Nje ya silaha za nyuklia, Urusi haIna kingine cha kuitishia Marekani

The Evil Genius

JF-Expert Member
Mar 21, 2014
5,464
17,303
Baada ya mgogoro wa kivita wa Ukraine kuanza, waziri wa mambo ya nje wa Urusi Bwana Sergey Lavrov alitahadharisha kuhusu matumizi ya Nyuklia na kusema Urusi haitasita kutumia silaha za nyuklia pale itakapobidi.

Sasa naanza kuelewa kwamba ile ilikua ni defense mechanism ili kuficha udhaifu wa Urusi kwenye silaha.

Nimesema hayo kwa sababu zifuatazo.

Moja, Mwaka 2018 wakati Urusi wakifanya sherehe ya kuushinda unazi na sherehe hizo huambatana na maonyesho ya silaha mpya, Putin alitangaza silaha mpya za kisupasonic (supersonic missiles) zinazoitwa Kinzhal missiles na kusema hakuna mfumo wowote wa ulinzi Duniani wa kuzizuia, na kusema kwamba Urusi hua hatua 10 mbele kwenye uzinduzi wa technolojia mpya ya silaha kabla ya wapinzani wao, akimaanisha Marekani.

Mwaka jana mwezi wa 8, waziri wa ulinzi na Urusi Bwana Surgey Shoigu pamoja na watengenezaji wa silaha za kinzhal walisema hizo silaha hazina mfumo wa ulinzi Duniani, hakuna.

Cha kushangaza na kusikitisha juzi Ukraine kwa kutumia mfumo wa kizamani wa Marekani wa Patriotic missiles defense system waliweza kutungua silaha za Kinzhal bila kizuizi chochote.

Sasa kama silaha ambazo Urusi inasema ni za kisasa na za teknolojia ya mbele zaidi ya wenzake zinaweza kutunguliwa na mfumo wa kizamani wa Patriotic missiles defense system, Urusi amebakia na nini?

Pili, juzi hapa ndege isiyo na rubani ama drone ilitunguliwa ikiwa juu ya ya paa ya nyumba anayoishi Putin.

Urusi ikawatuhumu Ukraine na Marekani kwamba wanataka kumuua Putin.

Swali la kujiuliza, Urusi haina mfumo wa ulinzi wa anga hadi drone isafiri kutoka Ukraine hadi Moscow bila mfumo wa anga wa Urusi kuitambua? Hii ina maana kwamba Marekani ama Ukraine wakitaka kumuua Putin ni dakika sifuri tu kwa sababu hana mfumo wa ulinzi wa anga wa kumlinda.

Binafsi nilikua namkubali sana Putin lakini kwa haya madhaifu makubwa yaliyotokea hapa karibuni naanza kua na mashaka na uwezo wa kijeshi wa Urusi.

Urusi alichobakisha ni silaha za nyuklia tu otherwise ni maneno tu.
 
Hovyo.
Hata USA Ina silaha za nyukilia.
USA Haina Cha kuisumbua wala kuitisha Urusi katika medani za kivita.
Rejeo ni hii SMO ya Urusi.
Urusi Ingekua dhaifu USA na mashoga zake NATO wangeshaingia na wanajeshi wao kuisaidia ukraine.lakni wanaiogopa Urusi.
Kama unabisha niambie kwa Nini hawajaingia kama walivyoingia Iraq na Yugoslavia.?
 
Usikariri vita ni bunduki na risasi.

Dollar inatumbukia kwenye shimo reefu.
Screenshot_20230314-140022.jpg
 
Russia = Nyuki wa mashineni na amebaki kuwa Object of Admiration kwa magaidi na wenye kuunga mkono ugaidi. No more.
 
Acheni vichekesho, watu wanakufa huko Ukraine ujue. And, walemavu na wakimbizi chungu nzima. Endeleeni kushupaza shingo hadi zivunjike.
Kuua raia wa Ukraine sio kuonyesha uwezo mkubwa wa kijeshi cha kujiuliza je Urusi imekamilisha malengo yake kwa muda alioupanga kuua raia na kushambulia raia wasioweza kujitetea huo ni udhaifu wa jeshi la Urusi
 
Baada ya mgogoro wa kivita wa Ukraine kuanza, waziri wa mambo ya nje wa Urusi Bwana Sergey Lavrov alitahadharisha kuhusu matumizi ya Nyuklia na kusema Urusi haitasita kutumia silaha za nyuklia pale itakapobidi.

