Nitagombea Urais - Kisandu Deogratius

Baba Clara

Member
May 10, 2011
94
27
NITAGOMBEA URAIS

Watanzania wanahitaji MABADILIKO na MABADILIKO haya hayawezi kuja bila Watanzania KUAMUA. Na bila Mtanzania mmoja kujitoa kuongoza MABADILIKO haya, na mimi ni mmoja wao. Nimedhamiria, ninaweza kuwa raisi wa Tanzania leo, kesho au keshokutwa. Watanzania wanahitaji kujua KISANDU Deogratius ni nani?Anafanya nini na ana malengo gani kwa mustakabali wa Taifa la Tanzania.

Mwalimu Nyerere alipewa mamlaka makubwa ya kuongoza nchi yetu akiwa hajawahi kushika madaraka makubwa serikalini kama Uwaziri (kabla ya uhuru), na wala hajawahi kuwa Mbunge lakini aliweza kuwaunganisha watanzania na kupata uhuru wa kisiasa. Sasa ni wakati wa kufanya mageuzi ya kiuchumi. Kazi hii lazima iongozwe na Mtanzania Mmoja na mimi ni mmoja wao ambaye sijawahi kuwa Mbunge wala Waziri zaidi ya uongozi ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Tulidhani Marais ambao wameliongoza Taifa letu wakiwa na uzoefu wa Ubunge, Uwaziri n.k. kabla ya kupata nafasi ya Urais wangeweza kuliongoza Taifa hili kwa ufanisi zaidi kushinda Mwalimu Nyerere lakini badala yake wameonyesha udhaifu mkubwa ambao unatupa tafsiri kwamba taifa hili halihitaji kiongozi wenye uzoefu mkubwa bali kiongozi mwenye maono, umakini, uadilifu na hofu ya Mungu.

Mwanasiasa yoyote mwenye kipaji na maono hawazi jana na leo, anawaza jana, leo, kesho, keshokutwa na mtondogoo n.k. Jambo la msingi ni kutazama ni kwa jinsi gani tunaweza kupata UKOMBOZI WA PILI WA TAIFA LETU.

NIMEDHAMIRIA, NINAWEZA, Nitagombea Urais

Deogratius KISANDU
Katibu Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA)
Mkoa wa Tanga
3 Octoba 2012
 
kuna maraisi wa taasisi mbalimbali , labda hata anautaka uraisi wa CHAWAPUTA ..............TEH TEH
 

Mwalimu Nyerere ....... aliweza kuwaunganisha watanzania na
kupata uhuru wa kisiasa. Sasa ni wakati wa kufanya mageuzi ya kiuchumi.

Ukimsoma vizuri Bwana Deogratius KISANDU, hupati shida kuelewa kuwa, pamoja na kuwa ni haki ya kila mmoja Kikatiba kugombea Uongozi, lakini Kisandu katika hili hana tofauti na Nape Nnauye-Vuvuzela! Kisandu ni sawa na speaker inaakisi na kuvumisha sauti na maneno isiyoyaasisi (angalia maneno yenye rangi nyekundu na bluu utanielewa) Na hii ni mkakati mzuri wa kuyeyusha dhamira iliyomo ndani ya muasisi wa matangazo na matamko ya Urais, Ujana na Uraisi, Ujana na Ujenzi wa Uchumi, Uzee na Uhuru, n.k
 
Ukimsoma vizuri Bwana Deogratius KISANDU, hupati shida kuelewa kuwa, pamoja na kuwa ni haki ya kila mmoja Kikatiba kugombea Uongozi, lakini Kisandu katika hili hana tofauti na Nape Nnauye-Vuvuzela! Kisandu ni sawa na speaker inaakisi na kuvumisha sauti na maneno isiyoyaasisi (angalia maneno yenye rangi nyekundu na bluu utanielewa) Na hii ni mkakati mzuri wa kuyeyusha dhamira iliyomo ndani ya muasisi wa matangazo na matamko ya Urais, Ujana na Uraisi, Ujana na Ujenzi wa Uchumi, Uzee na Uhuru, n.k

Ina maana mkuu huyu bwana kuna mtu anamsemea?
 
Mbeya wanasema rais wao ni sugu, kuna wanacdm wengine wanataka Lema agombee pia. Sasa kama watz wamefikia kuchagua hawa wawili basi hata mbuzi ana haki ya kugombea.ni haki yake huyu jamaa.
 
Aah, kweli cdm kuna demokrasia yaani kila mtu anatangaza nia ya kugombea Urais, wangekuwa hao wanaotangaza kuwania wapo ccm wangekiona cha moto, wamuulize shibuda'
 
.... more to come so as to pre-empty ZZK
Umeusoma vema mchezo. Kama ni somo umepata 100/100
Rais.jpg
 
Mbeya wanasema rais wao ni sugu, kuna wanacdm wengine wanataka Lema agombee pia. Sasa kama watz wamefikia kuchagua hawa wawili basi hata mbuzi ana haki ya kugombea.ni haki yake huyu jamaa.

MH!Lema?
 
Ni haki yake kutangaza.Siku hizi hata wanywa gongo wanaweza kutangaza nia.Haya Twende...Wa pili huyo...Mwingine!....
 
Back
Top Bottom