Nilivyoteseka na tatizo la nguvu za kiume

UZZIMMA

JF-Expert Member
Nov 20, 2014
406
456
Katika maisha yangu niliishi nje ya ulimwengu wa zinaa. Hakika sikuwa mzinifu hata pale nilivyopata vishawishi vikali vya uzinifu nilivikwepa kwa jitihada kubwa sana.

Sikuwa na rekodi yoyote kuhusu kuwa na msichana na wala kufanya zinaa.

NDUGU WAINGIA WASIWASI NA MIMI.

Baadhi ua ndugu, jamaa, marafiki pamoja na majirani wakaingia shaka na mimi. Na hali ya kuwa mimi sikuwa na shaka yoyote.Kila nikijiangalia asubuhi nimesimama barabara Ila tu sitaki uzinifu.

Siku moja ilitokea mama, baba na kaka wakanikalisha kikao kwa lengo la kunihoji, kwanini hawajasikia wala kuona nikiwa na mwanamke? Mimi nikawathibitishia kwa mdomo kuwa sina tatizo lolote, ni mzima wa afya.
Niliweka kisa hiki humu ndani mwaka 2019.



Mambo yakapita ilhali mama ndiye mwenye wasiwasi mkuu.

MASHAMBULIZI MATATU YANAFELI.

Nilikutana na mashambulio matatu kabla ya kuoa.

LA KWANZA: kuna mfanyakazi wa ndugu yangu mmoja aliniita chumbani usiku na kunilazimisha kunipa kitumbua. Nilikataa kutokana na imani na msimamo wangu. Nilishinda dudu limesimama takriban usiku mzima. (Binti alikuwa na shepu yule). Hili nililifelisha mwenyewe kwa sababu za kiimani.

LA PILI: binti wa watu tulikuwa na promise ya kunitembelea akaja geto.

Shetani akanishawishi nikajikuta dude limesimama namchezea yule binti. Kadili ninavyomchezea nazidi kunywea, huku binti akilalamika kuwa yupo katika siku zake. Sikumuamini kwa sababu ndio maneno ya wasichana wanaokataa kukupa mchezo.

Na mimi huku nimenywea nikaanza kupata mawazo.

Hatimaye akanionesha damu za period nikashukuru ameniokoa. Kwa sababu nilikuwa nishanywea. Nikamruhusu akaondoka.

Hapo sikuhisi kuwa ni tatizo kwa sababu nilikuwa mtu wa imani nikasema "kunywea kwa dude langu na binti kutoka damu ya hedhi (alisema ilimtoka ghafla na sio siku zake) Mwenyezi Mungu kaniepusha na zinaa"

LA TATU: Kidemu nilikishawishi nikakale mzigo kakaingia laini. Nafika geto kama kawaida dude limesimama nganganga.

Naanza kumchezea. Kadili ninavyomchezea nazidi kunywea.Hakugundua hilo. Akanaiambia nitumie kondom. Hapo nikaleta kisingizio cha mimi kuhairisha mchezo.

Nilieleza kwa ufupi kisa hiki 2019


Yote hayo nilijipa imani kuwa Mungu ananilinda na zinaa. Kumbe ilikuwa ni tatizo tayari.

USIKU WA KWANZA KATIKA NDOA

Kwa umri wangu wote wa miaka 27 sikuwahi kufanya uzinzi zaidi ya yale majaribio matatu, ambapo moja nilidhamiria kulikwepa mengine mawili nilishindwa kutimiza.

Siku nalala na mke wangu kwa mara ya kwanza sikuwa na wasiwasi hata chembe. Sikuwa na shaka ya aina yoyote. Ingawa baadhi ya ndugu zangu walitilia shaka, hasa mama.

Kwa kuwa nilioa mahala ambapo si makazi yangu, ikabidi twende tukalale guest na mke wangu.

