Nishati ya kutumia majumbani

Mtumiabusara

JF-Expert Member
Nov 18, 2009
473
40
Jamani watanzania wenzangu,
Naomba tushauriane ni nishati gani nafuu ya kutumia majumbani kupikia hasa kwa watu wa kipato cha chini au cha kati tunaoishi mjini? Maana bei ya gesi au mkaa ni zaidi ya Sh. 50,000. Umeme ndo huo huwezi kupikia na haupatikani kwa uhakika. Mafuta ya taa sina uhakika kama yanaweza kukidhi haja.

Hivi kwa nini tusitumie gesi asilia kutoka mikoa ya kusini kupikia badala yake tunategemea gesi ya kutoka nje? Ambayo bei yake hatuwezi kuidhibiti?
 
Mkuu hii ni hoja nzuri na ngumu kidogo.
Kwanza kabisa mimi ni mdau katika nishati na ninapenda watu watumie nishati ambayo inapatikana wakati wote, bei poa na rafiki wa mtumiaji (haina madhara).

Suala la kutumia gesi yetu lina utata mwingi kwakuwa "wenye nguvu" hawataki kuona unapata nishati ya bei poa "kwani wao hawatauza ile ya kwao wanayoileta toka majuu".-NOTE: Biashara ya mafuta na gesi yote inafanywa na "wenye nguvu".
Gesi yetu ya asili ina uwezo wa; KUTUMIKA MAJUMBANI KUPIKIA, KUZALISHA UMEME NA KUJAZA KWENYE MAGARI YOTE KUANZIA BAJAJI HADI MABASI YA GHOROFA. Kwa kulijua hili "wenye nguvu" wanaona giza mbele yao, hivyo wanahakikisha "hatutoki" kwenye kununua vya kwao.

Ushauri wangu; Wakati tukisubiri "uhuru wa Tanganyika/Tz" unaweza kutumia teknolojia ya "BIOGAS" ambayo mini ni mtaalam. Kwa mtu yeyote mwenye nafasi katika maeneo ya nyumbani kwake, awe na mifugo au hana anaweza kuzalisha biogas kwaajili ya kupikia na kwaajili ya matumizi mengine. Ili biogas izalishwe "mtambo wa biogas"(Biodigester) unatakiwa kusanifiwa, kujengwa na vifaa vyake kufungwa tayari kwa matumizi. Mtambo mdogo ambao unatosha matumizi ya familia utachukua siku 25-30 kuujenga na ukishajengwa unadumu miaka 35-40. Kama uko interested kupata taarifa zaidi ni-PM.

Faida za mtambo wa biogas ni pamoja na; Kutumia nishati ambayo unazalisha mwenyewe, unaipata wakati unapoitaka, unazalisha mbolea ya asili (organic manure), mazingira yanakuwa safi na salama, hakunaa madhara ya moshi, inalipa ndaani ya miaka kati ya 3-5.
 
Mkuu hii ni hoja nzuri na ngumu kidogo.
Kwanza kabisa mimi ni mdau katika nishati na ninapenda watu watumie nishati ambayo inapatikana wakati wote, bei poa na rafiki wa mtumiaji (haina madhara).

Suala la kutumia gesi yetu lina utata mwingi kwakuwa "wenye nguvu" hawataki kuona unapata nishati ya bei poa "kwani wao hawatauza ile ya kwao wanayoileta toka majuu".-NOTE: Biashara ya mafuta na gesi yote inafanywa na "wenye nguvu".
Gesi yetu ya asili ina uwezo wa; KUTUMIKA MAJUMBANI KUPIKIA, KUZALISHA UMEME NA KUJAZA KWENYE MAGARI YOTE KUANZIA BAJAJI HADI MABASI YA GHOROFA. Kwa kulijua hili "wenye nguvu" wanaona giza mbele yao, hivyo wanahakikisha "hatutoki" kwenye kununua vya kwao.

Ushauri wangu; Wakati tukisubiri "uhuru wa Tanganyika/Tz" unaweza kutumia teknolojia ya "BIOGAS" ambayo mini ni mtaalam. Kwa mtu yeyote mwenye nafasi katika maeneo ya nyumbani kwake, awe na mifugo au hana anaweza kuzalisha biogas kwaajili ya kupikia na kwaajili ya matumizi mengine. Ili biogas izalishwe "mtambo wa biogas"(Biodigester) unatakiwa kusanifiwa, kujengwa na vifaa vyake kufungwa tayari kwa matumizi. Mtambo mdogo ambao unatosha matumizi ya familia utachukua siku 25-30 kuujenga na ukishajengwa unadumu miaka 35-40. Kama uko interested kupata taarifa zaidi ni-PM.

