Nitakuwa tofauti na Mh. Spika kuhusu hili la Bandari ya Bagamoyo

Na Thadei Ole Mushi.

Spika wa Bunge kaishangaa Serikali kuanza kutengeneza Reli badala ya Kuanzia na bandari. Si mara ya kwanza Kwa Mh Ndugai kusema kuhusu ujenzi wa BANDARI hii mwaka 2019 alisema hata wachina wanatushangaa na wakatufananisha na MTU aliyetanguliza mkokoteni mbele halafu punda nyuma. Kwa maana ya kwamba kujenga Reli ni kutanguliza Mkokoteni Mbele halafu Punda nyuma.

Wachina wana hamu na ujenzi wa Bandari hiyo kuliko hata watanzania wenyewe. Je ni kweli wachina wanatupenda kiasi hicho?

Fact

Mwaka juzi China ilianza kushikilia mashirika muhimu ya Zambia baada ya Zambia kushindwa kulipa madeni inayodaiwa na China.

China ilishikilia Shirika la Utangazaji la nchi hiyo pamoja na Shirika la Umeme la Zambia (ZESCO) na bado wataendelea kutaifisha mashirika mengine kadri muda utakavyokwenda.

Huko Sri-Lanka nako wameshikilia Bandari ya nchi hiyo kwa Lengo lile lile la kulipa madeni ya China.

John Perkins kupitia kitabu chake Confession of an Economic Hit man anatufunulia jinsi sera ya Conspiracy inavyofanya kazi.

Perkins anaelezea kazi aliyokuwa akiifanya bila yeye kujua kwenye Kampuni la MAIN (Consulting and engineering Company)

Aliajiriwa kama mfanyakazi kwenye kampuni hilo ambalo ni Kampuni binafsi ila shughuli zake ziliathiriwa na mkono wa Serikali (Ujasusi) bila yeye kujua.

Kazi yake kubwa ilikuwa ni kushawishi nchi maskini zikope mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa katika nchi zao. Miradi kama vile ujenzi wa miundombinu ya Reli,Ujenzi ya Umeme ambayo utasaidiwa kukopeshwa aidha na World bank, IMF au USAID.

Perkins alikuja kugundua kuwa njia hii ya kukopesha mikopo mikubwa ambayo hailipiki ni njia mojawapo ya Taifa la Marekani kuendelea kupata maeneo ya kunyonya katika nchi maskini.

Perkins anatoa mifano jinsi alivyofanikisha kuingiza Indonesia kwenye Mtego huo na nchi nyingine nyingi.

Kwa nchi ambazo zinaendelea na zenye rasilimali kama Gesi, Madini na mafuta Marekani huwa hawalali kwenye kuhakikisha inatafuta kuwakopesha.

China nayo imeaanza kunufaika na Sera hii ya conspiracy kila mahali wanajenga ushawishi mkubwa kutoa mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa. Wanajua mikopo hii hailipiki hivyo wanaweza kunufaika wao.

Bandari ya Bagamoyo ikikamilika inafunika zote Afrika Mashariki, hivyo wateja wengi watahamia Bagamoyo ambayo itakuwa inaendeshwa na mchina baada ya sisi kukosa fedha za kumlipa mchina. Najiuliza Je China inaweza kutupenda kwa kiasi hicho? Je tunaweza kumlipa mchina?

Ole Mushi
0712702602

View attachment 1746890
"Siku Moja mtanikumbuka, najua mtanikumbuka kwa mazuri sio kwa mabaya, kwa maana na sacrifice maisha yangu kwa ajili ya watanzania masikini". Mchina ni mkoloni ajaye hapa Africa, anatafuta kila jinsi aweke miguu yake kwa kisingizio cha kutusaidia kuwekeza. Hawana huruma kiasi hicho, kwa mwendo huu nchi hii itakuwa kama Enzi za mzee ruksa aka shamba la Bibi. RIP JPM.
 
Muda umefika wauweke wazi mkataba nasi tuusome..tuweze kutoa maamuzi..sio kuwasikia wao KILA siku
 
Je, tunao ushahidi au ni propaganda kuwa Wachina wanakamata mali za nchi eti kwa kuwa nchi hiyo imeshindwa kulipa deni? Wanakamata bila makubaliano, bila matakwa ya mkataba? Leteni hiyo rasimu ya mkataba wa Bagamoyo nasi tuichambue. Kama kweli ni mbaya sisi si wajinga tutaona na tutakataa. Tusiukatae mradi kwa kuwa ni wa Bagamoyo, au ulioasisiwa na akina Kikwete, huku tukisingizia yasiyoonekana
Bagamoyo lazima ijengwe.Hatuwezi kuwa wajinga tena.Mnaomshabikia mwendazake jamazeni.Someni ripoti ya CAG jinsi mabilioni yalivyopotea.Ndugai yupo sahihi kabisa.KUMBUKENI HII NI AWAMU YA SITA.
 
