowazaa waliobaki walikuwa katika utendaji kazi na laana inayoendelea ni upuuzwaji kama huu wakati wenzetu huenzi kwa kumaanisha watu waliofanya vizuri katika mabara yao afrika tunamzungumzia vibaya mtu aliyefanya chochote japo kwa kujitahidi na LAANA BADO NDO KWANZA ZINAANZA

AFRIKA WIVU NA UBINAFSI USIO NA SABABU UNATUMALIZA, NJE WANAJUA KUHESHIMU BIDII NA JUHUDI ZA WATU WALIOFANYA MAMBO MAKUBWA, wakituambia sisi tunaustaarabu wa nyani tusikasirike, utaanzaje kumlaani mtu aliyepigania uhuru tena bila damu haingii akiini, badala yake tunapenda kutafuta mapungufu muda wote hata kwenye kile kilichojitahidi kuwa kizuri
Unakuta tunajua kuwaelezea vizuri watawala wa nje kuliko waliowahi kututawala weupe wamejua kunadi vya kwao na kuvikubali kuchukuliana navyo nakuvitangaza kuwa bora kuanzia nchini mwao hadi duniani na afrika tumekubali na zaidi tunadiriki kupaka matope vya kwetu nakutukuza vyao hivi kama ukianza kumwongelea vibaya baba wa taifa ni kitu gani utaongelea vizuri ikiwa tu Bba wa Taifa ndo mwanzilishi wa mifumo ya siasa taratibu za serikali na mambo mengine.

Baadae tunasema tunataka kuendelea kwenda wapi na roho za kizandiki.........
MFANO MZUNGU AKITAKA KUTUAMINISHA NYERERE NI MBAYA tutasadiki sababu hatujawahi kukubali vya kwetu na sasa hivi hata baba wa taifa tunadiriki kumlaani.

Hata Hitler Ujerumani hawamnangi ovyo bado kuna NAFASI wanaitambua kwa namna flani njoo afrika sasa

Ni kama stori ya LIBYA ambayo waliamini Gadaffi Muamar ni mbaya sasa wanafahamu na wanaelewa vizuri nani ni mbaya kikweli kwelii......

Kweli aliyetuloga labda alipatana na Mwenyezi Mungu! hatutakaa tuwe waelewa kamwe
 
Nyerere si alisaidiwa na Jeshi la Mzungu asipinduliwe mwaka 1964?

Mzungu aliamua tu kutupa uhuru kwa hiyari alikuwa anasubiri tu watu wenye akili wakauombe awape
Hakuna mtu anayependa kuona mtu mwingine anafanikiwa ila tuu huwa anashindwa cha kufanya ili akuzuie. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa wakoloni, hawakupenda kutupa uhuru bali migogoro yao wenyewe ndio ilipelekea wakajikuta wamejifunga vitanzi ambavyo hawawezi kutoka
 
Hivi Muhunda bado unaishi ndani ya kile kibabu pale Butiama??

Nchi hii ina malango mengi sana ya Kuzimu, na Mzee ndiye aliyaruhusu kuwepo sababu ya kuamini sana katika ushirikina.
Kuna taarifa kuwa huwenda walimchomoamo mapema tu kabla hata hajafa.

Mengine ni siri ya Taifa.
Ukiwa una ushahidi mwagika basi..
 
Kifimbo mbona MZEE Kenyatta na moi wamekua navyo????kuna watu ni mabingwa wakusema mabaya ya wengine kana kwamba wako wasafiii.uokote tope umponde mwenzako mikono yako itabaki misafi kweli???MZEE jk alikua wakipekeee
 
Kifimbo mbona MZEE Kenyatta na moi wamekua navyo????kuna watu ni mabingwa wakusema mabaya ya wengine kana kwamba wako wasafiii.uokote tope umponde mwenzako mikono yako itabaki misafi kweli???MZEE jk alikua wakipekeee
Kifimbo mbona MZEE Kenyatta na moi wamekua navyo????kuna watu ni mabingwa wakusema mabaya ya wengine kana kwamba wako wasafiii.uokote tope umponde mwenzako mikono yako itabaki misafi kweli???MZEE jk alikua wakipekeee
Hadi Kim Jong kuna picha anatembea na fimbo............kama sijakosea
 
Mambo siyo Shwari kabisa.
Nafsi za watanzania/Watanganyika wengi zinalia na Zina huzuni Sanaa.

Rais wa Nchi huwa anakuwa na uhalali na Taifa na wananchi wake.
kinachofanyika Raia wengi wa Nchi za kiafrika huwa wanauzwa na viongozi wao (Spirituality)

Na ndiyo maana Mambo hayaendi na ikatokea mtu aliyeuzwa akafariki Basi nafsi Yake huwa na uchungu na kisasi kikuu mnoo.

na yule mtu ambaye anauza wenzake akifariki,basi kwa kipimo kile kile atateseka Mara 100.

kuna watu Kama kina Mengi wamechukua vya Watu Sanaa (Spirituality)
Leo hii wakifa wanaonekana wa thamani,machoni pa watu lakini (Spirituality) huwa si kitu na uwa na dhiki kuu!!!
 
Mambo siyo Shwari kabisa.
Nafsi za watanzania/Watanganyika wengi zinalia na Zina huzuni Sanaa.

Rais wa Nchi huwa anakuwa na uhalali na Taifa na wananchi wake.
kinachofanyika Raia wengi wa Nchi za kiafrika huwa wanauzwa na viongozi wao (Spirituality)

Na ndiyo maana Mambo hayaendi na ikatokea mtu aliyeuzwa akafariki Basi nafsi Yake huwa na uchungu na kisasi kikuu mnoo.

na yule mtu ambaye anauza wenzake akifariki,basi kwa kipimo kile kile atateseka Mara 100.

kuna watu Kama kina Mengi wamechukua vya Watu Sanaa (Spirituality)
Leo hii wakifa wanaonekana wa thamani,machoni pa watu lakini (Spirituality) huwa si kitu na uwa na dhiki kuu!!!
Mzee Mengi kachukua/kapora kipi cha watu mkuu ?!

...asked out of curiosity !
 
Back
Top Bottom