NSSF tunataka majibu ya tuhuma kuhusu 'udini'

NSSF tunataka majibu ya tuhuma kuhusu 'udini'

Status
Not open for further replies.
Uongo mwingine hauna kichwa wala miguu.

Kwa kuwa Dau ni Muislaam, basi staff wote wa NSSF ni Waislaam?

Hiyo ni Islamophobia.

Waambie waambie!wameanza kisa DAU ni muislamu.
 
Kuna Kazi zilitolewa July za operation officers mpaka leo hawajaita watu....hii inakaaje?

Lazima watu waamini hizo tuhuma.

"Mi huwa nasema ni rahisi sana kwa mtu aliyeajiliwa anayelipwa vizuri kumpuuza mtafuta ajira"

Kwahiyo unamaanisha hizo kazi za operations officers wamepewa waislam kinyemela?
 
umeshawahi kutembelea branch mbali mbali za NSSF?kama bado nenda halafu utakuja na jibu Mimi mdogo wangu aliambiwa na mtoto Dada yake Dau kwamba angekuwa muislamu angempeleka moja kwa moja kwa dau apate kazi ila am not blaming maana kuna institution kibao wanajazana wakurya, wachaga hata kwenye benki za kikristo eg mkombozi maendeleo na efatha huezi kukuta muislamu

Huoni huyo mdogo wako hana vigezo vya kushindana kwenye soko la ajira ndio maana akawa anatafuta njia ya mkato kwa kuonana na dau? ...nikikwambia kuwa dadaake dau alimwambia kigezo cha yeye kuwa muislam kama njia ya kujivua kwenye udalali wa kumtafutia kazi baada ya kuona ndugu yako ni mtupu kichwani utanikatalia? ......tuwe tunafikiri kabla ya kuandika
 
Hizi ni stress za kukaa kijiweni mda mrefu bila ajira, enyi ndugu zangu kumbukeni sana kauli ya mmasai Lowasa, Ajira kwa vijana ni Bomu linalosubiri kulipuka, acheni hizo habari za udini, binafsi nimeshatuma maombi sehemu mbali mbali kama wadau wengine, kuna sehemu niliitwa kwa interview na zingine sijaitwa ikiwepo hiyo ya Operations officer pia nipo huo upande unaodaiwa unapendelewa pale NSSF, kikubwa ninachokiheshimu ni ule ujumbe wa mwisho ambao hata UTUMISHI wanaweka kene Tangazo lao kuwa 'Only shortlisted Candidates can be contacted for interview' Nilishafanya kazi taasisi moja tena hiyo ni full islamic kuanzia jina lake mpaka mmliki wake iko mbezi beach pale lakini cha kufurahisha wakristo wapo wanapiga mzigo kama kawa na wengine wanaendelea na swala zao kama kawa, ila ni ngumu taasisi kama Efatha bank kukuta muslim anafanya kazi pale, tupunguze jazba ajira bongo ni kwereeeee.....!!!
 
Mzushi wewe mchonganishi....wewe unaongelea udini NSSF na mwenzako au wewe yuleyule unaongelea udini LAPF;TRA;GPSA;TPA sijui tukueleweje. Kama una idhibati kuwa watu wameajiriwa kwa udini hebu ulete lakini usitake kutuvurugia watendaji waadilifu wanaoendesha mashirika kwa mafanikio makubwa....Nikuulize swali...Crecencius Magori na John Msemo ni waislamu???
Wadau,
Kama tunavyofahamu Tanzania ni nchi isiyoongozwa kwa misingi ya dini fulani japokuwa wanaoutuongoza wana dini. Kwangu mimi naona ni jambo jema endapo hatutaangalia dini zetu ili tupate au kutoa huduma mbalimbali za kijamii. Ni hivi majuzi mfuko wa jamii ya watanzania wote NSSF imetangaza nafasi lukuki za kazi lakini zimo tuhuma ambazo zinatolewa na watu wanaodai ni wafanyakazi na wenginesio wafanyakazi kuwa NSSF kuna udini eti kama hauna 'sigda' haupati kazi au kama wewe si Abubakari au Hamisi haupati kazi. Tuhuma hizi ni mbaya na kubwa kwa mfuko unaoitwa wa jamii. Eti ili wakuajiri si kwamba umefaulu interview bali kwa majina na dini yako. Ni jambo linalohitaji ufafanuzi na ushahidi wa kutosha aidha kukubali au kukataa kuwa kuna udini au hakuna maana litaleta mpasuko kwa taifa. Moto wa dini ni rahisi kuuanzisha na kuuchochea lakini ni ngumu kuumaliza. Kesho tutaskia na PPF kuna 'UDINI' Keshokutwa tutaskia mahakamani kuna udini na mwisho itakuwa ni jeshi na ikulu kuna udini huku mamlaka zikiwa kimya.
 
