Nyalandu acha siasa katika misiba

Nyalandu acha siasa katika misiba

You need to know Nyalandu ni mwenyekiti wa lile shirika hapa Tanzania na hata kabla ya wazungu wale kwenda ngorongoro wakakutana na ajal walkua wametoka Singida kukagua miradi wanayofadhili na walkua na Nyalandu kW wiki nzima sasa sjui shida yako we we mwenye post ni nin? Kuona Nyalandu akiratibu hiyo support au? Tuache ujinga wakati mwingine.Fanya na we we tuone ili tujifunze kwako
yaani umesema ukweli mkuu. Matatizo hutokea hapa nchini ila hili la watoto liligusa watu wengi mno jamani. Tofauti na kagera ambapo vifo havikuzidi kiasi hiki. Nyalandu kafanya kazi kubwa sana tangu mwanzo. Tunahitaji kubadilika kidogo humu ndani. Sio mkisifiwa na lowasa kwamba mnafanya kazi nzuri kwenye mitandao ndo mnakurupukia kila kitu alimradi kimefanywa na mwana CCM. Ndio maana huwa sijifichi wakati mwingine kumsifu mkt wa chadema bwana MBOWE kwa Aina ya siasa za kistaarabu na unyenyekevu ambao huwa anauonesha pale anapojenga hoja.
 
Kama ilivyo Ada y'a Wageni wanaotoka nchi Za magharibi walimalizia shughuli zao iliyowaleta hapa nchini Uwa wanatumia muda wao kutalii hao wazungu wa Samaritan pulse walipomaliza shughuli yao jimboni Kwa Nyalandu walipata muda wa kwenda kuangalia Mali Asili yetu Ndiyo siku hiyo walikuwa wanarudiarusha tayari kwa Safari ya kurudi Us tuache majungu kwenye maisha ya watu Kuweni na moyo wa huruma kWA wenzenu nyie ukoo wa wanywa mbege migombani
Hebu tueleze ni connection gani Nyalandu kaifanya ili kusaidia hao watoto kwenda kutibiwa US?
 
Nimekuona na nimekushangaa ukiwa busy Arusha unazengea zengea kama nzi karibu na bucha, unatafuta nini Arusha? Hivi huu msiba ni wa Taifa ama kuna masrahi ya watu hapa?

Hata kama una mashirika yako lakini kufikia hatua ya kumwambia mkuu wa mkoa eti pesa itàkayochangwa ihusike kujenga hospitali, si jambo baya lakini mbona haya sikuyaona ukiyasema kule Kagera kwenye tetemeko? Lwakatare alisimama akaomba misaada ya kisaikolojia kwa baadhi ya wahanga ila sijawahi kuisikia hata sauti yako moja. Ama kwako Tz ni hapo Arusha tu? Achia mbali kuzungumza, sikuwahi kukushuudia ukizengea kule hata kwenda kusema pole tu ila leo uko busy Arusha. Watanzania ubaguzi wetu, chuki na roho za kwanini tusipoangalia vitatupeleka pabaya, ubaguzi ni mkubwa sana. Na hawa wanaojiita viongozi wa siasa ndo wako mstari wa mbele kushadadia.

Nyarandu, siku ikitokea kwingine kama ilivyoyokea Arusha usiache kwenda kutoa msaada kwani kusaidia eneo unalotoka tu ukawaacha wengine wasiokuwa na wa kuwasaidia si sawa, unaleta tafsiri mbaya sana
Hujuwi kama Nyalandu na Marekani ni chanda na Pete ?
 
Kwanza hiyo kazi imefanywa na wale wazungu watatu na hilo shirika ndio limewasafirisha.

Nyalandu anatajwa kusaidia tu kuishawishi serikali kutoa passport lakini kazi kubwa imefanywa na wale wazungu watatu ambao ndio waliwatoa wale watoto kutoka kwenye lile gari lililopata ajali(wreckage) na kisha kuanza mipango ya kuwahamishia US kwa matibabu zaidi.

Sio maneno yangu haya na kwa ushahidi fungua hii link hapa chini:

Iowan missionaries help to save 3 kids in Tanzania bus crash

Yeye tunaweza kumshukuru kwa kuwa kiungo tu kati ya serikali na wasamaria hawa.
Ningependa kufahamishwa"amesaidia kupatikana kwa passport,, kivipi? Kwani yeye ni waziri wa mambo ya ndani?
 
You need to know Nyalandu ni mwenyekiti wa lile shirika hapa Tanzania na hata kabla ya wazungu wale kwenda ngorongoro wakakutana na ajal walkua wametoka Singida kukagua miradi wanayofadhili na walkua na Nyalandu kW wiki nzima sasa sjui shida yako we we mwenye post ni nin? Kuona Nyalandu akiratibu hiyo support au? Tuache ujinga wakati mwingine.Fanya na we we tuone ili tujifunze kwako
Vitoto vya Chadema vina wivu wa ajabu, sijui linataka nini katika Taifa ili
 
Watanzania baadhi Yetu hatuna moyo wa huruma Naaamini kwa MTU mwenye utu ameona na kudhamini kazi ya mh Nyalandu .Kaka yangu Nyalandu usisikilize wajinga na wapumbavu kazi uliyoifanya ni kubwa mno na ya kuiga .Mungu atakulipa kwa mema yote uliyoyafanya. Thanks. A lot brother........
 
Kagera hapakuwa na Wazungu,
Mzungu hata akienda India kwa wabaguzi wa Rangi namba moja duniani atapewa heshima tele na tena atakabidhiwa na mke kabisaaa..!
kwa hiyo usishangae ya nyalandu kujikomba kwa hao Wazungu.....
 
Lengo ni watoto watibiwe, acheni kutafuta sifa za kipuuzi.
Haswaa, watu waache sifa/chuki za kipuuzi. Na usinichanganye na wapuuzi kabla sijakurudi na wewe.
Nina post kibao kuhusu hii ajali kazisome kabla ya kuanza kutoa post za kishabiki za jumla jumla.
Sasa wewe inakuuma nini kuwa Nyalandu kasaidia hao watoto kupata matibabu?
Yaani chuki yote na gubu ni sababu ni Nyalandu baasi...
Kuna watu watoto hawa kupata msaada na kutibiwa imewauma sana wakati wao hawana msaada wowote waliotoa.
Waacheni watoto watibiwe na tuliofiwa tuomboleze kwa amani.
Huu ujinga wenu hatuutaki.
 
Back
Top Bottom