Nitagombea ubunge Jimbo la Segerea – Dar es Salaam

Nitagombea ubunge Jimbo la Segerea – Dar es Salaam

Ngoja na mimi nitangaze nia....
Kumbe Segerea ni parahisi eeh
 
NITAGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SEGEREA – DAR ES SALAAM.


Ndugu zangu, kesho Jumatatu 09 Machi 2015 saa 4.00 asubuhi, nitachukua fomu ya kuwania ubunge katika jimbo la Segerea kama ambavyo taratibu za ndani ya chama changu zinaruhusu. Hakutakuwa na mbwembwe vifijo wala nderemo kwa sababu bado hatutajajua kwa hapa Dar Es Salaam jimbo gani litaachwa kwa chama gani au ikiwa wagombea wa vyama vyote vya UKAWA watakutanishwa na kupigiwa kura ya maoni, vyovyote vile iwavyo niko tayari kukabiliana na demokrasia ya ndani ya chama changu na hata ndani ya UKAWA.

Hivi sasa nina umri wa miaka 32 tu lakini nikiwa nimepitia kila aina ya uzoefu wa kiuongozi, kisiasa n.k. Naamini kuwa nina uzoefu wa kutosha kuwavusha wana Segerea mahali ambako nimeishi kwa takribani miaka 12 huku shughuli zangu zote za ujasiriamali zikiwa jimboni humu. Ninalifahamu jimbo hili vizuri, watu wake, matatizo yao na changamoto zinazowakabili. Zaidi ya yote nina uwezo wa kushirikiana na wananchi tukioneshana njia ya kuzitatua changamoto hizi na wakati ukifika nitazieleza huku nikiweka wazi njia za kupita.

Pamoja na kwamba nina elimu ya darasani ya kutosha, uzoefu wa uongozi usio na shaka na tabia na mienendo ya maadili huku nikiwapenda watu wa kila namna, natambua kuwa kazi ya kuwa mbunge ni zaidi ya hayo, inahitaji weledi, wepesi, staha na heshima, kujali, kuwa karibu na watu na kujitolea kwa hali na mali kuwapigania wale ambao haki zao na mahitaji yao yanacheleweshwa – kaliba ya namna hii imejengeka na sina shaka kuwa ninakidhi sifa na vigezo hivi vya nyongeza.

Mimi ni muumini wa demokrasia, nitasaidia wagombea wote waliojitokeza kunipinga na kushindana nami ikiwa kutakuwa na haja hiyo, sitamtukana wala kumsema vibaya yeyote yule, kazi yangu kuelekea Oktoba ni kujinadi na kueleza sifa zangu na uwezo wangu huku nikivihusianisha na utatuzi wa matatizo ya wananchi wa Segerea kwa kushirikiana na wananchi.

Nawaomba wanachama wengine wa vyama vya UKAWA wenye sifa, vigezo na uwezo wajitokeze kwa wingi. Sote tutapimwa kwa uwezo na vigezo vyetu na mwisho wa siku atapatikana mmoja wetu na ataungwa mkono na sisi sote. Baada ya Oktoba 2015, Segerea itakuwa na mpambanaji mpya, mbunge wa wananchi na atakayepigana hadi tone la mwisho la damu kwa ajili ya wananchi wake. Na labda mtu huyo atakuwa ni mimi.

Nawatakia kila la heri na kwa ambao wangependa kunifahamu zaidi wanaweza kusoma katika kiunganishi hiki https://www.facebook.com/JuliusSundayMtatiro/posts/578218822317742:0

Julius Mtatiro,
+255 787 536 759, 0755 855 144, Juliusmtatiro@yahoo.com

machipi member, udsm member i support you 100%,
 
Safi sana. Lakini naomba utoe nini ambacho makongoro ameshindwa kutimiza na vitu gani ambayo kwa uzoefu wako unahisi unahitaji kurekebisha.
 
Jimbo la Mpendazoe hilo.

Yatakukuta yaleyale ya Ubungo, ulirukia jimbo ambalo Mnyika alikuwa kajipanga kwa muda mrefu, it's like hilo. Mpendazoe kajipanga muda mrefu na anafahamika na kasikia

Sasa wewe miezi 6 unataka jimbo?

Mpendazoe Segerea ndio kashapoteza.
Hawezi sarakasi za kulinda matokeo so kumpa kura ni sawa na kuuza kura.
Arudi tu Kishapu wanakopita bila kupambana.
 
Kaka Julius hongera kwa kuonyesha dhamira mungu akupe nguvu na ulinzi. Tunahitaji siasa za kistaarabu na sio matusi. Mimi kama mwanachama wa CCM nakukaribisha ulingoni kiroho safi.
 
Mtatiro tupo pamoja.....nategemea chama changu CDM kukuunga mkono 100% kazi imeanza.
 
Changamoto za wananchi ni mengi sn je umeshiriki vipi kuzitatua au watu wanasubiri mpk upate uongozi ndiyo uzitatue

Seriously speaking. Hivi anayetatua shida za wananchi ni mbunge(hakusanyi kodi anasimamia tu serikali) au serikali inayokusanya kodi? Sasa we ulitaka afanye nini kama yeye si mkusanya kodi? Nilitegemea uelekeze malalamiko yako zaidi kwenye serikali ya chama tawala(CCM) badala ya "individual". Halafu na wewe unataka uitwe GT!!!! Embarassing!!!
 
