Nipo tayari kujiuzuru endapo itathibitika-waziri wa miundombinu

Waziri wa miundombinu wa zanzibar hamad masud mh.Hamad Masudi amesema yupo tayari kujiuzuru
Sosi:bbc

Hapo kwenye Red ndiyo ujinga wa viongozi wengi, "eti nipo tayari kujiuzuru endapo tume itadhibitisha uzembe"! Tume gani tusubiri wakati hiyo Meli ilikuwa na idadi kubwa ya abiria kuliko uwezo wake?

Ni uzembe gani anaosubiri utamkwe na tume? Au anadhani tume itasema waziri alitakiwa kwenda kuhesabu idadi ya watu?. Ebu asitupotezee wakati kwa kujifanya yeye muwajibikaji wakati hajui lolote.

Kwa taarifa yake; Leo nimesikia abiria wakilalamika na kusema jana abiria wa kwenda pemba kwa boat ya "Seagull" walizuiwa kuingia bandarini kwa sababu idadi ya abiria kwenye boat ilikuwa ishatitosha japo na wao walikuwa wamekatiwa ticket za boat hiyo hiyo. Aliyekuwa anafanya kazi ya kuhesabu na kuzuia watu kuingia ni serikali si mwenye boat!

Kama huyo waziri anajua utaratibu huu uliotumika jana kwenye boat hii iweje asijue kuwa utaratibu huo ulikiukwa kwa meli ya Spice? Nilisikia kwa masikitiko kuwa abiria walionusurika wakilalamika eti walitaka wapunguzwe na mizigo ipunguzwe wakapuuzwa!!!!!!!

Waziri huoni uzembe bado? Huyo waziri hana tofauti na viongozi wengine anaojaribu kujitofautisha nao (Like Husein Mwinyi na milipuko ya mabomu)!
 
Mwinyi alijiuzulu lakini baadaye alirudi kwa tiketi ya urais na hivyo kupoteza kabisa umaana wa kuwajibika kwake awali. Mimi sioni kama Afrika kuna kuwajibika na wala sioni sababu ya kumbebesha lawama huyo waziri. Isitoshe matatizo na ajali zetu zinatokana na umasikini wetu sasa watu watajiuzulu wangapi kila siku. Si tunateuwa mawaziri kila siku?
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Kwa mtazamo kama wako nchi hii hatutafika popote kwa sababu hakuna atakaeona umuhimu wa kuwajibika kama kiongozi mwenye dhamana sehemu aliyopo. Pia waendeshaji wa shughuli mbalimbali pia hawatajali kuzingatia sheria na taratibu kwani hakuna atakae wachukulia hatua maana hata wakikosea wanaotegemewa kuchukua hatua hawatajiuzulu!
 
Sio Mfako kwa Tanzania tu nadhani kwa Afrika yote aliweka Mfano...

Lakini aliporudi Madarakani kwanini aliteleza na kuanzisha Azimio la Zanzibar? kuondoa JKT na Sasa Wanaliweka Tena?

Atatupa kiswahili fasaha kuhusu Jambo Hilo?

Kila maamuzi huwa na busara wakati yanapofanywa, unalijuwa Azimio la Zanzibar lilihusu nini au unalisema tu. Kuhusu JKT, Mwinyi kachukuwa nchi kavu mpaka Benki Kuu imechmwa moto, hakuna fedha hata moja ya kigeni, kila kitu hohehahe, uamuzi wa kusimamisha JKT ulikuwa mzuri sana kwani ilifikia wale vijana wanaokwenda huko wanateseka tu, ilibidi hata mlo wa siku upunguzwe, Mwinyi akafanya la maana kuifuta kwa wakati ule.

Mwinyi ni kichwa kilichoitowa hii nchi kutoka watu wasio hata na dawa za kupigia mswaki, wala kandambili za kuendea chooni. Sijui kama ulikuwepo wakati Mwinyi anachukuwa hii nchi au una hadithiwa tu. Nadhani ungekuwepo ungemuona Mwinyi kuwa ni Muokozi wa Taifa aliloliua Nyerere. Tuulize tuliokuwepo.
 
Kila maamuzi huwa na busara wakati yanapofanywa, unalijuwa Azimio la Zanzibar lilihusu nini au unalisema tu. Kuhusu JKT, Mwinyi kachukuwa nchi kavu mpaka Benki Kuu imechmwa moto, hakuna fedha hata moja ya kigeni, kila kitu hohehahe, uamuzi wa kusimamisha JKT ulikuwa mzuri sana kwani ilifikia wale vijana wanaokwenda huko wanateseka tu, ilibidi hata mlo wa siku upunguzwe, Mwinyi akafanya la maana kuifuta kwa wakati ule.

Mwinyi ni kichwa kilichoitowa hii nchi kutoka watu wasio hata na dawa za kupigia mswaki, wala kandambili za kuendea chooni. Sijui kama ulikuwepo wakati Mwinyi anachukuwa hii nchi au una hadithiwa tu. Nadhani ungekuwepo ungemuona Mwinyi kuwa ni Muokozi wa Taifa aliloliua Nyerere. Tuulize tuliokuwepo.

Na yeye alipoondoka alimuachia kiasi gani Mkapa?? Huyu mwinyi unayemsifia kila siku si ndiye alifungua mlango wa ufisadi na unyonyaji kwa raia wa nchi hii kwa kuua azimio la arusha na kupachika azimio la zanzibar.

Mwinyi huyu huyu ambaye mke wake alikamatwa na lyatonga akiifilisi nchi kwa kutorosha nyara za serikali kwenda nje ndo unamuona mwokozi??

Huu ubaguzi mbaya sana, unakutafuna tu taratibu mwishowe utakumaliza.
 
Jana nilimsikia huyu waziri akisema kuna uwezekano yeye ndiye atakayeunda hiyo tume
 
Waziri wa miundombinu wa zanzibar hamad masud mh.Hamad Masudi amesema yupo tayari kujiuzuru
Sosi:bbc

utamaduni unanzishwa kwa kujitoa bila zengwe...........................ajali hii ni uzembe sasa anasubiri nini?
 
imedhibitika tayari, abiria walikuwa zadi ya 1500 kwenye meli na walisema uongo kuwa ni 500!
Jiuzuru basi!!!

 
Ki
Na yeye alipoondoka alimuachia kiasi gani Mkapa?? Huyu mwinyi unayemsifia kila siku si ndiye alifungua mlango wa ufisadi na unyonyaji kwa raia wa nchi hii kwa kuua azimio la arusha na kupachika azimio la zanzibar.

Mwinyi huyu huyu ambaye mke wake alikamatwa na lyatonga akiifilisi nchi kwa kutorosha nyara za serikali kwenda nje ndo unamuona mwokozi??

Huu ubaguzi mbaya sana, unakutafuna tu taratibu mwishowe utakumaliza.

Kila mtawala ana mazuri na mbaya yake, tusigongane vichwa. Tuangalie mbele kujenga Tanzania mpya.
 
Back
Top Bottom