Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,502
- 16,712
- Thread starter
- #181
Vizuri!.Admissionletter umejaribu kutuelimisha na kutupa picha pana ya hiyo referendum.Tuelimishane kidogo, hakuna njama za kuimega Sudan. Referrendum ni utekelezaji wa kipengele muhimu cha Mkataba wa amani wa Sudan (CPA) uliofikiwa 2005. Mkataba huu ulikuwa ni ushindi mkubwa kwa wasudan na jumuiYa ya kimataifa kwani ulimaliza vita iliyodumu kwa zaidi ya miaka 30 (1956-1972) na (1983-2005) na kusababisha vifo vwa watu wapatao milioni mbili!! Wakati mkataba huu unafikiwa hii vita ilikuwa "chronic" na jina na John Garang lilikuwa "never miss" kwenye BBC. Katika Mkataba wa CPA, kulikuwa na kipengele kwamba ndani ya Miaka mitano baada ya kusainiwa mkataba kama serikali ya Sudan ikishidwa kufanya muungano uwe kuvutio ("to make unity attractive") kwa watu wa Southern Sudan, basi watu wa Southern Sudan watakuwa na haki ya kuamua hatma yao kwa kupitia Referrendum. Mpaka sasa serikali ya Sudan haijafanya chochote (tangu 2005) kuwaridhisha watu wa Southern Sudan wakubali "unity," kwa hiyo watatumia haki (chini ya CPA na "Referrendum Law" iliyopitishwa kutekeleza CPA) kupiga kura ku-"separate." Kwa hiyo hizi si njama. Ni wasudan wenye wameamua na bunge limeridhia kwa kupitisha sheria ya "Referrendum." Lingine la kufahamu ni kwamba wananchi wa Southern Sudan wamepoteza kabisa imani ("trust") na Serikali kwani wamenyanyaswa kwa muda mrefu. Hivi majuzi Riek Machar, Makamu wa rais wa Serikali ya Southern Sudan aliulizwa msimamo wake kuhusu "Referremdum" akasema kwa hali ilivyo sasa, hata kama Serikali ya Sudan ikifanya maendeleo ya haraka haraka na kuindeleza Juba (mji Mkuu wa nchi mpya ya Southern Sudan) kabla ya Rererendum na kufanana na Dubai, yeye hatapigia kura kuunga "unity" sababu haiamini serikali ya Sudan!!
Pamoja na hivyo suala la kuwepo njama halikwepeki.Hii kwamba bunge limepitisha sheria ya referendum haina maana kuwa wamefanya kwa kupenda.
Nchi za magharibi ni hatari sana katika njama na mashinikizo.Nchi nyingi za hulazimishwa kufanya vitu wasivyovipenda baada ya kuona hawana pa kutokea.Wamezungukwa na vitisho makamio ya kila namna mengine hupitishiwa kwenye umoja wa mataifa,moja ya chombo chao cha kushinikiza matakwa yao.Mfano mmojawapo angalia Tanzania ilivyolazimika kuingia kwenye vyama vingi pamoja na kwamba kura ya maoni ilionesha kuukataa mfumo huo.
Nina uhakika Sudan haipendelei kujitenga na ndugu zao wa kusini lakini walilazimika kubadili taratibu na katiba yao ili kujipunguzia bughdha zinazoongozwa na Marekani.
Huyu Riek Machar na Salva Kiir wala si watu wa kutilia maanani maneno yao,ni watu ambao hawako huru katika kufikiri kwao.Wamewekwa mbele ili malengo ya nchi za magharibi yatimie ,baada ya hapo watatupwa nje kwa mbinu mbali mbali.Tulikuwa nao wengi kule Mazar Sharif kaskazini ya Afghanistan.