Nitagombea Urais - Kisandu Deogratius

Nitagombea Urais - Kisandu Deogratius

KISANDU: SIJATUMWA NA CHAMA WALA NA ZITTO.

Baada ya tamko langu la kutaka kugombea urais la jana tarehe 8/10/2012 limeleta sura tofauti na mitazamo tofauti, wengine wakini chafua kwenye mitandao yakijamii na wengine hata kunipigia simu za kunipinga. Wapo wanaosema nimetumwa na CHADEMA ili kupunguza nguvu ya kaka ZITTO ili aonekane wa kawaida sana, wapo wanaosema nimetumwa na ZITTO ili kuendelea kumjengea mazingira, wapo walio sema mimi natoka kanda ya kaskazini na ni mkristu. Haya ni mitazamo ya watu isiyo fanyiwa utafiti kwa kile wanachokisema.

Hivi hii dhana ya mtu akiongea anachofikiri, watu wanasema katumwa, inatokana na nini? kwani mtanzania hawezi kusema mpaka atumwe? Nasema tena NITAGOMBEA URAIS na staacha mpaka kieleweke. Mimi sija tumwa na mtu nimetumwa na Mungu hivyo wamulaumu Mungu. Roho yangu ni kuonesha ukweli kuhusu upendo wangu kwa watanzania wenzangu. Roho ya Kisandu ni nyeupe kama saruji. Upendo wa Kisandu kwa watanzania ni kuwatumikia watanzania, nawashangaa wabunge vijana wanao sema eti vijana wasikurupuke. Wabunge wa aina hii hawawatakii mema watanzania maana hawapendi kuona rutuba ya vijana kama Kisandu tena mwenye uchungu na watanzania.
Mimi sitokei kanda ya kaskazini, nipo huko Tanga kikazi kwa nafasi yangu ya uongozi ndani ya chadema huko Tanga, ambako ndiko na elimu yangu ya chuo kikuu nilikoipatia kabla ya ile ya diploma ya elimu niliyo ipata pale chuo cha ualimu Tabora. Mimi nimzaliwa wa wilaya ya kahama, mkoani shinyanga, tena shule ya msingi mpaka sekondari nimesoma hukohuko. Labda kwasababu niligombea ubunge 2010 jimbo la lushoto(Tanga), wasome katiba vizuri wajue sifa za kugombea Ubunge.

Unajua kundi fulani linakereka sana kutaka kuwa mtumishi wa watanzania, usomi siyo kuvaa tai, suruali za vitambaa, suti au usharobaro bali ni kuhamasisha wananchi ili walete mabadiliko yenye maendeleo na sio kusifia ujinga unaosemwa na kila kiongozi unayemwamini.

Mimi na sikitika sana mtu anaponisema vibaya, ndio maana najiuliza maswali mawili, ni nani anayesema na kwanini anasema? Huenda nayeye si yeye na mimi naweza sema katumwa kuniharibia. Nasema tena hamuwezi kuzuia mipango ya Mungu isitimie, Urais nitagombea maana uhuru na maendeeo huhusiana kama kuku na yai lakini ukiweza kuwa na akili timamu, wakati kila mtu ameigizwa wazimu, wewe ni mtu maarufu. Wananchi watanzania wote wana akili timamu, uozo wa viongozi wao wanauona unaharufu mbaya sana na Plato aliwahi kusema " uovu ni tokeo la kukosa maarifa" sasa viongozi wetu huenda wamekosa maarifa ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayodaiwa na wananchi silalamiki sana lakini nasema tu.

Ni fursa pekee sasa vijana kuikomboa Tanzania na kuepuka na ule upungufu usemao vijana ni taifa la kesho. Nasasa vijana ni Taifa la Leo.

Deogratius Kisandu
Katibu wa Baraza la Vijana wa chadema mkoa wa Tanga.
9 oktoba 2012

Mwana siasa ni lazima awe na ngozi ngumu, sasa wewe jana tu leo umekurupuka kujitetea, ngoja kidogo. Hata hivyo si vibaya kujiridhisha, lakini kazi hiyo kama kwa bahati mbaya kweli utaipata hutaiweza. Furahisha baraza tu. Unafikiri Urais wa nchi ni ukatibu kata ama diwani? Ndugu yangu usipoteze nguvu nyingi katika hili wewe kajaribu ubunge, hata huo ubunge naona hutaupata pia.

Ushauri wa bure, wewe concentrate tu kwenye M4C, achana na mambo ya kugombea uongozi, muda bado mrefu sana. Sisi tutawatambua watu kwa matendo yao sio maneno.
 
KISANDU: SIJATUMWA NA CHAMA WALA NA ZITTO.


Ni fursa pekee sasa vijana kuikomboa Tanzania na kuepuka na ule upungufu usemao vijana ni taifa la kesho. Nasasa vijana ni Taifa la Leo.

Deogratius Kisandu
Katibu wa Baraza la Vijana wa chadema mkoa wa Tanga.
9 oktoba 2012


Sasa kwa nini usisubiri kesho ndo ugombee.Sijakuelewa.TRASH
 
Naona anamwiga mtanga mwenzie Mr. Misosi. Nitoke vipi
 
Huyu mgombea wa urais kanistua kweli kweli! Dah! Yaani ana roho safi kama SARUJI!
 
