Nyalandu acha siasa katika misiba

Nyalandu acha siasa katika misiba

Utakufa kwa kihoro kisa wivu.

Vipi mbona hukuhoji juu ya yule Mbwiga aliyelilia kuongea msibani kwa hoja ya wapiga kura wake ila msiba wa juzi hajaenda kuizika ile family iliyopoteza watu watano kisa hakukuwa na vyonbo vya habari vikirusha matangazo live.

Nachojua Nyarandu anapewa headlines kwenye hii issue ya watoto baada ya shirika la Samaritan ambalo yeye ni mwenyekiti wake hapa Tanzania kuamua kutoa msaada wa matibabu kwa hao watoto.

Hao wazungu waliotoa msaada siku ya ajali ambao wewe unawaona wa maana Sana yeye ndiye mwenyeji wao na ndiye aliratibu hata hiyo safari ya wao kwenda huko Ngorongoro.
 
Mkuu nimerusha maandishi yanayoonyesha kuwa Nyalandu ndiye aliyeunganisha hili dili kwa kuwaweka pamoja Samia na hao madaktari, Samia alipopewa ombi hilo la kutoa kibali akasema aongee na Jpm kwanza na hao madktari wa nje nao wakaomba wawasiliane na nchi yao kwanza, so aliyeleta wazo la watoto kupelekwa nje na kuwezesha hilo ni Nyalandu

thanks
 
Huyu Nyarandu ni mjinga kama wajinga wengine. Anatafuta sifa za kijinga baada ya Rais wake kumchunjia baharini. Kabaki kutapatapa tu.
Nyalandu anaweza kuwa mjinga kama mimi na wewe tu, lakini mtu akifanya jema moja katika mabaya mengi, si tusifie hata jema hilo?
(Tuseme hivi: japo ni mjinga lakini kafanya vema kuwa kiungo kwa watoto kutibiwa nje ya nchi)
Jamani mtu afanye jema gani ili akidhi kusifiwa?
SOMA HAPA
1da7ef3368af80d051a7b9263fba3412.jpg
 
Hiyo tiktak ya jana kuwa kuwa fedha imebadilishiwa matumizi bila kuwauliza wadai mmeona ee. Mimi naona tu, kuwadanganya watanzania wa leo na teknolojia hii ni ngumu sawa na kazi ya kuchimba mawe baharini.ni hayo tu waheshimiwa.
 
Jamaa alitaka Lema ndiye atoe msaada kwenye hii issue kisa ndiye mbunge wa Arusha.

Connections pekee anazoziweza Lema Ni za kuratibu waendesha Bodaboda na wanywa viroba washiriki maandamano.

Hao watoto angepiga nao picha Tu na kuwaacha hapo hapo Mount Meru hospital.
 
Nimekuona na nimekushangaa ukiwa busy Arusha unazengea zengea kama nzi karibu na bucha, unatafuta nini Arusha? Hivi huu msiba ni wa Taifa ama kuna masrahi ya watu hapa?

Hata kama una mashirika yako lakini kufikia hatua ya kumwambia mkuu wa mkoa eti pesa itàkayochangwa ihusike kujenga hospitali, si jambo baya lakini mbona haya sikuyaona ukiyasema kule Kagera kwenye tetemeko? Lwakatare alisimama akaomba misaada ya kisaikolojia kwa baadhi ya wahanga ila sijawahi kuisikia hata sauti yako moja. Ama kwako Tz ni hapo Arusha tu? Achia mbali kuzungumza, sikuwahi kukushuudia ukizengea kule hata kwenda kusema pole tu ila leo uko busy Arusha. Watanzania ubaguzi wetu, chuki na roho za kwanini tusipoangalia vitatupeleka pabaya, ubaguzi ni mkubwa sana. Na hawa wanaojiita viongozi wa siasa ndo wako mstari wa mbele kushadadia.