VIchwa vibovu.

Katika moja ya mkutano na waandishi habari. Mkurugenzi wa bandari alisema walijadiliana sana na wachina hadi 2018 kuhusu mkataba huo, lakini kuna mambo ambayo China haikutaka kuyaondoa na mazungumzo yakafa. Sasa naona Boss huyu anapiga kampeni kwa vigezo dhaifu kabisa!

Yaani presentation aliyofanyiwa China ndo iwe nzuri kwake kwa miaka 5 iliyopita! Lazima kuna jingie nje ya presentation.
 
Na Thadei Ole Mushi.

Spika wa Bunge kaishangaa Serikali kuanza kutengeneza Reli badala ya Kuanzia na bandari. Si mara ya kwanza Kwa Mh Ndugai kusema kuhusu ujenzi wa BANDARI hii mwaka 2019 alisema hata wachina wanatushangaa na wakatufananisha na MTU aliyetanguliza mkokoteni mbele halafu punda nyuma. Kwa maana ya kwamba kujenga Reli ni kutanguliza Mkokoteni Mbele halafu Punda nyuma.

Wachina wana hamu na ujenzi wa Bandari hiyo kuliko hata watanzania wenyewe. Je ni kweli wachina wanatupenda kiasi hicho?

Fact

Mwaka juzi China ilianza kushikilia mashirika muhimu ya Zambia baada ya Zambia kushindwa kulipa madeni inayodaiwa na China.

China ilishikilia Shirika la Utangazaji la nchi hiyo pamoja na Shirika la Umeme la Zambia (ZESCO) na bado wataendelea kutaifisha mashirika mengine kadri muda utakavyokwenda.

Huko Sri-Lanka nako wameshikilia Bandari ya nchi hiyo kwa Lengo lile lile la kulipa madeni ya China.

John Perkins kupitia kitabu chake Confession of an Economic Hit man anatufunulia jinsi sera ya Conspiracy inavyofanya kazi.

Perkins anaelezea kazi aliyokuwa akiifanya bila yeye kujua kwenye Kampuni la MAIN (Consulting and engineering Company)

Aliajiriwa kama mfanyakazi kwenye kampuni hilo ambalo ni Kampuni binafsi ila shughuli zake ziliathiriwa na mkono wa Serikali (Ujasusi) bila yeye kujua.

Kazi yake kubwa ilikuwa ni kushawishi nchi maskini zikope mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa katika nchi zao. Miradi kama vile ujenzi wa miundombinu ya Reli,Ujenzi ya Umeme ambayo utasaidiwa kukopeshwa aidha na World bank, IMF au USAID.

Perkins alikuja kugundua kuwa njia hii ya kukopesha mikopo mikubwa ambayo hailipiki ni njia mojawapo ya Taifa la Marekani kuendelea kupata maeneo ya kunyonya katika nchi maskini.

Perkins anatoa mifano jinsi alivyofanikisha kuingiza Indonesia kwenye Mtego huo na nchi nyingine nyingi.

Kwa nchi ambazo zinaendelea na zenye rasilimali kama Gesi, Madini na mafuta Marekani huwa hawalali kwenye kuhakikisha inatafuta kuwakopesha.

China nayo imeaanza kunufaika na Sera hii ya conspiracy kila mahali wanajenga ushawishi mkubwa kutoa mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa. Wanajua mikopo hii hailipiki hivyo wanaweza kunufaika wao.

Bandari ya Bagamoyo ikikamilika inafunika zote Afrika Mashariki, hivyo wateja wengi watahamia Bagamoyo ambayo itakuwa inaendeshwa na mchina baada ya sisi kukosa fedha za kumlipa mchina. Najiuliza Je China inaweza kutupenda kwa kiasi hicho? Je tunaweza kumlipa mchina?

Ole Mushi
0712702602
Na Thadei Ole Mushi.

