Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Taarifa kwa vyombo vya habari: Kujibu taarifa zilizotolewa kwenye gazeti siku ya Jumapili, tarehe 21 Juni 2009
Mara, Juni 23 2009 Uongozi wa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara unapenda kukanusha vikali shutuma zilizotolewa na gazeti la Mtanzania la Juni 21 2009, likidai kwamba watu 21 na zaidi ya ngombe 200 kutoka Kata ya Kibasuka, wilaya ya Tarime wamekufa kutokana na kunywa maji yenye Kiwango Kidogo cha Uasidi kwenye Maji ya Mto Tigithe. Taarifa hiyo iliyoandikwa na mwandishi wake Bw Christopher Gamaina ikimnukuu kwa kirefu Diwani wa Kata ya Kibasuka na kuvumisha kuwa vifo hivyo vimesababishwa na uvujaji wa maji kutoka Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.
Tunapenda kusema kwamba malalamko haya si ya kweli na ni batili. Taarifa hiyo haikufanyiwa uchunguzi, ina malengo mabaya, na siyo ya msingi kabisa; jambo ambalo limethibitishwa na mamlaka zinazohusika.
Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania inapenda kutoa ufafanuzi kama ifuatavyo;
- Mnamo Juni 15 2009 Mgodi wa Dhahabu wa North Mara ilipokea nakala ya barua ya malalamiko kutoka kwa Diwani wa Kata ya Kibasuka iliyotumwa kwa ofisi ya Waziri Mkuu.
- Barua hiyo ilidai kwamba watu 18 na zaidi ya ngombe 200 kutoka kata ya Kibasuka wilaya ya Tarime wamekufa kutokana na kunywa maji yenye kiwango kidogo cha uasidi ya mto Tigithe .
- Mara baada ya kupata taarifa hizo mgodi wa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara uliwasiliana na mamlaka husika ili kuzihimiza kufanya uchunguzi.
- Mnamo tarehe 21 Juni 2009, timu ya uchunguzi iliundwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime kuchunguza malalamiko hayo.
- Timu hiyo iliyowajumuisha Afisa Afya Mkuu wa Wilaya, Afisa Maendeleo ya Kilimo na Mifugo wa Wilaya, Mkuu wa Polisi wa Wilaya pamoja na Afisa Afya wa Mkoa walitembelea vijiji vilivyotajwa kwenye barua hiyo ambavyo ni pamoja na kituo cha afya cha Nyarwana, ambacho kwa mujibu wa barua hiyo kilikuwa na taarifa muhimu za kuthibitisha shutuma hizo. Timu hiyo ya uchunguzi iliongea na mkuu wa kituo hicho na kuchunguza kumbukumbu za matibabu ambapo zote zilishindwa kuthibitisha shutuma hizo.
- Zaidi ya hayo wakati Diwani wa Kata ya Kibasuka alipokutana na timu hiyo ya uchunguzi, alishindwa kuthibitisha vifo vya watu hao 21 aliowaripoti. Pia alishindwa kuandaa mkutano na wafugaji wa ngombe 200 aliodai wamekufa na vilevile alishindwa kuonyesha mizoga yao. Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pia ilitoa taarifa kwamba Diwani huyo wa Kata baadae alidai kwamba vyombo hivyo vya habari vilimnukuu vibaya.
Mgodi wa Dhahabu wa North Mara inakusudia kufungua rasmi malalamiko kwa Baraza la Habari Tanzania na kuchukua hatua zozote muhimu ili kuepusha shutuma zisizo na ukweli zinazokusudia kuchafua heshima yake na kusababisha msuguano na jamii inayouzunguka.
Kuhusu Shirika la Dhahabu la Barrick
Shirika la Dhahabu la Barrick ni kampuni ya uchimbaji madini inayoongoza ulimwenguni. Hisa za Barrick zimeorodheshwa katika soko la hisa la huko Toronto na New York.
Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania inaendesha migodi minne nchini Tanzania. Ambayo ni Bulyanhulu, North Mara, Tulawaka na Buzwagi.
Imetolewa na:
Teweli Kyara Teweli
Uhusiano na Mawasiliano
Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania,
Kitalu 1736, Br. Hamza Aziz,
S.L.P 1081, Dar es Salaam
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
NB:
Kwanini Barrick?
Kwanini uchunguzi wa mambo ya namna hii usiwe na SOP yake inayofuatwa nchi nzima badala ya kila tukio kutafutiwa njia yake ya kuchunguza?
Kwanini tume ya Haki za Binadamu isipewe jukumu la kuchunguza tuhuma za aina hii au kitengo fulani chini ya Jeshi la Polisi na taasisi za haki?
Last edited by a moderator: