Njombe: Daktari mbaroni wizi wa vifaa vya ujenzi wa hospitali

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,304
Watu wanne wakiwamo watumishi wawili wa Serikali na mlinzi wamekamatwa kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya ujenzi katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Makambako mkoani Njombe.

Taarifa za wizi huo zimetolewa leo Februari 9, 2024 na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Butusyo Mwambelo alipozungumza na Mwananchi Digital.

Amesema wizi wa vifaa hivyo unadaiwa kutokea jioni ya Januari 31, 2024.

Amesema waliokamatwa ni na daktari aliyekabidhiwa funguo za stoo, na mtunza stoo ambaye alikabidhiwa kutunza vifaa hivyo vya ujenzi.

Kaimu kamanda amesema pia mlinzi aliyekamatwa baada ya kupekuliwa nyumbani kwake alikutwa na vifaa vingine vya hospitali hiyo.

"Kweli tukio la wizi limetokea likafunguliwa jalada la uchunguzi na mkurugenzi kuunda kamati ya ufuatiliaji wa jambo hilo, ikaonekana vifaa vya ujenzi na umeme vimeibiwa," amesema Mwambelo.

Mganga mkuu wa halmashauri ya mji wa Makambako, Dk Alexander Mchome amethibitisha kutokea wizi huo na kudai upo utaratibu wa kutoa taarifa na anayeruhusu kuzitoa ni mkurugenzi wa halmashauri.

Source - Mwananchi
 
Back
Top Bottom