Nokia is back, Nokia 6 yazinduliwa China

Nokia is back, Nokia 6 yazinduliwa China

Ni simu ya kawaida tu, itabewa na RAM + Camera, ndo maana ni bei rahisi.
 
Dolby Atmos ndo nini Mkuu!?
Dolby Atmos ni audio decoding format ambayo imetolewa na Dolby Digital Laboratories, kampuni inayojihusisha na sound engineering. Ili kuelewa vizuri Dolby Atmos nitaanzia nyuma zaidi.
Dolby Digital Laboratories walianza na Dolby stereo ambayo ilihitaji spika 2 kimsingi kwa kuwa stereo ni 2 channel audio ila katika kumbi za sinema zilitumika spika 4 kwa kusambaza hizo 2 channels katika spika 4. Lengo ni kuhakikisha mziki unasambaa katika ukumbi mzima. Nyumbani spika 2 zilitosha. Mziki katika stereo ulikuwa mzuri zaidi ukilinganisha na ule wa spika moja yaani 1 channel audio (monaural au mono).
Kisha Dolby Laboratories walifanya maendeleo ya kitekinolojia na kuibuka na Dolby Digital Surround Sound decoding format. Hii format ilikuja na multichannel audio yaani channels zaidi ya 2. Na hii ikahusisha kuwepo spika maalum ya low frequency sounds ijulikanayo kama subwoofer. Kwa hiyo multichannel audio kimsingi inakuwa katika 5:1 channels. Wakati mwingine 2:1 au hata 7:1 channels. Hiyo namba ya kwanza inawakilisha idadi ya spika za kawaida na hiyo 1 ni subwoofer.
Kuna tofauti gani kati ya Dolby stereo na Dolby Digital Surround?
2. Mfano unaposikiliza mziki kwenye Dolby stereo system spika zote 4 zinatoa sauti zote kwenye mziki mfano sauti za gitaa,drums,trumpets ,saxaphone,organ na sauti za waimbaji. Kila spika inatoa sauti zote kwenye mziki kwa hiyo lengo la kuweka spika 2 au 4 ni kueneza mziki kwenye ukumbi ili usikike vizuri sehemu zote.
Sasa inapokuja upande wa Dolby Digital Surround sauti za muziki zinagawanywa katika mikondo (channels) mbali mbali na kila spika inapokea audio channel maalum na sio zote. Kwa mfano subwoofer ni kwa ajili ya low frequency sounds mfano bass sounds au mingurumo ya sauti nzito. Spika zingine zina handle sauti zingine za mziki au sauti za waimbaji. Kwa hiyo katika surround sound unaweza kusikia sauti ya trumpet au mwimbaji kwenye spika moja tu kati ya spika 6 au 8. Au kama kuna waimbaji 2 wanaimba kwa kupokezana/kujibizana unaweza kusikia sauti ya mwimbaji mmoja kwenye spika A na anayemjibu sauti inatokea spika B. Unaweza kuona hapa kuwa Digital Surround sound inavyoufanya mziki kuwa halisia zaidi yaani unajihisi kama vile uko kwenye live event na sio mziki uliorekodiwa tu. Ndio maana spika lazima ziwe nyingi katika Surround Sound ukifananisha na Stereo Sound. Kwa hiyo hawa Dolby Digital Technologies wameubadilisha(revolutionalized) mziki uliyorekodiwa kwa teknolojia yao ya Digital Surround sound.
Sasa je Dolby Atmos ndio nini?
Ukielewa Dolby Digital Surround ni rahisi kuelewa Dolby Atmos kwa sababu Dolby Atmos ni maboresho ya Dolby Digital Surround (=advanced Digital Surround).
Kama tulivyoona Dolby digital surround ina mikondo mingi ya sauti (multichannel audio) na spika zinapangwa mbele katikati na nyuma katika ukumbi na zinazunguka kote ukumbini ili kueneza sauti vizuri na kuongeza live experience. Standard channels ni hadi 8 (7:1).
Lakini unapokuja kwenye Dolby Atmos audio channels zimeongezeka sana kwa sababu licha ya spika za chini pia kuna za juu zinazofungwa kwenye dari. Sababu ya kuweka spika juu ni kushughulika na sauti ambazo kwa kawaida (naturally) hutokea juu kama mgurumo wa ndege, radi, nk. Kwa hiyo Dolby Atmos inaongezea uhalisia ( live experience) kwenye sauti unazosikiliza.
Sasa kuna tofauti gani kati ya Dolby Digital Surround na Dolby Atmos? Ili uelewe fikiria uko katika jumba la sinema unaangalia movie. Mbele yako kuna ndege inakuja. Kwenye Digital Surround utasikia mgurumo ukitokea kwenye spika za mbele, baada ya muda ndege inaposogea zaidi na kupita juu yako mgurumo unahamia spika za nyuma. Unakuwa kama uko kwenye tukio lenyewe.
Lakini kwenye Atmos utasikia mgurumo kwenye spika za mbele, jinsi ndege inavyosogea sauti inahamia spika za juu mbele, baadaye juu katikati kisha juu nyuma na hatimaye nyuma chini. Kwa hiyo utafuatatilia huo mgurumo hatua kwa hatua hadi ndege itakapopotea. Si utajiona kama uko nje na ni ndege halisi? Kwa kweli Dolby Atmos imeongeza sana uhalisia( live experience)
Sasa je kama Atmos inahitaji spika nyingi inawezekanaje kupata live experience kwenye spika 2 tu mfano headphones za simu, iPod, nk?
Tekinolojia ya Dolby inawezesha spika mbili kupata Surround sound na hata Atmos kwani utasikia sauti zikitoka direction tofauti tofauti mfano, mbele, nyuma,juu,kulia na.kushoto lakini sio kwa ufanisi kama vile unavyotumia spika nyingi.
Nimeeleza kifupi lakini natumaini umeelewa.
 
