Sudan haijauwa watu kama inavyofanya Marekani na umoja wa mataifa ya Ulaya magharibi-NATO.Hawafanyi hivyo kwenye eneo moja tu bali nchi zote za waislamu.Wanavunja miundo mbinu na kuangamiza mazingira.Kwa vile wanaouliwa ni waislamu sijakusikia ukilaumu.
Kwamba raia wa Sudan Kusini wamekufa kwa mamilioni kutokana na vita vya wenye kwa wenyewe, huo ni ukweli ambao hauwezi kupingika. Mimi sijaandika popote wala sijatamka kuwaunga mkono Wamarekani wala watu wa Magharibi kwa ujumla. Katika hili Waafrika tumekuwa na sauti moja. Ndio maana waafrika kwa ujumla wetu tuliungana kupingana na udhalimu wa kikoloni na tukapata uhuru.
Sasa huwezi kuleta hoja kuwa kwa kuwa Marekani ni wababe, basi tusizungumzie udhalimu wa serikali ya Sudani dhidi ya raia wake.
Ukiwapongeza watu wanaojitetea hadhi zao za kibinadamu na kwamba hawawezi kutulia mpaka wahakikishe kuheshimika kwao naamini uko pamoja na mashujaa wa kiislamu wa Iraq,Taliban wa Afghanistan na Hamas wa Palestina.Ikiwa si hivyo basi hujui unachokisema umekuwa kama kasuku tu.Huwezi kuaminika hayo unayoyaeleza kuhusu Sudan.Ni ukasuku tu unaoukufanya uandike.
Mimi nimepost na kujibu kilicho kwenye thread hii uliyoianzisha wewe Ami. Na ya humu yanahusu Sudan. Ningeanza kuzungumzia kuzungumzia kuhusu Iraq, Afghanistan na Palestina ningekuwa nimetoka nje ya mada.
Msimamo wangu ni huu: Popote pale ambapo ubinadamu unadhalilishwa hatuna sababu ya kuunga mkono. Na udhalimu dhidi ya binadamu unafanywa na serikali ya Sudan pia, jambo ambalo ndilo linahusika na thread hii, na hatuwezi kukanusha tu eti kwa kuwa Iraq, Afghanistan na Palestina nao wanaua binadamu.
Naongeza pia kuwa siungi mkono kitendo chochote kinachopelekea kuua raia wasio na hatia wakiwemo akina mama na watoto kwa njia kama za kujilipua au kurusha mabomu sehemu za kiraia (makazi ya watu, shule, hospitali n.k.) kwa kisingizio chochote kile. Kwa hiyo vitendo vya majeshi ya Israel, Wafuasi wa Taliban, Hamas, Al qaeda, Al Shabab, Majeshi ya Marekani na Washirika wake, popote pale wanapoua raia wasio na hatia sikubaliani navyo. No excuse in this. Je Ami unafurahia kujilipua kwa Al qaeda na Al Shabab? Unanitaka niunge mkono hilo?
Katika posts zangu naomba unioneshe mahali popote nilipounga mkono Marekani au nchi za magharibi katika udhalimu wao please. Au kwako nikikosoa Serikali ya Sudani ndio nimeunga mkono Magharibi. Kama unamaanisha hivyo basi kutakuwa na udhaifu mkubwa kwenye logic yako.
Bwana Ami, unaonesha ushabiki wa wazi kwa waarabu. Nami naona kuwa huo ndio ukasuku. Kwamba waarabu hawafanyi udhalimu, hawajawahi kufanya udhalimu na hawawezi kufanya udhalimu. Umewakweza kama malaika vile. Lakini hili si kweli, na hapa ndio iko wazi kuwa uko brain washed. Waarabu nao ni binadamu na kama binadamu wengine wote, nao wana mapungufu yao kama binadamu mmoja mmoja na kama mataifa pia. Tena kuna walio na ukatili uliopea dhidi ya Binadamu,
killing in the name of God. Historia pia imetuthibitishia hilo. Mbona hata hapa Kwetu tu Zanzibar ilibidi wazee wetu wachukue mapanga dhidi ya Serikali ya Sultani?
Waafrika tunapaswa kuungana kweli na kukumbatia haki za raia wote. Yeyote anayekiuka haki hizo hata kama ni Mwafrika mwenzetu lazima tumpinge. Vilevile hata kama ni mzungu au Mwarabu, kama ni Mwislamu au Mkristo au mpagani lazima tumpinge pia.
Sumu ya udini inabidi kuiangalia sana. Kutetea matendo ya mtu, kundi la watu au taifa kwa kigezo kuwa ni wa dini yako au kuwapinga kwa kuwa si wa dini yako bila kuangalia zaidi ni upofu mbaya sana. Waarabu na Wazungu wanachekelea wakiona Waafrika tunamezwa na hilo.
Serikali ya Sudan imeshindwa katika kuwathibitishia raia wake kuwa Binadamu wote ni sawa, na kuwa wote wana haki sawa. Sasa serikali hiyo kwa nguvu ya mashujaa wa Sudan Kusini imelazimika kuitisha kura hii ya maoni.
Waache Wasudan waamue mambo yao kwa ajili ya kunusuru heshima ya utu wa Wasudan Kusini.
Kwa heri Bwana Ami.