Nitagombea Urais - Kisandu Deogratius

Nitagombea Urais - Kisandu Deogratius

Sifa zake kama anamaanisha kugombea urais wa taasisi ya kidini, manake hizo sifa alizojipamba nazo.!
 
Utani na kazi. Hon.President and Commender in Chief Kisandu..Ku.

Ushauri wa Bure:
pamoja na kazi kubwa ya cdm kupitia M4c kuna haja ya kuwa na semina elekezi za safu za uongozi wa chama ngazi zote kutabainisha lengo la chama na mstabakali kwa ujumla towards 2015 !

Isije ikawa watu wanakaza misuli na M4C huku ndoto ni kupata vyeo na c ukombozi wa wanachi.

Tuyasikie tu kwa majirani kunakojengwa mitatandao. CDM needs internal politicisation much as required as mass mobilisation.

kujiunga na CDM tu haitoshi, ni kupewa pia elimu ya siasa ya chama na kuwa muumini.

chukua mfano mtu anapookoka, au kusilimu, haachwi bila mafundisho lukuki!

hii sio demokrasia kutangaza kila asubuhi kuwania uraisi kwa mtu aliyesrious na party cause!

Kaka.. Unaweza kupinda ulimi kumshauri Mtu ukadhani ana weledi lau kiduchu Wa kusikia, Kumbe ukaambulia 00. Embu ona, Kwa Jotoridi la mvumo wa kisiasa Na Ujenzi wa chama unaoendelea Haijuzu Mtu timam akaingiza kitu kipya Kwenye bongo Za watu ilihali pana Movement inayoendelea ya kujenga chama.. Mbona Muda upo tu ambapo secretariat ya chama itapanga kila mwenye dukuduku ataliwasilisha hapo.. Why now talking loudly.. Hii inaitwa Nini ..
 
Kikwete amafanya urais uwe rahisi kila mtu anatamani kwenda kutalii ulaya na kuvutwa na vitoroli kama jk,kweli hata mimi ninaweza kuwa amiri jeshi mkuu kha!

Jamani mbav zetu wengine.. Ha ha haaaa.. Imagine kila kona Kati ya Mtu Tisa mmoja lazima apwayuke kuutaka urais.. Aisee..
 
With all due respect this must be presidential silly season for seeking political credits which may be will help to polish the name up the ladder. Let us wait and see if the mission will hold water tightly after being accomplished. Samahani lakini.

Sent from BlackBerry 8520 authorized by JamiiForums.
 
Mimi nitaendelea kulia na Kamati Kuu CDM mpaka pale watakapotoa mwongozo kuhusu hizi fujo za watu wasiojua kupima upepo.Kamati kuu mnaweza kuwapuuza hawa wanaoleta ujinga chamani lakini niwahakikishie sisi tunaokaa huku chini na wanachama wanakereka kupita maelezo.Kuna mwanachama mmoja aliniambia juzi kwa masikitiko makubwa kwamba.....'CDM sasa wanachukua njia ileile ya CCM ya kugawa chama chao vipandevipande'....Haya ni maneno mazito sana..Tafakarini enyi Kamati Kuu....
 
Nyie "gombeeni", wajanja tutauchukua hata bila "kugombea".

Basi mwenzenu nilikuwa nachangia sred nikidhani iko makini kumbe mweshimiwa kaamua kuweka Comedian JF.. Manake kila comment nayosoma unacheka hadi mbav zinananihii.. Nyie watu acheni kuweka post Za Vituko..
 
Watu wakini wanafikiria kukijenga chama hasa vijijini - usiku na mchana wapo kuhimiza watu kujiunga na CDM, wengine wamekaa tu wakifikiria urais - kweli duniani kuna watu.

Kabla ya kufikiria Urais kwa tiketi ya CDM (Chama ambacho kinakuwa kwa kasi na kinapendwa na wananachi) Jiulize umekisaida nini ili kiingie madarakani 2015?

