Halafu mtu ananyanyuka na povu na jasho kumtetea mtu kama huyu. Zitto amejishusha sana na haaminiki tena!! Huwezi kutetea mtu kama huyu unless nawe una maslahi huko. Pengine sasa tunamwelewa Zitto toka wakati ule alipolazimisha lile suala la majenereta TANESCO.
Huyu Mhando hakuwa wa kumfukuza tu bali kumfilisi na kumfunga hadi afie jela yaani kifungo cha maisha. Huwezi kupewa dhamana katika shirika la umma halafu unafanya biashara na mkeo tena ya wizi. Nadhani mlisikia taarifa ya wizi mwingine wa manunuzi ya vile 'vikombe' vya Tanesco inatolewa juzi kwenye TV live. Mzungumzaji alikuwa anawasifu waliotoa taarifa kuwa ni 'whistle blower'.
Kheri mzee mwenye hekima na misimamo kuliko kijana mnafiki na kigeugeu. Zitto agenda yako ya umri sasa tunaona haina mashiko kama haya ndiyo unataka kuyaendekeza. Kama unajifanya hukujua kinachoendelea siku zote huko TANESCO, haya mpaka sasa mbona uko kimya ebu toa comments juu ya nyaraka hizi tusikie! Nadhani sasa umebaki ni jina tu lakini moyo na ubongo si yule tuliyembeba wakati amefukuzwa Bungeni!!
Sio kuwaacha kabisa ila nimejaribu kuangalia katika jicho la kuyatatua haya matatizo kwanza alafu from there tujenge utamaduni wa kuwajibika once mtu anapokosea, nikalinganisha na hiyo ya South Africa though maudhui yanatofautiana ila nimeangalia kwa nchi yetu kuna issue ya watu wanaingia katika uongozi kwa makundi hivyo inakuwa ngumu kumchulia hatua mwana mtandao mwenzao anapofanya kosa (that's why nikasema kuna haja ya kukaa chini na kuelezana ukweli ili huu utamaduni ukome maana mtu anafanya kosa alafu analindwa na kama atalipuliwa anajenga chuki, najua ni ngumu ila nikafananisha na SA kama kuna uwezekano tuje na utaratibu mpya wa kwamba makundi ni kwa ajili ya kuoigiana kampeni lakini isiwe ndio sababu ya ufanye utakacho na kulindwa kisa ulikuwa bega kwa gega katika kuhakikisha mgombea wenu anaingia katika uongozi).......
Kwani 2008 Mhando alikuwa Mkurugenzi wa Tanesco? au hii ya MC Donald Mwakamele inahusiana vipi na nafasi ya Mhando kule Tanesco?. Labda fikra zangu, naona hii ya 2011 inambada kimaadili ila ya 2008 ipo too personal between him and the said MC Donald...wataalamu wanaweza kutujuza zaidi hayo mahusiano yaliingilia vipi Tanesco......
Kuna watu wakishaona jina la Zitto au yeyote wasiyempenda basi huwa hawaangalii context isipokuwa wanachukua kineno wanachohisi kinatimiza haja zao na kuishia hapo. Kama alihitaji uchunguzi ufanyike tatizo liko wapi? Kama leo atakuja na utetezi baada ya ushahidi kuzidi kuonekana hapo ndo kuna issue!!!
Mkuu pole sana kwa kwikwi,Naona ulikuwana unatafuta upenyo wa kutoa chuki,hasira na kikohozi dhidi ya zitto
Umefunguja,japo sioni unazungumzia nini.
HIVI umeambiwa ZITTO ndiye Auditor wa mapato ya TANESCO,Hivi unadhani Zitto ndiye CAG wa Tanzania?
Utetezi wa zitto dhidi ya huyo Mhando ulikuwa katika kipengele kipi?Au unatabia ya Ku-generalize mambo kama under 18?
Zitto na kilichoandikwa hapo kwenye DOCUMENTS kunauhusiano gani?
Labda yawezekana hujasoma document hiyo imeandikwa nini,ila tu kiu cha kutapika majungu kilikufika ghafla ukaamua kuelekea kwenye kukoment bila kusoma.Rudi tena kasome inahusu nini,Sio kukimbilia kumtaja Zitto kwenye madudu yako
..........Kuna kila dalili kuwa imeibuka vita ya wazi kati ya Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), huku Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco aliyesimamishwa kazi, William Mhando, akipigiwa debe la wazi na wabunge.
Taarifa zilizopatikana kwenye ofisi za Bunge zinasema kuwa Kamati ya Nishati na Madini inajipanga kukwamisha bajeti ya wizara hiyo kama Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco aliyesimamishwa kazi, Injinia Mhando, hatarejeshwa kazini huku wizara ikisisitiza kuwa amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi wala hajafukuzwa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, naye ana msimamo kuwa Mhando ameonewa na wizara inaweza kujiokoa kwa kumrejesha ofisini kisha ufanywe uchunguzi maalumu utakaoendeshwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG)............
CHANZO>>Vita kubwa TANESCO
Naelewa J K nia yako njema ya kuweka mambo sawa pia naikubali tunapopishana ni jinsi kushughulikia madudu yaliyopo na hasa hili donda ndugu la kulindana na kugawana rasilimali zetu. inabidi hili litufikirishe.