Sisi tuko katika M4C, nyinyi wenzetu mko katika kugombea Uraisi, tuwaeleweje. Wagombea tuko wengi ila sasa tunatengeneza chama chetu ili mmoja wetu akiteuliwa ashinde. Hivi nyie mchango wenu katika chama ni nini. Mtueleze hata kabla ya huo uraisi.

Charity starts at home.
 
KISANDU: SIJATUMWA NA CHAMA WALA NA ZITTO.

Baada ya tamko langu la kutaka kugombea urais la jana tarehe 8/10/2012 limeleta sura tofauti na mitazamo tofauti, wengine wakini chafua kwenye mitandao yakijamii na wengine hata kunipigia simu za kunipinga. Wapo wanaosema nimetumwa na CHADEMA ili kupunguza nguvu ya kaka ZITTO ili aonekane wa kawaida sana, wapo wanaosema nimetumwa na ZITTO ili kuendelea kumjengea mazingira, wapo walio sema mimi natoka kanda ya kaskazini na ni mkristu. Haya ni mitazamo ya watu isiyo fanyiwa utafiti kwa kile wanachokisema.

Hivi hii dhana ya mtu akiongea anachofikiri, watu wanasema katumwa, inatokana na nini? kwani mtanzania hawezi kusema mpaka atumwe? Nasema tena NITAGOMBEA URAIS na staacha mpaka kieleweke. Mimi sija tumwa na mtu nimetumwa na Mungu hivyo wamulaumu Mungu. Roho yangu ni kuonesha ukweli kuhusu upendo wangu kwa watanzania wenzangu. Roho ya Kisandu ni nyeupe kama saruji. Upendo wa Kisandu kwa watanzania ni kuwatumikia watanzania, nawashangaa wabunge vijana wanao sema eti vijana wasikurupuke. Wabunge wa aina hii hawawatakii mema watanzania maana hawapendi kuona rutuba ya vijana kama Kisandu tena mwenye uchungu na watanzania.
Mimi sitokei kanda ya kaskazini, nipo huko Tanga kikazi kwa nafasi yangu ya uongozi ndani ya chadema huko Tanga, ambako ndiko na elimu yangu ya chuo kikuu nilikoipatia kabla ya ile ya diploma ya elimu niliyo ipata pale chuo cha ualimu Tabora. Mimi nimzaliwa wa wilaya ya kahama, mkoani shinyanga, tena shule ya msingi mpaka sekondari nimesoma hukohuko. Labda kwasababu niligombea ubunge 2010 jimbo la lushoto(Tanga), wasome katiba vizuri wajue sifa za kugombea Ubunge.

Unajua kundi fulani linakereka sana kutaka kuwa mtumishi wa watanzania, usomi siyo kuvaa tai, suruali za vitambaa, suti au usharobaro bali ni kuhamasisha wananchi ili walete mabadiliko yenye maendeleo na sio kusifia ujinga unaosemwa na kila kiongozi unayemwamini.

Mimi na sikitika sana mtu anaponisema vibaya, ndio maana najiuliza maswali mawili, ni nani anayesema na kwanini anasema? Huenda nayeye si yeye na mimi naweza sema katumwa kuniharibia. Nasema tena hamuwezi kuzuia mipango ya Mungu isitimie, Urais nitagombea maana uhuru na maendeeo huhusiana kama kuku na yai lakini ukiweza kuwa na akili timamu, wakati kila mtu ameigizwa wazimu, wewe ni mtu maarufu. Wananchi watanzania wote wana akili timamu, uozo wa viongozi wao wanauona unaharufu mbaya sana na Plato aliwahi kusema “ uovu ni tokeo la kukosa maarifa” sasa viongozi wetu huenda wamekosa maarifa ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayodaiwa na wananchi silalamiki sana lakini nasema tu.

Ni fursa pekee sasa vijana kuikomboa Tanzania na kuepuka na ule upungufu usemao vijana ni taifa la kesho. Nasasa vijana ni Taifa la Leo.

Deogratius Kisandu
Katibu wa Baraza la Vijana wa chadema mkoa wa Tanga.
9 oktoba 2012
Kisandu hebu acha mambo yako ya utani utani bwana,tumeisha cheka inatosha,sasa nakupa ushauri kama kaka yako,CHADEMA kwa Kahama inapendwa sana lakini haijawahi kupata mgombea strong,huyu Lembeli ni Mwepesi sana sema hajapata mpinzani wa uhakika.Hebu jipange 2015 ukagombee ubunge Kahama,USIPOTEZE MUDA KUONGELEA KITU AMBACHO ROHONI UNAJUA NI NGUMU KAMA KUCHOTEA MAJI KWENYE PAKACHA,labda kama unataka uwekwe kwenye historia kama wakina DOVUTWA au MZIRAY kuwa uliwahi kugombea urasi basi.
 
