Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha, Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.

Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----

Tatizo la Nyaroro ni kwamba mtu mwenye mawazo kama yake ndio anaona yupo makini, lakini mara nyingi ni mchemkaji tu! mada zake zimekuwa zinamwingizia kipato kikubwa kwa wale wanaofikiri kwamba ''kukubaliana naye ndio kuwa mzalndo''
 
du u! nyaronyo mwita kicheere namkumbuka katika ndoto yake ya mh.edward ngoyai lowasa kuanzisha CHAMADE.nilidhani atabaki hko leo utukufu umetoka wapi kwa aliyekunyima ujira kupitia ujumbe wa bunge la katiba mpya.ongeza bidii atakuona
 
Tatizo wajamaa wa lumumba wengi ni vilaza sana,nashindwa kuelewa jinsi gani wamepewa hiyo project B7?yaani fasihi imewapiga chenga?hawa hakika ndio wale wa div 5,kila wachangiapo wao ni matusi tu,Nyaronyo kadhibitisha babo uelewa wa wlio wengi Tanzania ni wa kukariri tu,aya ongezeni matusi na kejeli
 
Nimegundua watu wengi wavivu wa kusoma kama si kutafakari.Mtu anajitoa kujibu hoja kwa kusoma tu heading bila kujua maudhui ya andiko lenyewe!Hii ni kujiaibisha tu!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 

Huyu si alisema Kikwete anamchukia bila ya sababu? Kafuata nini tena huko CCM?


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...cheere-kikwete-ananichukia-bila-sababu-3.html

Nyaronyo-Mwita-Kicheere.jpg

Soma tena na usome taratibu
 
Kichwa cha kuku hakistahamili kilemba.kicheere ni kilemba na maccm kichwa cha kuku.hilo haliwezekani.hapo?
 
Naombeni kupata orodha ya waandishi wanaotoa makala zao kwenye magazeti nchini Tanzania kwa kutumia lugha ya mafumbo kama afanyavyo Kicheere Mwita Nyaronyo.
 
Nimegundua FASIHI ANDISHI inawavuruga sana L7000 Kwa vile wengi wao hukimbilia kukoment hata kama hajasoma na kuelewa mwandishi alikuwa ana amanisha nini.
 

Huyu si alisema Kikwete anamchukia bila ya sababu? Kafuata nini tena huko CCM?


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...cheere-kikwete-ananichukia-bila-sababu-3.html

Nyaronyo-Mwita-Kicheere.jpg

Nyaronyo Kichere anatumia lugha ya picha kupeleka ujumbe kuwa CCM ni chama hovyo, kinalea wezi,wauza meno yatembo na madawa ya kulevya, ndio mana anasema anataka kuhamia huko kwani akiua tembo atasamehewa kama wale majangili 40.
Ukimsoma kwa makini utagundua anatumia lugha kuiponda CCM.
Nimjuavyo Kicherere nafikri atakua ni watu wa mwisho mwisho kutoka CHADEMA kuhamia CCM,
 
saluti kwa Nyaronyo, nyie endeleeni kubishana ila sisi wanafasihi tumemuelewa vizuri
 
Sidhani kama CCM wanaweza kumpokea huyu hata wakipewa bure. Huyu ni mmoja wa waliomwandikia Rais KIMEMO cha kutaka ateuliwe kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba, taarifa zimevuja.

Kumbe wengine huwa mna wa nunua. napita tu.
 
ila yasije yakamkuta kama yule mwandishi mahiri wa miaka ya 90 marehemu Stan Katabaro
 
Nimegundua watu wengi wavivu wa kusoma kama si kutafakari.Mtu anajitoa kujibu hoja kwa kusoma tu heading bila kujua maudhui ya andiko lenyewe!Hii ni kujiaibisha tu!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

Watasoma saa ngapi wakati wao wanalipwa kwa post kuitukana Chadema?
 
Mkuu New Force 2015 kwanza heshima kwako

Huku nyumbani Arusha kuna mitaa inayoitwa Matejoo na Ngarenaro ni hodari sana kwa utengenezaji/uuzaji na unywaji wa pombe hatari aina ya gongo maarufu kwa majina ya piwa au nyeupe.

Kipindi cha kampeni ccm hujinadi majukwani kwa kuwaambia wananchi kuwa "mkiichagua Chadema ndio itakuwa mwisho wa kupika na kuuza piwa maana chadema haijui kuwa hiyo piwa ndio inayotumika kusomesha watoto zao."

Naimani ccm itapokea wanachama wengi sana toka Matejoo na Ngarenaro. Nyaronyo Kicheere njoo toa kadi za ccm huku.
 
Back
Top Bottom