1. "Rais aliomba akafie nyumbani kwake, maana alisema hawezi kupona.
2. Alishangaa nilipomwambia sina mamlaka ya kuruhusu hilo.
3. Aliomba aitiwe Paroko wake, Pd Makubi na Kard. Pengo ambao walifika na kumpa upako wa wagonjwa!
4. Alikata roho mbele yetu wakuu wote watatu wa vyombo vya usalama.
5. Makamu wa rais, Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi hawakuwepo Dar. Tukaamua kuwaita Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi ambao walifika na kuwapa taarifa ya msiba.
6. Ilibidi tutumie njia nyingine kumjulisha makamu wa rais ambaye ndiye alitakiwa kutangaza taarifa ya msiba.
7. Kulikuwa na mjadala kipi kianze kati ya mazishi na kumwapisha makamu wa rais kuwa rais.
8. Wengi walishauri yafanyike mazishi kwanza, lakini nilishauri uapisho uanze kwanza, kwa sababu marais wa nchi nyingine walitakiwa wapokelewe na rais wa nchi.
9. Lilikuja suala la gwaride la uapisho ambapo walishauri kusiwe na gwaride. NILIWAKATALIWA kwa sababu aliyekuwa anaapishwa ni amiri jeshi mkuu,na lazima bendera ya amiri jeshi mkuu ipandishwe kwa gwaride. Kinyume na hilo, jeshi LISINGEMTAMBUA kama amiri jeshi mkuu.
10. Kulikuwa na baadhi ya mawazo, kwamba inakuwaje juu ya makamu wa rais kushika nafasi ya urais. Nadhani walisahau kuwa katiba ya nchi inasema nini, ikiwa rais aliye madarakani anafariki au akishindwa kuongoza. Nami nilisema ni vema utaratibu huo ukafuatwa na ni jambo jema.
INASIKITISHA KWA KWELI. hata hivyo, ndugu zangu, tujiandae kwa vitu viwili au vitatu, hata wale watu wa hali za kawaida na wa hali za chini. cha kwanza, jiandae nini utaachia watoto wako utakapokufa ghafla (ukifikiria hili utakuwa pia na nidhamu ya kuishi, acha dhambi usife mapema), pili, jiandae kufa katika Bwana, ni bora ufe katika Kristo kuliko kufa ukiwa na dhambi (bila kuokoka), mwisho ambalo linafanana na la pili, andaa moyo wako, kwamba ikiwa hautakufa hadi Yesu arudi basi usiachwe.
kuna kitu kingine, achana na imani potofu, imani ambayo hata mitume hawakuwa nayo, unapokuwa mgonjwa, kuita padre (ambaye hata hajaokoka ila ni mshika dini) ati akupake mafuta. mafuta hayasafishi dhambi, unatakiwa kutubu dhambi zako ili usamehewe, kafara la Damu ya Yesu Kristo ndilo linafuta dhambi, sio mafuta yaliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu, Yesu hakufa bure, hakuna mbadala wake. Biblia inasema aziungamaye dhambi zake atasamehewa ila yule anayezificha hatafanikiwa. padre naye ana dhambi zake, akupake mafuta wewe usamehewe dhambi au akupeleke mbinguni si angeyaoga kabisa yeye ili aende mbinguni kulivyo kuzuri? mbona tumekuwa vipofu?
Mwisho, kesheni basi kwa maana hamjui siku wala saa. unaweza kuwa rais, waziri, kiongozi wa dini, askofu n.k, utakuwa personally accountable kwa Mungu, hivyo ni jukumu lako kutengeneza moyo wako na Mungu kibinafsi ukiwa hapa duniani, baada ya kifo ni hukumu hakuna kuombewa na padre ili maiti isamehewe dhambi, never.