No control over Religious radio stations over hate speeches

No control over Religious radio stations over hate speeches

ndg yangu Jesuit,
unajaribu kukwepa ukweli ulio wazi kwamba vyombo vingi vya habari vimeacha vision na mision zao na kujikita kwenye propaganda za kisiasa kiasi cha chakuchafua nchi.
nani kakwambia neno kiroho waislam hawalitumii? labda wewe ni mamluki ndio hujui, sisi tunaamini dini inakupa suluhisho la nafsi, mwili na roho. sasa kiroho unachosema nimekosea ni wapi? au unashangaa mwislam kulishambilia gazeti la kiislam? umesoma makala ya majid leo kuhusu redio Iman?

ndg yangu, kuna kipindi lazima uwe fair na usishabikie mambo ya kipuuzi hata kama yanafanywa na mtu wa kwenu. " mtoto wako anachezea kitu cha hatari kama sumu wewe utamucha ailambe afe au utamsaidia na kumkanya"
 
Sikubaliani na hoja yako hii kwa sababu katiba yetu haikatazi gazeti kushabikia chama cha kisiasa na hata ktk nchi zenye demokrasia iliyokomaa kama Uingereza kuna magazeti yanayoshabikia vyama vya Labor na consevative! sasa ni kawaida Annur kushabikia CUF bila kujali anaeongoza chama hicho ni Muislamu au ni Mkristo ndio maana Marehemu Mzee Mageni Musobi(Mkristo alipokuwa Mwenyekiti wa CUF tangu 1992-95 gazeti la Annur lilikuwa upande wa CUF! Gazeti hili lilianzishwa rasmi mwaka 1991!

Sasa haiwezekani Annur wakamsapoti Muislamu anaegombea Urais kupitia CHADEMA hata kama atakuwa anasali mara 5 kwa siku! kwa sababu Annur wako upande wa CUF kutokana na Sera za CUF za haki sawa kwa wote na wala sio sababu za udini!

Annur huenda wamepunguza kidogo mashambulizi yao dhidi ya chama tawala kipindi hiki sio kwa kuwa Rais alieko madarakani ni Muislamu bali kumbuka CUF kwa sasa pia wako Serikalini!

Wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi Gazeti la Annur lilikuwa limchambua na kumshambulia sana Mzee huyu na kama utataka ushahidi nitapost baadae! sasa Mwinyi alikuwa Muislamu au Mkirsto?

Kumbuka pia gazeti la Annur liko huru wala halina ubia wowote na Misikiti au Waislamu kwa ujumla hivyo maoni yao kuhusu vyama vya kisiasa ni maoni binafsi toka kwa jopo la uhariri hivyo tusiwahukumu Waislamu wote kwa kuwa Annur linamuelekeo wa Kiislamu!

Magazeti ya Lengo, mkombozi, Msema Kweli ni baadhi ya magazeti yenye muelekeo wa Kikristo na tulishuhudia uchaguzi uliopita jinsi walivyokuwa wakipigia debe chama cha CDM na hasa mgombea wake! lakini hawakuvunja sheria!

Hata magazeti ya Tanzania daima, Mwanahalisi, na kidogo Raia mwema ingawaje ni magazeti yasio na uhusiano na dini yoyote lakini yanaonekana kushabikia sana Chadema! ni haki yao wala hawavunji sheria ya nchi!

Uhuru, Habari leo, Mtanzania, Daily News nk, nayo yana julikana yako upande gani! zamani kulikuwa na gazeti likiitwa Dimba na hili likiegemea sana upande wa NCCR_Mageuzi!