Sasa naanza kuelewa kwamba ile ilikua ni defense mechanism ili kuficha udhaifu wa Urusi kwenye silaha.

Nimesema hayo kwa sababu zifuatazo.

Moja, Mwaka 2018 wakati Urusi wakifanya sherehe ya kuushinda unazi na sherehe hizo huambatana na maonyesho ya silaha mpya, Putin alitangaza silaha mpya za kisupasonic (supersonic missiles) zinazoitwa Kinzhal missiles na kusema hakuna mfumo wowote wa ulinzi Duniani wa kuzizuia, na kusema kwamba Urusi hua hatua 10 mbele kwenye uzinduzi wa technolojia mpya ya silaha kabla ya wapinzani wao, akimaanisha Marekani.

Mwaka jana mwezi wa 8, waziri wa ulinzi na Urusi Bwana Surgey Shoigu pamoja na watengenezaji wa silaha za kinzhal walisema hizo silaha hazina mfumo wa ulinzi Duniani, hakuna.

Cha kushangaza na kusikitisha juzi Ukraine kwa kutumia mfumo wa kizamani wa Marekani wa Patriotic missiles defense system waliweza kutungua silaha za Kinzhal bila kizuizi chochote.

Sasa kama silaha ambazo Urusi inasema ni za kisasa na za teknolojia ya mbele zaidi ya wenzake zinaweza kutunguliwa na mfumo wa kizamani wa Patriotic missiles defense system, Urusi amebakia na nini?

Pili, juzi hapa ndege isiyo na rubani ama drone ilitunguliwa ikiwa juu ya ya paa ya nyumba anayoishi Putin.

Urusi ikawatuhumu Ukraine na Marekani kwamba wanataka kumuua Putin.

Swali la kujiuliza, Urusi haina mfumo wa ulinzi wa anga hadi drone isafiri kutoka Ukraine hadi Moscow bila mfumo wa anga wa Urusi kuitambua? Hii ina maana kwamba Marekani ama Ukraine wakitaka kumuua Putin ni dakika sifuri tu kwa sababu hana mfumo wa ulinzi wa anga wa kumlinda.

Binafsi nilikua namkubali sana Putin lakini kwa haya madhaifu makubwa yaliyotokea hapa karibuni naanza kua na mashaka na uwezo wa kijeshi wa Urusi.

Urusi alichobakisha ni silaha za nyuklia tu otherwise ni maneno tu.
Kama huwezi kutofautisha kati ya subsonic, supersonic na hypersonic speed who can take you seriously??


Russia analo conventional bomb lijulikanalo kama father of all bombs au wewe hujawahi kulisikia - sasa linganisha yield ya bom hilo la Kimerikan aina ya mother of all bombs na bomb halafu rudi hapa jamvini tuzungumze - tatizo lenu mna inflate sana military capabilies za Merikani mkiulizwa hivi ni lini Merikani aliwahikupigana vita na Taifa lenye uwezo mkubwa kijeshi na Merikani ikashinda - tukionacho sisi ni Merikani kukusanya kusanya vinchi vidogo vidogo vya Ulaya kwenda kuvamia Banana Republics - Merikani huwa haivamii military weak Nations akiwa peke yake - what does that tell you - hapo tunazungumzia conventional bombs - lakini kwa kuongezea kuonyesha kwamba Urusi silele mama jaribu kufatili bomb la thermonuclear lililo lipuliwa na Urusi zaidi ya miaka sitini na kitu mpaka sasa hakuna taifa lolote lilolo wahi kufunja rekodi hiyo mainginia/wanasayansi walitaka bomb hilo liwe na uwrzowamufikia 100MT lakini wakawa concern namadhara yanayo weza kusababishwa na mlipuko wa bomb hilonfio maana walipunguza nguvu zake kifikia 50MT - Amerika hajiwahi kuvunjarekodihiyompaka sasa huu nimwaka wa 60+ Tzar La Bomba bado halina mfano we Duniani - acheni kuangalia movies za Hollywood na CNN - Russia kitu ingine - Biden hasipokuwa makini akaendeleza jeuri zake - mwisho wasiku atajuta kuzaliwa kwa kuliingiza taifa lake kutaka kushindana na Ivan the terrible.
 
Kama huwezi kutofautisha kati ya subsonic, supersonic na hypersonic speed who can take you seriously??