Kisandu hebu acha mambo yako ya utani utani bwana,tumeisha cheka inatosha,sasa nakupa ushauri kama kaka yako,CHADEMA kwa Kahama inapendwa sana lakini haijawahi kupata mgombea strong,huyu Lembeli ni Mwepesi sana sema hajapata mpinzani wa uhakika.Hebu jipange 2015 ukagombee ubunge Kahama,USIPOTEZE MUDA KUONGELEA KITU AMBACHO ROHONI UNAJUA NI NGUMU KAMA KUCHOTEA MAJI KWENYE PAKACHA,labda kama unataka uwekwe kwenye historia kama wakina DOVUTWA au MZIRAY kuwa uliwahi kugombea urasi basi.
Eti mkuu, akazane na M4C halafu tuone mchango wake. Tanga inamshinda, itakuwa Tanganyika?
 
Ni maumbile ya binadamu hatuwezi kuyakwepa kabisa! tuache maumbile ya kibinadamu yachukue asili yake!!! Kwani siku zote watu huvuja jasho,damu hata kupoteza maisha kutafuta mali, ukombozi, au mafanikio ya aina yeyote lakini mafanikio hayo yakishapatikana wanaokuja kufaidi ni wengine kabisa ambao hata ukiwauliza hicho wanachokifaidi sasa asili yake ni wapi hawajui.....!! Kwa maana hiyo hakuna haja ya kupoteza muda kuwakatisha tamaa wanaotaka kula mafanikio ya cdm waacheni kwani hayo ni maumbile ya mwanadamu.
 
Kikwete amafanya urais uwe rahisi kila mtu anatamani kwenda kutalii ulaya na kuvutwa na vitoroli kama jk,kweli hata mimi ninaweza kuwa amiri jeshi mkuu kha!
 
ILA SINA UHAKIKA NA HIYO ROHO YAKO MAANA UMESEMA NI NYEUPE KAMA SARUJI,SINA UHAKIKA HIYO SARUJI NI YA WAPI WAZO HILL AU TANGA CEMENT!!!! nadhani ulitaka kuandika Theluji!!! Au mmeku!!
 
Jamaa ameona akianza na kutaka kugombea URAIS atakuwa ameweka mazingira mazuri ya Ubunge. Jamaa kwanza ajiulize huko Tanga amefanya nini cha Maana cha kumpa ngumu za kuomba uraisi? Yaaani wanaume washinde Vijijini wakipiga M4C halafu wengine waje na matamko ya uraisi. Huu ni ujinga. Leo hii HECHE akisema anataka kugombea uraisi watu wengi sana watamwelewa,kwa sababu jamaa amehamishia makazi yake vijijini akifanya senstaization meeting. Sasa huyu MWEHU ashinde ofisini then aje na ngonjera za uraisi.
 
Mie Nasema kila siku kuwa Na shahada sio kuelimika watu wengine wanabisha Sasa oneni wenyewe..Na bado tutashuhudia mengi tu.. We ngojea muda uzidi kuyoyoma, urais, kila Mtu nataka kuwa rais . Aseeee mie nadhani katiba iruhusu kuwa Na marais Kama hamsini hivi at least kila angle rais.. Kabweka Wa kwamtogole anataka urais, mwatufileni wa mbambabey anautaka urais, Karoli wa magomeni naye anautaka, bado akina Bhasilisa, Budege, Punyetu, Mbano wote wanautaka huo urais, juzi hapa Yule mama Sofia wa Gongolamboto si kadai nae anauwania..

Hivi nani huyo anayegawia watu huo urais si awape tu, tunang'oana meno bure..Mtu akisema nataka kuwa rais Basi watu wanatetemeeeeeka Kumbe mwenzao anamaanishan rais wa shirikisho la vilabu vya pombe Za kienyeji, rais wa wabeba magunia sokoni, rais wa mchezo wa kujificha polipo, rais wa shoe-shine organizesheni, rais wa nanihii.. Soo many President.. Don't worry give them..

Lakini Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hatuwezi kuchagua Punguani Tena..!!
 
Utani na kazi. Hon.President and Commender in Chief Kisandu..Ku.

Ushauri wa Bure:
pamoja na kazi kubwa ya cdm kupitia M4c kuna haja ya kuwa na semina elekezi za safu za uongozi wa chama ngazi zote kutabainisha lengo la chama na mstabakali kwa ujumla towards 2015 !

Isije ikawa watu wanakaza misuli na M4C huku ndoto ni kupata vyeo na c ukombozi wa wanachi.

Tuyasikie tu kwa majirani kunakojengwa mitatandao. CDM needs internal politicisation much as required as mass mobilisation.

kujiunga na CDM tu haitoshi, ni kupewa pia elimu ya siasa ya chama na kuwa muumini.

chukua mfano mtu anapookoka, au kusilimu, haachwi bila mafundisho lukuki!

hii sio demokrasia kutangaza kila asubuhi kuwania uraisi kwa mtu aliyesrious na party cause!
 
Ningekuwa mimi ningetafuta kwanza wa "KUNIFUNDA"!

hovyoooooooooooooooooooooo!:A S embarassed:
 
Muacheni jamani aelezee anachokitaka. Hizo ndio ndoto zake! Time will tell.
 
Back
Top Bottom