Nukuu za mwalimu Nyerere

Nukuu za mwalimu Nyerere

Ustaadh

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2009
Posts
413
Reaction score
19
Mwalimu Nyerere amekuwa ananukuliwa kwa misemo yake ambayo wakati mwingine imekuwa vigumu kuielewa. Mojawapo ni ifuatayo hapa chini. Kwa wenye uelewa mkubwa, hapa Mwl. Nyerere alimaanisha nini?

Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni" - Mwl. J. K. Nyerere
 
Alikuwa anazungumzia ufisadi, kwamba mafisadi hawawezi kupelekana mbele ya haki.
Tunashuhudia ukweli wake leo.
 
Nothing profound or special, just stating the obvious.
 
Mwalimu Nyerere amekuwa ananukuliwa kwa misemo yake ambayo wakati mwingine imekuwa vigumu kuielewa. Mojawapo ni ifuatayo hapa chini. Kwa wenye uelewa mkubwa, hapa Mwl. Nyerere alimaanisha nini?

Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni" - Mwl. J. K. Nyerere
Ustadh,
Vipi umeshindwa kumbaini Ustadh Mwenzio; Ustadh J K Nyerere alituwekea wazi picha rasmi ya hisia za Watanzania juu yake yeye (Nyerere)Kama PAKA Mkubwa na wale wanaomzunguka kiuongozi ni Paka wadogo walioko Chini yake. Na Watanzania mliobaki ni PANYA mnaochukia na mliochoshwa na Chama Chake Serekali yake Sera zake Utendaji na Utekelezaji wake. Na DAWA ni hiyo Afungwe Kengele.
Lakini yukowapi wa kazi hiyo. Unakumbuka wale MGAMBO mpaka Mvunguni na wana Nguvu za Utendaji kuliko Polisi.Na Paka Wadogo waliridhishwa anaeharibu hapa anahamishiwa pale kwa hiyo Paka Mkuu was always OK.
 
Ni Eleven Years After, tangu Mwl atutoke. Wanajamvi hebu yeyote anayekumbuka nukuu yoyote alioitoa Mwalimu katika hotuba zake aiweke hapa jamvini.


Mojawapo ni hii: '' Mtu aliyejiandikisha kupiga kura, halafu siku ya Uchaguzi haendi kupiga kura, Huyo ni Mpumbavu'' JK Nyerere
 
Dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, sawa na kula nyama ya mtu,dhambi ya ubaguzi haiishi inaendelea tu,
leo utabagua kwa kusema sisi ni wanzanzibari hawa ni watanganyika ,
kesho utasema sisi ni wanzanzibari hawa ni wanzanzibara.
Lazima utaendelea utaona kuna mpemba na muunguja.......:.............utaendelea tu haiishi sawa na kula nyama ya mtu
 
"Ukiona mtu anakwambia jambo la kipumbavu na yeye mwenyewe anajua kuwa unajua ni la kipumbavu..ukilikubali ujue amekudharau"...J.K. Nyerere.
 
" Wakati wa utawala wa awamu ya kwanza si kwamba rushwa haikuwepo, ilikuwepo lakini tulikuwa wakali sana.. Ikithibitika mahakamani kuwa mtu ametoa au kupokea rushwa hatukumuachia hakimu nafasi ya kutoa hukumu peke yake. Tukasema atakwenda ndani kwa miaka miwili na viboko 24....kumi na viwili siku anaingia kumi na viwili siku anatoka akamuonyeshe na mkewe" JK Nyerere!
 
..mnaingia karne ya 21 mmepanda basi la ukabila,mnaona sifa kuulizana makabila......mnataka kutambika?
 
Siku chama kilipokuwa kinamuaga mzee Kawawa (alipostaafu rasmi siasa za majukwaani), katika hotuba ya shukrani alisema, pamoja na mambo mengine: ‘Naahidi nitakufa nikiwa mwanachama mwaminifu wa CCM.'

Ilipofika zamu ya Mwalimu Nyerere kuzungumza, akasema: ‘Rashid una roho ngumu. Utakufa mwanachama mwaminifu wa CCM? Mimi siwezi kuyasema haya. CCM inaweza kubadilika. Siku ikiacha misingi, nami naachana nayo, kwa sababu CCM si mama yangu. Ninaye mama mmoja na siwezi kupata mwingine...'
 
akuna vyama vya upinani vyenye uwezo wa kuingoa ccm madarakani upinzani wa kweli utatoka ccm wenyewe kwa wenyewe wtatofautiana kisha waanzisha chama chao
 
Nyerere alikuwa mu-wazi sana na hata ikafikia akaongelea kuhusu CCM kuwa hicho chama kwa sasa kina '‘kansa ya Uongozi ambapo isipotibiwa itakiua chama kizima" na akathubutu hata kusema anatamani kuona chama kingine cha upinzani kitakachoweza kukiondoa madarakani,ila akasema hadi sasa bado hajaona chama kingine na kwa hiyo pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama chochote ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM.
Wosia wa Baba wa Taifa.

Ole wako Tanzania ;
Tusipoisaidia!
Niwezalo Nimefanya,
kushauri na kuonya,

Nimeonya Tahadhali,
Nimetoa ushauri,
Nimeshatoka kitini,
Zaidi nifanye nini?

Namlilia Jalia
Atumlikie njia
Tanzania ailinde
waovu wasiivunje

Nasi tumsaidie
Yote tusiya mwachie
Amina tena Amina
Amina Tena na Tena.
:dance:
 
Mwalimu nyerere hakuwa malaika lkn anastaili kuitwa mwenye heri,aliona mbali alikuwa na maono, kauli ya mwalimu nyerere kuwa maendeleo ni watu na sio vitu ki ukweli kwa sasa imeanz kujitokeza na kuonekana kwenye jamii yetu, tuna maendeleo ya vitu tena vingi sana lkn njaa maradhi na umaskini umeongezeka kwa kasi sana na ukitaka kujua hilo fanya utafiti vijijini zamani watu walikuwa na mifugo,walilima kahawa pamba na kadhalika.

Viwanda vilikuwepo ajira zilikuwa nje nje huduma za maji zilikuwepo za kutosha na kwa bei nafuu sana lkn kwa sasa ni shida tupu.
Maendeleo yaliyopo sasa hivi ni vitu tu barabara magorofa tv na kadhalika lkn maisha ya kawaida ya mtanzani yamekuwa shubiri hayashikiki kabisa
 
1- watanzania wakikosa kuyaona maendeleo ndani ya CCM watayafuata nje ya CCM.
2-CCM itauliwa na wanaccm wenyewe.
3-Kiongoz bora atatoka ndani ya CCM.
4-Wapinzani wa kweli watatoka ndani ya CCM.
Swali
1- inamaana watanzani wameyakosa maendeleo ndani CCM?
2-Ndo CCM inauliwa na wenyewe kama ilivyotabiriwa?
3-Ndani ya upinzani hakuna kiongoz aliebora hadi lowasa kutoka CCM na kwenda kupewa rungu ya kupeperusha bendera ya ukawa/chadema?
5- Lowasa ndo mpinzni wa kweli? Au zile kauli za mwalimu zilikuwa na maana gani na pia tunazihusisha vipi na haya yanayojiri kipindi hiki ndani ya nchi yetu?
Hebu twende sawa wanajamii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom