Nitagombea ubunge Jimbo la Segerea – Dar es Salaam

Nitagombea ubunge Jimbo la Segerea – Dar es Salaam

Mtatiro unazijua changamoto za Tabata?

Unaweza kuzitaja na utazitatuaje?
 
uache zile zako za kulalamika na kila kitu kibaya..watu kama nyie hata mkishindwa kitu hutafuta wa kumlaumu badala ya kutafuta suluhu..tabia badili lazima uwe na macho mawili la baya na la zuri sio jicho moja tu la mabaya na mazuri huyaoni ili hali wengine wanayaona watu watakuona mlalamishi na walalamishi si wajenzi maana wao failure zao hutafuta mtu wa kumlaumu nazo chukua hii kama uko serious
 
Sio kama, ndio ukweli wenyewe!, kama ilivyo kwa Ubungo nako wanatoka mkoa fulani.

My Take.
Mtatiro anachagulika zaidi kuliko Mpendazoe!.
Mtatiro ni born and breed in opposition, Mpendazoe ni CCM aliyepotezwa maboya na CCJ, akajiunga Chadema because he had no option!, na amino nawaambie saa hizi anajuta!, anatamani kurudi zake CCM, ndio maana hasikiki kabisa katika harakati!, hivyo kama ni kweli bado ana nia na opposition, ashauriwe aende Kishapu. Jimbo la Segerea ni la Mtatiro!.

Kwa majimbo ya Dar es Salaam, karibu yote yatakwenda UKAWA isipokuwa Ilala! na Kigamboni!.

Pasco.
Kwani Mpendazoe bado yupo?
 
Kwani Mpendazoe bado yupo?
Kwa vile siku hizi wanasiasa wana hama kwa kujitangaza, Mpendazoe bado yupo Chadema kwa vile hajatangaza vinginevyo!, ila ukimya wake tuu ndio unanishangaza na kunipa maswali bila majibu!.

Pasco
 
Julius Mtatiro

Umeandika mambo ya msingi sana isipokuwa moja tu la idadi ya mitaa tuliyoshinda UKAWA uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kwa majimbo ya UKONGA na SEGEREA.

Kumbukumbu nilizo nazo zinaonyesha kama ifuatavyo:
UKONGA:
CHADEMA MITAA 10 (WENYEVITI)
CUF MITAA 4 (WENYEVITI)

SEGEREA:
CHADEMA MITAA 16 (WENYEVITI)
CUF MITAA 11 (WENYEVITI)

Kwa Majimbo yote mawili msimamo upo hivi:
CHADEMA MITAA 26
CUF MITAA 15

Sasa hiyo mitaa 33 unayoisema sijui umeipata wapi kiongozi na kwamba cuf ndiyo ina mitaa mingi kuliko Chadema nalo sio kweli hata kidogo.

Ni muhimu ukapitia upya kumbukumbu zako ili kuondosha mkanganyiko na upotoshaji uliotokea ktk mabandiko yako.

Mmeanza kunyukana mapema na sasa mnabishana nani ana mitaa mingi na nani hana, mwisho wa siku kila mmoja atataka kusimama kivyake na huo ndio utakuwa mwisho wenu.

Kwa majimbo yote CCM imeshinda kwa % ngapi vs UKAWA?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu yangu JAKACKSERU,

Hata hiyo UKONGA ina wagombea wazuri tu wa CHADEMA akiwemo Kamanda Mwita Waitara, ngoja tusubiri kujua UKAWA inagawanaje majimbo ndipo tutahitimisha masuala haya. Lakini kwa namna nilivyojipanga sitakuwa na kinyongo kumuunga mkono mgombea yeyote wa UKAWA ikiwa atapitishwa kugombea Segerea.

Sina tabia ya kupigania madaraka kwa sababu najua kuna masuala mengi ya kufanya kuliko kuongoza. Jambo la msingi ni kuwa UKAWA itapata mgombea imara SEGEREA. Wana Segerea wameichoka CCM na wanahitaji kiongozi imara zaidi, ukiongea nao wanakueleza hawachagui chama, watahitaji kuwa na kiongozi imara kutoka chama chochote kati ya vyama vyetu na kwamba huyo ndiyo chaguo lao. Mimi ni mmoja wa watu wanaohitaji ridhaa hiyo na wapo wenzangu, sote tutapimwa, atakayepitishwa tutampigania.

Na jambo la mwisho unalopaswa kujua ni kuwa vyama vya CHADEMA na CUF vinahitajiana mno UKONGA na ukiangalia hata matokeo ya serikali za mitaa utagundua kuwa kati ya mitaa takribani 33 ya UKAWA, CUF ndiyo ina mitaa mingi. Hii ndo hali ya kisissa ya sasa. Lakini CUF kuwa na mitaa mingi SEGEREA mwaka 2014 au CHADEMA kupata kura nyingi za ubunge mwaka 2010 siyo hoja ya vyama hivi viwili kuweka u-vyama wao mbele na kusahau ushirikiano.

UKAWA ikiweka mgombea mmoja Segerea itashinda kwa kishindo. Ikivurugana na kila chama kikajiwekea mgombea sote tutaanguka.

