Nitatoa zawadi ya 200,000

Jumapili nenda hapo kkkt kimara utamuona anasimama hapo alipopigia picha, akitaka kupiga nyingine au umwambie mchungaji atangaza hapo kanisani!
Lakini isije ikatokea ukamwaga machozi hapo kanisani maana ndipo hapo Bashite alipomwaga machozi!
Ha..ha..haa.has.has.ha
 
Uyo jamaa aliekataa kurudisha hela nae analo kosa maana kataarifiwa na yeye kakiri kuwa hela imeingia na kapewa offer ya elfu 50 lakini hakurudisha na hapatikani hewani
hata ka ni wewe mpunga umeingia wa kutosha alafu uko majalala utarudisha.?........kama ni kesi na iwe sirudishi...na kama unavojua huu wakati mpunga umekuwa scarce sababu ya baba Jesca
 
hahahha haya mambo bwana nilikosea nkamtumia jamaa mkwanja flan badae nkamcheki anirudushie alicho nijibu nilicheka peke yangu kwa upole alinambia

"bro nna dhiki ya kufa mtu, nkisema ntakurudishia ni uongo nisamehe sana bro."
Afadhali ya huyo alie kuambia ukweli, na kweli kuna wakati tunapaswa kusamehe
 
Naomba nikupuuze tafadhali....
 
Reactions: Pep

Barikiwa sana mkuu
 

Barikiwa sana mkuu
 
hahahha haya mambo bwana nilikosea nkamtumia jamaa mkwanja flan badae nkamcheki anirudushie alicho nijibu nilicheka peke yangu kwa upole alinambia

"bro nna dhiki ya kufa mtu, nkisema ntakurudishia ni uongo nisamehe sana bro."
Hahaha
 
Mkuu kwanza pole sana kwa yaliyotokea. Kwa kipindi km hiki kupoteza pesa inauma sana! Lkn naomba na me nitoe ushauri kidogo ingawa unaonekana hupendi kusikia ushauri wenye mwelekeo hasi.

Kosa lako la kwanza ni kutuma pesa kimakosa kwa kukosa umakini.

Kosa la pili hukujali ulipotuma mpaka ulipostuliwa na anayekudai.

Kosa la tatu baada ya kupiga simu huduma kwa wateja uliambiwa pesa imetolewa hukupaswa kumpigia cm ulitakiwa uanzie hapo kumtafuta.

Kwa sheria za fedha zilivyo huyo jamaa siyo mwizi(ingawa kiuhalisia ni mwizi) kwa sababu amefanya miamala yote halali. Yaani umemtumia muamala ukakamilika,mpaka akaenda kutoa na kwenyewe muamala ukakamilika. Yaani kiukweli hata hiki unachokifanya unaongeza makosa.

Kuweka picha yake mtandaoni unafanya kosa kwa sababu inawezekana kabisa mtumiaji wa hiyo SIM card anaweza asiwe yeye. Anaweza akawa anatumia mtu mwingine kabisa kutokana na udanganyifu wa freelancer aliyemsajilia hiyo sim card.

Ushauri: tumia njia za kistaarabu zaidi unaweza kumpata na mkaongea ki-rafiki unaweza kuokoa japo nusu. Hii ya ubabe huenda ukaendelea kupoteza pesa wakati unahitaji pesa.

Mwisho. Ushauri siyo kitu cha lazima unaweza kuuchukua au kuuacha. Pole tena mkuu Ushimen
 
Sasa laki mbili itakufikisha wapi. Wabongo njaa kweli. Mtu badala ya kufanya ustaarabu kumrudishia mwenzako pesa yake, wewe unaamua kuitoa na kutelekeza laini yako na namba yako kisa laki mbili. Tabia mbaya sana hii.
 
Mkuu Ushimen nimemcheki kijana Facebook yake naona yupo tu anatamba ila Instagram ndio kaweka Private!

Nahisi kumpata ni rahisi ila kuipata hela ndio inaweza kuwa ngumu!

Halafu dogo anafanana na Bashite nahisi wana undugu!
 
hahahha haya mambo bwana nilikosea nkamtumia jamaa mkwanja flan badae nkamcheki anirudushie alicho nijibu nilicheka peke yangu kwa upole alinambia

"bro nna dhiki ya kufa mtu, nkisema ntakurudishia ni uongo nisamehe sana bro."
Mie kuna siku wakala aliniwekea 800,000/- badala ya 80,000/- nikaona baadae kuwa kazidisha hela. Kesho yake nikarudi nikamuuliza jana umeniwekea sh ngapi akasema elfu themanini. Nkamwambia angalia meseji zako. Mama wa watu alitahamaki nikamrudishia 720,000/- huyo mama kila akiniona anahadithia watu maana hakuamini.

Maisha haya ni uaminifu tu. Mtu akikosea sio sababu ya kuona una bahati maana huwezi kujua shida utakazomuachia. Pia ni laana na mikosi kumdhulumu mtu usiyejua tabu zake
 
Pole sana,ngoja nikupe ujanja kidogo,nenda tigo waombe namba 3 alizokuwa anawasiliana nazo mara kwa mara.ukipata hizo namba 3 mpigie mmoja kati ya hao atakusaidia.hii Mimi iliwahi nisaidia kumpata mtuhumiwa.
Post zote zifutwe ibaki hii tu,.. Ume ena
 
Asante na asante kwa ushauri
 
Sasa laki mbili itakufikisha wapi. Wabongo njaa kweli. Mtu badala ya kufanya ustaarabu kumrudishia mwenzako pesa yake, wewe unaamua kuitoa na kutelekeza laini yako na namba yako kisa laki mbili. Tabia mbaya sana hii.
Mkuu, jamaa nilitumia pesa nyingi kidogo.
Hiyo laki mbili ndio nimeitangaza kama zawadi kwa atakae niwezesha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…