Spika wa Bunge kaishangaa Serikali kuanza kutengeneza Reli badala ya Kuanzia na bandari. Si mara ya kwanza Kwa Mh Ndugai kusema kuhusu ujenzi wa BANDARI hii mwaka 2019 alisema hata wachina wanatushangaa na wakatufananisha na MTU aliyetanguliza mkokoteni mbele halafu punda nyuma. Kwa maana ya kwamba kujenga Reli ni kutanguliza Mkokoteni Mbele halafu Punda nyuma.

Wachina wana hamu na ujenzi wa Bandari hiyo kuliko hata watanzania wenyewe. Je ni kweli wachina wanatupenda kiasi hicho?

Fact

Mwaka juzi China ilianza kushikilia mashirika muhimu ya Zambia baada ya Zambia kushindwa kulipa madeni inayodaiwa na China.

China ilishikilia Shirika la Utangazaji la nchi hiyo pamoja na Shirika la Umeme la Zambia (ZESCO) na bado wataendelea kutaifisha mashirika mengine kadri muda utakavyokwenda.

Huko Sri-Lanka nako wameshikilia Bandari ya nchi hiyo kwa Lengo lile lile la kulipa madeni ya China.

John Perkins kupitia kitabu chake Confession of an Economic Hit man anatufunulia jinsi sera ya Conspiracy inavyofanya kazi.

Perkins anaelezea kazi aliyokuwa akiifanya bila yeye kujua kwenye Kampuni la MAIN (Consulting and engineering Company)

Aliajiriwa kama mfanyakazi kwenye kampuni hilo ambalo ni Kampuni binafsi ila shughuli zake ziliathiriwa na mkono wa Serikali (Ujasusi) bila yeye kujua.

Kazi yake kubwa ilikuwa ni kushawishi nchi maskini zikope mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa katika nchi zao. Miradi kama vile ujenzi wa miundombinu ya Reli,Ujenzi ya Umeme ambayo utasaidiwa kukopeshwa aidha na World bank, IMF au USAID.

Perkins alikuja kugundua kuwa njia hii ya kukopesha mikopo mikubwa ambayo hailipiki ni njia mojawapo ya Taifa la Marekani kuendelea kupata maeneo ya kunyonya katika nchi maskini.

Perkins anatoa mifano jinsi alivyofanikisha kuingiza Indonesia kwenye Mtego huo na nchi nyingine nyingi.

Kwa nchi ambazo zinaendelea na zenye rasilimali kama Gesi, Madini na mafuta Marekani huwa hawalali kwenye kuhakikisha inatafuta kuwakopesha.

China nayo imeaanza kunufaika na Sera hii ya conspiracy kila mahali wanajenga ushawishi mkubwa kutoa mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa. Wanajua mikopo hii hailipiki hivyo wanaweza kunufaika wao.

Bandari ya Bagamoyo ikikamilika inafunika zote Afrika Mashariki, hivyo wateja wengi watahamia Bagamoyo ambayo itakuwa inaendeshwa na mchina baada ya sisi kukosa fedha za kumlipa mchina. Najiuliza Je China inaweza kutupenda kwa kiasi hicho? Je tunaweza kumlipa mchina?

Ole Mushi
0712702602

View attachment 1746890
Kama masharti ni yaleyale we are finished!
 
Na Thadei Ole Mushi.

Spika wa Bunge kaishangaa Serikali kuanza kutengeneza Reli badala ya Kuanzia na bandari. Si mara ya kwanza Kwa Mh Ndugai kusema kuhusu ujenzi wa BANDARI hii mwaka 2019 alisema hata wachina wanatushangaa na wakatufananisha na MTU aliyetanguliza mkokoteni mbele halafu punda nyuma. Kwa maana ya kwamba kujenga Reli ni kutanguliza Mkokoteni Mbele halafu Punda nyuma.

Wachina wana hamu na ujenzi wa Bandari hiyo kuliko hata watanzania wenyewe. Je ni kweli wachina wanatupenda kiasi hicho?

Fact

Mwaka juzi China ilianza kushikilia mashirika muhimu ya Zambia baada ya Zambia kushindwa kulipa madeni inayodaiwa na China.

China ilishikilia Shirika la Utangazaji la nchi hiyo pamoja na Shirika la Umeme la Zambia (ZESCO) na bado wataendelea kutaifisha mashirika mengine kadri muda utakavyokwenda.

Huko Sri-Lanka nako wameshikilia Bandari ya nchi hiyo kwa Lengo lile lile la kulipa madeni ya China.

John Perkins kupitia kitabu chake Confession of an Economic Hit man anatufunulia jinsi sera ya Conspiracy inavyofanya kazi.

