Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewaapisha Mawaziri wateule wanne na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ikulu Chamwino Jijini Dodoma
Mawaziri ni Dkt. Stergomena Tax Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, January Makamba Waziri wa Nishati, Prof. Makame Mbarawa Waziri wa Ujenzi na Dkt. Ashatu Kijaji Waziri wa Habari na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Pia, Dkt. Eliezer Feleshi amekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali
====
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ametaka kuwepo Mikataba bora ya Nishati hususan ya Umeme. Amesema hayo wakati wa Uapisho wa Viongozi walioteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan
Amesema, "Tuna matatizo makubwa kwenye Nishati ya Petroli, Dizeli na jamii zake zote. Bei ya Petroli isipande kama inavyokwenda, tuangalie mbinu mbadala"
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema iliyokuwa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo sasa itakuwa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo
Amesema amehamisha Idara ya Habari ili Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari iweze kutimia kwani kimekuwa ni kilio cha Wadau wa Sekta ya Habari kwa muda mrefu
Amefafanua, "Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo ilikuwa inamezwa na Habari. Nimeona niiachie ionekane kwa uwazi zaidi kwasababu Sanaa ni Ajira kwa Vijana wengi'
Amewataka Wakuu wa Mikoa kuwapanga Wamachinga ambao sasa wameonekana kuenea kila sehemu hadi mbele ya maduka na kufanya wenye maduka baadhi kutoa bidhaa na kumpa Machinga auze
Amesema kitendo hicho kinaikosesha Serikali kodi, kwani Mmachinga halipi kodi lakini mwenye duka anatakiwa kulipa kodi. Amewataka Wamachinga kufuata Sheria zilizopo
Amesema wakati wa kuwapanga hataki kuona ngumi, kupigana, kumwaga bidhaa, kuchafuliana bali hatua zichukuliwe vema bila mwenye maduka na Wamachinga kuudhika
Rais Samia Suluhu Hassan amesema kazi ya Waziri kwenye Wizara ya Ulinzi sio kubeba mzinga wala kupiga bunduki, bali ni kusimamia Sera na Utawala wa Wizara
Amesema, "Nimeamua kuvunja 'myth au taboo' ya muda mrefu kwamba Wizara ya Ulinzi lazima akae Mwanaume mwenye misuli yake. Nimempeleka Dkt. Stergomena Tax huko kwasababu ya upeo aliopata akiwa SADC"
Ameongeza, "Yeye anajua vema Askari wetu waliopo Msumbiji na DR Congo, kwanini wapo huko na mifumo yao. Atamsaidia vizuri CDF katika upande huo"
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendeshwa kwa matendo makali na sio maneno makali akifafanua, "Matendo makali ni kwenda kwa Wananchi na kutoa huduma inayotakiwa"
Ameeleza, "Msinitegemee nikae hapa nianze kufoka ovyo. Kwasababu nafanya kazi na watu wazima, ni imani yangu tunapozungumza tunaelewana"
Amesema, mabadiliko katika Baraza la Mawaziri na Viongozi wengine Wizarani bado yataendelea
Mawaziri ni Dkt. Stergomena Tax Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, January Makamba Waziri wa Nishati, Prof. Makame Mbarawa Waziri wa Ujenzi na Dkt. Ashatu Kijaji Waziri wa Habari na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Pia, Dkt. Eliezer Feleshi amekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali
====
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ametaka kuwepo Mikataba bora ya Nishati hususan ya Umeme. Amesema hayo wakati wa Uapisho wa Viongozi walioteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan
Amesema, "Tuna matatizo makubwa kwenye Nishati ya Petroli, Dizeli na jamii zake zote. Bei ya Petroli isipande kama inavyokwenda, tuangalie mbinu mbadala"
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema iliyokuwa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo sasa itakuwa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo
Amesema amehamisha Idara ya Habari ili Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari iweze kutimia kwani kimekuwa ni kilio cha Wadau wa Sekta ya Habari kwa muda mrefu
Amefafanua, "Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo ilikuwa inamezwa na Habari. Nimeona niiachie ionekane kwa uwazi zaidi kwasababu Sanaa ni Ajira kwa Vijana wengi'
Amewataka Wakuu wa Mikoa kuwapanga Wamachinga ambao sasa wameonekana kuenea kila sehemu hadi mbele ya maduka na kufanya wenye maduka baadhi kutoa bidhaa na kumpa Machinga auze
Amesema kitendo hicho kinaikosesha Serikali kodi, kwani Mmachinga halipi kodi lakini mwenye duka anatakiwa kulipa kodi. Amewataka Wamachinga kufuata Sheria zilizopo
Amesema wakati wa kuwapanga hataki kuona ngumi, kupigana, kumwaga bidhaa, kuchafuliana bali hatua zichukuliwe vema bila mwenye maduka na Wamachinga kuudhika
Rais Samia Suluhu Hassan amesema kazi ya Waziri kwenye Wizara ya Ulinzi sio kubeba mzinga wala kupiga bunduki, bali ni kusimamia Sera na Utawala wa Wizara
Amesema, "Nimeamua kuvunja 'myth au taboo' ya muda mrefu kwamba Wizara ya Ulinzi lazima akae Mwanaume mwenye misuli yake. Nimempeleka Dkt. Stergomena Tax huko kwasababu ya upeo aliopata akiwa SADC"
Ameongeza, "Yeye anajua vema Askari wetu waliopo Msumbiji na DR Congo, kwanini wapo huko na mifumo yao. Atamsaidia vizuri CDF katika upande huo"
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendeshwa kwa matendo makali na sio maneno makali akifafanua, "Matendo makali ni kwenda kwa Wananchi na kutoa huduma inayotakiwa"
Ameeleza, "Msinitegemee nikae hapa nianze kufoka ovyo. Kwasababu nafanya kazi na watu wazima, ni imani yangu tunapozungumza tunaelewana"
Amesema, mabadiliko katika Baraza la Mawaziri na Viongozi wengine Wizarani bado yataendelea