Nyaraka: Mkutano wa CHADEMA na Rais Kikwete - Ikulu ya Dar es Salaam

kitendo cha zanzibar kufanya marekebisho ya katiba yao yanayokwenda kinyume na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Tatizo la Tanzania ni kuwa sheria hazifuatwi. Tumegeuka kama katika hadithi ya George Owell ya Shamba la Wanyama, kila mmoja anabadilisha sheria, ikiwemo katiba, kwa maslahi yake. Tukumbuke masuala ya Muungano yalikuwa 11 tu, ghafla bin vu tunaona yamekuwa mara mbili. Kwa misingi hiyo ya kufuata maslahi, kutofuata sheria na hakuna wa kusema lolote kwani akisema itabidi na yeye aulizwe, Tanzania Bara walimwaga mboga, Tanzania Visiwani wamemwaga ugali.

Kama tungelikuwa makini tangu mwanzo, haikupaswa watu wawili kusaini Muungano bila ya ridhaa ya nchi, kuongeza vifungu vya mambo ya Muungano bila ya ridhaa ya wananchi, na Zanzibar kubadili katiba bila ya ridhaa ya Watanzania wote. Leo hii kila mmoja ana sheria zake kwa maslahi yake, kuanzia balozi wa nyumba kumi hadi "mkku wa kaya". Hivi ndivyo tulivyo na ndivyo tunavyokwenda.
 
Juma Duni Haji alikuwa analijibu swali hilo kupitia ITV usiku huu.

Alimtaja Nyerere kuwa ndiye aliyeifuta Tanganyika na waraka alikuwa nao mkononi anausoma, siukumbuki ni upi.

Uwezo wa watu wengine wa kufikiri ni wa ajabu kabisa. Mtu umepewa akili na uwezo wa kutafakari mambo, ukisema ati Juma Duni Haji kalijibu swali hilo kupitia ITV na eti Nyerere ndio aliifuta Tanganyika, that doesnt take us anywhere. Hilo sio jibu, ni ishara za uwezo hafifu wa mtu kufikiria. Mtu mzima anayeshindwa kujiuliza swali hili kisha akapewa majibu "Nyerere aliifuta" na akaridhika nalo kifikra ni mfu na hana thamani yoyote katika jamii anayoishi.

Kama Tanganyika iliungana na Zanzibar tukaunda nchi ya Tanzania, leo hii kuna nchi ya Zanzibar, swali linalokuja kichwani, Tanganyika iko wapi? Leo hii tunasema tunasherehekea miaka 50 ya uhuru, wa nchi ipi? Uliona wapi watu wakisherehekea birthday ya marehemu? Tanganyika haipo, inakuwaje leo tunaendelea kusherehekea uhuru wake? watanganyika wapo lakini hawana identity, tunataka tuwarudishie identity yao. Swali rahisi tu la kutoa jibu watu wanakimbilia kwa Nyerere, ndio uwezo wetu wa kufikiri ulipofikia kweli?
 
awa jamaa walifanya mlinganyo huu;

t[SUB]1[/SUB]+ z = t

where t[SUB]1[/SUB]= tanganyika
z= zanzibar
t= tanzania

but t[SUB]1[/SUB] ~ t
then the equation becomes t + z = t

hapo ndipo TANGANYIKA yangu ilipo fia duh !!!!!
H

Mkuu umesahau kitu kimoja, assumption of the equation

but t[SUB]1[/SUB] ~ t because t1 >>>>> z
hence;
t1 + z = t
 
I wish ... Tungepata kwa KINA makubaliano Rasmi Kati ya Rais na CDM yaliyofikiwa kutokana na nyaraka hizi!!

Bila ya kuwa na makubaliano ya hoja moja hadi nyingine basi mkutano huu utakuwa hauna maana kwa sababu hakuna chochote kitakachobadilika. Vile vile, maneno tu hayatatusaidia kuijenga Tanzania.
 