Perkins anaelezea kazi aliyokuwa akiifanya bila yeye kujua kwenye Kampuni la MAIN (Consulting and engineering Company)

Aliajiriwa kama mfanyakazi kwenye kampuni hilo ambalo ni Kampuni binafsi ila shughuli zake ziliathiriwa na mkono wa Serikali (Ujasusi) bila yeye kujua.

Kazi yake kubwa ilikuwa ni kushawishi nchi maskini zikope mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa katika nchi zao. Miradi kama vile ujenzi wa miundombinu ya Reli,Ujenzi ya Umeme ambayo utasaidiwa kukopeshwa aidha na World bank, IMF au USAID.

Perkins alikuja kugundua kuwa njia hii ya kukopesha mikopo mikubwa ambayo hailipiki ni njia mojawapo ya Taifa la Marekani kuendelea kupata maeneo ya kunyonya katika nchi maskini.

Perkins anatoa mifano jinsi alivyofanikisha kuingiza Indonesia kwenye Mtego huo na nchi nyingine nyingi.

Kwa nchi ambazo zinaendelea na zenye rasilimali kama Gesi, Madini na mafuta Marekani huwa hawalali kwenye kuhakikisha inatafuta kuwakopesha.

China nayo imeaanza kunufaika na Sera hii ya conspiracy kila mahali wanajenga ushawishi mkubwa kutoa mikopo kwa ajili ya miradi mikubwa. Wanajua mikopo hii hailipiki hivyo wanaweza kunufaika wao.

Bandari ya Bagamoyo ikikamilika inafunika zote Afrika Mashariki, hivyo wateja wengi watahamia Bagamoyo ambayo itakuwa inaendeshwa na mchina baada ya sisi kukosa fedha za kumlipa mchina. Najiuliza Je China inaweza kutupenda kwa kiasi hicho? Je tunaweza kumlipa mchina?

Ole Mushi
0712702602

View attachment 1746890

Thadei Ole Mushi na Ndugai nyie ni wanasiasa ,Je Zitto Mchumi Mbobezi alishauri nini kwenye ujenzi wa bandari ya bwagamoyo?
 
VIchwa vibovu.

Katika moja ya mkutano na waandishi habari. Mkurugenzi wa bandari alisema walijadiliana sana na wachina hadi 2018 kuhusu mkataba huo, lakini kuna mambo ambayo China haikutaka kuyaondoa na mazungumzo yakafa. Sasa naona Boss huyu anapiga kampeni kwa vigezo dhaifu kabisa!

Yaani presentation aliyofanyiwa China ndo iwe nzuri kwake kwa miaka 5 iliyopita! Lazima kuna jingie nje ya presentation.
Kuna mataifa yanaitamani hii nchi vibaya mno, wanatamani hata sote tupotee waje ku dominate. No wonder kila mara JPM alikuwa akisema "mnazani tunapendwa Sana" , kumbe kuna vitu aliviona tokea mbali. Kwa mamikataba ya hovyo, tutajikuta tu nauza nchi vipande vipande kwa unafiki wa Wanasiasa wetu. Shame on you Ndugai.
 
Watanzania kwa nguvu ile ile tuliyotumia kuvunja uzio wa uwanja wa ndege machoni pa vyombo vya ulinzi usalama siku ya kuaga mwili wa JPM tutumie nguvu hiyo hiyo na zaidi kumfirisi Spika Job Ndugai, tunafahamu vitega uchumi vyake kuanzia zile apartment zake nk tuzitie kiberiti, nyumba zake zote na mali tuzichome....tukikalia kucheka na kulalamika watazoea, si mnakumbuka yaliyotokea baada ya Nyerere kufariki jinsi mikataba ya kuchimba madini ilivyosainiwa kwa mwendo kasi....sasa historia inajirudia, upole wetu ni mauti yetu! Tutawaachia watoto wetu na wajukuu mzigo wa madeni!
 
Issue hii inabidi waijadili kwa upana zaidi
Kabla ya kuitekeleza!

Ova
 
Mjadala huu ungenoga zaidi kama huo mkataba mzima ungewekwa katika tovuti ili kila anayependa ausome; kisha tufanye debate sisi wazalendo tunaopinga huu mradi na wale wanaounga mkono huu mradi.

Inasikitisha mradi mbovu kama huu ambao naamini pengine hata chifu Mangungu asingeukubali lakini leo hii unatetewa na watu ambao ni wasomi! Hivi nini kifanyike ili somo la uzakendo liwaingie watanzania wote?
Sasa ndugai ana usomi gani ?
 