Faida za mtambo wa biogas ni pamoja na; Kutumia nishati ambayo unazalisha mwenyewe, unaipata wakati unapoitaka, unazalisha mbolea ya asili (organic manure), mazingira yanakuwa safi na salama, hakunaa madhara ya moshi, inalipa ndaani ya miaka kati ya 3-5.

Mkuu nashukuru kwa ufafanuzi wako. Labda unaweza kutujulisha gharama za huo mradi ili watu wote wenye interest tuweze kunufaika. Lakini nichojiuliza wataalam wetu wa uchumi, waheshimiwa wabunge na wadau wengine hivi kweli wote kwa pamoja tunashindwa kujenga hoja ya kutetea suala hili ambalo litatupunguzia ugumu wa maisha?
 
mkuu hii ni hoja nzuri na ngumu kidogo.
Kwanza kabisa mimi ni mdau katika nishati na ninapenda watu watumie nishati ambayo inapatikana wakati wote, bei poa na rafiki wa mtumiaji (haina madhara).

Suala la kutumia gesi yetu lina utata mwingi kwakuwa "wenye nguvu" hawataki kuona unapata nishati ya bei poa "kwani wao hawatauza ile ya kwao wanayoileta toka majuu".-note: Biashara ya mafuta na gesi yote inafanywa na "wenye nguvu".
Gesi yetu ya asili ina uwezo wa; kutumika majumbani kupikia, kuzalisha umeme na kujaza kwenye magari yote kuanzia bajaji hadi mabasi ya ghorofa. Kwa kulijua hili "wenye nguvu" wanaona giza mbele yao, hivyo wanahakikisha "hatutoki" kwenye kununua vya kwao.

Ushauri wangu; wakati tukisubiri "uhuru wa tanganyika/tz" unaweza kutumia teknolojia ya "biogas" ambayo mini ni mtaalam. Kwa mtu yeyote mwenye nafasi katika maeneo ya nyumbani kwake, awe na mifugo au hana anaweza kuzalisha biogas kwaajili ya kupikia na kwaajili ya matumizi mengine. Ili biogas izalishwe "mtambo wa biogas"(biodigester) unatakiwa kusanifiwa, kujengwa na vifaa vyake kufungwa tayari kwa matumizi. Mtambo mdogo ambao unatosha matumizi ya familia utachukua siku 25-30 kuujenga na ukishajengwa unadumu miaka 35-40. Kama uko interested kupata taarifa zaidi ni-pm.

Faida za mtambo wa biogas ni pamoja na; kutumia nishati ambayo unazalisha mwenyewe, unaipata wakati unapoitaka, unazalisha mbolea ya asili (organic manure), mazingira yanakuwa safi na salama, hakunaa madhara ya moshi, inalipa ndaani ya miaka kati ya 3-5.
u

mkuu unacho sema ni sahihi kabisa 100% biogas ni nzuri sana na ukisha install ndo imetoka wewe ni kutumia tu,

ila mkuu kila kitu kina vikwazo vyake, kwa upande wa biogas vikwazo vyake ni hivi

1. Biogasi inatumiwa kwa mtu mwenye nyumba yake tu, vipi walio panga?

2. Mkuu kwa walio panga hii haiwezekani kabisa,

3 hata kama umejenga nyumba yako inatakiwa uwe na eneo la kutosha make mfumo wa choo za biogasi ni tofauti na hizi tulizo zizoea.

Biogas ni nzuri sana lakini uwe na nyumba yako mwenyewe, ukiwa umepanga kwenye magorofa ya nhc hii kitu haiwezekani
 
u

mkuu unacho sema ni sahihi kabisa 100% biogas ni nzuri sana na ukisha install ndo imetoka wewe ni kutumia tu,

ila mkuu kila kitu kina vikwazo vyake, kwa upande wa biogas vikwazo vyake ni hivi

1. Biogasi inatumiwa kwa mtu mwenye nyumba yake tu, vipi walio panga?

2. Mkuu kwa walio panga hii haiwezekani kabisa,

3 hata kama umejenga nyumba yako inatakiwa uwe na eneo la kutosha make mfumo wa choo za biogasi ni tofauti na hizi tulizo zizoea.