We kama unaweza kusoma magazeti yote yasome na chomoa lolote zuri na lenye maslahi kwa taifa letu na lililo baya waachie wenye magazeti! huu ndio ukomavu na uhuru wa kujieleza![/QUOTE]

nimekuelewa ndg yangu mpendwa, lakini unajua visio ya gazeti Anoor ni kuwa sauti ya waislam?
nakubaliana na wewe kwamba baadhi ya vyombo vya habari vimeegemea chama fulani, lakini ni ushuri wangu wala siwalazimishi kwani hawavunjisheria kama ulivyonifundisha. mimi ningependa magazeti ya dini yajikite kwenye dini na yale ya siasa yaendelee na huduma ya siasa.

siwezi kushituka nikikuta habari za siasa ya uchochezi UHURU, T.DAIMA, RAI, MWANANCHI na mengineyo we know their mission, sasa haya ya dini kwa nini yashabikie siasa? tena si siasa ya kawaida ni ya kichichozi, kibaguzi na fitina.

Nakushukuru sana ndg yangu kwa shuke uliyonipa, umenifumbua macho zaidi, kwani binadamu siku zote anajifunza.
 
Ni ujinga na upumbavu kudhani kuwa asiye mwislam ni mpinzani wa uislam. Viongozi wetu lazima wakemee upuuzi wa aina hii.
 
Kama kuna chombo chochote cha habari ambacho mwananchi anaona kuwa hakimridhishi au kukutosheleza udadisi wake njia pekee ya kukiadhibu chombo hicho ni kutokukichangia .. yaani kutonunua au kutosiiliza. Kwa kadiri ya kwamba wanawanunuzi na wasikilizaji ndivyo nao wanavyoamini kuwa wanalo soko. Hata habari za kichochezi, za matusi, au udaku zina mashabiki wake.
 
mtoto wa nyoka ni nyoka, mtoto wa shetani ni shetwani, dini ya shetani ni shetani tu hata ifanyeje, hata ikijifanya mpole au mnyenyekevu, mfuga majini ni mfuga majini tu habadiliki, kuanzia roho nafsi na mwili....kwa wale wenye uelewa sawa na wangu, kilichobaki ni KUPIGANA VITA VYA ROHO na si vya mwili, manake vya mwili wanaweza sana, ila vya roho hawawezi kabisa. wengi wameshashindwa vya rohoni ndo maana makucha ya mwilini yanachipua....mwenye sikio la kusikilia na asikie, mwenye akili na aelewa niyasemayo!

Naona hujaielewa mada husika inazungumzia nini.
 
Hao waandishi wa hilo gazeti sio waislamu safi, ninavyojua mimi uislamu unafundisha amani, upendo na mshikamano. mwislamu wa kweli hawezi kupoteza mda kukashifu dini zingine, wala kupandikiza chuki, hao wanaoandika makala na habari za chuki wana ajenda zao. Na nina mashaka na uislam wao. Uislam ni dini ya amani, wasiichafue. Nawaomba waislam safi muwakemee hao mamluki ktk dini yenu na Mungu atawabariki.
 
ndg yangu Jesuit, <br />
unajaribu kukwepa ukweli ulio wazi kwamba vyombo vingi vya habari vimeacha vision na mision zao na kujikita kwenye propaganda za kisiasa kiasi cha chakuchafua nchi.
nani kakwambia neno kiroho waislam hawalitumii? labda wewe ni mamluki ndio hujui, sisi tunaamini dini inakupa suluhisho la nafsi, mwili na roho. sasa kiroho unachosema nimekosea ni wapi? au unashangaa mwislam kulishambilia gazeti la kiislam? umesoma makala ya majid leo kuhusu redio Iman?

ndg yangu, kuna kipindi lazima uwe fair na usishabikie mambo ya kipuuzi hata kama yanafanywa na mtu wa kwenu. &quot; <font color="magenta">mtoto wako anachezea kitu cha hatari kama sumu wewe utamucha ailambe afe au utamsaidia na kumkanya&quot;</font>
Tunakubaliana kuwa uchochezi wa aina yeyote haufai. Tatizo wewe unalaumu "effect" wakati mimi nataka ulamu "cause" Pia umechapia kwenye hoja ndogo ya mwisho nilipo sema waislamu hawatumii neno kiroho sijasema hawalielewi, uislamu hauna huo utengano wa mwili na roho, hilo linasisitizwa katika ukristo. Ni sawa na neno mhashamu, muadhama nk ingawa ni ya kiswahili yanatumiwa zaidi na wakristo. Nani kakuambia Mjengwa ni muislamu?
 