Ndugu yangu JAKACKSERU,

Hata hiyo UKONGA ina wagombea wazuri tu wa CHADEMA akiwemo Kamanda Mwita Waitara, ngoja tusubiri kujua UKAWA inagawanaje majimbo ndipo tutahitimisha masuala haya. Lakini kwa namna nilivyojipanga sitakuwa na kinyongo kumuunga mkono mgombea yeyote wa UKAWA ikiwa atapitishwa kugombea Segerea.

Sina tabia ya kupigania madaraka kwa sababu najua kuna masuala mengi ya kufanya kuliko kuongoza. Jambo la msingi ni kuwa UKAWA itapata mgombea imara SEGEREA. Wana Segerea wameichoka CCM na wanahitaji kiongozi imara zaidi, ukiongea nao wanakueleza hawachagui chama, watahitaji kuwa na kiongozi imara kutoka chama chochote kati ya vyama vyetu na kwamba huyo ndiyo chaguo lao. Mimi ni mmoja wa watu wanaohitaji ridhaa hiyo na wapo wenzangu, sote tutapimwa, atakayepitishwa tutampigania.

Na jambo la mwisho unalopaswa kujua ni kuwa vyama vya CHADEMA na CUF vinahitajiana mno UKONGA na ukiangalia hata matokeo ya serikali za mitaa utagundua kuwa kati ya mitaa takribani 33 ya UKAWA, CUF ndiyo ina mitaa mingi. Hii ndo hali ya kisissa ya sasa. Lakini CUF kuwa na mitaa mingi SEGEREA mwaka 2014 au CHADEMA kupata kura nyingi za ubunge mwaka 2010 siyo hoja ya vyama hivi viwili kuweka u-vyama wao mbele na kusahau ushirikiano.

UKAWA ikiweka mgombea mmoja Segerea itashinda kwa kishindo. Ikivurugana na kila chama kikajiwekea mgombea sote tutaanguka.

Ni hayo tu.

J. Mtatiro.

Julius Mtatiro

Umeandika mambo ya msingi sana isipokuwa moja tu la idadi ya mitaa tuliyoshinda UKAWA uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kwa majimbo ya UKONGA na SEGEREA.

Kumbukumbu nilizo nazo zinaonyesha kama ifuatavyo:
UKONGA:
CHADEMA MITAA 10 (WENYEVITI)
CUF MITAA 4 (WENYEVITI)

SEGEREA:
CHADEMA MITAA 16 (WENYEVITI)
CUF MITAA 11 (WENYEVITI)

Kwa Majimbo yote mawili msimamo upo hivi:
CHADEMA MITAA 26
CUF MITAA 15

Sasa hiyo mitaa 33 unayoisema sijui umeipata wapi kiongozi na kwamba cuf ndiyo ina mitaa mingi kuliko Chadema nalo sio kweli hata kidogo.

Ni muhimu ukapitia upya kumbukumbu zako ili kuondosha mkanganyiko na upotoshaji uliotokea ktk mabandiko yako.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu yangu JAKACKSERU,

Hata hiyo UKONGA ina wagombea wazuri tu wa CHADEMA akiwemo Kamanda Mwita Waitara, ngoja tusubiri kujua UKAWA inagawanaje majimbo ndipo tutahitimisha masuala haya. Lakini kwa namna nilivyojipanga sitakuwa na kinyongo kumuunga mkono mgombea yeyote wa UKAWA ikiwa atapitishwa kugombea Segerea.

Sina tabia ya kupigania madaraka kwa sababu najua kuna masuala mengi ya kufanya kuliko kuongoza. Jambo la msingi ni kuwa UKAWA itapata mgombea imara SEGEREA. Wana Segerea wameichoka CCM na wanahitaji kiongozi imara zaidi, ukiongea nao wanakueleza hawachagui chama, watahitaji kuwa na kiongozi imara kutoka chama chochote kati ya vyama vyetu na kwamba huyo ndiyo chaguo lao. Mimi ni mmoja wa watu wanaohitaji ridhaa hiyo na wapo wenzangu, sote tutapimwa, atakayepitishwa tutampigania.

Na jambo la mwisho unalopaswa kujua ni kuwa vyama vya CHADEMA na CUF vinahitajiana mno UKONGA na ukiangalia hata matokeo ya serikali za mitaa utagundua kuwa kati ya mitaa takribani 33 ya UKAWA, CUF ndiyo ina mitaa mingi. Hii ndo hali ya kisissa ya sasa. Lakini CUF kuwa na mitaa mingi SEGEREA mwaka 2014 au CHADEMA kupata kura nyingi za ubunge mwaka 2010 siyo hoja ya vyama hivi viwili kuweka u-vyama wao mbele na kusahau ushirikiano.

UKAWA ikiweka mgombea mmoja Segerea itashinda kwa kishindo. Ikivurugana na kila chama kikajiwekea mgombea sote tutaanguka.

Ni hayo tu.

J. Mtatiro.

Unabusara sana, I admire you brother..
 
Seriously speaking. Hivi anayetatua shida za wananchi ni mbunge(hakusanyi kodi anasimamia tu serikali) au serikali inayokusanya kodi? Sasa we ulitaka afanye nini kama yeye si mkusanya kodi? Nilitegemea uelekeze malalamiko yako zaidi kwenye serikali ya chama tawala(CCM) badala ya "individual". Halafu na wewe unataka uitwe GT!!!! Embarassing!!!

Ili uwe mbunge ni lazima utatue matatizo ya wananchi kwanza km mtu mtaa anaoishi ameshindwa hata kuoganizi wakazi kusafisha mtaa atawezaje kuwaunganisha wananchi kujiletea maendeleo ubunge siyo kwenda kumwaga matusi bungeni
 
Safi sana, ila sitegemei ukimbozi wa nchi hii kuanzia Dar!!!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Back
Top Bottom