Nukuu 10 za Jenerali Mabeyo

Nukuu 10 za Jenerali Mabeyo

Katiba inavunjwa kila mara na kuleta madhara makubwa kwa nchi..watu wasiofaa kuwa viongozi wanakuwa viongozi kupitia uchaguzi haramu unaovunja katiba ya nchi kwa kupata viongozi wasiostahili kuwa viongozi.

Unapotokea nafas ya kiti cha urais ni nafasi pia ya kujisahihisha inawezekana hao walitaka kuvunja katiba wakati huo wa msiba wangeleta nafuu na kurekebisha makosa yaliyofanyika na pengine hali ingekuwa njema kuliko ilivyo sasa..ukisoma jinsi Mungu alimuweka Mfalme Daudi badala ya Mfalme Sauli si kwa njia inahojenga amani..

Lakini angalia baada ya Mfalme Daud kushika madaraka mambo yalibadilika kuwa mazuri zaidi ya wakati wa Mfalme Sauli..sisi ndio tunasema katiba ilitaka kuvunjwa na si Mungu alipanga nini baada ya Rais aliyekuwepo kufariki...!
 
1. "Rais aliomba akafie nyumbani kwake, maana alisema hawezi kupona.
2. Alishangaa nilipomwambia sina mamlaka ya kuruhusu hilo.
3. Aliomba aitiwe Paroko wake, Pd Makubi na Kard. Pengo ambao walifika na kumpa upako wa wagonjwa!
4. Alikata roho mbele yetu wakuu wote watatu wa vyombo vya usalama.
5. Makamu wa rais, Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi hawakuwepo Dar. Tukaamua kuwaita Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi ambao walifika na kuwapa taarifa ya msiba.
6. Ilibidi tutumie njia nyingine kumjulisha makamu wa rais ambaye ndiye alitakiwa kutangaza taarifa ya msiba.
7. Kulikuwa na mjadala kipi kianze kati ya mazishi na kumwapisha makamu wa rais kuwa rais.
8. Wengi walishauri yafanyike mazishi kwanza, lakini nilishauri uapisho uanze kwanza, kwa sababu marais wa nchi nyingine walitakiwa wapokelewe na rais wa nchi.
9. Lilikuja suala la gwaride la uapisho ambapo walishauri kusiwe na gwaride. NILIWAKATALIWA kwa sababu aliyekuwa anaapishwa ni amiri jeshi mkuu,na lazima bendera ya amiri jeshi mkuu ipandishwe kwa gwaride. Kinyume na hilo, jeshi LISINGEMTAMBUA kama amiri jeshi mkuu.
10. Kulikuwa na baadhi ya mawazo, kwamba inakuwaje juu ya makamu wa rais kushika nafasi ya urais. Nadhani walisahau kuwa katiba ya nchi inasema nini, ikiwa rais aliye madarakani anafariki au akishindwa kuongoza. Nami nilisema ni vema utaratibu huo ukafuatwa na ni jambo jema.

..badala ya paroko na kadinali wangeitwa Lissu, Mdude, Mo Dewji, Ney wa Mitego, ili atubu makosa yake, wamsamehe, na kumuombea pumziko la amani.
 
Mzee Yese angeweza kupinga wazo la Mzee Samweli la kumwita Daudi kutoka machungani kuhudhuria gwaride la utambuzi kumpata mrithi wa Sauli kwa kuweka mbele VIGEZO VYA KIBINADAMU..umri, uzoefu wa vita, umbo nk ambavyo kwa sasa ndio hiyo katiba mnayosema ilitaka kuvunjwa..

Nadhani wangekubali katiba ivunjwe kama ambavyo vigezo vya Mzee Yese na wenzake walivyokubali vikawekwa kando na hatimaye Daudi akapatikana kuwa mfalme mrithi wa Sauli! Tunahitaji katiba mpya ili itupe pia Baraza la ushauri la Taifa..Presidential National Advisory Council litakalofanya kazi kama ya Samweli..mambo ya uongozi wa nchi hayawezi kuamuliwa na sifa au utaratibu wa kibinadamu siku zote..kuna nyakati kunahitajika vitu vingine zaidi ya katiba!

Na katiba si msahafu au Biblia inaweza badilishwa au kuvunjwa kuruhusu jambo jema kutokea! Angalia mambo yanayotokea Haiti kwa sasa..na katiba ipo, wamefikaje hapo..!
 
..badala ya paroko na kadinali wangeitwa Lissu, Mdude, Mo Dewji, Ney wa Mitego, ili atubu makosa yake, wamsamehe, na kumuombea pumziko la amani.
jina kubwa ila ulichoandika sasa...[emoji23]
aliyekwambia hao ndio wanatoa msamaha nani? paroko wake alimaliza kazi
 
1. "Rais aliomba akafie nyumbani kwake, maana alisema hawezi kupona.
2. Alishangaa nilipomwambia sina mamlaka ya kuruhusu hilo.
3. Aliomba aitiwe Paroko wake, Pd Makubi na Kard. Pengo ambao walifika na kumpa upako wa wagonjwa!
4. Alikata roho mbele yetu wakuu wote watatu wa vyombo vya usalama.
5. Makamu wa rais, Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi hawakuwepo Dar. Tukaamua kuwaita Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi ambao walifika na kuwapa taarifa ya msiba.
6. Ilibidi tutumie njia nyingine kumjulisha makamu wa rais ambaye ndiye alitakiwa kutangaza taarifa ya msiba.
7. Kulikuwa na mjadala kipi kianze kati ya mazishi na kumwapisha makamu wa rais kuwa rais.
8. Wengi walishauri yafanyike mazishi kwanza, lakini nilishauri uapisho uanze kwanza, kwa sababu marais wa nchi nyingine walitakiwa wapokelewe na rais wa nchi.
9. Lilikuja suala la gwaride la uapisho ambapo walishauri kusiwe na gwaride. NILIWAKATALIWA kwa sababu aliyekuwa anaapishwa ni amiri jeshi mkuu,na lazima bendera ya amiri jeshi mkuu ipandishwe kwa gwaride. Kinyume na hilo, jeshi LISINGEMTAMBUA kama amiri jeshi mkuu.
10. Kulikuwa na baadhi ya mawazo, kwamba inakuwaje juu ya makamu wa rais kushika nafasi ya urais. Nadhani walisahau kuwa katiba ya nchi inasema nini, ikiwa rais aliye madarakani anafariki au akishindwa kuongoza. Nami nilisema ni vema utaratibu huo ukafuatwa na ni jambo jema.
Duh
 
basi kama sio ushkaji wa ngosha na mabeyo uliomfanya amlinde popote... na kama asingekua dar wakati mzee anakata moto, basi wahuni wangepiga tukio zito tungejionea kasheshe....
mi kama ,mabeyo ndio aliyelazimisha mambo yaende yalivyoenda
power... huyo order moja tu jeshi lipo mtaani mwisho kutembea saa 12 jioni
 
Jenerali kaongea machache kati ya Mengi.

Bashiru Ali ana uhusika wake mkubwa tu baada ya dikteta kufariki.

Pia Bashiru Ali ndio alikuwa mtu wa kwanza kutenguliwa na Mama Abduli baada ya Mama Abduli kushika usukani hivyo Bashiru Ali anabaki kuwa SG aliyehudumu muda mfupi kwenye historia yetu (mwezi 1) kisha akapewa ubunge wa kuteuliwa katika zile slot 10.

Watanzania walivyo wasahaulifu hawajawahi kugundua michoro ya huyu mtu hadi kutenguliwa kwake maana ndio alimpangia Mama Abduli ziara Tanga makusudi ili watimize lengo lao.
 
Namba 6 mmmmh

Binafsi nadhani mihimili yote ilitakiwa iwe inapewa taarifa ya kila kinachoendelea
Watu wa karibu kabisa na rais tena karibu sana ni vyombo vya ulinzi na usalama na wala sio hiyo mihimili mingine, mkilijua hilo wala hamtakuwa na tatizom, huu mjadala wengi wenu umewazidi sana kiufahamu ila basi kwa sababu ya ujuaji mwingi.
 
10. Kulikuwa na baadhi ya mawazo, kwamba inakuwaje juu ya makamu wa rais kushika nafasi ya urais. Nadhani walisahau kuwa katiba ya nchi inasema nini, ikiwa rais aliye madarakani anafariki au akishindwa kuongoza. Nami nilisema ni vema utaratibu huo ukafuatwa na ni jambo jema.

Oooh...kumbe zile tetesi ilikuwa ni kweli
 
Back
Top Bottom