Nyarandu, siku ikitokea kwingine kama ilivyoyokea Arusha usiache kwenda kutoa msaada kwani kusaidia eneo unalotoka tu ukawaacha wengine wasiokuwa na wa kuwasaidia si sawa, unaleta tafsiri mbaya sana

Roho mbaya tuuu hii
 
Yaani watu watoe pesa za pole kwa wafiwa halafu wakajengee hospitali! Hivi ccm hakuna waliobaki na akili kabisa?
 
Unaposema kuwa hao wazungu walikuwa wanatoka jimboni kwa Nyarandu kuja ARUSHA ili kurudi US.
Ebu tuwambie kuwa ilikuwaje wapite Rotia wakati njia ya kutoka Jimbo la Nyarandu ni Minjingu via Makuyuni?

Siku ya Kuwaaga marehemu pale Stadium Arusha, wale wazungu watatu walitangaza wazi kuwa kama hali za majeruhi zitaendelea kuwa mbaya, wao wapo tayari kuwasafirisha kwenda US kwa matibabu na watagharamia gharama zote.
Ebu tueleze Nyalandu aliwatafuta hao wazungu lini.

Tuache kiki kwenye misiba
Yawezekena kweli ni rafiki zake lkn hakuna ushawishi wowote alio ufanya Nyalandu kwa wale watu. Kilicho wasukuma wafadhili wale kutoa msaada ni hali halisi waliyo iona siku ya ajali. Baba yule saivi imekua kama yeye ndo karatibu kila kitu.
 
Nina shida sana na Nyarandu. Aliwahi kualikwa kwenye mahafali ya chuo kikuu kimoja Mwanza akaahidi hadharani kutoa milioni 100 kuanzisha mfuko wa staff development katika chuo hicho. Cha kushangaza hata senti hakutoa.
 
20170515_111106-COLLAGE.jpg
Kwa mara nyingine jana nimeshuhudia maajabu mengine ya wanasiasa kutaka kupiga kiki za nguvu mahali pasipo takiwa. Kulikuwa na sababu gani kuandaa meza na hotuba wakati wa kuwaaga wagonjwa waliokuwa wanahitaji dharula kama mlivyo tuambia awali?
Hivi waliokuwa wanahutubiwa hapo ni hao watoto au waliokuwepo hapo au taifa kwa ujumla?
Hivi ilikuwa sahihi kuwalaza wagonjwa hapo hadhara ili mtoe hotuba zenu? Kwa nini wagonjwa hawakuingizwa kwanza kwenye ndege ili muendelee na hizo hotuba zenu,au mliogopa ndege itaondoka kabla hamjamaliza kukiki?
Najua mtakasilika lakini huu ndio ukweli najiuliza mengi lakini naachia hapo, ni hayo tu waheshimiwa!!!
 
Umeshanyonya? Nakubali kuwa wewe ni hasara ya Taifa. Unaleta hoja za kipuuzi jukwaani.

Cheti feki huyu anataabu sana.
 
Hawana kitu, ndo lililobaki saivi, wanataka waonekane kua ni watu wenye utu.. Kumbe wanafki tu.
 
Hata mimi nilishangaa sana!.Watu wame elimika sana sasa hivi,wasifikiri kuzindua,kuhutubia na mbwembwe nyinginezo zisizo na tija ndio zitawapaisha,no!.
 
Umeshanyonya? Nakubali kuwa wewe ni hasara ya Taifa. Unaleta hoja za kipuuzi jukwaani.

Cheti feki huyu anataabu sana.
kwenye utabibu kuna kitu kinaitwa privacy ya mgonjwa hiyo kanuni ikizingatiwa? Ndio maana nasema kuna maswali mengi yanapaswa kujibiwa.
 
Hata walewafadhili watakuwa walisikitishwa sana na huu upuuzi, ugonjwa ule unahitaji matibabu ya haraka, sasa kuwaanika pale na kuhutubia sijui ili iweje?! Kuna kiki lakini hii ni upuuzi ulio pitiliza, hivi ingekuwa pale kuna watoto wao wa kuwazaa wangewachelewesha ili watoe hotuba?!
 
Back
Top Bottom