Niolewe na yupi - ushauri wako ni muhimu

Niolewe na yupi - ushauri wako ni muhimu

masanzakona Kwahiyo hadi unakuja kuomba ushauri,hao wote wanaendeleza kukumwagilia?

Kifupi upweke ulishausahau tangu ulipoanza kasi ya kuwamudu wote watatu kwa mpigo.

hii ni baada ya kudivorce na aliyekuwa mume wangu 2007
Nini ilikuwa sababu ya divorce?

Nakushauri, usiwe na yeyote kati yao kwakuwa kama umeweza kuwamudu wote watatu, basi utakayemchagua utaishia kumdanganya tu, kwani umezoea kuchapwa na bakora tatu tofauti...vinginevyo utuambie ni aje utaweza kuzoea moja kwa maisha yako yote.

Yaani wewe umekuwa ni "nguli" la mapenzi.
 
Last edited by a moderator:
Jambo usislolijua ni sawa na usiku wa giza, ni bora kukaa kimya sio lazima kuchangia kama huna cha maana cha kusema. Uko kingono ngono thats why na mawazo yako ni ya kingono ngono na unawaza ngono tu, pole!

wewe hivi kweli una umri huo ulioandika hapa?maana naona kama kichwani umeme mdogo?
 
du!!!!dada huo ufisadi, wenzio hawana hata mmoja wewe una watatu?Angalia wasije kuwa wanakuigizia tu kumbe wametamani tu asset twako!Akili ku mkichwa!
 
Nimepitia thread hii, naona people zinawaza mgegedo tu hivi hamwezi kushauri hadi mmponde mtu kwamba anatoa k kwa watu 3. Mshautini mtu kutoka na kile anachoomba kushauriwa

Mleta thread, wewe ndo unawajua hao watu vizuri so fuata moyo wako unavyokuelekeza
 
Dunia duara hii kaka, mwingine analia hatongozwi, hata wa kumuambia jambo hayupo lakini msanzakona anawashortlist

du!!!!dada huo ufisadi, wenzio hawana hata mmoja wewe una watatu?Angalia wasije kuwa wanakuigizia tu kumbe wametamani tu asset twako!Akili ku mkichwa!
 
na wewe unampenda yupi...?naona unayapa kipaumbele mambo ya "ana nyumba" na "anataka nimzalie watoto wawili" kipaumbele kuliko furaha ya moyo wako..kama ukikosa furaha na amani hivyo vingine vyote havina maana...
Mkuu muda kidogo sijakuona maeneo haya, pole na majukumu ya hapa na pale najua unaweza kuwa upo humuhumu lakini unacheza maeneo tofauti

Kazi njema mkuu
 
Tuache kujadili zinaa hapa. Huyu mama anawachanganya wanaume 3, na kila mmoja anajiona ni yeye pekee. Ushauri wangu, kama unamwamini Kristo, kimbia haraka Kanisani ukaombe msamaha kwa zinaa unayofanya. Hii ni Kwaresma, Mwogope Mungu wewe!
 
Nimepitia thread hii, naona people zinawaza mgegedo tu hivi hamwezi kushauri hadi mmponde mtu kwamba anatoa k kwa watu 3. Mshautini mtu kutoka na kile anachoomba kushauriwa

Mleta thread, wewe ndo unawajua hao watu vizuri so fuata moyo wako unavyokuelekeza

ram; mgegedo ndo chanzo cha mada lazima kitafsiriwe ili kupata jibu na ushauri kwa mleta mada.
 
ila nilichojifunza kwa wanawake hakuna mkubwa wala mdogo wote wanategemea akili za kutoka nje hata kama watoa ushauri hawana vigezo! duh hata kwenye mapenzi na ndoa mnaomba hata wasio na ndoa ushauri wa ndoa zenu! mawanawake banaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa ptuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!
 
wewe hivi kweli una umri huo ulioandika hapa?maana naona kama kichwani umeme mdogo?
kama sio ngono watoto wako na mfanya kazi hawawezi kukutoa upweke? wewe unataka ngono halalishi kwa mwavuli wa wa upweke! na kama wewe ni mkiristo unajua hao wawili huwezi kuoana nao kwa sababu dini itakuruhusu kama mumweo wa kwanza amekufa! jibu ni kwamaba kama unataka kualalisha ngono yako ni uolewe na muislam! unatupotezea muda hapa wakati unajua jibu! halafu once a widow always a widow!
 
Kwani wewe unampenda yupi, olewa na yule umpendaye. Labda kama unaolewa for the sake of kuolewa tu.
 
Kwanza na mshukuru Mungu kwa rehema na baraka mbali mbali anazonijalia katika maisha yangu kila iitwapo leo.

Wana-MMU ninakuja kwenu nikihitaji ushauri juu ya hili suala, kiukweli maisha ya upweke yamenichosha, hii ni baada ya kudivorce na aliyekuwa mume wangu 2007. Mimi ni mama nina watoto wawili, 36yrs, mkristo. Nina nyumba yangu mwenyewe na asset kadhaa, baada ya kuchoshwa na upweke nimeona ni wakati muafaka wa kupata mwenzi mwingine. Nayamudu maisha yangu vizuri tu tatizo ni huo upweke tu, so naombeni mnishauri kuhusu hawa watu hapa chini.


1. Huyu ni mkaka 38yrs hajawahi kuoa ila ana mtoto mmoja, ni mafanyabiashara lakini pia ni mwanafunzi wa chuo fulani hapa nchini. Ana kiwanja, hajajenga so anaishi nyumba ya kupanga, ameonesha nia ya dhati ya kutaka kuishi na mimi pamoja na watoto wangu ila atapenda pia nimzalie watoto wawili. Nikifikiria hapo pa kuzaa watoto wawili nachanganyikiwa kabisa

2. Huyu ni mkaka, 36yrs, hajawahi kuoa ila na mtoto mmoja, ni mwajiriwa kwenye NGO na anasoma online chuo kikuu kimoja huko marekani. Ndio kwanza ameanza ujenzi wa nyumba yake, ananipenda mimi na watoto wangu, nae anapenda Mungu akijalia nimzalie watoto wawili. Hapo kwenye kuzaa nachanganyikiwa lkn pia namuona bado ana ujana mwingi

3. Huyu ni baba, 45yrs, ana familia yake, ana mke na watoto 3, ameajiriwa ofisi ya mtu binafsi, ana nyumba kadhaa, ananipenda kwa dhati, anaipenda familia yangu sana na anajitoa kwa hali na mali, kama tukioana anapenda nimzalie mtoto mmoja tu. Naweza kumzalia mtoto mmoja kama Mungu atapenda, tatizo ni hiyo familia na dini, yeye ni muislam, so anataka mimi niwe bi mdogo

Ushauri wako please, ukiona haikuhusu tafadhali potezea

mfupa uliyemshinda fisi binadamu utauweza? halafu mi nashangaa unajiweza halafu unataka kuolewa, si uowe tu mbona wenzio siku hizi wanaoa?
 
masanzakona Kwahiyo hadi unakuja kuomba ushauri,hao wote wanaendeleza kukumwagilia?

Kifupi upweke ulishausahau tangu ulipoanza kasi ya kuwamudu wote watatu kwa mpigo.


Nini ilikuwa sababu ya divorce?

Nakushauri, usiwe na yeyote kati yao kwakuwa kama umeweza kuwamudu wote watatu, basi utakayemchagua utaishia kumdanganya tu, kwani umezoea kuchapwa na bakora tatu tofauti...vinginevyo utuambie ni aje utaweza kuzoea moja kwa maisha yako yote.

Yaani wewe umekuwa ni "nguli" la mapenzi.

Hakuna mapenzi ya hivo, hawapendi wote kama kweli kishatembea nao wote, huo sasa ni umalaya
 
kama sio ngono watoto wako na mfanya kazi hawawezi kukutoa upweke? wewe unataka ngono halalishi kwa mwavuli wa wa upweke! na kama wewe ni mkiristo unajua hao wawili huwezi kuoana nao kwa sababu dini itakuruhusu kama mumweo wa kwanza amekufa! jibu ni kwamaba kama unataka kualalisha ngono yako ni uolewe na muislam! unatupotezea muda hapa wakati unajua jibu! halafu once a widow always a widow!

acha kukurupuka wewe hayo maneno yako mjibu mleta uzi sio mimi tafadhari
 
yaan ni kazi kwelikweli.ila angalia anaye kufaa na kuupendeza moyo wako kasha uamue.
 
Back
Top Bottom