Nadhani ukiutazama huo waraka wa magwanda wanashindwa kuelewa kuwa Zanzibar ni nchi, ina Rais wake, ina Katiba yake, ina Bendera yake, ina Wimbo wake wa Taifa. Na hapa ni nchi zimeungana tu, na hata huo waraka uliwekwa wa 1964 ni amendment tu, jee waraka orijino kabla haujawa amended uko wapi?

..haswa mama!

..sasa bila kuyumbisha maneno,, hiyo nchi ya pili iliyoungana na nchi ya Zanzibar inaitwaje na imeenda wapi baada ya muungano mbona nyenzake ipo, Rais wake ni nani, bendera yake ni ipi, wimbo wake wa Taifa ni upi???!!!

..Au hiyo nchi iliyoungana na Zanjibar ndio hii inayoitwa Tanzania bara? Nimesoma historia ya Afrika sijawahi kukutana na nchi inayoitwa Tanzania bara na sijaona nchi iliyobadilisha jina na kuitwa Tanzania bara!! Je baada ya muungano mbona Zanjibar inaendelea kuwepo na hiyo nchi nyingine imepotezwa katika ramani ya dunia?..God damn it!!

We need our IDENTITY,, We need our DIGNITY,, We need our TANGANYIKA back!!!!

..Think Global...Act Local..
 
Mimi nadhani tufike mahala tuwe wakweli tu katika nafsi zetu. MIUNGANO yote duniani sasa hivi ime/inasambaratika. Huu wa kwetu upo kwa nguvu ya dola tu tangu siku nyingi.

Nitatoa mifano michache:

-USSR haipo tangu mwanzoni mwa miaka ya 90.
-Chekoslovakia haipo.
-Yugoslavia haipo.
-Sudan imezaa Sudan ya Kusini na Darfur inakuja.
-Ethiopia imezaa Eritrea na Ogaden inakuja.
- Somalia sasa hivi kuna Somaliland na Puntland.
-Ubelgiji hata kuunda serikali moja ni taabu.

Kosa lilifanyika tangu mwanzo kwenye Muungano wetu huu. Nimewahi kumsikia Mwalimu akisema alichoambiwa na Karume mwaka 1964. Karume alitaka iwe NCHI moja. Mwalimu akamkatalia. Hili likawa doa la kwanza kabisa la Muungano huu. Haliwezi kurekebishika.

Zanzibar sasa ni NCHI kamili ingawa tunajidanganya kuwa ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Siku Maalim Seif akipata nafasi hata ya kukaimu ataitangaza Zanzibar kuwa Jamhuri.

Tatizo limekuwa kubwa zaidi baada ya JK kushindwa kuilinda na kuitetea Katiba ya JMT. Mabadiliko ya hivi karibuni kwenye katiba ya Zanzibar yalipaswa kutangazwa kuwa ni batili. Rais wetu amekaa kimya.

Na unafiki huu utatusumbua sana. Kinachoendelea kufanyika sasa ni kujaribu kuulinda muungano kwa gharama yoyote hata kwa kutumia udikteta kwamba Mwananchi huruhusiwi kuuliza uliza mantiki ya Muundo wa Muungano wenyewe. Swali, je tutaendelea mpaka lini kuwa na Muungano ambao wahusika wenyewe (partners) wana manung'uniko mengi?
 
Tumechoka kukuelimisheni! Kila siku tunakuambieni ili tuweze kujadili haya mambo ya Muungano, basi kwanza itafuteni Tanganyika. Hili hamutaki na sio kwamba hamujuwi ipo wapi hiyo Tanganyika.

Baada ya bakubaliano ya Mw. Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume kukubaliana kuziunganisha nchi mbili hizi, hili suali la ikpo wapi Tanganyika liliwahi kuulizwa na Salim Rashid na Jumbe kama sijakosea. Wawili hawa na wengine kati ya wana Mapinduzi waliliona hii kasoro na walijuwa ina nia mbaya huko mbeleni kama tuavyo hivi sasa. Jibu La Sheikh Abeid ilikuwa "ahaa kama haipo si shauri zao" Hakujuwa kama Mw. Nyerere ni msomi na mjanja mithili ya sungura!!!

Baada ya muungano ule tu, katiba iliy tumika ni hiyo hiyo ya Tanganyika, kilichofanyika baada ya Tanganyika ilibadilishwa na kuwekwa Tanzania na katiba hiyo hiyo ndio iliyowekwa mambo ya Muungano. Siku ya pili yake wafanyakazi wote wa Tanganyika walijulikana kama watumishi wa Jamuhuri ya watu wa Tanzania. Kiti cha umoja wa mtaifa ni hicho hicho cha Tanganyika nicho kilicho tumika kama ndio kiti cha Tanzania UN.

Sisi tunafurahia tunaposikia Watanganyika wanadai nchi yao, lakini hili dharura kusikia. Na kwanini hamuitaki irudi? Munajuwa fika kwamba mukifanikiwa kuimeza Zanzibar, basi ni rahisi Tanganyika kurudi ni kazi ya kubadilisha jina tu na kurudi kwenye jina lake halisa...

Kama nyinyi hamutaki irudi sisi Wa-Zanzibari tutaipigania irudi. Ndio maana tukawa tunampogeza JK Mrisho kwa kukubali kusikiliza kilio chetu. Hawezi kufanya mambo kwa kujiamulia yeye mwenyewe tu, lazima na Mkuu wetu wa nchi atiye baraka zake. Zanzibar ni nchi bwana miaka kenda, kama Juma Duni Mtumwa, basi na iwe hivyo lakini katu hatuto kubali kuburuzwa na tundu, tobo, pipa....
 
Nimeona kwanini walikaa kwa siku mbili ! Na nimegundua kwa nini taarifa kwa vyombo vya habari iliandikwa vile! Kumbe mambo yalikuwa mazito sana, si saizi ya akina Wassira!
 
Acheni ujinga wenu hata kama Muungano Zanzibar waende kivyao na sisi tubaki na Tanzania yetu,mimi sitaki kusikia upuuuzi unaoitwa Tanganyika

wazanzibari waende wapi wakati tanzania ni yao pia? au hujui?. hapa mambo yapo hivi, chao ni chao na chetu ni chao!!! kuwezi kuafanya tanzania iwepo ilihali wazanzibari hawapo. huyu faza foxy anasema kweli. hivi utasemaje zanzibar siyo dola wakati ina bendera, ina raisi, ina jeshi? hata kama hilo jeshi litapewa jina la kipemba, bado ni jeshi. wadanganyika ni watanganyika na si wazanzibari. bali watanzania ni wale yatima wa marehemu tanganyika na wazanzibari
 
Jamani Tanganyika Ipo na kuna baadhi ya sehemu humu Tanzania zinatumia sheria za Tanganyika,cha msingi TIMU YA CHADEMA IMEMWAGA TAARIFA MUHIMU KWA RAIS KUWA WATANZANIA WANATAKA NINI?

Nasubilia kwa hamu kusikia CHADEMA WANASEMAJE NA NINI TAMKO LAO RASMI KULINGANA NA MAZUNGUMZO YAO NA RAIS JAKAYA KIKWETE.

Lakini swala la MUUNGANO NINA HAMU NALO SANA KWA KUWA TUMEFIKA WAKATI WA KUWA NA SERIKALI MOJA,KAMA WAZANZIBAR HAWATAKI WAACHWE,MWALIMU NAE NI BINADAMU SIO MUNGU INGAWA ALIFORESEE TABIA ZA UBAGUZI LAKINI SIO LAZIMA KULAZIMISHA KUISHI NA MTU ANAEKUPA MASHARTI AKIJISIKIA YEYE NDIE ATIMIZIWE UKIJISKIA WEWE HAPANA ATI?