Guys simu imeingia sokoni na review zimeanza kutoka

Camera review vs one plus 3t


chief asante sana kwa hii video nahisi wale watu ambao hawaijui mwaka huu watakubali kuwa nokia ni king wa camera na design

hii Nokia 6 inabishana na iphone 6 na samsung S7 kwenye camera
 
Ni simu ya kawaida tu, itabewa na RAM + Camera, ndo maana ni bei rahisi.
mkuu nahisi umeanza kutumia smartphone miaka hii 3 iliyopita,nokia sio simu tu anafanya bali ni vitu vingi anatengeneza ebu google neno "withings" utakubali vitu anavyodeal navyo nokia
 
chief asante sana kwa hii video nahisi wale watu ambao hawaijui mwaka huu watakubali kuwa nokia ni king wa camera na design

hii Nokia 6 inabishana na iphone 6 na samsung S7 kwenye camera
Mhh.. S7 tena? wakati inazidiana kidogo sana na One plus 3 ambayo camera yake yenyewe haifiki nusu ya HTC 10, Xperia X, LG G5 na iPhone 7 sembuse Galaxy s7 na baba yao Pixel Xl (Smartphone Camera king 2016).

Tusubiri high end flagship yao itoke ndio tuongee sasa hivi ni mapema sana kusema the king is back. Nokia (jina) kumshida HTC, LG, Pixel na Sony itakuwa ngumu sana sembuse Samsung (mwenye R&D budget sawa na Gdp ya Nchi nyingi) mwenye sales projection za S8 at 60Million units
 
wale wa flagship utakuja WAHEED SUDAY kuna leaks za flagship ya Nokia hapa



seems kulikuwa na nokia 8 ces kwenye banda la qualcomm kuna jamaa amechukua video

-5.7 quad hd
-super amoled display
-24mp camera yenye OIS na EIS (optical image stabilization na electrical image stabilization) angalia video kuona isivyoathirika na mtikisiko
-nokia logo inayowaka (vita vya matunda vitaanza)
-speaker mbili za mbele
-64 na 128gb storage na 4gb na 6gb ram pamoja na sd card hadi 256gb
-snapdragon 835 au 821

samsung atapata shida mno mwaka huu hasa kwa upande wa camera kwa nokia atasumbuka acha tusubiri february kwenye maonesho ya innovation pale Barcelona
 