Wadau,
Kama tunavyofahamu Tanzania ni nchi isiyoongozwa kwa misingi ya dini fulani japokuwa wanaoutuongoza wana dini. Kwangu mimi naona ni jambo jema endapo hatutaangalia dini zetu ili tupate au kutoa huduma mbalimbali za kijamii. Ni hivi majuzi mfuko wa jamii ya watanzania wote NSSF imetangaza nafasi lukuki za kazi lakini zimo tuhuma ambazo zinatolewa na watu wanaodai ni wafanyakazi na wenginesio wafanyakazi kuwa NSSF kuna udini eti kama hauna 'sigda' haupati kazi au kama wewe si Abubakari au Hamisi haupati kazi. Tuhuma hizi ni mbaya na kubwa kwa mfuko unaoitwa wa jamii. Eti ili wakuajiri si kwamba umefaulu interview bali kwa majina na dini yako. Ni jambo linalohitaji ufafanuzi na ushahidi wa kutosha aidha kukubali au kukataa kuwa kuna udini au hakuna maana litaleta mpasuko kwa taifa. Moto wa dini ni rahisi kuuanzisha na kuuchochea lakini ni ngumu kuumaliza. Kesho tutaskia na PPF kuna 'UDINI' Keshokutwa tutaskia mahakamani kuna udini na mwisho itakuwa ni jeshi na ikulu kuna udini huku mamlaka zikiwa kimya.

Hizi shutuma sidhani kama ni za kweli, kuthibitisha hili kuwa si kweli ingia www.nssf.org.tz then About us, Management, Management team, hapo majina ya viongozi wote yapo then utachambua lipi ni la upande wako na lipi siyo, but sure iko kitu sidhani kama ni kweli.
 
NSSF
1. Mkurugenzi Mkuu. Ramadhani Dau. Muislamu
2. Mkurugenzi wa Fedha. Ludovic Mrosso. Mkristo
3. Mkurugenzi wa shughuli. Cresentius Magori. Mkristo
4. Mkurugenzi wa Kompyuta. I. Halfani. Muislamu
5. Mkurugenzi wa Utumishi. Bi Chiku Matessa. Muislamu
6. Mkurugenzi wa uwekezaji. Yacoub Kidula. Muislamu
7. Mkurugenzi wa Ndani. Pauline Mtunda. Mkristo
8. Meneja wa uhusiano. Bi Eunice chiume. Mkristo
9. Mkuu wa usalama. Ramadhani Nasibu. Muislamu
10. Meneja kitengo maalum. Davis Senkoro. Mkristo
11. Mkuu wa Idara ya Sheria. Chedrick Komba. Mkristo
12. Mkuu wa Tathmini ya Mfuko. Sadi Shemliwa. Muislamu
 
NSSF
1. Mkurugenzi Mkuu. Ramadhani Dau. Muislamu
2. Mkurugenzi wa Fedha. Ludovic Mrosso. Mkristo
3. Mkurugenzi wa shughuli. Cresentius Magori. Mkristo
4. Mkurugenzi wa Kompyuta. I. Halfani. Muislamu
5. Mkurugenzi wa Utumishi. Bi Chiku Matessa. Muislamu
6. Mkurugenzi wa uwekezaji. Yacoub Kidula. Muislamu
7. Mkurugenzi wa Ndani. Pauline Mtunda. Mkristo
8. Meneja wa uhusiano. Bi Eunice chiume. Mkristo
9. Mkuu wa usalama. Ramadhani Nasibu. Muislamu
10. Meneja kitengo maalum. Davis Senkoro. Mkristo
11. Mkuu wa Idara ya Sheria. Chedrick Komba. Mkristo
12. Mkuu wa Tathmini ya Mfuko. Sadi Shemliwa. Muislamu



N:B
Mkitaka niwawekee na Mifupo mingine ya Hifadhi ya jamii tulinganishe muone jinsi Wagalatia wanavyowabania vijana wa kiislamu.