Tunakubaliana kuwa uchochezi wa aina yeyote haufai. Tatizo wewe unalaumu "effect" wakati mimi nataka ulamu "cause" Pia umechapia kwenye hoja ndogo ya mwisho nilipo sema waislamu hawatumii neno kiroho sijasema hawalielewi, uislamu hauna huo utengano wa mwili na roho, hilo linasisitizwa katika ukristo. Ni sawa na neno mhashamu, muadhama nk ingawa ni ya kiswahili yanatumiwa zaidi na wakristo. Nani kakuambia Mjengwa ni muislamu?

sawa bwana Jesuit nimekupata, mi nilidhani Mjengwa ni muislam, kumbe sivyo. asante kwa kunielekeza.
 
nimekuelewa ndg yangu mpendwa, lakini unajua visio ya gazeti Anoor ni kuwa sauti ya waislam?
nakubaliana na wewe kwamba baadhi ya vyombo vya habari vimeegemea chama fulani, lakini ni ushuri wangu wala siwalazimishi kwani hawavunjisheria kama ulivyonifundisha. mimi ningependa magazeti ya dini yajikite kwenye dini na yale ya siasa yaendelee na huduma ya siasa.

siwezi kushituka nikikuta habari za siasa ya uchochezi UHURU, T.DAIMA, RAI, MWANANCHI na mengineyo we know their mission, sasa haya ya dini kwa nini yashabikie siasa? tena si siasa ya kawaida ni ya kichichozi, kibaguzi na fitina.


Nakushukuru sana ndg yangu kwa shuke uliyonipa, umenifumbua macho zaidi, kwani binadamu siku zote anajifunza.[/QUOTE]




Ndugu Suleman unaushahidi gani kama gazeti la Annur vision yake ni kuwa sauti ya umma? fafanua hapa nikuelewe!
Narudia kukukumbusha ya kuwa dini ya Kiislamu na Siasa havitangamani bali pete na chanda! ktk Uislamu hakuna ya Mungu na ya Kaysari! na mfano mzuri ni Mtume Muhammad(SAW) alikuwa ni Imamu ktk Msikiti mtakatifu wa Madina na Makka na wakati huo huo saa za kazi alikuwa akikaa na baraza lake mawaziri kuendesha Serikali na wakati wa vita na maadui alikuwa frontline akipigana!

Nadhani si haki kuwaekea mipaka magazeti ya kidini nini waandike! na unapodai Gazeti kama la Annur huandika siasa za kichochezi naomba utuekee hapa huo uchochezi ili tuweze kuchambua kama kweli ni uchochezi au labda tafsiri yako ya uchochezi ni tofauti na tafsiri halali ya uchochezi!


Unapo pendekeza kuwa magazeti yasio ya kidini yabaki kuhubiri Siasa na yale ya kidini yajikite tu ktk kuhubiri Dini nadhani si sawa huku ni sawa na kudhibiti uhuru wa uandishi na uhuru wa kujieleza kwa wahariri wa magazeti na huku ni kuvunja katiba yetu inayoweka wazi uhuru huo!

Asante!
 