Nilimuandaa vya kutosha mpaka mtoto karoa. Sasa tatizo likaja palepale kila nikimchezea nazidi kusinyaa. Mwishoe nikamueleza mke wangu. Mke wangu alifanya kila namna kunitomasa lakini wapi, dude halikusimama. Mwishoe ilibidi tulale huku nikiwa na mawazo tele. Mke wangu alinipa moyo na kunifariji kwa kuniambia hizo ni stress za harusi.

Kuna rafiki yangu aliyenisindikiz kuoa, alinigundua kama nina mawazo sana, hadi akaniuliza. Baada ya kuniuliza kwa muda mrefu, nikamuelezea kilichonitokea. Nilimuelezea huku nalia kwa kwikwi.

Basi ule usiku wa kwanza katika ndoa, ndipo nligundua kuwa MIMI NINA TATIZOZO LA NGUVU ZA KIUME.

Nilizungumzia uzi huu miezi minne kabla ya ndoa.



NAANZA KUTUMIA VIAGRA.

Kama kawaida, ile siku ya kwanza na ya pili nilivyoenda kuoa sikufanikiwa katika mchezo.

Safari ya kurudi nyumbani katika makazi yetu na mke wangu ikaanza. Nikiwa nawaza nifanyaje ili nifanikiwe. Baada ya kupekua mtandaoni ndipo nikagundua kuna vidonge vinaitwa viagra.

Siku nafika tu nyumbani nikaenda duka la dawa kuvitafuta. Nilivipata kirahisi sana (sikutegemea). Nikaomba maelezo ya kutumia vidonge kwa muuza dawa nikapata maelezo.

Nikanywa njiani ili mke wangu asijue. Nafika nyumbani baada ya dakika ishirini kitu kinasimama chenyewe, baada ya kula nikaingia mchezoni. Nilimgalagaza mke wangu sana. Nilitamani niende tatu ila mke wangu yeye akaomba poo. Anaomba poo mimi bado nina mzuka. Siku ikapita maisha yakaenda

Ikawa ndio kawaida yangu. Kila nikitaka kwenda mchezoni nameza viagrq bila mke wangu kujua.
Kuna muda nameza viagra halafu mke wangu anahairi mechi. Huwa nalalamika hadi basi.

Kuna muda najaribu bila viagra nashindwa kabisa. Nikawa namwambia mke wangu muda mwengine mashine inakubali muda mwengine inakataa. Kumbe muda inayokubali natumia viagra.

NAANZA KUHANGAIKA NA DAWA.

Kutokana na hali hio kunifedhehesha sana nikaanza kutafuta dawa sehemu mbalimbali hasa za mitishamba.


Nilitumia dawa inaitwa MR MCAHAKAMCHAKA, MKUYATI n.k. Zote hizo hazikuleta mafanikio yoyote.

INAENDELEA UPDATE


















UPDATE UPDATE UPDATE UPDATE

NAANZA KUHANGAIKA NA DAWA.


Kutokana na hali hio kunifedhehesha sana nikaanza kutafuta dawa sehemu mbalimbali hasa za mitishamba.


Nilitumia dawa inaitwa MR MCAHAKAMCHAKA, MKUYATI n.k. Zote hizo hazikuleta mafanikio yoyote.


Nikitaka kujaribu dawa niliyoitumia kama imefanya kazi, siku ya mechi situmii viagra. Na hapo nashindwa kusimamisha ipasavyo nahairisha mechi.


Nikawa namwambia mke wangu muda mwengine mashine inakubali muda mwengine inakataa. Kumbe muda inayokubali natumia viagra.


VIAGRA YAACHA KUFANYA KAZI KATIKA MWILI WANGU.


Nilitumia viagra takriban miezi miwili ambapo ni mara tano kwa miezi yote hio.


Mwanzoni naanza kutumia viagra ndani ya dakika 20 tu napata matokeo na inachelewa kuondoka. Lakini kadili ninavyoitumia nachelewa kupata matokeo na inawahi kuisha nguvu. Ikafika hatua nikinywa nasubiri masaa matatu ndio ifanye kazi. Hivyo baada ya kunywa kama saa nne inabidi nilale hadi saa saba kisha niamke, nimuamshe mke wangu tufanye.


Ikafika hatua hata nikila havifanyi kazi kabisa.


Nakumbuka siku moja nilikunywa kidonge kimoja ikagoma. Hapohapo nikaongeza kidonge cha pili vyote vikagoma.


Siku hio ndipo nikagundua kuwa hili tatizo lipo seriously.


NAANZA KWENDA HOSPITALI RASMI.


Tangu siku hio vidonge viwili vya viagra viliponigomea, nikaanza kwenda hospitali.


Nikakutana na nesi (nikidhani dokta) baada ya kumuelezea tatizo langu, akaniandikia vipimo vya SPERM.


Baada ya kupima sperm nikagundulika nina low sperm count na abnormal sperm 60℅.


Yaani sperm walikuwa wachache 3milion/ml na inatakiwa minimum wawe 15milion/ml.


Licha ya uchache wao ni 40℅ tu ndio normal. Wenye uwezo mzuri yaani ACTIVE.


Nikaandikiwa dawa za kuongeza na kurubisha sperm. Nikatumia kama mwezi sikuona mafanikio.


Nakumbuka baada ya kwenda hospitali kuna siku nilikutana na mtu fulani wa makamo katika mambo yangu ya biashara. Baada ya kumaliza maongezi ya biashara, nikamuelezea tatizo langu kwa kuwa hapo kwake nilivyoenda niligundua kuwa alikuwa ni mtaalamu wa tiba za asili.(kulikuwa na vikopo vingi vya dawa).


Yule mtaalam akaniuliza jina langu, akaliandika kwenye karatasi akaangalia kiganja cha mkono wake wa kulia akaniambia yafwatayo. "Kijana una majini wawili. Mmoja ni wako wa asili na mwengine umetupiwa na mtu. Na huyu uliyetupiwa ndiye anakutesa. Ulitupiwa baada ya ugomvi wa kunyang'anyia mwanamke. Na mwanamke huyo ni mrefu kidogo, mweusi na ana mwili kiasi."


Nikamuuliza kuhusu suluhisho akasema, "lete kuku wawili wa kienyeji, na pesa shilingi laki moja".


Hapo ndipo nikahisi nahadithiwa PAUKA PAKAWA.


Vile naondoka akanifwata akasema "imenijia data mpya, mke wako anasumbuliwa na tumbo mara kwa mara. Ana kitu kibaya tumboni mwake. Hivyo baada yako wewe tutamtibu na mke wako".


Baada ya kuniambia hivyo nikaondoka na sijarudi tena.


NABADILI RASMI MFUMO WANGU WA MAISHA.


Nikakutana na watu wa FOREVER. Nikatumia bidhaa yao inaitwa MULTI MACA. Muda mchache baada ya kutumia nikaanza mazoezi kila asubuhi. Nikaanza kula matunda kwa wingi.


Asubuhi nakula tikiti na ndizi, mchana nakula mlo wa kawaida usiku tikiti na ndizi na matunda mengine. Nikamaliza dozi ya FOREVER MULT MACCCA lakini sikufanikiwa nilipoenda mchezoni. Nikarejesha mrejesho kwa aliyeniuzia dawa akanishauri ninunue na package nzima ya AROVEKA JEL na ARGI PLUS. Kwa kuwa niliona ni gharama sana nikaacha kununua.


Niliendelea kutumia juisi ya tikiti iliyochemshwa pamoja juisi ya limao (mitandao mingi waliieleza hii kama ni natural viagra), maji mengi ya kutosha, bila kuacha mazoezi. Nikawa nakula vitunguu swaumu asubuhi nikiamka na usiku kabla ya kulala.


Nilifanya hivyo kwa umakini na uaminifu wa hali ya juu sana.


Baada ya wiki tatu nikaomba mechi.


Kiukweli nilishindwa, sikuweza.


Kesho yake nikatumia viagra, ambayo mara ya mwisho nilikunywa mbili na haijafanya kazi. Hakika hapo viagra ilifanya kazi mara mbili ya nilivyotumia siku ya kwanza.


KWA MARA YA KWANZA NAFANYA BILA MSAADA WA VIAGRA.


Kumbuka imeshafika miezi mitatu kuelekea minne ya ndoa yetu. Siku moja baada ya mazoezi makali na kuzingatia milo nilijaribu nikafanikiwa kwenda round moja bila viagra. Ingawa nilienda hio round baada ya wife kunitomasa sana, lakini nilifurahi. Furaha yangu ni kwa kuwa ni mara ya kwanza tangu nazaliwa naenda bila booster. Nikajaribu kesho yake nikashindwa. Nikawa narejea viagra nazo zinagoma.


NARUDI HOSPITALI KWA MARA YA PILI.


Nikarudi hospitali kumueleza daktari akaniandiki vipimo vya homoni za uzazi na ULTRA SOUND. Baada ya kupima homoni nikagundulika nina kiwango kikubwa cha homoni 8.2.


Ultra sound nikagundulika na tatizo la varico celes. Kwa ufupi hili ni tatizo la kupanuka kwa mishipa ya vein katika korodani.














UPDATE UPDATE UPDATE UPDATE
SEHEMU YA MWISHO.




NAANZA KUTAFUTA TIBA YA VARICO CELES.

Niliwahi kuomba ushauri juu ya varicocele katika jukwaa la afya humu jamii forum.


Hakika sikupata jibu. Nilitembelea baadhi ya hospitali sikufanikiwa kupata specialist.


Nakumbuka katika kuhangaika, nilimpata jamaa mmoja akasema atanitibia. Akaniambia nimtumie pesa laki tisa nika mkimbia.


Kuna daktari nilimuelezea akasema varico Celes haikuwa sababu ya mimi kutosimama.


Akasema ataisaidia. Nikawa nampigia simu akawa hapokei, nikampotezea.


Kuhusu kipengele hiki niliwahi kuomba msaada jamii forum




NAMWELEZA KAKA YANGU NA ANANIPELEKA KWA MTAALAMU.


Mke wangu akawa ananisihi nieleze tatizo hili kwa ndugu zangu. Nikamueleza kaka yangu tu. Kaka akanipeleka kwa mtaalamu aliyeelekezwa.


Baada ya kufika kwa mtaalamu huyo wa kienyeji nikamuelezea. Akauliza jina langu na la mke wangu kama yule wa mwanzo.


Naye huyu akaniambia nina jini nililolipata kutokana na mimi kutumia mafuta mazuri na kutoka mitoko ya ujana


Akaniagiza nilete pesa ya dawa anitibie nikamkimbia mazima.



Kipindi chote hicho tunalia na mke wangu kila wakati wa tendo. Kwa maana mambo hayawi. Viagra zote ziligoma miezi mitano ya ndoa.



NAKUTANA NA MMASAI ALIYETATUA TATIZO LANGU.



Kwa kuwa nilishatumia dawa nyingi za wamasai bila mafanikio, kuna siku nikakutana na mmasai fulani.



Nikamueleza yule mmasai kuwa nataka dawa ya kutia adabu. Kisha nikamwambia yule mmasai ninyi wamasai siku hizi dawa zenu feki.



Mmasai yule alikasirika akasema una bei gani nikupe dawa. Nikasema nina elfu mbili.



Akasema. Lete hio elfu mbili yako ukatumie kisha kesho ukija hio sio bei yake.



Akasema ninunu maji nusu lita. Akachanganya dawa zake akanipa nikanywe nusu saa kabla ya tendo.



Nikafanya hivyo. Baada ya nusu saa ikanijia hali ambayo haikuwahi kunijia kabla. Nilisimama zaidi ya nondo. Nikapeleka moto kwa siku mbili.