"Siku Moja mtanikumbuka, najua mtanikumbuka kwa mazuri sio kwa mabaya, kwa maana na sacrifice maisha yangu kwa ajili ya watanzania masikini". Mchina ni mkoloni ajaye hapa Africa, anatafuta kila jinsi aweke miguu yake kwa kisingizio cha kutusaidia kuwekeza. Hawana huruma kiasi hicho, kwa mwendo huu nchi hii itakuwa kama Enzi za mzee ruksa aka shamba la Bibi. RIP JPM.
Wachina walianza mchezo wao zamani. Hata SA wamevamia hatari na sekta yao huko ni Insurance. Sasa huo mchezo walijaribu Kabanga Nickel ambapo 50% ilikuwa Barrick na 50% Glencore. Terms zao za kijinga Barrick wakagoma kuuza shares zao. Maana nasikia wanaprocess cheap and impure nickel - na kuuza bei ya chini na kufanya soko la nickel kushuka.
 
Hili lipost likubwa uliloweka hapa halina maana yoyote, hawa akina Ndugai wako huko bungeni kwa wizi wa kura na uliona ni sawa uchaguzi ule. Kama watu wameingia bungeni kwa wizi wa kura, unashangaa nini wakiwa na misimamo yenye utata? Subiri uone wezi wa kura watakavyofanya uharibifu ndani ya nchi hii.
Spika Ndugai anavyobadilika haraka kesho unaweza kuskia akitaka Tuvunje Ukuta wa Mererani
 
Naona wameamua kufanya upuuzi kwasababu sheria zipo kwa ajili ya wezi wa kuku tu.

Sasa Ndungai wakiingia kwenye mikataba ya kinyonyaji tutafukua hata kaburi lake na kupiga pingu
Spika Ndugai anavyobadilika haraka kesho unaweza kuskia akitaka Tuvunje Ukuta wa Mererani
 
VIchwa vibovu.

Katika moja ya mkutano na waandishi habari. Mkurugenzi wa bandari alisema walijadiliana sana na wachina hadi 2018 kuhusu mkataba huo, lakini kuna mambo ambayo China haikutaka kuyaondoa na mazungumzo yakafa. Sasa naona Boss huyu anapiga kampeni kwa vigezo dhaifu kabisa!

Yaani presentation aliyofanyiwa China ndo iwe nzuri kwake kwa miaka 5 iliyopita! Lazima kuna jingie nje ya presentation.
Yaaan mtu alionyeshwa picha tu, sijui video ya project jamaa kashawishikaa kaona hapa ndioo penyewe. Akasahaau kuomba kuona hata mkataba wa mradi.
Yaan matumiz mabaya ya akili kbs duu.
 
Mjadala huu ungenoga zaidi kama huo mkataba mzima ungewekwa katika tovuti ili kila anayependa ausome; kisha tufanye debate sisi wazalendo tunaopinga huu mradi na wale wanaounga mkono huu mradi.

Inasikitisha mradi mbovu kama huu ambao naamini pengine hata chifu Mangungu asingeukubali lakini leo hii unatetewa na watu ambao ni wasomi! Hivi nini kifanyike ili somo la uzakendo liwaingie watanzania wote?
Na mimi naafikiana na hili, kwanini wasiutoe public tuone?
 
Kuna mataifa yanaitamani hii nchi vibaya mno, wanatamani hata sote tupotee waje ku dominate. No wonder kila mara JPM alikuwa akisema "mnazani tunapendwa Sana" , kumbe kuna vitu aliviona tokea mbali. Kwa mamikataba ya hovyo, tutajikuta tu nauza nchi vipande vipande kwa unafiki wa Wanasiasa wetu. Shame on you Ndugai.
Hayo ni maneno ya Magufuli kwa wasio na elimu. Tanzania ina rasilimali, lakini si nyingi hivyo, na wala siyo kwamba kila bepari anapatamani Tanzania. Biashara na utajiri si kwa malighafi hizi tu. Wale matajiri wanaoongoza wako kwenye biashara ya tehama, siyo dhahabu au almasi. Kuhusu Bandari ya Bagamoyo, kama wewe umeusoma mkataba tupatie na sisi hapa tuuchambue. Magufuli alishazoea kutupatia hadithi kama zile za kupima korona kwenye mbuzi, kwale na nanasi, je, nani alithibitisha upimaji huo? Lete mkataba hapa!
 
Back
Top Bottom