Kwa taarifa yako Uislamu hautenganishwi na Siasa! ktk Uislamu hakuna falsafa ya KAISARI MPE KAISARI na YA MUNGU MPE MUNGU! Enzi za utawala wa kidikteta umepitwa na wakati huu ni wakati wa mtu au kutoa maoni yake bila uoga mradi asivunje sheria!
Gazeti la Annur ni gazeti halali kabisa limeandikishwa kisheria na hufuata maadili ya uandishi wa habari! Mhariri wake O. Msangi namfahamu binafsi ni msomi na muadilifu na uchambuzi wake wa habari ni wa kina na uliofanyiwa utafiti! haandiki kibubusa bali anachoandika huwa naushahidi!
Sasa kama wewe King Suleman unategemea Gazeti la Annur liwe linaandika habari za pepo na moto na ahera tu, ningekushauri ukanunue vitabu viko vingi vyenyekuelezea habari za Ahera! lakini Annur halitawacha kuandika makala yoyote muhimu zinazohusu uhusiano wa mtu na mola wake, na uhusiano wa mtu na jamii yake inayoizunguka!
Unataka kuturudisha ktk enzi za ukiritimba wa Awamu ya kwanza na kauli ya "USICHANGANYE DINI NA SIASA" kauli hii haina nafasi ktk dunia ya leo ya utandawazi, uwazi, uhuru wa vyombo vya habari, nk!
Ndugu yangu kama wewe umechoka kulisoma hili gazeti hakuna anaekulazimisha! magazeti yako mengi, kuna TANZANIA DAIMA; MWANANCHI; RAIA MWEMA, MWANAHALISI na hata ukitaka magazeti ya udaku na umbea pia utayapata! ukitaka kusoma habari za ngono salama au ngono hatari pia yako magazeti ya aina hiyo nk. nk.
Mwisho, nakushangaa kushambulia gazeti la Annur lakini umeshindwa kuona hayo magazeti mengine yanayochochea ufuska na kusababisha gonjwa baya la ukimwi lisiishe nchini mwetu kwasababu ndio yanayosomwa kwa wingi![/QUOTE]
Nashukuru kwa ushauri wako ndg yangu,lakini angalia msingi wa gazeti letu je upo sahihi kushabikia siasa za upande mmoj? je siku Chadema wakimuweka candidate wa kiislam kwenye post ya uraisi na CCM wakamuweka mkristo, gazeti letu liko tayari kulamba matapishi kwa kuwasifia chadema wanao waona mashetani na kukiponda ccm wanaowaona wako safi?
kama kweli wanataka kuandika habari za siasa basi wawe neutral na fair kwa kila kada na hiyo ndiyo misingi bora ya tasnia ya habari, kwa mtazamo wangu, naamini gazeti letu linatumiwa na mtu au taasisi fulani kuandika wanayoandika kwa kisingizio cha uhuru wa habari, mbona zamani waliandika mambo mema?
hapo penye bluu,
ndg yangu sio kwamba nashabikia magazeti ya kifilauni na vipeperushi vya ngono. mimi ni mmojawapo wa watu wanaoshambulia sana hivyo vijarida, na sina nia mbaya n gazeti la AN-NUUR, ila natamani warudi kwenye reli, nayapinga sana magazeti machafu na picha zake mkuu, ila leo nimeona nisikune wenzangu tu na mimi nijikune na kujisafisha kwanza