Urais CDM si hoja ya msingi kwa sasa watu watawashangaa sana wakati watu wanapanda mbegu shambani wewe na mwenzako mnapiga mahesabu ya kulangua mazao. Hoja kwa sasa ni kwa namna gani chama kitawafikia watanzania walioko vijijini hasa ukizingatia Jiografia ya nchi yetu.

Sasa chama kikiwa tayari basi tunakaa na tunamchagua mwakilishi wetu atakaye peperusha bendera ya chama. hatuzuii wanachama kuchukua kutoa maoni yake ila huu si muda muafaka. kwa sasa tunataka mchango wako mwenye M4C.

Watu wanapigwa mabomu huko kwenye harakati za ukombozi wewe na mwenzako mko ofisini mnasubiria urais --shame.
 
KISANDU: SIJATUMWA NA CHAMA WALA NA ZITTO.

Baada ya tamko langu la kutaka kugombea urais la jana tarehe 8/10/2012 limeleta sura tofauti na mitazamo tofauti, wengine wakini chafua kwenye mitandao yakijamii na wengine hata kunipigia simu za kunipinga. Wapo wanaosema nimetumwa na CHADEMA ili kupunguza nguvu ya kaka ZITTO ili aonekane wa kawaida sana, wapo wanaosema nimetumwa na ZITTO ili kuendelea kumjengea mazingira, wapo walio sema mimi natoka kanda ya kaskazini na ni mkristu. Haya ni mitazamo ya watu isiyo fanyiwa utafiti kwa kile wanachokisema.

Hivi hii dhana ya mtu akiongea anachofikiri, watu wanasema katumwa, inatokana na nini? kwani mtanzania hawezi kusema mpaka atumwe? Nasema tena NITAGOMBEA URAIS na staacha mpaka kieleweke. Mimi sija tumwa na mtu nimetumwa na Mungu hivyo wamulaumu Mungu. Roho yangu ni kuonesha ukweli kuhusu upendo wangu kwa watanzania wenzangu. Roho ya Kisandu ni nyeupe kama saruji. Upendo wa Kisandu kwa watanzania ni kuwatumikia watanzania, nawashangaa wabunge vijana wanao sema eti vijana wasikurupuke. Wabunge wa aina hii hawawatakii mema watanzania maana hawapendi kuona rutuba ya vijana kama Kisandu tena mwenye uchungu na watanzania.
Mimi sitokei kanda ya kaskazini, nipo huko Tanga kikazi kwa nafasi yangu ya uongozi ndani ya chadema huko Tanga, ambako ndiko na elimu yangu ya chuo kikuu nilikoipatia kabla ya ile ya diploma ya elimu niliyo ipata pale chuo cha ualimu Tabora. Mimi nimzaliwa wa wilaya ya kahama, mkoani shinyanga, tena shule ya msingi mpaka sekondari nimesoma hukohuko. Labda kwasababu niligombea ubunge 2010 jimbo la lushoto(Tanga), wasome katiba vizuri wajue sifa za kugombea Ubunge.

Unajua kundi fulani linakereka sana kutaka kuwa mtumishi wa watanzania, usomi siyo kuvaa tai, suruali za vitambaa, suti au usharobaro bali ni kuhamasisha wananchi ili walete mabadiliko yenye maendeleo na sio kusifia ujinga unaosemwa na kila kiongozi unayemwamini.

Mimi na sikitika sana mtu anaponisema vibaya, ndio maana najiuliza maswali mawili, ni nani anayesema na kwanini anasema? Huenda nayeye si yeye na mimi naweza sema katumwa kuniharibia. Nasema tena hamuwezi kuzuia mipango ya Mungu isitimie, Urais nitagombea maana uhuru na maendeeo huhusiana kama kuku na yai lakini ukiweza kuwa na akili timamu, wakati kila mtu ameigizwa wazimu, wewe ni mtu maarufu. Wananchi watanzania wote wana akili timamu, uozo wa viongozi wao wanauona unaharufu mbaya sana na Plato aliwahi kusema “ uovu ni tokeo la kukosa maarifa” sasa viongozi wetu huenda wamekosa maarifa ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayodaiwa na wananchi silalamiki sana lakini nasema tu.