Siku nyengine nikamfwata yule mmasai kutaka dawa tena. Akaniuzia 15,000 badala ya elfu mbili. Nikanunua tena kwa mara ya mwisho tulifurahia tendo wote.



MMASAI ANANIPONESHA KABISA



Baada ya kununua dawa za mmasai mara kadhaa, nikamwambia aniletee dawa ya kuponesha kabisa. Akaniambia nimpe elfu themanini nikampa.



Akanipa dawa niliotumia mwezi mzima.



Tena habari njema wakati natumia dawa zile za mmasai kama booster nilimpa mke wangu uja uzito.



Baada ya mwezi kuisha mke wangu akawa mja mzito. Nikawa napeleka moto huku ana ujauzito, bila viagra bila booster ya aina yoyote. Tena moto moto kweli.



Mwanzo tulikuwa tunafanya siku za hatari tu kwa lengo la mtoto na sio starehe.



Na mimi ikikaribia siku za hatari nilikuwa nakosa amani kutokana na hali yangu.



SASA NIMEKUWA KERO KWA MKE WANGU.



Kuokana na hali yangu kuwa shwari tena nganganga sasa namsumbua mke wangu.



Nikipewa usiku, asubuhi nataka. Nilitamani nikeshe nafanya mapenzi tu. Ila mke wangu anaomba po.



Muda mwengine nafsi ya kuchepuka inanijia ili nijikizi haja zangu ambazo mke wangu hawezi kunihimili lakini nikikumbuka mke wangu alivyo nivumilia, nashindwa kabisa kufanya hivyo.



HITIMISHO
Siuzi dawa, sina dawa ninayoijua wala sina mahusiano na wauza dawa. Ila kwa furaha yangu tu nimetoa ushuhuda.
Pia nimetoa uzi huu ili wengine wajifunze chochote kutokana na nilichopitia
Tulilia kama watoto mimi na mke wangu.
Sifa zimwendee mke wangu kipenzi, kwa kunivumilia kipindi chote cha matatizo yangu. Hakika sikuona dalili yoyote ya kufikiria kuchepuka. Kikubwa aliomba sana Mungu.
Mwenyezi Mungu awabariki na kuwalinda. Tumtegemee Mungu tutashinda.

MWISHO



UPDATE UPDATE UPDATE

UPDATE YA DHARURA

Na katika ushuhuda wangu sisemi kuwa dawa ambazo hazikunitibu hizo NI ZA UONGO.
La hasha bali mimi HAZIJANITIBU.

Na dawa ambayo mimi imenitibu sisemi kuwa ndio inatibu. La hasha ila MIMI IMENITIBU.

Nasisitiza sitangazi dawa humu.



MWISHO.
 
Haiingii akilini mpk unafikia miaka 27 hujawah kabisa kusex na mwanamke afu ghafla bin vuu, eti unatwambia mkeo unajua kumuanda vya kutosha mpk unajua kwamba kaloa.

Twambie hizo skills ulizitoa wapi?

Au ulikua mwangalia pucha za ngono na kujichua?
Naunga miguu pamoja nawe mtoa mada umetupiga n kitu kizito puani unataka kupromote nn
 
Haiingii akilini mpk unafikia miaka 27 hujawah kabisa kusex na mwanamke afu ghafla bin vuu, eti unatwambia mkeo unajua kumuanda vya kutosha mpk unajua kwamba kaloa.

Twambie hizo skills ulizitoa wapi?

Au ulikua mwangalia pucha za ngono na kujichua?
Mitandao yote hio inayofundisha jinsi ya kumuandaa mwenza.

Nilijifunza mengi kabla ya kuoa ili nisije kukosea katika tendo. Nilisoma pia vitabu vyenye muongozo wa elimu ya ndoa kwa mujibu wa imani yangu.

Ingekuwa ni kijana wa miaka ya 1620 nisingeweza kujua hayo ya kumuandaa mwenza.
 
Back
Top Bottom