Nisipowaambia ukweli nitahukumiwa siku ya mwisho. Haya ni machukizo kwa Mungu

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,755
Yesu Kristo ambaye ndiye NENO la Mungu alituachia injili na Roho Mtakatifu kutuongoza safari ya Mbinguni.

Mambo yafuatayo ni machukizo mbele za Mungu
  1. Bikira Maria kws sababu hakuna maandiko yanayosapoti ibada ya kupitia Maria ili kumfikia Yesu au Mungu
  2. Ibada ya Sanamu. Yapo makanisa yamesimika sanamu kwenye makanisa hayo na watu wsnapiga goti kuomba rehema kupitia sanamu hizo wskiamini wapo salama
  3. Sanda, Yesu alituachia Imani na siyo historia hizi zilizopikwa na shetani na kulikabidhi kanisa lieneze uongo na kuwapoteza wengi
  4. Holly grail. Kikombe cha karamu ya mwisho. No such a thing
  5. Kubatiza watoto. Watoto wsnabarikiwa na wakubwa wanabatizwa baada ya kumkiri Yesu kama Bwana na Mwokozi wake. Mtoto anazaliwa huru hadi atakapoamua kuongoka kumfuata Yesu ndo anafanyika kuwa mkristo na mwanafunzi wa Yesu.
  6. Ibada za ndoa. Jambo hili limewekwa na kanisa kudhibiti waumini. Ndoa Takatifu ni pale ambapo mtu mume akishamaliza taratibu za kumposa mwanamke na hapo wanakuwa tayari wanandoa. Kuwaita watumishi wa Mungu kuombea ndoa ni jambo jema lakini watumishi hao wa Mungu kujitwalia mamlaka ya kufunga na kuvunja ndoa ni kukufuru agizo la Mungu kwenye eneo hilo
  7. Ibada za mazishi. Imenenwa kuwa kufa ni mara moja na baada ya kifo ni Hukumu. Hata Yesu hakufanyiwa ibada ya maziko. Hakuna sala wala tendo lolote linaloweza kubadilisha hatima ya mtu baada ya kifo chake. Jambo pekee liwezekanalo ni kumfufua endapo itampendeza Mungu. Kufanyiwa ibada baada ya kufa ni makufuru mbele za Mungu.
  8. Mungu kuchanganywa na Kaisari. Yesu alisema hauwezi kutumikia mabwana wawili ambapo utampenda mmoja na mwingine utamchukia. Huwezi kumpenda Mungu kisha ukaipenda fedha. Fedha ni mamlaka ya kidunia na watumishi wote walioingia kwenye mamlaka za dunia huku wakiwa na kofia zao za utumishi wana nafasi yao motoni kwa sababu wamekaidi injili na kushiriki karamu za kinyama na uharibifu.
Marko 16: 15-16
Basi enendenj mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa

Mwenye kuongeza neno la uvuvio aongezee yanayotukumbusha utume na agizo la Yesu Bwana wetu
 
Ahsante kwa kutukumbusha na mimi naongezea DINI ya Kweli ni AMANI na UPENDO (PEACE and LOVE).
Umenena kweli kabisa.

Kama hauna upendo kwa watu unaowaona leo basi hauwezi kumpenda Mungu asiyeonekana.

Tutayashuhudia matendo yake makuu na hakika tunamuona kila siku anavyotubariki hata katika nyakati ngumu
 
Ingependeza sana kama andiko lingesema chochote kuhusu katazo la kuoa mke mmoja na matumizi (sahihi?) ya pombe.
Binafsi sikubaliani na yote mawili Kwa kuwa hakuna mistari inayoagiza hivyo
 
Yesu Kristo ambaye ndiye NENO la Mungu alituachia injili na Roho Mtakatifu kutuongoza safari ya Mbinguni.
Hakika mkiisikia injili yatosha kuwa ushahidi siku ya hukumu kwa sababu siyo wote watakaoingia ufalme wa Mungu.

Hiyari ni yako na Roho Mtakatifu akushuhudie ndani yako kwenye hili
mleta mada akasome biblia ya vitabu72siyo ya66 hapo ataona kuhusu maelezo yake ya namba7
 
Kila mtu apigane vita vyake ya kiroho kwa imani aliyonayo
ukisoma aya hizi naamini utafahamu kuwa vita vya kiroho siyo jambo binafsi
👇👇👇


Mathayo 28:19
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

Mathayo 28:20
na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
 
Ingependeza sana kama andiko lingesema chochote kuhusu katazo la kuoa mke mmoja na matumizi (sahihi?) ya pombe.
Binafsi sikubaliani na yote mawili Kwa kuwa hakuna mistari inayoagiza hivyo
Ingawa Mungu hakumhukumu baba yetu Ibrahim kwa kuzaa na mjakazi, vivyo hivyo hakumkatilia mbali Daudi ambaye alikuwa mafia kwenye wake za watu na hata hakumuondolea utajiri, mamlaka na hekima mfalme Suleiman hata alipokuwa na michepuko 700.
Lakini kumbuka nyakati hizo Haki ya mtu kwa Mungu ilihesabiwa kupitia matendo ya sheria ya Mussa.

Yesu Kristo amesema hapa
👇👇👇

Mathayo 19:5
akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

Mathayo 19:6
Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.


Mathayo 19:9
Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.

Mathayo 19:10
Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.

Mathayo 19:11
Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.

 
Back
Top Bottom