View attachment 509507 Kwa mara nyingine jana nimeshuhudia maajabu mengine ya wanasiasa kutaka kupiga kiki za nguvu mahali pasipo takiwa. Kulikuwa na sababu gani kuandaa meza na hotuba wakati wa kuwaaga wagonjwa waliokuwa wanahitaji dharula kama mlivyo tuambia awali?
Hivi waliokuwa wanahutubiwa hapo ni hao watoto au waliokuwepo hapo au taifa kwa ujumla?
Hivi ilikuwa sahihi kuwalaza wagonjwa hapo hadhara ili mtoe hotuba zenu? Kwa nini wagonjwa hawakuingizwa kwanza kwenye ndege ili muendelee na hizo hotuba zenu,au mliogopa ndege itaondoka kabla hamjamaliza kukiki?
Najua mtakasilika lakini huu ndio ukweli najiuliza mengi lakini naachia hapo, ni hayo tu waheshimiwa!!!