Biogas ni nzuri sana lakini uwe na nyumba yako mwenyewe, ukiwa umepanga kwenye magorofa ya nhc hii kitu haiwezekani

Mkuu Komandoo na wengine; Teknolojia ya biogas ni pana sana, vikwazo vyote ulivyozungumzia hapo juu vyaweza kuvukwa. Kwa wenye nyumba zao na nafasi watafaidi zaidi kwa kupata mtambo wa kudumu muda mrefu bila longolongo. Kwa walio kwenye nyumba za kupanga na wana nafasi ningewashauri kujadiliana na land lords wao ili waingie jv ya kujenga huu mtambo.
Kwa wale walio kwenye nyumba za kupanga na wasio na nafasi au wenye nafasi lakini hawawezi kufanya lama nilivyoshauri hapo juu, pia wale walio kwenye NHC na hata maghorofani; unatakiwa uwe na space kama 2sqm ili kuweza kuweka mtambo wa kuhamishika. Sehemu ya verandah au balcony ni ideal kwaajili ya hili. Mitambo hii ya kuhamishika si imara kama ile mingine.

Kwa mitambo yote aina mbili nilizotaja haihitaji kuunganishwa na choo. (i.e it's not mandatory).

Karibuni kwenye nishati mbadala!
 
Mkuu eucalyptos tupe japo kontact zako basi, kusema tu 'karibuni kwenye nishati mbadala', wapi? kumbuka hii ni JF, be open.
 
Chief Eucalyptos, im in. But ungeweka hadharani estimated cost za hiyo plant kwa matumizi ya nyumban ingekuwa vizuri zaidi na ingekuwa na effect kubwa zaidi kwa wadau wa JF. Thanks
 
Biogas kwa mkoa wa DAR,Pwani kuna offer ya COSTEC ,wanakutengenezea kwa gharama ya laki2 tu.
ni mradi uliofadhiliwa na wazungu.unachotakiwa ni kutoa eneo na vifaa vya ujenzi.
 
Biogas kwa mkoa wa DAR,Pwani kuna offer ya COSTEC ,wanakutengenezea kwa gharama ya laki2 tu.
ni mradi uliofadhiliwa na wazungu.unachotakiwa ni kutoa eneo na vifaa vya ujenzi.
Then gharama yake ni zaidi ya laki2.
 
nazungumzia gharama za labour na utalaam.unatakiwa uwe na eneo na vitofali size ya tofali za kuchoma,kokoto/mawe,na plastic pipes za 1/2 "'
 
@ eucalyptos
Thanks kwa useful info; najua utakuwa unazungumzia Biogas from kitchen waste, kwa wale wasio na mifugo. Lkn kwa umaskini na kipato chetu waTZ wengi, do u know how much waste tunaproduce? Kwa waste ninamaanisha mabaki ya chakula (maganda ya ndizi, nyanya, ukoko etc).

How many liters of gas do a family of 5 need to cook 3 meals a day? Na how many liters of kitchen waste does a digester need to produce that amount of gas?

Nafikiri ni vyema na ni busara kuwaambia watu kuwa; huwezi zalisha gas ya kutumia siku nzima bila kukusanya mabaki ya chakula from hotels etc; pia njia nyingine kama supplement ni solar heaters, ambayo if u have warm water utapunguza cooking time hivyo energy pia!
 
Chief Eucalyptos, im in. But ungeweka hadharani estimated cost za hiyo plant kwa matumizi ya nyumban ingekuwa vizuri zaidi na ingekuwa na effect kubwa zaidi kwa wadau wa JF. Thanks

Kama huna mifugo na uko kwenye nyumba ya kupanga; the minimum you need ni:-
1.two simtanks na bomba la Maji taka kubwa
2.some few plumbing fittings
3.bacterias (from mavi ya ng'ombe)
4.jiko la gas (modified for methane)
5. lots of water.

1000l gives you 2 hrs of cooking time but requires at least 20l of uji uji wa mabaki ya chakula!

Check na website ya ARTI hasa India
 
WAKUU NASHUKURU KWA MAONI MAZURI,ila bado tuna changamoto kubwa, hiyo biogas inaweza kupata vikwazo vya kupata hizo taka
 
Nadhani suala la bei bado ni muhimu, minimum cost that someone will have to apy ni kiasi gani ndugu?!?!?!?!
 
Nadhani suala la bei bado ni muhimu, minimum cost that someone will have to apy ni kiasi gani ndugu?!?!?!?!

About 600,000/= to 1,000,000/= kwa materials na pia yategemea amount ya cooking gas one needs.

Ila challenge kubwa ni hiyo mabaki ya chakula; kwa wenye migahawa this is the type of energy ifaayo, kwani unamanage waste zako.
 
Back
Top Bottom