Ni hayo tu.

J. Mtatiro.
Hapo sasa unatetea kwa uongo ili uonekane ukweli,Segerea CDM ilipata viti vingi vya mitaa uchaguzi uluopita kuliko CUF. Tetea wewe kuwa na sifa za kuteuliwa kupitia UKAWA,lakini usitake kutaguta sifa kwa kusema uongo ilhali hata kwenye uchaguzi wenyewe hukushiriki hata kwenye harakati kusaidia kupata hivyo viti vya serikali za mitaa.
 
NITAGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SEGEREA – DAR ES SALAAM.


Ndugu zangu, kesho Jumatatu 09 Machi 2015 saa 4.00 asubuhi, nitachukua fomu ya kuwania ubunge katika jimbo la Segerea kama ambavyo taratibu za ndani ya chama changu zinaruhusu. Hakutakuwa na mbwembwe vifijo wala nderemo kwa sababu bado hatutajajua kwa hapa Dar Es Salaam jimbo gani litaachwa kwa chama gani au ikiwa wagombea wa vyama vyote vya UKAWA watakutanishwa na kupigiwa kura ya maoni, vyovyote vile iwavyo niko tayari kukabiliana na demokrasia ya ndani ya chama changu na hata ndani ya UKAWA.

Hivi sasa nina umri wa miaka 32 tu lakini nikiwa nimepitia kila aina ya uzoefu wa kiuongozi, kisiasa n.k. Naamini kuwa nina uzoefu wa kutosha kuwavusha wana Segerea mahali ambako nimeishi kwa takribani miaka 12 huku shughuli zangu zote za ujasiriamali zikiwa jimboni humu. Ninalifahamu jimbo hili vizuri, watu wake, matatizo yao na changamoto zinazowakabili. Zaidi ya yote nina uwezo wa kushirikiana na wananchi tukioneshana njia ya kuzitatua changamoto hizi na wakati ukifika nitazieleza huku nikiweka wazi njia za kupita.

Pamoja na kwamba nina elimu ya darasani ya kutosha, uzoefu wa uongozi usio na shaka na tabia na mienendo ya maadili huku nikiwapenda watu wa kila namna, natambua kuwa kazi ya kuwa mbunge ni zaidi ya hayo, inahitaji weledi, wepesi, staha na heshima, kujali, kuwa karibu na watu na kujitolea kwa hali na mali kuwapigania wale ambao haki zao na mahitaji yao yanacheleweshwa – kaliba ya namna hii imejengeka na sina shaka kuwa ninakidhi sifa na vigezo hivi vya nyongeza.

Mimi ni muumini wa demokrasia, nitasaidia wagombea wote waliojitokeza kunipinga na kushindana nami ikiwa kutakuwa na haja hiyo, sitamtukana wala kumsema vibaya yeyote yule, kazi yangu kuelekea Oktoba ni kujinadi na kueleza sifa zangu na uwezo wangu huku nikivihusianisha na utatuzi wa matatizo ya wananchi wa Segerea kwa kushirikiana na wananchi.

Nawaomba wanachama wengine wa vyama vya UKAWA wenye sifa, vigezo na uwezo wajitokeze kwa wingi. Sote tutapimwa kwa uwezo na vigezo vyetu na mwisho wa siku atapatikana mmoja wetu na ataungwa mkono na sisi sote. Baada ya Oktoba 2015, Segerea itakuwa na mpambanaji mpya, mbunge wa wananchi na atakayepigana hadi tone la mwisho la damu kwa ajili ya wananchi wake. Na labda mtu huyo atakuwa ni mimi.

Nawatakia kila la heri na kwa ambao wangependa kunifahamu zaidi wanaweza kusoma katika kiunganishi hiki https://www.facebook.com/JuliusSundayMtatiro/posts/578218822317742:0

Julius Mtatiro,
+255 787 536 759, 0755 855 144, Juliusmtatiro@yahoo.com

Sasa ninaanza kuamini kwamba kweli huu MUUNGANO wa UKAWA hautafika popote kabla ya kuvunjika na kusambaratika kwasababu ya UROHO wa madaraka!

Kama Viongozi wa juu wa vyama kama huyu Julius Mtatiro hawajui hata makubaliano yanayounda umoja wa UKAWA kuhusu kuachiana majimbo, Je wanachama wengine hali itakuwaje?!

Nitataja makubaliano mawili tu ya UKAWA kuachiana majimbo, ambayo nilikuwa nafikiri yatakuwa kwenye finger tips za Julius Mtatiro. Make no mistake I have nothing against Mtatiro, lakini ninasimamia principles.

