Niulize jambo lolote kuhusu mziki wa Mchiriku/Mnanda

Ashaaaa niambie ukweli kama hunitaki usinitapeli... ilikua balaaa

kondakta kaja juu akasema haiwezekani kupanda bure imeruhusiwa jeshi la polisi..
mnanda sema tu hawauelewi

Btw Asha imeimbwa na jack simela au
Kumbe ulijuaaaaaa, unamimba yanguuu, ilikuaje tena kuniambia,ukaniambiaa imetokaaaa, mashetani yametoa mimbaa!
 
Jamaa waliendaga ulaya kufanya show, wazungu wanashangaa jamaa wanapanda na visturi na kinanda cha watoto, ila sound ilipoanza wanaona sturi inatumika kama ala! Mizuka ikapanda, jamaa anaimba "We Baba Dulaaaaaaaaaaa" wazungu wanaitikia "Eee Eee'...

Mnanda/mchiriku mtamu sana!
 
Jamaa waliendaga ulaya kufanya show, wazungu wanashangaa jamaa wanapanda na visturi na kinanda cha watoto, ila sound ilipoanza wanaona sturi inatumika kama ala! Mizuka ikapanda, jamaa anaimba "We Baba Dulaaaaaaaaaaa" wazungu wanaitikia "Eee Eee'...

Mnanda/mchiriku mtamu sana!
Hiyo stuli kiufundi inaitwa "Taiming",ni moja kati ya vyombo muhimu sana kwenye mziki huo.
 
nani Superstar wa mchiriku bongo
Hakuna kigezo rasmi cha kumpata super star namba moja bongo,sababu allmost masuperstar wekubwa wengi kila mtu alitamba zama zake,mfano kuanzia miaka ya mwishoshoni mwa themanini kuja tisini hakuna bendi iliyokuwa maarufu zaidi ya Hisani Gari kubwa kutoka Mwanyamala,baadae kidogo Tumaini Jabali(wasanii hao hao wa Hisani walikua wanachepuka kufyatua albamu ki maslai yao),mbeleni Fadhira nao walivuma wakati mwisho wakaja kukimbiza Jagwa hususani baada ya kuja baba J kutoka Chaukucha Family hiyo ni kwa upande wa Kinondoni(Mwananyama),njoo Temeke,wakati Uraibu wanatamba wengine walikua vidampa,lakini baadae Topaz wakatikisa,kisha Atomic Music na Kombora ikiwa balaa,mbele Kidogo New Kiwembe,Kijumuia na Seven Survivor ikawa patashika nguo kuchanika.

Hivyo kila kitabu na zama zake!!!.
 
Mkuu tuma humu hizo ngoma zote..yanini tukufate pm mkuu..
emoji120.png
emoji120.png
Tatizo nyimbo za mnanda nyingi ni ndefu hivyo zinatumia mb nyigi,so bado sijakua na ujuzi wa kuzi
 
Hakuna kigezo rasmi cha kumpata super star namba moja bongo,sababu allmost masuperstar wekubwa wengi kila mtu alitamba zama zake,mfano kuanzia miaka ya mwishoshoni mwa themanini kuja tisini hakuna bendi iliyokuwa maarufu zaidi ya Hisani Gari kubwa kutoka Mwanyamala,baadae kidogo Tumaini Jabali(wasanii hao hao wa Hisani walikua wanachepuka kufyatua albamu ki maslai yao),mbeleni Fadhira nao walivuma wakati mwisho wakaja kukimbiza Jagwa hususani baada ya kuja baba J kutoka Chaukucha Family hiyo ni kwa upande wa Kinondoni(Mwananyama),njoo Temeke,wakati Uraibu wanatamba wengine walikua vidampa,lakini baadae Topaz wakatikisa,kisha Atomic Music na Kombora ikiwa balaa,mbele Kidogo New Kiwembe,Kijumuia na Seven Survivor ikawa patashika nguo kuchanika.

Hivyo kila kitabu na zama zake!!!.
wewe kweli ni shabiki wa mchiriku
 
Hakuna kigezo rasmi cha kumpata super star namba moja bongo,sababu allmost masuperstar wekubwa wengi kila mtu alitamba zama zake,mfano kuanzia miaka ya mwishoshoni mwa themanini kuja tisini hakuna bendi iliyokuwa maarufu zaidi ya Hisani Gari kubwa kutoka Mwanyamala,baadae kidogo Tumaini Jabali(wasanii hao hao wa Hisani walikua wanachepuka kufyatua albamu ki maslai yao),mbeleni Fadhira nao walivuma wakati mwisho wakaja kukimbiza Jagwa hususani baada ya kuja baba J kutoka Chaukucha Family hiyo ni kwa upande wa Kinondoni(Mwananyama),njoo Temeke,wakati Uraibu wanatamba wengine walikua vidampa,lakini baadae Topaz wakatikisa,kisha Atomic Music na Kombora ikiwa balaa,mbele Kidogo New Kiwembe,Kijumuia na Seven Survivor ikawa patashika nguo kuchanika.