Ni fursa pekee sasa vijana kuikomboa Tanzania na kuepuka na ule upungufu usemao vijana ni taifa la kesho. Nasasa vijana ni Taifa la Leo.

Deogratius Kisandu
Katibu wa Baraza la Vijana wa chadema mkoa wa Tanga.
9 oktoba 2012


You are talking absolutely NONSENSE!
What qualifications do you have? Kawaida kila chama kina utaratibu wa kupata mgombea wake wa urais. Sijui mwenzetu utakuwa umepitishwa na nani kugombea huo Urais mwaka 2015 kupitia CDM.
Yaawezekana kabisa umetumwa na maadui wa CDM ili kujaribu kuleta chokochoko na vurugu ndani ya chama.

Natilia shaka kwamba yamkini wewe inawezekana kabisa ukawa ni mamluki wa CCM. Ngoja tusubiri hatima ya madai yako.
 
Nimtume nani aende?Unitume mimi nitume BWANA.Nitakwena kutangaza neno lako wewe,mataifa yasikie yakufuate wewe.Unitume mimi nitume Bwana.
 
bado rafiki yangu SHIBUDA, yeye hautaki urais?
 
Mkuu Ritz;
Haya mgombea mwingine huyu tuone mwenyekiti Mtei atasemaje

Chama
Gongo la mboto DSM
 
JF nadhani sasa ipange utaratibu wa kutoza gharama za matangazo kama haya, familia ya Nyerere wao tayari wanatoza tozo kuangalia kaburi, natumaini uongozi wa JF hii ni fursa yenu sasa na si watu kutangaza majina yao bure.
 
You are talking absolutely NONSENSE!
What qualifications do you have? Kawaida kila chama kina utaratibu wa kupata mgombea wake wa urais. Sijui mwenzetu utakuwa umepitishwa na nani kugombea huo Urais mwaka 2015 kupitia CDM.
Yaawezekana kabisa umetumwa na maadui wa CDM ili kujaribu kuleta chokochoko na vurugu ndani ya chama.

Natilia shaka kwamba yamkini wewe inawezekana kabisa ukawa ni mamluki wa CCM. Ngoja tusubiri hatima ya madai yako.
Aisee umekwenda mbali sana, ni kwanini unampromote sisimizi kama huyo? ana uwezo upi wa kuleta chokochoko ndani ya chama? labda awaletee choko choko wasambaa huko Tanga wamtandike tu.
 
Kuna watu vibuyu kweli kweli.
Yani watu wanapanda mazao wewe unafikiria kuyavuna...hata palizi na kupiga dawa hufikirii...
Majanga haya!!
 
Mimi nachukuwa fomu ya kugombea uenyekiti wa CCM Taifa.

Karibu sana ugombee CCM ni chama cha kidemokrasia haiongozwi kwa maamuzi ya baba mkwe; kama una sifa za kutosha njoo kwenye chama huru

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Mimi nachukuwa fomu ya kugombea uenyekiti wa CCM Taifa.

Hahahahaha thubutu yake..... Kile ni cheo cha mtu mmoja kwa 10yrs bila kupingwa wala kuleta vyoko vyoko......demokrasia ya CCM hiyo.
 
Bora hapa umejaribu kuongea mwenyewe bila kumuita ritz, nimependa haya maendeleo.

Karibu sana ugombee CCM ni chama cha kidemokrasia haiongozwi kwa maamuzi ya baba mkwe; kama una sifa za kutosha njoo kwenye chama huru

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Back
Top Bottom