Kama kuna chombo chochote cha habari ambacho mwananchi anaona kuwa hakimridhishi au kukutosheleza udadisi wake njia pekee ya kukiadhibu chombo hicho ni kutokukichangia .. yaani kutonunua au kutosiiliza. Kwa kadiri ya kwamba wanawanunuzi na wasikilizaji ndivyo nao wanavyoamini kuwa wanalo soko. Hata habari za kichochezi, za matusi, au udaku zina mashabiki wake.

asante bro, uhauri wako ni bomba. mimi roho ilikuwa inaniuma sana kuona habari kama hizi kwenye media za dini hususani redio na magazeti
 
Walau wewe ni mmoja kati ya waislamu wachache wenye uwezo wa kuliona hilo. hongera mkuu, ila si unajua kwenye masuala ya dini kuna watu wenye njaa? wahariri na wamiliki wa hayo magazeti (An Nuur na Al huda) wamo kwenye payroll ya Rostam. Wapo viongozi wa dini ambao wanataka kujinufaisha kupitia nafasi walizopewa na waumini kinyume na matarajio y awaumini wao. JE HUKU NAKO SI KUCHANGANYA DINI NA SIASA? au ni mpaka tamko litoke kwa maaskofu!
 
Kwa taarifa yako Uislamu hautenganishwi na Siasa! ktk Uislamu hakuna falsafa ya KAISARI MPE KAISARI na YA MUNGU MPE MUNGU! Enzi za utawala wa kidikteta umepitwa na wakati huu ni wakati wa mtu au kutoa maoni yake bila uoga mradi asivunje sheria!

Gazeti la Annur ni gazeti halali kabisa limeandikishwa kisheria na hufuata maadili ya uandishi wa habari! Mhariri wake O. Msangi namfahamu binafsi ni msomi na muadilifu na uchambuzi wake wa habari ni wa kina na uliofanyiwa utafiti! haandiki kibubusa bali anachoandika huwa naushahidi!

Sasa kama wewe King Suleman unategemea Gazeti la Annur liwe linaandika habari za pepo na moto na ahera tu, ningekushauri ukanunue vitabu viko vingi vyenyekuelezea habari za Ahera! lakini Annur halitawacha kuandika makala yoyote muhimu zinazohusu uhusiano wa mtu na mola wake, na uhusiano wa mtu na jamii yake inayoizunguka!

Unataka kuturudisha ktk enzi za ukiritimba wa Awamu ya kwanza na kauli ya "USICHANGANYE DINI NA SIASA" kauli hii haina nafasi ktk dunia ya leo ya utandawazi, uwazi, uhuru wa vyombo vya habari, nk!

Ndugu yangu kama wewe umechoka kulisoma hili gazeti hakuna anaekulazimisha! magazeti yako mengi, kuna TANZANIA DAIMA; MWANANCHI; RAIA MWEMA, MWANAHALISI na hata ukitaka magazeti ya udaku na umbea pia utayapata! ukitaka kusoma habari za ngono salama au ngono hatari pia yako magazeti ya aina hiyo nk. nk.

Mwisho, nakushangaa kushambulia gazeti la Annur lakini umeshindwa kuona hayo magazeti mengine yanayochochea ufuska na kusababisha gonjwa baya la ukimwi lisiishe nchini mwetu kwasababu ndio yanayosomwa kwa wingi!
hongera tz kwanza kwahakika maelezo yako yakina yamejaa hekima na nimajibu sahihi kwa mtoa mada.hongera sana
 
Mwananchi ikisema kidogo wanatishiwa kufungiwa hivi hilo gazeti usalama wa taifa hawalioni?
 
nimekuelewa ndg yangu mpendwa, lakini unajua visio ya gazeti Anoor ni kuwa sauti ya waislam?
nakubaliana na wewe kwamba baadhi ya vyombo vya habari vimeegemea chama fulani, lakini ni ushuri wangu wala siwalazimishi kwani hawavunjisheria kama ulivyonifundisha. mimi ningependa magazeti ya dini yajikite kwenye dini na yale ya siasa yaendelee na huduma ya siasa.

siwezi kushituka nikikuta habari za siasa ya uchochezi UHURU, T.DAIMA, RAI, MWANANCHI na mengineyo we know their mission, sasa haya ya dini kwa nini yashabikie siasa? tena si siasa ya kawaida ni ya kichichozi, kibaguzi na fitina.