Hivyo kila kitabu na zama zake!!!.
Dah bro, una KINA cha kutosha kwenye huu Mziki!
 
Usemacho ni kweli,lakini kwa vile halikuwahi kufanyika pambano la kitaifa la mziki wa mnanda basi itoshe kusema mnanda hauna bingwa!.

Kwanini?,kwanza kwenye mziki wa mnanda kuna kitu kikuu kinaitwa #Tune(mapigo au miondoko),kuna mziki wa Kinondoni,bendi kama Hisan Gari kubwa,Tumaini Jabali,Fadhira,Jagwa,Chaukucha,na hata Wanyamwezi familly,wao wana mapigo yao na mashabiki wao kindakindaki.

Na kuna mziki wa Temeke,bendi kama Seven Survivor,Atomic,Topaz,Kombora,Buti Kubwa,Miami Yankees,Kijumuia New kiwembe na hata Uraibu.Hivyo basi kila mpenzi wa muziki huu ana mapenzi binafsi kutoka kwenye band husika.

Hivyo hatuwezi kuitimisha kwamba fulani alikua bora kuliko mwengine ilihali halikuwahi kufanyika shindano na kila mmoja ana band yake
Ukiangalia Kwa vigezo vingi Juma Mpogo aliwazidi wenzake hasa kwenye utunzi
 
Topaz (Rasmi Topaz Advantage)band hii ilipotea kitambo sana,kwani baada ya manguli wa bendi hiyo kuanzia Omary Omary ambae alitoka na kwenda kuanzisha bendi yake mpya Atomic Advantage
Atomic advantage je wapo?
 
Mkama Shapu mdau mkubwa wa mchuliku.. Kile kikundi chake cha Mchiliku kilitwaje?

Hisani ngoma ilikiwa na mwimbaji wake wa kike, Aligongwa na gari asubuhi mitaa ya Faya, Kutokana na ile ajali wakatunga nyimbo uke mwimbo nimeusahau jina.. Unaitwaje? Kama uko nao tuwekee hapa...
Hussein Mwinyi sasa Rais Zanzibar alikuwa mdau mkubwa wa Hisani ngoma (Mchiliku) unakumbuka aliwahi kutungiwa nyimbo? Mbali na ule ya aliyotungiwa Baba yake Mzee Mwinyi kipindi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

Mkuu huu mziki ni full masela.. Old is Nile..
 
Ukiangalia Kwa vigezo vingi Juma Mpogo aliwazidi wenzake hasa kwenye utunzi
Ni kweli usemacho lakini kwa mustakabali mzima wa mziki wa mchiriku huwezi kutamka hivyo,ingawa mimi mwenyewe ni mpenzi wa Juma Mpogo na bendi yake ya Seven,na niko njiani kuandaa documentary yao chini ya kiongozi aliebaki #Nasosoro Mwipi(capten Chollo boy)lakini kamwe siwezi kutamka kwamba Mpogo alikua Alpha na Omega!!.
 
Mkama Shapu mdau mkubwa wa mchuliku.. Kile kikundi chake cha Mchiliku kilitwaje?

Hisani ngoma ilikiwa na mwimbaji wake wa kike, Aligongwa na gari asubuhi mitaa ya Faya, Kutokana na ile ajali wakatunga nyimbo uke mwimbo nimeusahau jina.. Unaitwaje? Kama uko nao tuwekee hapa...
Hussein Mwinyi sasa Rais Zanzibar alikuwa mdau mkubwa wa Hisani ngoma (Mchiliku) unakumbuka aliwahi kutungiwa nyimbo? Mbali na ule ya aliyotungiwa Baba yake Mzee Mwinyi kipindi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

Mkuu huu mziki ni full masela.. Old is Nile..
Mkama Shapu huyu alikua ni askari polisi aliewahi kufanya kazi mitaa ya Temeke na baadae kituo cha Msimbazi kama sikosei,huyu alikua ni mdau mkubwa wa mziki wa mchiriku kwa wakati huo na bendi ya mwanzo maarufu kuipa saport ni bendi ya Night Star iliyokuwa chini ya Haidari Kesi.

Kuhusu bendi ya Hisani Gari kubwa iliyokuwa na maskani yake pale Mwananyamala Ujiji na ukaribu na familia ya Mwinyi hilo sina uhakika nalo sana, bali ninachokumbuka ni kuwa Hisani wao katika albam yao ya kwanza Hisani Garikubwa Vol.1 iliyotoka 1986 walimtunguia wimbo walioupa jina la #Ally Mwinyi(Nahodha wetu hodari) sababu nyakati hizo ndio katoka kuchukua hatamu za uongozi wa nchi mwaka 85.

Na kuhusu hili la msanii wao wa kike kufariki kwa ajali ya gari pale faya wacha nilifanyie kazi,sababu nina connection ya kutosha ya baadhi ya wasanii wa iliyokua bendi hiyo ambao bado wako hai,mfano aliewahi kuwa mpiga ngoma(Kulwa) ambae kwa sasa natambulika kama Sheshi Jr aliyo
 
Back
Top Bottom