Sasa ninaanza kuamini kwamba kweli huu MUUNGANO wa UKAWA hautafika popote kabla ya kuvunjika na kusambaratika kwasababu ya UROHO wa madaraka!
Kama Viongozi wa juu wa vyama kama huyu Julius Mtatiro hawajui hata makubaliano yanayounda umoja wa UKAWA kuhusu kuachiana majimbo, Je wanachama wengine hali itakuwaje?!
Nitataja makubaliano mawili tu ya UKAWA kuachiana majimbo, ambayo nilikuwa nafikiri yatakuwa kwenye finger tips za Julius Mtatiro. Make no mistake I have nothing against Mtatiro, lakini ninasimamia principles.
Makubaliano No 1. Majimbo yote yanayongozwa na chama kinachounda UKAWA. Chama hicho ndiyo kitakuwa na jukumu la kumteua mgombea atakayepeperusha bendera ya UKAWA. Maana yake nini? Majimbo ya Ubungo, Kawe CHADEMA ndiyo kitakuwa na jukumu la kumteua mgombea atakayepeperusha bendera ya UKAWA. Vivyo hivyo kwa Kasulu NCCR Mageuzi, Wawi CUF etc
Makubaliano no 2. Majimbo ambayo yanaongozwa na CCM, ambapo 2010 vyama vinavyounda UKAWA vilisimamisha wagombea, chama kilichoshika nafasi ya pili nyuma ya CCM ndiyo kitapewa jukumu la kumteua mgombea atakayepeperusha bendera ya UKAWA. Maana yake nini? Katika Jimbo la Segerea 2010 chama kilichoshika nafasi ya pili nyuma ya CCM ni CHADEMA. Hivyo kutokana na matokeo hayo Chama chenye Jukumu la kumteua mgombea wa UKAWA ni CHADEMA sio CUF ya Julius Mtatiro, kama makubaliano hayo yatafuatwa kama yalivyo.
MAONI YANGU. Kama kweli viongozi wa UKAWA wako serious na muungano huu, inabidi watoe/waweke wazi makubaliano hayo kwa wanachama na wapenzi wao nchi nzima, mapema sana iwezekanavyo ili kuondoa chaos. Kama kiongozi wa juu kama Julius Mtatiro hajui hayo makubaliano, huko kwenye majimbo kwenye wanachama wa kawaida hali iko je, itakapofika wakati wa kuachiana majimbo. Tatizo viongozi wa nchi hii huwa hawa learn through history, hali hii ilitakiwa kushugulikiwa mapema tu na UKAWA, baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa serikali za mitaa kwani ilishaanza kujitokeza.
Pili viongozi wa UKAWA wanatakiwa ku stick kwenye makubaliano yanayounda UKAWA bila kuangalia SURA YA MTU au WADHIFA wa mtu katika kutekeleza makubaliano waliyojiwekea. Kama wakianza kuhamisha post za magoli eti kwasababu huyu ni Mtatiro, Ben Saanane (no offense intended), make no mistake hawatafika popote. Mind you CCM is watching you, kwasababu kusambaratika kwa UKAWA ndiyo KARATA ya mwisho itakayowaokoa CCM.
You can just ignore my plea/advise at your own peril, But you have been warned!