Russia analo conventional bomb lijulikanalo kama father of all bombs au wewe hujawahi kulisikia - sasa linganisha yield ya bom hilo la Kimerikan aina ya mother of all bombs na bomb halafu rudi hapa jamvini tuzungumze - tatizo lenu mna inflate sana military capabilies za Merikani mkiulizwa hivi ni lini Merikani aliwahikupigana vita na Taifa lenye uwezo mkubwa kijeshi na Merikani ikashinda - tukionacho sisi ni Merikani kukusanya kusanya vinchi vidogo vidogo vya Ulaya kwenda kuvamia Banana Republics - Merikani huwa haivamii military weak Nations akiwa peke yake - what does that tell you - hapo tunazungumzia conventional bombs - lakini kwa kuongezea kuonyesha kwamba Urusi silele mama jaribu kufatili bomb la thermonuclear lililo lipuliwa na Urusi zaidi ya miaka sitini na kitu mpaka sasa hakuna taifa lolote lilolo wahi kufunja rekodi hiyo mainginia/wanasayansi walitaka bomb hilo liwe na uwrzowamufikia 100MT lakini wakawa concern namadhara yanayo weza kusababishwa na mlipuko wa bomb hilonfio maana walipunguza nguvu zake kifikia 50MT - Amerika hajiwahi kuvunjarekodihiyompaka sasa huu nimwaka wa 60+ Tzar La Bomba bado halina mfano we Duniani - acheni kuangalia movies za Hollywood na CNN - Russia kitu ingine - Biden hasipokuwa makini akaendeleza jeuri zake - mwisho wasiku atajuta kuzaliwa kwa kuliingiza taifa lake kutaka kushindana na Ivan the terrible.
Tu assume kwamba una akili sana na una hoja.

Pili tu assume kwamba wewe ni Urusi na sasa silaha yako ya kisasa na unayoiamini sana kuliko zote imekamatwa na adui ambae ulisema hana uwezo wa kuikamata.Je hapo utakua umebaki na nini zaidi cha kujilinda nacho iwapo adui amekamata silaha yako tegemeo.

Hilo ndio lilikua swali sasa wewe ambae una akili sana umeshindwa kuelewa ama kujibu hilo swali umeanza kuleta ngonjera na hadithi zisizo na kichwa wala miguu.

Narudi kwenye assumption yangu ya awali kwamba una akili, nahitimisha kwamba huna akili.
 
Tu assume kwamba una akili sana na una hoja.

Pili tu assume kwamba wewe ni Urusi na sasa silaha yako ya kisasa na unayoiamini sana kuliko zote imekamatwa na adui ambae ulisema hana uwezo wa kuikamata.Je hapo utakua umebaki na nini zaidi cha kujilinda nacho iwapo adui amekamata silaha yako tegemeo.

Hilo ndio lilikua swali sasa wewe ambae una akili sana umeshindwa kuelewa ama kujibu hilo swali umeanza kuleta ngonjera na hadithi zisizo na kichwa wala miguu.

Narudi kwenye assumption yangu ya awali kwamba una akili, nahitimisha kwamba huna akili.
Haya mambo ya akili yanaingia ingiaje hapa??

Mimi ni mwanasayansi nazungumza ninayo yajua mimi na watu wengi Duniani wanajua sana ukweli huo wa kujali facts and figures na sio mambo ya siasa - wstu wengi wana kasumba ya kuzuga Dunia kwamba Amerika zaidi kwenye masuala ya silaha za Conventional nikawatajia bomb moja ambalo ni conventional lenye uwezo mkubwa kuliko la Kimerikani baada ya kulinganisha mother of all bombs na Urusi la father of all bombs sikusokia mtu akipinga - ndio nikazungumzia kidogo kuhusu thermonuclear arsenal nako nikasema Urusi zaidi pamoja na very modern and lighyeninf fast delivery systems - lakini bado watuwana endelea kubishi baada ya kukalilishwa maneno kwamba Duniani ndege hatari ni F-35 (Waamerika waliyo copy kutoka Urusi) F-16 ambayo hata MiG-21 iliyo uu dwa 1955 bado inaiipiku kwa spidi na ikiwekewa very modern AAM, canon na avionic MiG-21 inaweza kuzitungia zote bila ya wasi wasi - USA inaweza kuwa na ndege nyingi za kibita lakini Warusi wana formifable air defense systems za kuzitungua karibu zote - kupanga ni kuchagua Wamerika waliona wawekeze zaidi kwenye ndege za vita Waurisi on the other end wakaona ni vema kuwekeza katika silaha za kulinda anga la Urusi - mwenye busata kati ya mayaifa hayo mawili ni nani - jibu unalo.
 
Back
Top Bottom