Umejibu vizuri sana ndugu... Na umeonesha kujibu hoja kwa mifano na ushahidi. Sio watu kukurupuka na kuanza kukejeli bila ufafanuzi. Ndiyo hayo ambayo mleta mada alipaswa kujibiwa.
 
Uongo mwingine hauna kichwa wala miguu.

Kwa kuwa Dau ni Muislaam, basi staff wote wa NSSF ni Waislaam?

Hiyo ni Islamophobia.

Kuna kijana wetu ana sifa, ameshafanya application kwa kazi zilizotangazwa wiki iliyopita(deadline ya 15 Dec 2014)

Tutaleta data hapa muda ukifika.
 
Hapa bongo hakuna udini. Ila wakristo wapo wengi kwenye maeneo mbali mbali
 
Tunasikia huu ni mwongozo wa mkurugenzi mkuu ndio maana mifuko hii inasuasua tu
 
Suluhisho hapo nafikiri ni kwa nafasi zote hata za mashirika kupelekwa sekretariati ya ajira ili kuondoa migogoro hiyo. Ila watu wa aina fulani kuwa wengi haimaanishi kwamba wanaajiriwa kiupendeleo. Mi nafikiri ni imani tu imejengeka na pengine hata mtu mmoja tu aliwahi fanya hivyo basi inachukuliwa kama ndio sera ya hilo shirika.
 
PPF

1. Mkurugenzi Mkuu Bw. William Erio Mkristo
2. Mkurugenzi wa Operations Bi. Maina Mallya Mkristo
3. Mkurugenzi wa Sheria Bi. Vupe Ligate Mkristo
4. Mkurugenzi wa Fedha Bw. Martin Mmari Mkristo
5. Mkurugenzi wa Uwekezaji Bw. Steven Alfred Mkristo
6. Mkurugenzi wa Kompyuta Bi Carina Wangwe Mkristo
7. Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani Hosea Kashimba Mkristo
8. Mkurugenzi wa Utumishi Julius Mganga mkriisto
 
we ni zuzu na TRA, TANAPA nako sio mashirika ya umma?

Zuzu huwa anajibiwa na zuzu, kilichotakiwa kutolewa majibu ni tuhuma za kuwepo kwa udini katika mfuko wa nssf kwakuwa ni taasisi ya umma. Mtu akitoa mfano wa crdb na si taasisi ya umma sio sahihi. Na tuhuma zinaweza kuwa kweli au si kweli ni ufafanuzi tu wenye unatakiwa wala si kejeli. Naona umeshaanza kugundua zuzu ni nani hapo.
 
Kuna kijana wetu ana sifa, ameshafanya application kwa kazi zilizotangazwa wiki iliyopita(deadline ya 15 Dec 2014)

Tutaleta data hapa muda ukifika.

Anza kwa kutuletea data za majina ya wafanyakazi wa NSSF waliopo sasa hivi, yanini kuandikia mate na wino upo?
 
Hivi katika ajira unaangalia dini au qualification ya mtu? Acheni ujinga wa kujadili mambo ya udini hayana tija yoyote.
 
Suluhisho hapo nafikiri ni kwa nafasi zote hata za mashirika kupelekwa sekretariati ya ajira ili kuondoa migogoro hiyo. Ila watu wa aina fulani kuwa wengi haimaanishi kwamba wanaajiriwa kiupendeleo. Mi nafikiri ni imani tu imejengeka na pengine hata mtu mmoja tu aliwahi fanya hivyo basi inachukuliwa kama ndio sera ya hilo shirika.

Well said mkuu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom