MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Najua wengi walidhania nitafanya kwa maana ya "ku do" - lol - , lakini ninachotaka kuongelea ni tabia ya AJIZI, USIRI, UCHOVU, DHARAU...ya kuacha jambo la kufanya leo ukasema "nitafanya kesho". Iwe ni kujibu PM, simu, sms, barua...kuacha chombo ulichokulia usiku uje kukosha asubuhi, kurundika nguo chafu mpaka ukakosa nafasi, umepaka rangi nyumba ikabaki sehemu ndogo sasa ni mwaka wa nne hujarejea kupaka hapo; miezi minne ulibadilisha makazi mpaka leo mizigo mengine imo ndani ya maboksi, taa ya stoo iliungua, lakini badala ya kubadilisha unaingia stoo na tochi....Mambo ni mengi yanayotufanya tuwe na ajizi na kuna misemo mingi ya ajizi:
- Ajizi nyumba ya njaa.
- Ajizi mwizi wa wakati
- Kesho haifiki
- Kesho kesho mavituzi yakuwa
- Tusiliache kesho tunaloweza kulifanya leo
Iko hata nyimbo moja ya zamani, "Bomoa tutajenga kesho".
Nianze na mimi. Ajizi zangu kubwa ni kujibu na/au kuandika sms na barua; na kwenda kumwona mtu. Ninakaa mpaka siku zinapita sana kiasi cha kushindwa baadae nianzie wapi.
Wewe je, ajizi yako iko wapi? Ni kitu gani ulipaswa kukifanya ukakiacha kwa ajili ya kesho na mpaka leo bado hujakifanya au ulikifanya siku, wiki, miezi miaka kadhaa baadae?
- Ajizi nyumba ya njaa.
- Ajizi mwizi wa wakati
- Kesho haifiki
- Kesho kesho mavituzi yakuwa
- Tusiliache kesho tunaloweza kulifanya leo
Iko hata nyimbo moja ya zamani, "Bomoa tutajenga kesho".
Nianze na mimi. Ajizi zangu kubwa ni kujibu na/au kuandika sms na barua; na kwenda kumwona mtu. Ninakaa mpaka siku zinapita sana kiasi cha kushindwa baadae nianzie wapi.
Wewe je, ajizi yako iko wapi? Ni kitu gani ulipaswa kukifanya ukakiacha kwa ajili ya kesho na mpaka leo bado hujakifanya au ulikifanya siku, wiki, miezi miaka kadhaa baadae?