Nakushukuru sana ndg yangu kwa shuke uliyonipa, umenifumbua macho zaidi, kwani binadamu siku zote anajifunza.



Ndugu Suleman unaushahidi gani kama gazeti la Annur vision yake ni kuwa sauti ya umma? fafanua hapa nikuelewe!
Narudia kukukumbusha ya kuwa dini ya Kiislamu na Siasa havitangamani bali pete na chanda! ktk Uislamu hakuna ya Mungu na ya Kaysari! na mfano mzuri ni Mtume Muhammad(SAW) alikuwa ni Imamu ktk Msikiti mtakatifu wa Madina na Makka na wakati huo huo saa za kazi alikuwa akikaa na baraza lake mawaziri kuendesha Serikali na wakati wa vita na maadui alikuwa frontline akipigana!

Nadhani si haki kuwaekea mipaka magazeti ya kidini nini waandike! na unapodai Gazeti kama la Annur huandika siasa za kichochezi naomba utuekee hapa huo uchochezi ili tuweze kuchambua kama kweli ni uchochezi au labda tafsiri yako ya uchochezi ni tofauti na tafsiri halali ya uchochezi!

Unapo pendekeza kuwa magazeti yasio ya kidini yabaki kuhubiri Siasa na yale ya kidini yajikite tu ktk kuhubiri Dini nadhani si sawa huku ni sawa na kudhibiti uhuru wa uandishi na uhuru wa kujieleza kwa wahariri wa magazeti na huku ni kuvunja katiba yetu inayoweka wazi uhuru huo!
Asante![/QUOTE]

ni bahati mbaya najaribu kulitafuta hili gazeti online ili nikuwekee baadhi ya habari zake ungegundua ninachosema. kama umebahatika kulisoma gazeti la ijuamaa tar 14-20/1/11 ungeona taarifa zao karibu kurasa zote ni za siasa za kidini.

lakini pia naendelea kukushukuru sana kwa ushauri wako, unanielekeza vitu vingi na mimi naendelea kujifunza, hii ndio faida mojawapo ya Jamii Forum. thanks mkuu
 
Salaam wana JF,
sina nia ya kuanzisha uhasama wa kidini kwenye hii mada,
lakini palipo na ukweli ni lazima usemwe kwa faida ya jamii husika.

gazeti letu pendwa la An-Nuur silielewi lina mwelekeo gani kwa sasa na hususani toka kipndi cha uchaguzi mpaka sasa vuguvugu la katiba mpya. Ni siasa za uchochezi ndio zimetawala kati kurasa zote za gazeti, mara CHADEMA mara maaskofu wht is this?

kama kuna mtu amebahatika kulisoma hili gazeti la ijumaa tar. 14-20/1/1011, ataungana na mim
i
moja kwa moja kwamba hili gazeti limeacha msingi wake na kupapatikia siasa na uchochezi wa kidini badala ya mafundisho ya kidini kama tunavyotarajia.

waislam wengi hununua gaziti tukitarajia mafundisho angalau ya kiroho na mada za kifamilia, lakini hakuna kitu ni uchochezi wa kidini na siasa chafu kama vile ni gazeti la chama fulani cha siasa,
hayo pia yapo kwa ndg zetu Radio Imaan.

jamani vyombo vyetu vya habari vya kiislam ninani katuroga mpaka mmefika hapa mlipo? Sisi adui yetu mkubwa ni shetani na sio ukristo wala dini yoyote. Tufundisheni mafundisho ya Mtume na maadili mema ya dini sio siasa.

mwisho,
moto wa gazeti letu ni "Sauti ya waislam" . Kwa mtindo mlionao si sauti ya waislam wote, wengine sasa hatununui hilo gazeti maana hamna dini ni mambo yale yale tunayoweza kuyaona kwenye UHURU,MZALENDO,RAI,HABARI LEO na mengine...
Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
Suleiman.

siuseme kilichoandikwa ndio tukijadili, sio kuleta hoja sizizo na mashiko, mbona hulizungumzii gazeti la msemakweli.
 
siuseme kilichoandikwa ndio tukijadili, sio kuleta hoja sizizo na mashiko, mbona hulizungumzii gazeti la msemakweli.

Ebo! Nyani kweli haoni ku....le. Na wewe si useme gazeti la msemakweli la lini limeandika nini ndo tujadili sio kuleta hoja za maji taka hapa. Mnaanzisha magazeti ya An nuur na Al huda kutangaza udini na kuwaita wenzenu makhafir?
 
Ebo! Nyani kweli haoni ku....le. Na wewe si useme gazeti la msemakweli la lini limeandika nini ndo tujadili sio kuleta hoja za maji taka hapa. Mnaanzisha magazeti ya An nuur na Al huda kutangaza udini na kuwaita wenzenu makhafir?
mkuu tujadili hoja kisomi na sio kuleta jazba bila ya kuwa na mashiko.Waislam ni ulul' albab.
Rejea gazeti la msema kweli
tarehe 28.2.1993 lenye anuani "TAMKO RASMI LA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA MINTAARAFU KASHFA ZA KIDINI."

Halafu rejea Msema Kweli Toleo Na. 040, Jumapili Desemba 6-12, 1998
 
Ni ujinga na upumbavu kudhani kuwa asiye mwislam ni mpinzani wa uislam. Viongozi wetu lazima wakemee upuuzi wa aina hii.

Mimi naona kinachotafutwa hapa na hawa ndugu (wamashaka) waislamu wa vikaratasi vya uchochezi, ni kutaka mgazeti ya kikristo yaingie kwenye mtego wao huo wa uchochezi! Uzuri wakristo wanajuwa adui yao ni shetani tu siyo mwislamu au uislamu ama CCM au CUF. Wakristo hata wale wa kawaida kabisa wanajua na wanatambua hivyo.

Mwanakijiji usione hivi vkaratasi vinaendelea kutolewa bila kubugudhiwa, hata kama wanunuzi watavisusia kisinunuliwe hata kimoja, utaona vinaendelea kutoka siku hadi siku! Humo lazima kuna ufadhili wa mafisadi siyo bure!

Pia kuna tangazo lilitoka kwenye TV likisema "...kama kuna chombo cha habari kimetoa habari ikakukera una haki ya kupeleka malalamiko yako TCRA..." (kama sikosei-mtanisahihisha) Sasa inakuwaje vikaratasi hivi havipelekwi kwa "Ocampo" wake.
 
ni bahati mbaya najaribu kulitafuta hili gazeti online ili nikuwekee baadhi ya habari zake ungegundua ninachosema. kama umebahatika kulisoma gazeti la ijuamaa tar 14-20/1/11 ungeona taarifa zao karibu kurasa zote ni za siasa za kidini.

lakini pia naendelea kukushukuru sana kwa ushauri wako, unanielekeza vitu vingi na mimi naendelea kujifunza, hii ndio faida mojawapo ya Jamii Forum. thanks mkuu[/QUOTE]


Nashukuru mkuu kama tuko pamoja ila naomba ufafanuzi kidogo kuhusu kauli yako hapo juu kuwa tarehe 14-20 ANNUR kurasa zote zilikuwa ni za siasa za kidini! naomba ufafanuzi kidogo una maana gani kwa "Siasa za Kidini" au unamaana kuchanganya dini na siasa? au ni siasa kuchanganya na dini? na kama issue ni kuchanganya, jee, kuna ubaya wowote wa mchanganyiko huo? kwani mafunzo ya Uislamu sio mchanganyiko tu wa Dini na Siasa unakubaliwa bali inatakiwa kukoroga sawa sawa ili Dini na Siasa vinoge na kwenda sambamba!

Natanguliza amani na shukrani Mkuu!
 
Back
Top Bottom