IMEFIKA WAKATI KIZAZI CHA DIGITAL GENERATION [DG] COMPUTER GENERATION Kutokuishi kwa makaratasi na NGUVU YA DOLA tuishi kwa hiari na maelewano.Kwa kuwa wengine tumeikuta TANZANIA na HATUIJUI TANGANYIKA VIZURI JAPO IPO, TUKO TAYARI KUILUDISHA TANGANYIKA KWA UMMA KWA WIKI, MIEZI AU MWAKA WA MPITO WAKATI WA KUUNDA KATIBA. TUILUDISHE KUTOKA KWENYE MAENEO MACHACHE AMBAKO WANAITUMIA NA KUIFANYA ITUMIKE KWA WENGI KISHA MCHAKATO UKIKAMILIKA TUIZIKE RASMI KULUDI KWENYE TANZANIA YETU MPYA TUKIWA NA NCHI YETU MPYA NA TUKIWA HATUNA ZANZIBAR.

TUSIIISHI KWA USANII WA KUWAPENDEZESHA MATAIFA ETI WANATAMANI KUONA MUUNGANO WA TANZANIA KAMA REFERENCE KWAO , WAKATI KIUKWELI KWETU NI MATATIZO HATUELEWANI KILA SIKU MANENO MANENO.MUDA WA KUISHI KWA MAGUVU UMEKWISHA DUNIANI.WAKATI DUNIA INASUMBULIWA NA ASILIA [NATURE] LEO HII SISI BADO TUNANG'ANG'ANIANA KANA KUWA WATANGANYIKA [TANZANIA] PASIPO ZANZIBAR SIO LOLOTE NA SI WATU.

KUPITIA UJIO WA KATIBA MPYA AMBAYO ITAPATIKANA KWA NJIA AMBAYO PIA IMESHAURI NA CHADEMA KAMA RAIS ATAFUATA USHAURI TUINGIE KWENYE MCHAKATO.

NINA HAKIKA KWA ASILIMIA MIA [100%] WAZANZIBAR WANAITAKA ZANZIBAR,TUWAACHIE NCHI YAO,HAKIKA WATATWANGANA HAWA SI MUDA MLEFU NA KWA KUWA WANATUJUA TUNAWAJUA HAWACHELEWI MMOJA MMOJA KULUDI MBIO MBIO.WAKILUDI WAUNGUJA TUNAWAAMBIA WATAKUWA MKOA WA UNGUJA WAKIFUATA WAPEMBA TUNAWAAMBIA KUWA WANAKUJA KUWA MKOA WA PEMBA IMETOKA WANASAINI TUNASONGA NA HAKUNA TENA FYOKO FYOKO ZA KIAARABU.

INAONEKANA KWA WENGI HUMU JAMVINI HAWAJUI KAMA TANGANYIKA IPO NA INAFANYA KAZI KILA SIKU, KWENYE BAADHI YA MASHIRIKA NA OFISI ZA SERIKALI.NI KUAMUA KUPITIA MCHAKATO WA KATIBA MPYA TANGANYIKA ILUDI KWA WANANCHI WOTE RASMI,KISHA KWA KUWA KIZAZI KIPYA [NEW GENERATION] KINAJUA TANZANIA BASI KUPITIA SANDUKU LA KATIBA MPYA WALUDISHIWE TANZANIA YAO ISIYO NA ZANZIBAR.
 
Waungwana nina maswali machache baada ya haya maongezi:

1. Kwa hiyo rais atasaini mswaada uwe sheria?
2. Je akishaisaini kama ilivyo bila kuingiza mapendekezo ya chadema, kutakuwa na nafasi tena ya kuingiza vitu vipya ndani ya sheria ambavyo kwenye mswaada havikuwepo?
3. Je kuna uwezekano (au kisheria inaruhusiwa) kwa rais kubadilisha mswaada na kuingiza mambo ambayo hayakupitishwa na bunge kabla ya kusaini mswaada uwe sheria?

Tukıwa mımı na wewe bado tunajıulıza swalı hılı tayarı Raıs wako keshasıgn Muswada!
Amedharau hoja za CDM pamoja na kumsısıtızıa kuwa suala hılı sı la CDM&CCM balı nı kwa maslah ya Taıfa.
Raıs anamandate ya kukataa muswada wıth reason as to why he declıned the bıll thereafter Bunge lıngeweza kujadılı mapendekezo ya Raıs then kuurudısha tena Muswada kwa Raıs.
Kıukwelı Raıs wetu anachukulıa hılı suala kırahısı rahısı wakatı lınaweza kumcost endapo CDM watasıkıka zaıdı kwa wananchı ambayo ndo Nguvu ya Umma.
 
[h=4]Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Pandu Ameir Kificho, ametaka mchakato wa kuelekea uundwaji wa Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki, kuzingatia ukweli kwamba nchi wanachama zina historia tafauti.[/h]



Katika mahojiano haya na Mohammed Khelef, Spika Kificho, anasema ni jambo la muhimu kwa historia kuchukuwa nafasi yake, na kuzingatia ukweli kuwa nchi wanachama zina maumbile tafauti. Zanzibar ni moja ya nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na ingawa inawakilishwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia Tanzania, kuna mambo mengi ambayo ya Jumuiya ambayo si ya Muungano.
 
Waache wanasiasa waitwe wanasiasa,....
Laiti tungekua tunaishi tukijua tutakufa na baada ya kifo kuna maisha mengine
sehemu mbili tofauti,tungewekeza huko.
 
[h=1][/h]Written by amini // 29/11/2011 // Habari // No comments


MUSIJE MUKAPIGWA CHANGA TU LA MACHO NA KAKA ENI MUKAJAZISWA FORM ZAKUOMBA KAZI BADA YA MAKUBALIANO YENU YAKUIRUDISHA TANGANYIKA?.

[caption id="attachment_34111" align="alignnone" width="245" caption="SISI TUKO PEMBA TUMESHUHULIKA NA KUCHUMA KARAFUU, KWA HIO JK CHADEMA UGOMVI WA NDUGU."] [/caption].
NA NUKUU VIFUNGU VYA KABRACHI LA CHADEMA
.Katika ukusanyaji na uratibu wa maoni ya wananchi juu ya Katiba Mpya na masuala ya muungano wametaka ziundwe tume mbili za katiba, moja itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya kwa ajili ya masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanganyika na ya pili itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya masuala ya Muungano.
Wameeleza tume ya katiba itakayohusu masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanganyika iwe na wajumbe na sekretarieti watakaotoka Tanganyika wakati tume ya katiba itakayohusu masuala ya Muungano iwe na wajumbe na sekretarieti watakaotoka katika pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano kwa msingi wa usawa wa uwakilishi.
Waraka huo umependekeza sheria ibadilishwe ili kuweka utaratibu wa kuanzishwa tena kwa Serikali ya Tanganyika itakayoweza kujadiliana mustakabali wa Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa usawa.
Walitaka serikali mpya ya Tanganyika itakayoundwa ijadiliane upya na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya mambo ya Muungano na muundo wa Muungano wenyewe.
“Sheria ibadilishwe ili kuweka utaratibu wa kuitishwa kwa kura ya maoni juu ya Muungano na muundo wake.”
Hongera Chadema kamba iwe hio hio Kurudisha Tanganyika yenu yenye historia ya wazee wenu waliopigania uhuru wan chi yenu Tanganyika na sio Tanzania kama Dodoma walivyo yapindicha mambo?.Sisi Zanzibar kauli yetu ni ile ile rudisheni Tanganyika tujadiliane upya mambo ya Muungano laa hamutaki hivyo basi Muungano ufe.
Madamu kashalikoroga Kikwete nilazima alinywe au mumnyeshe kwa nguvu Chadema, shikeni uzi huo huo Kikwete anaogopa kushikwa machati na ndugu zake atawatii lolote mutakalo niwenyewe kwa wenyewe huko vita vya ndugu sisi Wazanzibar hatuna haja yakuwaingilia ispokuwa mambo yahusuyo Zanzibar tu.
 
Back
Top Bottom