Makubaliano No 1. Majimbo yote yanayongozwa na chama kinachounda UKAWA. Chama hicho ndiyo kitakuwa na jukumu la kumteua mgombea atakayepeperusha bendera ya UKAWA. Maana yake nini? Majimbo ya Ubungo, Kawe CHADEMA ndiyo kitakuwa na jukumu la kumteua mgombea atakayepeperusha bendera ya UKAWA. Vivyo hivyo kwa Kasulu NCCR Mageuzi, Wawi CUF etc

Makubaliano no 2. Majimbo ambayo yanaongozwa na CCM, ambapo 2010 vyama vinavyounda UKAWA vilisimamisha wagombea, chama kilichoshika nafasi ya pili nyuma ya CCM ndiyo kitapewa jukumu la kumteua mgombea atakayepeperusha bendera ya UKAWA. Maana yake nini? Katika Jimbo la Segerea 2010 chama kilichoshika nafasi ya pili nyuma ya CCM ni CHADEMA. Hivyo kutokana na matokeo hayo Chama chenye Jukumu la kumteua mgombea wa UKAWA ni CHADEMA sio CUF ya Julius Mtatiro, kama makubaliano hayo yatafuatwa kama yalivyo.

MAONI YANGU. Kama kweli viongozi wa UKAWA wako serious na muungano huu, inabidi watoe/waweke wazi makubaliano hayo kwa wanachama na wapenzi wao nchi nzima, mapema sana iwezekanavyo ili kuondoa chaos. Kama kiongozi wa juu kama Julius Mtatiro hajui hayo makubaliano, huko kwenye majimbo kwenye wanachama wa kawaida hali iko je, itakapofika wakati wa kuachiana majimbo. Tatizo viongozi wa nchi hii huwa hawa learn through history, hali hii ilitakiwa kushugulikiwa mapema tu na UKAWA, baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa serikali za mitaa kwani ilishaanza kujitokeza.

Pili viongozi wa UKAWA wanatakiwa ku stick kwenye makubaliano yanayounda UKAWA bila kuangalia SURA YA MTU au WADHIFA wa mtu katika kutekeleza makubaliano waliyojiwekea. Kama wakianza kuhamisha post za magoli eti kwasababu huyu ni Mtatiro, Ben Saanane (no offense intended), make no mistake hawatafika popote. Mind you CCM is watching you, kwasababu kusambaratika kwa UKAWA ndiyo KARATA ya mwisho itakayowaokoa CCM.

You can just ignore my plea/advise at your own peril, But you have been warned!
 
Mmeanza kunyukana mapema na sasa mnabishana nani ana mitaa mingi na nani hana, mwisho wa siku kila mmoja atataka kusimama kivyake na huo ndio utakuwa mwisho wenu.

Kwa majimbo yote CCM imeshinda kwa % ngapi vs UKAWA?

Hakuna minyukano yoyote hapa, kinachotokea ni kuwekana sawa tu ili kila mmoja afahamu na kutambua nani ni nani katika majimbo haya mawili ya Segerea na Ukonga.

Lakini pia hii ni kumsaidia ili apate takwimu sahihi mapema ili ikitokea amekabidhiwa kijiti cha UKAWA awe anafahamu ni kwa kiwango gani Ukawa ina support ya wananchi katika jimbo husika.
 
Maswali mawili tu Mtatiro:

Je kwa nini umechagua jimbo Segerea na isiwe majimbo mengine ya Dar es Salaam?
Je Chama chako kinakubalika kiasi gani jimboni humo kuringanisha na vyama vingine vinavyounda UKAWA?

Reference: Unaweza kutumia kura za uchaguzi mkuu 2010, na huu wa serikali za mtaa.
 
Kila la heri.hivi sasa ni saan nne kasoro dakika5 natumaini upo njiani kwenda kuchukua fomu.
 
Hakuna minyukano yoyote hapa, kinachotokea ni kuwekana sawa tu ili kila mmoja afahamu na kutambua nani ni nani katika majimbo haya mawili ya Segerea na Ukonga.

Lakini pia hii ni kumsaidia ili apate takwimu sahihi mapema ili ikitokea amekabidhiwa kijiti cha UKAWA awe anafahamu ni kwa kiwango gani Ukawa ina support ya wananchi katika jimbo husika.

Exactly. museee!
 
Duh!
Nitasikitika sana UKAWA mkisambaratika kwa sababu ya kugombea majimbo.

Punguzeni ubinafsi tafadhali; na zingatieni makubaliano mliyojiwekea.
 
Mtatiro nakukubali sana...Tangu tuko chuo kikuu...Kamanda nenda kamanda
 
Si kosa kwa manachama yeyote anayeunda UKAWA kutangaza nia kuwania Udiwani, Ubunge na URAIS kwa muda huu.

Navyojua mimi, makubaliano ya UKAWA ni kwamba kila chama kitafuata taratibu zote za michakato yao ndani ya vyama kama katiba zao zinavyotamka kuwapata wagombea wote kuanzia ngazi ya Udiwani hadi RAIS.

Baaba ya hapo vyama hivi vinavyounda UKAWA vitakutana, kwa kufuata makubaliano yao basi watafikia uteuzi wa mgombea mmoja atakayewakilisha UKAWA katika kila nafasi.

Alichofanya Mtatiro ni kutanganza nia kugombea ubumbe jimbo la Segerea kwa tiketi ya chama chake - hii ni hatua ya awali ndani ya chama chake, kwa mantiki hiyo hajakiuka chochote kile kinachohusu UKAWA.
 
Back
Top Bottom