Nivea
JF-Expert Member
- May 21, 2012
- 7,459
- 4,748
WAO WANAWAKOPESHA Matajiri wasiojua kurudisha wanategemea nini?tena hovyo hovyo tu wacha wafilisike ilmradi watu wachii wapate hela zao za hifadhi,MAGAMBA YAKISHAINGIA MAHALI NDIO FINAL REPORT HIZO SIKU ZOTE.ALAFU WATAWABANA WATU WENGINE WACHINI NAKUWAACHA WADENI WAO WAKUBWA.Wanajamvi heshima mbele,
NSSF imeanza zoezi la kuwabembeleza/kulazimisha wateja wake wakubwa [waajiri] kutoa mchango yao ya kila mwezi kabla ya wakati.Ni kawaida waajiri kupeleka michango ya kila mwezi mmoja nyuma[mfano mshahara wa mwezi tano michango yake inatakiwa ipelekwe mwezi sita],sasa NSSF inawataka waajiri wakubwa [waajiri wenye idadi kubwa ya wafanyakazi] kupeleka michango ya wafanyakazi mwezi mmoja mbele au mwezi huu wa sita ili kukabiliana na hali mbaya ya fedha inayoliandama shirika hilo la wafanyakazi nchini.
Taarifa toka chanzo cha uhakika ndani ya shirika hilo zinadai serekali imechota fedha toka NSSF kwaajili ya kugharamia mishahara ya watumishi wake baada ya chanzo chake muhimu cha mapato TRA kushindwa kupata fedha za kutosha kulipa mishahara ya watumishi wa serekali pamoja na shughuli nyingine muhimu.
Zipo taarifa za uhakika serekali ina mkakati wa kuwalazimisha wanachama wote wa NSSF na mashirika mengine ya hifadhi ya jamii kutokulipwa mafao yao hadi wafikishe umri wa kustaafu.Mkakati utasaidia kukabilia na upungufu mkubwa wa fedha unaotarajiwa kutokea kwakuwa fedha zinazochotwa na serekali hazitarajiwi kurejeshwa.
Source:Ngongo@Arusha.