Nitumie njia gani niisahau pombe?

Nitumie njia gani niisahau pombe?

Kama hulewi chakari,hutukani watu,hupigi watu,etc huwa unajutia kitu gani sasa?Yaani unakunywa zako pombe kisha unaenda zako nyumbani kirohoo safi kabisa halafu unajuta tena?Huwa unajutia nini?
Najuta kutumia hela ovyo..halafu hata kusali siwezi tena aah
 
Yaan nimeshtuka saa kumi alfajiri nikawa najuta sana kwanini nimekunywa tena? Imekuaje? Mpaka sahiz nipo kitandan hata kazin sijaenda nimesema nitafute njia leo ya kunisaidia niache kabisa
Hio ni kawaida tu kwa sababu leo ni J3 ila ikifika Ijumaa kiu ya pombe itarudi upyaaa.
 
Najuta kutumia hela ovyo..hlf hata kusali siwez tena aah
Jifunze kunywa pombe kisayansi.Ukinywa pombe kisayansi ni tamu sana.Mimi huwa naenda mara chache kula kitimoto kwa bia zangu mbili kisha narudi nyumbani,na tena huwa naenda mwenyewe bila kampani.Kwa mwezi naweza enda mara nne au mara mbili,tofauti na hapo sinywi pombe.
 
Pombe si kitu kibaya ila binadamu wanaitumia vibaya. Pombe inaburudisha baada ya kazi ngumu. Raha ya pombe ni kunywa kiasi kidogo tu. Kama ni bia, moja au mbili zinatosha. Unasikiaje raha baada ya bia 5 au 7?

Mwanzo wa Wazungu kuanzisha Public Houses au Pubs ilikuwa ni sehemu ya wanaume kukutana na kubadilisha a mawazo. Kutokana na hali ya uchumi wanaume wengi wa ujira wa chini walimudu bia moja au mbili.

Siku hizi watu wanakunywa benefit yote. Matokeo yake ni kuongezeka kwa magonjwa yatokanayo na Pombe.
 
Jifunze kunywa pombe kisayansi.Ukinywa pombe kisayansi ni tamu sana.Mimi huwa naenda mara chache kula kitimoto kwa bia zangu mbili kisha narudi nyumbani,na tena huwa naenda mwenyewe bila kampani.Kwa mwezi naweza enda mara nne au mara mbili,tofauti na hapo sinywi pombe.
Tatizo mie bia mbili hazinikolei kabisa
 
Pombe si kitu kibaya ila binadamu wanaitumia vibaya. Pombe inaburudisha baada ya kazi ngumu. Raha ya pombe ni kunywa kiasi kidogo tu. Kama ni bia, moja au mbili zinatosha. Unasikiaje raha baada ya bia 5 au 7?

Mwanzo wa Wazungu kuanzisha Public Houses au Pub ilikuwa ni sehemu ya wanaume kukutana na kubadilisha a mawazo. Kutokana na hali ya uchumi wanaume wengi wa ujira wa chini walimudu bia moja au mbili.

Siku hizi watu wanakunywa benefit yote. Matokeo yake ni kuongezeka kwa magonjwa yatokanayo na Pombe.
Asee namie nimefikia kiwango ambacho mtu anayekunywa bia mbili namshangaa maana mie sizisii kichwan kabisa ni kama nimekunywa maji tu
 
Tatizo mie bia mbili hazinikolei kabisa
Basi wewe ni mlevi,mimi huwa sinywi bia ili nikolee au ili nilewe.Huwa nakunywa bia kama sehemu ya mlo wangu,yaani nikila kitimoto kwa bia zangu mbili huwa najisikia kushiba vizuri.
 
Tusaidiane namna bora bas mkuu
Ukiamua kuacha pombe unaaacha vizuri tu,ujue mambo mengi tunayoyafanya ni kujiendekeza,ukijinedekeza kufanya jambo flani inakujengea mazoeza na hali ya kutamani kufanya!! Kuna mtu alikuwa kila msosi lazima ashushie na soda yaani hawezi kupiga msosi bila soda pembeni lakini kwasasa kashaacha fresh tu! Weka dhamira kwamba kwasasa sitaki kunywa pombe na pia epuka vitu vinayokufanya utamamani pombe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom