Nisaidieni nakaribia kuumbuka

Nisaidieni nakaribia kuumbuka

Umejuaje mtoa mada anajua kingereza?

Wanaume tumeumbiwa tamaa,kugawa upendo kwa wanawake wawili ni kitu cha kawaida sana,katika wanaume 10 ni nan mwenye mwanamke mmoja (tuseme ukweli bila kuficha ),hili jambo la mahusiano zaid ya mwanamke mmoja kwa kweli ni sifa yetu wanaume,hata vitabu vingi vya dini utaona mitume walifanya hivyo.

Sasa nashanga kuna baadhi ya malaika humu jf wanamshambulia ambapo ukweli unawezakuta mtu ana michepuka hata minne.

"We tuliza akili,sikiliza moyo wako unamtaka yupi,najua uwezi kuwapenda wote sawasawa"
At least wee jamàa umevaa viatu vyangu. Umeangalia hili suala kwa jicho la tofauti.

Hivi mtu utajuaje kuwa chakula hiki ni kitamu zaidi ya kingine bila kuonja vyote Kisha uchague kimoja kilicho Bora zaidi ya kingine?
 
sasa ndoa ni yako, sisi ao wanawake hatuwajui na hatuelewi. yaani kuchagua yupi umuoe pia unashindwa. unajielewa kweli
 
Ungeitafsiri hii kwa lugha yetu ingewasaidia wengi sana,hasa hapa: "I just wish you don’t see your daughter crying for the same reason once she grows up. I wish your daughter doesn’t fall for someone like you.Just remember KARMA is there! Whatever you do will come round to you only. No one else is going to pay for your sins!".....
Kwa ushauri wa huyo jamàa nachelea kusema si mtu wa kawaida lazma atakuwa mchungaji, sheikh au nabiii maana ameandika vitu conki sana mpaka amegusa mtima wangu
 
Fanya hivi chukua simu zao kaa nazo siku tatu utapata matokeo yupi wa kuoa yupi wa kuacha au utawaacha wote. Inaonekana hata kuwachunguza bado unachovya tu
Hii inamake sense pia japo mbinu hii ikifeli ugumu utaamia kwangu
Maana kilammoja atataka nae akae na cm yangu siku 3 hapo ndiopo nitakapo dakwa ubaradhuli wangu
 
Hii inamake sense pia japo mbinu hii ikifeli ugumu utaamia kwangu
Maana kilammoja atataka nae akae na cm yangu siku 3 hapo ndiopo nitakapo dakwa ubaradhuli wangu
itafeli wapi wakati wewe ndio mwenye maamuzi ya mwisho? Be a man
 
Habari gani Watanzania wenzangu.

Naomba wadau mnisaidie ushauri wenu maana nipo njia panda. Mimi ni kijana umri miaka 30. Nina wanawake (mademu) wawili ambao nawapenda sana na kila mmoja ananipenda sana.

Kwakweli nimefanikiwa kuishi nao bila wao kujua kama ninawachanganya; nimedumu nao kwa miaka miwili sasa, na wote wananiamini sana na kila mmoja anaamini nitamuoa.

Sasa umefika wakati ambapo natakiwa nianze harakati za kuoa kama kumtambulisha mchumba kwa wazazi na kumchumbia. Napata wakati mgumu nimuache yupi na nimuoe yupi; wote ni wema sana kwangu na nakosa hata sababu ya ku-force ili nimuache mmoja

Wote ni wapole; nimesubiri mmoja anikosee nimuache lakini wapi, na ninapoelekea nakarbia kubambwa kwa ujinga niliowafanyia. Sasa nitumie kigezo gani kumuacha mmoja nibaki na mmoja nimuoe?

Naombeni msaada au nitumie kigezo gani ambao nitapata sababu ya kumuacha mmoja wao maana naona naaibika sio mda mrefuu.
Waite sehemu wote wawili ila iwe sehemu ya wazi isiwe ndani wanaweza kukudhuru then wape ukweli afu waachie maoni kutoka kwao kama wakiamua kukuacha wewe sawa kama wakiamua uwaoe wote sawa oa wote kama dr fulani hivi
 
Asante sana kwa ushauri wako japo ushauri wako umenifanya nijihisi mkosaji nisiyestahili kusamehewa. Umenifanya nijichukie mwenyewe na sijui nianzie wapi kurekebisha makosa niliyoyafanya.
Mkuu

Ni muhimu sana umegundua hiyo guiltiness. Ni 1st step kuelekea kupata ufumbuzi.

Sasa basi, tukirudi katika ukweli, hapo katika wanawake wawili hakuna hata mmoja anafaa kuwa mke wako.

Nadhani masula ya ndoa yanatakiwa yaje natural sana kutoka moyoni mwako. Sasa kama wewe upo neutral tu kwamba unaweza muoa yeyote kati ya hao hiyo ni indication ya kwanza kwamba hakuna wakwako hapo.

Solution

Saikolojia inaonesha watu hu respond positively mambo mabaya ya kuwaumiza pale wanapokua wengi kuliko mmoja mmoja (wanasema msiba wa wengi ni harusi)

Kwa minajili hiyo basi, wakutanishe hao watoto wazuri wote kwa pamoja, uwaeleze ukweli. Itakua disappointment kwao ila psychologically itawasaidia wakigundua kwamba WOTE WAWILI walikua deceived.

Pia, hilo litawafanya wakuone ‘kiumbe cha ajabu’, watakapokuona hivyo, pain itageuka kuwa hate.

Mwisho, kilicho trigger hasira zangu hapa sio wewe ku cheat (ku cheat kunaweza tokea, japo sio jambo zuri….ila sasa hiili ni suala private la mtu na mtu depending unaheshimu vipi mahusiano yako, na unaweza vipi kucontrol hisia zako), suala la wewe ku promise ndoa kwa wote wawili hilo ndilo baya sana, inawezekana kuna wana kadhaa hao wanawake wamewakataa kwasababu tu ya kusubiri NDOA HEWA yako.

Kwa msingi huo hapo juu, I am very sorry chief kama nimeku attack sana. No offence intended ndugu yangu akili kijiko
 
fanya hivi utamjua anayefaa kuwa mkeo; Kila mmoja kwa wakate wake, mzingue mpaka afike kiwango chake cha juu cha kukasirika na ujitahidi kuwa mvumilivu kupokea maneno machafu usiyoyategemea. hapo utajua undani wao kila mmoja alivyo then ufanye maamuzi kwa atakayevumilia.
Safi sana huu ni ushauri maridhawa kabisa nitaufanyia kazi bila shaka
 
We boya kwel.Et hawajui kama unatumia jf na ushasema hiyo avater ni picha yako
Mkuu licha ya kuwa hiyo picha ni yangu lakini haipo clear kiasi Cha kunijua kirahisi halafu nafahamu wao wapo bize sana na hata kupata muda wa kuingi jf ni mtihani sana
 
Hiv inakuaje mtu ana buy huu ujinga wa "nitakuoa"???
Mm sijawah aisee.
Hata mke wangu tu sikuwah kumuahid kama nitamuoa.
Kunaubaya gani ukimuahidi mtu utamuoa halafu usimuoe au ukamuoa kweli?
 
Back
Top Bottom