Matatizo ni kuwa sisi ambao tuko dini moja na hao wachochezi ( awe mkristu, muislamu, baniani n.k) tunachelea sana kuwakana kuwa hawatuwakilishi.
Mimi ningekuamini zaidi kama huko kwenye jukwaa la dini ungekuwa unawakemea waislamu wenzako wachache wanaotoa lugha ya matusi dhidi ya wakristu. Kuwashupalia wapuuzi wakikristu wakati unawaonea aibu wapuuzi wa dini yako hakutatupeleka mbali. Tunatakiwa WOTE kama jamii kukemea na kuvikana vitendo hivyo badala ya kujificha nyuma ya kivuli kuwa ni wachache tu wenye mawazo kama hayo. Tutajuaje kama wote mko kimya wakati wanayasema.
JokaKuu yuko sawa kabisa. Panatakiwa kuwa na zero tolerance vitendo kama hivi vinapotokea. Si kwa dini tuu. Uchochezi wa aina yoyote ( kikabila, rangi, jinsia, ulemavu n.k.) usipewe nafasi katika jamii yetu.
Ni kweli unalilosema. Jana nilipita Kariakoo jioni pale wanaposubiria magari ya kwenda Mtongani/Mbagala, loo...! Kulikuwa na lugha hizo! "Waambie 'makafiri' wenzako kuwa Ukristo siyo dini... uliletwa na paulo" Huwa inaniuma kuitwa kafiri kwa vile naamini ni tusi ni kama kumwambia mtu shetani.
Binafsi, siamini kuna kafiri duniani. As long as people exist, they must beileve in a religion. Even atheists have a religion because to say "God does not exist" is itself an affirmation of his existence for if he didn't exist they couldn't even have thought of his "non-existence". i.e Atheists also believe in God even if they think he doesn't exist.
Kurudi kwa hao jamaa wa Kariakoo, nilichowaambia ni kwamba wanapoteza muda bure kuanza kuhubiri kuhusu dini ya wenzao na kusahau kabisa wanachotakiwa kufanya katika dini yao.
Binafsi, naona ni 'projection' ya 'weaknesses' wanazoshindwa kuzishughulikia katika maisha au dini yao na kuzifanya kuonekana ziko nje ya maisha au dini yao wenyewe. Kwenye Uislamu kuna mambo mengi sana ya kuwahubiria watu na 'imagine' yote hayo taratibu yanaanza kupuuzwa au kusaulika na waumini au wahubiri wanaoshupalia Ukristo.
Dini yoyote 'legitimate' haidhoofiki kwa kupingwa na watu fulani hata kama wataweza kujieleza kuliko wengine. In fact, what those guys are doing is just to strengthen Christianity and weaken their own religion.
Kwangu mimi dini inajengwa wakati waumini wake wanashirikiana kuiimarisha zaidi na siyo kushirikiana kuongea kuhusu dini nyingine. Kila mtu ana uhuru wa kuamini kile anachoamini. Kama Wakristo wanaamini Yesu ni Mungu waache waamini na kama Waislamu hawaamini hivyo waache waendelee kutoamini. Kwangu mimi hakuna tofauti kwani naona wote hawa wako sahihi!
Lakini kutopeza muda kuonyesha nani anaamini kweli na nani haamini haisaidii kitu. Binafsi naamini wote tunaamini Mungu mmoja yuleyule lakini 'interpretations' zetu ndiyo tofauti.
Niilishatoa mfano wa chupa kuwa: 'suppose' chupa ipo mezani na watu wameizunguka pande zote. Je, wakiambiwa kila mmoja achore jinsi anavyoiona pale alipo, wote watachora picha zinazofanana? Si kila mmoja atachora kutoka upande aliopo?
Anayeiangalia kutoka juu, picha yake haitakuwa sawa na yule anayechora kutoka chini au pembeni.
Lakini wote watakuwa wamechora kuhusu chupa. Hata Mungu ni hivyohivyo: Ni Mungu mmoja, lakini tunamg'amua (experience him) kwa namna tunavyomu'conceive' hata kama 'we conceive him wrongly but at least we conceive him'.
Na hizi 'perceptions' zetu kuhusu Mungu zinabadilika (boreka) kulingana na jinsi watu wanvyozidi kumng'amua zaidi.
Vilevile, Mungu anaendelea kujifunua kwetu siku hadi siku. Kwa hiyo, hakuna njia kamilifu ya kuweza kumwelezea Mungu jinsi alivyo.. he's beyond our philosophies and understanding! Kitu kimoja ambacho kingetusaidia ni hiki:
LOVE WHAT YOU BELIEVE IS TRUE AND RESPECT WHAT OTHERS BELIEVE IS TRUE!
Tukifanya hivyo, tutaondokana na mizozo tuliyo nayo. Mtu akinihubiria kuwa nimepotea, anajisumbua - anapoteza muda bure kwani naamini niko katika njia sahihi.
Ila akinielekeza namna ya kumpenda Mungu na watu zaidi, kunionyesha njia 'positively', kudumisha amani na ushirikiano, kuongeza uadilifu, kutenda matendo ya fadhila au kuwatendea watu haki - hapo nitamsikiliza. Kwani hayo ndiyo mahubiri haswa!