The true legend is back apple samsung sony htc lg pixel zote tupa kule
Naanza kujichanga saiv mpk ifke uku lazma nifate box
 
Mhh.. S7 tena? wakati inazidiana kidogo sana na One plus 3 ambayo camera yake yenyewe haifiki nusu ya HTC 10, Xperia X, LG G5 na iPhone 7 sembuse Galaxy s7 na baba yao Pixel Xl (Smartphone Camera king 2016).

Tusubiri high end flagship yao itoke ndio tuongee sasa hivi ni mapema sana kusema the king is back. Nokia (jina) kumshida HTC, LG, Pixel na Sony itakuwa ngumu sana sembuse Samsung (mwenye R&D budget sawa na Gdp ya Nchi nyingi) mwenye sales projection za S8 at 60Million units
hivi hizi pixels manufacturing wake ni nani mkuu maana camera zao ni hatari
 
oooohhhhh yeaaaah, Legend is back. Nadhani sasa hivi kwa huu mkwara, Samsung na mwenzake Apple wanaumiza kichwa namna ya kukabiliana na huyu mtu mzima. Maana hii kitu ya camera kutotoa picha yenye mitetemo si ya mchezo. Plus i am sure bei itakuwa chini ya bei ya Samsung na Apple.
 
around 540,000 ila ni simu ya china tu, simu zetu zitatoka tarehe 26 mwezi wa pili, nafkiri midcom wataendelea kuwa reseller wetu hapa bongo

ila kama unaitaka unaweza inunua online
Duuuh bora kununua online maana zikifika tz bei inaweza kupanda sana. ...Product za Nokia ziko poa sana. ..
 
