Nipo njiapanda, msaada wenu wanaJF

Nipo njiapanda, msaada wenu wanaJF

Kijana, sajili gari lako kwenye kampuni za Uber, bolt, taxify na little ride. Kwa kuwa huna ajira rasmi ni vema uendeshe mwenyewe, ukipata ajira inaliopa vizuri uza Hilo gari na uendelee na ujenzi.

Vv
asante sana mkuu kwa mawazo mazuri, ubarikiwe
 
Wakuu nilimaliza chuo mwaka 2018, nilitafuta ajira mpaka nikahisi kukata tamaa, Mungu amtupi mja wake nikabahatika kupata kazi katika kampuni binafsi uko mkoani (nje ya Dar es Salaam) hiyo kazi ni project tu ya miaka miwili, ile kazi nilifanya vizuri mpaka ikaisha kwa uaminifu mkubwa kabisa, katika kujichanga changa mpaka project inamalizika nikawa nimejichanga changa mpaka kupata kiasi flani cha pesa, nilikuwa na kiwanja maeneo ya Dar nikaweka msingi wa nyumba ya ramani niliokuwa nayo (nyumba simple, ambayo naamini uko mbeleni haiwezi nisumbua kujenga kwa kudunduliza).

Ndugu zangu nadhani mnajua sisi vijana tunakuwa na matamanio mengi sana kwenyee hii dunia, ususani sisi vijana wenye hizi age za miaka 25s-35 kunakuwa na matamanio makubwa ya kumiliki gari na nyumba nzuri, sasa kilichofuata pesa nyingine nikanunua gari aina ya IST niliagiza from japan (online buy).

Wakuu mpaka nakuja kuomba ushauri kwenu ni ili suala, Kwa sasa sina tena kazi yoyote ile ya kuniingizia kipato kabisa, maana ile project imesha isha kabisa, na kwenye account yangu nina shilingi milion moja tuu.

Naombeni ushauri wenu wa dhati kabisa, nifanyeje ili niweze japo kuiona kesho yangu ikiwa njema, sijui hii milion moja nafanyia nini ili niweze kutoka, na sijajua hii gari naifanyeje ili iweze kunitoa kimaisha, nimebaki kwenye wimbi kubwa la mawazo (kuna muda najutia kununua gari, ila imesha tokea na kuna muda mwingine nikiliangalia gari yangu naona kama sijafanya maamuzi baya sana maana nalipenda).

Sina mke wala mtoto, na nipo Dar es Salaam kwa sasa, niliwaza kuliingiza gari kwenye uber.. uko nako sijui kukoje

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu ambao siku nikikaa ntaona kabisa kweli jamiiforum ilinitoa sehemu mmoja kunipeleka sehemu nyingine, mbalikiwe sana.

Karinuni
Fungua genge kwa laki tano.Au tafuta dogo upate sehemu nzuri achome kuku utapiga pesa
 
Ukitaka kujua kwamba ushauli unaotolewa humu bado mwisho wasiku muhusika utatakiwa upambanue sana ugum wake ukoje sijaona mtualietoa ushauri unaoambatana naushuhuda hizo uber sijaona alieeleza namna inafanyika kuhusu vibari vyakufanyia biashara namengine mengi mm nafikiri usijilaum kununua gari maana hiyohela ungeweka tu sijui kama ingekuwepo
 
Ukitaka kujua kwamba ushauli unaotolewa humu bado mwisho wasiku muhusika utatakiwa upambanue sana ugum wake ukoje sijaona mtualietoa ushauri unaoambatana naushuhuda hizo uber sijaona alieeleza namna inafanyika kuhusu vibari vyakufanyia biashara namengine mengi mm nafikiri usijilaum kununua gari maana hiyohela ungeweka tu sijui kama ingekuwepo
asante sana mkuu, ubarikiwe sana, nimejaribu kupitia nyuzi za ushuhuda kuhusu uber..kwenye nyuzi zinginezo naona kuna gharama nyingi za kujisajili uko.
 
Uza gari, kiwanja na iyo ela nyingine ongezea tuzamie south Africa maana mwezi ujao tarehe 6 tunasepa mwanangu

Dizonga si hatari sana kule? Risasi Nje nje ,New Variant wa UVIKO19?? S.A vijana wengi wanajiingiza kwenye hustle za snow.(Bimbwi).
 
Ukweli nikwamba kama hujawahi kufanya biashara ni ngumu sana halafu pia mzunguko wabiashara kwasasa sio mzuri sana labda biashara ndogondogo ambazo sio lasimi sana hofu yangu hilo gari nalo linahitaji mgawo kwenye hiyo milioni lazima utalitumia naukilitumia kwasasa litahitaji huduma kwanza linaweza kukufanya ushindwe kufanya kazi frani ambazo wengi wanaona zahovyo nakuomba jitahidi kujishusha jione wakawaida usiangalie hatua ulizokuwa umefikia anza upya hauko kwenye hatua mbaya sana
 
Ukweli nikwamba kama hujawahi kufanya biashara ni ngumu sana halafu pia mzunguko wabiashara kwasasa sio mzuri sana labda biashara ndogondogo ambazo sio lasimi sana hofu yangu hilo gari nalo linahitaji mgawo kwenye hiyo milioni lazima utalitumia naukilitumia kwasasa litahitaji huduma kwanza linaweza kukufanya ushindwe kufanya kazi frani ambazo wengi wanaona zahovyo nakuomba jitahidi kujishusha jione wakawaida usiangalie hatua ulizokuwa umefikia anza upya hauko kwenye hatua mbaya sana
shukrani sana kaka, mungu akubariki sana
 
Kuuza gari na kuanza biashara mpya ni kazi sana..ni bora upige taxi kwa muda huku ukiendelea kusoma upepo..au mnadhani hii sio biashara?

Anaweza kuuza gari na kufungua biashara na isifanye fresh..mtaji ukapotea
 
Ucjari mkuu usiruhusu hofu ndani yako maisha nimagum kwawatu wengi sio peke yako .lichukulie umhimu tu mawazo mengi yametolewa hapa wengi wanania nzuri nawewe ila wazo kuu lazima litoke kwako ninaimani utatoka hatua hii mungu wetu ni mwema ukifanikisha hili usiache kusaidia wengine hata kuwatia moyo tunaokuombea utoke hatua hiyo niwengi pambana mkuu
 
Kuuza gari na kuanza biashara mpya ni kazi sana..ni bora upige taxi kwa muda huku ukiendelea kusoma upepo..au mnadhani hii sio biashara?

Anaweza kuuza gari na kufungua biashara na isifanye fresh..mtaji ukapotea
shukrani sana mkuu.
 
Ucjari mkuu usiruhusu hofu ndani yako maisha nimagum kwawatu wengi sio peke yako .lichukulie umhimu tu mawazo mengi yametolewa hapa wengi wanania nzuri nawewe ila wazo kuu lazima litoke kwako ninaimani utatoka hatua hii mungu wetu ni mwema ukifanikisha hili usiache kusaidia wengine hata kuwatia moyo tunaokuombea utoke hatua hiyo niwengi pambana mkuu
mungu akubariki sana mkuu, kwa nasaa yako kwangu.
 
Back
Top Bottom