Dolby Atmos ni audio decoding format ambayo imetolewa na Dolby Digital Laboratories, kampuni inayojihusisha na sound engineering. Ili kuelewa vizuri Dolby Atmos nitaanzia nyuma zaidi.
Dolby Digital Laboratories walianza na Dolby stereo ambayo ilihitaji spika 2 kimsingi kwa kuwa stereo ni 2 channel audio ila katika kumbi za sinema zilitumika spika 4 kwa kusambaza hizo 2 channels katika spika 4. Lengo ni kuhakikisha mziki unasambaa katika ukumbi mzima. Nyumbani spika 2 zilitosha. Mziki katika stereo ulikuwa mzuri zaidi ukilinganisha na ule wa spika moja yaani 1 channel audio (monaural au mono).
Kisha Dolby Laboratories walifanya maendeleo ya kitekinolojia na kuibuka na Dolby Digital Surround Sound decoding format. Hii format ilikuja na multichannel audio yaani channels zaidi ya 2. Na hii ikahusisha kuwepo spika maalum ya low frequency sounds ijulikanayo kama subwoofer. Kwa hiyo multichannel audio kimsingi inakuwa katika 5:1 channels. Wakati mwingine 2:1 au hata 7:1 channels. Hiyo namba ya kwanza inawakilisha idadi ya spika za kawaida na hiyo 1 ni subwoofer.
Kuna tofauti gani kati ya Dolby stereo na Dolby Digital Surround?
2. Mfano unaposikiliza mziki kwenye Dolby stereo system spika zote 4 zinatoa sauti zote kwenye mziki mfano sauti za gitaa,drums,trumpets ,saxaphone,organ na sauti za waimbaji. Kila spika inatoa sauti zote kwenye mziki kwa hiyo lengo la kuweka spika 2 au 4 ni kueneza mziki kwenye ukumbi ili usikike vizuri sehemu zote.
Sasa inapokuja upande wa Dolby Digital Surround sauti za muziki zinagawanywa katika mikondo (channels) mbali mbali na kila spika inapokea audio channel maalum na sio zote. Kwa mfano subwoofer ni kwa ajili ya low frequency sounds mfano bass sounds au mingurumo ya sauti nzito. Spika zingine zina handle sauti zingine za mziki au sauti za waimbaji. Kwa hiyo katika surround sound unaweza kusikia sauti ya trumpet au mwimbaji kwenye spika moja tu kati ya spika 6 au 8. Au kama kuna waimbaji 2 wanaimba kwa kupokezana/kujibizana unaweza kusikia sauti ya mwimbaji mmoja kwenye spika A na anayemjibu sauti inatokea spika B. Unaweza kuona hapa kuwa Digital Surround sound inavyoufanya mziki kuwa halisia zaidi yaani unajihisi kama vile uko kwenye live event na sio mziki uliorekodiwa tu. Ndio maana spika lazima ziwe nyingi katika Surround Sound ukifananisha na Stereo Sound. Kwa hiyo hawa Dolby Digital Technologies wameubadilisha(revolutionalized) mziki uliyorekodiwa kwa teknolojia yao ya Digital Surround sound.
Sasa je Dolby Atmos ndio nini?
Ukielewa Dolby Digital Surround ni rahisi kuelewa Dolby Atmos kwa sababu Dolby Atmos ni maboresho ya Dolby Digital Surround (=advanced Digital Surround).
Kama tulivyoona Dolby digital surround ina mikondo mingi ya sauti (multichannel audio) na spika zinapangwa mbele katikati na nyuma katika ukumbi na zinazunguka kote ukumbini ili kueneza sauti vizuri na kuongeza live experience. Standard channels ni hadi 8 (7:1).
Lakini unapokuja kwenye Dolby Atmos audio channels zimeongezeka sana kwa sababu licha ya spika za chini pia kuna za juu zinazofungwa kwenye dari. Sababu ya kuweka spika juu ni kushughulika na sauti ambazo kwa kawaida (naturally) hutokea juu kama mgurumo wa ndege, radi, nk. Kwa hiyo Dolby Atmos inaongezea uhalisia ( live experience) kwenye sauti unazosikiliza.
Sasa kuna tofauti gani kati ya Dolby Digital Surround na Dolby Atmos? Ili uelewe fikiria uko katika jumba la sinema unaangalia movie. Mbele yako kuna ndege inakuja. Kwenye Digital Surround utasikia mgurumo ukitokea kwenye spika za mbele, baada ya muda ndege inaposogea zaidi na kupita juu yako mgurumo unahamia spika za nyuma. Unakuwa kama uko kwenye tukio lenyewe.
Lakini kwenye Atmos utasikia mgurumo kwenye spika za mbele, jinsi ndege inavyosogea sauti inahamia spika za juu mbele, baadaye juu katikati kisha juu nyuma na hatimaye nyuma chini. Kwa hiyo utafuatatilia huo mgurumo hatua kwa hatua hadi ndege itakapopotea. Si utajiona kama uko nje na ni ndege halisi? Kwa kweli Dolby Atmos imeongeza sana uhalisia( live experience)
Sasa je kama Atmos inahitaji spika nyingi inawezekanaje kupata live experience kwenye spika 2 tu mfano headphones za simu, iPod, nk?
Tekinolojia ya Dolby inawezesha spika mbili kupata Surround sound na hata Atmos kwani utasikia sauti zikitoka direction tofauti tofauti mfano, mbele, nyuma,juu,kulia na.kushoto lakini sio kwa ufanisi kama vile unavyotumia spika nyingi.
Nimeeleza kifupi lakini natumaini umeelewa.
Kweli! Kuna app flani nili I download Inaitwa 3D sound iliniisisimua sana! Nilidhani ni aina fulani tu za Spika nangehitaji ili kupata aina hiyo ya sauti kumbe siyo? Hadi nilimuuliza mkuu CHIEF MKWAWA kama naweza kupata Headphones za 3D!(namwamini sana) akaniambia Hajui kuhusu hizo! Nikaamua kuachana nazo!! Ila kiukweli ukisikia sauti ya muziki wa Digital surround system utakuwa tayari ku spend hata milioni kadhaa just for it!! Thanks
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom