Kama upo dar maeneo ya kkoo, mjini posta, msasani, peninsular, upanga, kinondoni ya morocco, mikocheni, masaki obey, n.k Kuna fiber za kutosha kama zuku, Raha, Gofiber, n.k
fibre ni internet ya waya, unavutiwa waya hadi sehemu ulipo nyumbani kwako, ni internet ya waya lakini kuna kifaa utapewa kinaitwa wireless router, hiki kifaa kitakuwezesha utumie internet kwa wifi ya simu au laptop ama vifaa vingine vyenye wifi.
Kwa mfano internet ya fibre ya zuku inapatikana kino, kariakoo, msasani, peninsular, upanga,n.k utalipia elf 70 au zaidi (kuna vifurushi vina speed kali sana hivi vinafaa kama watumiaji mpo wengi)
utaweza kutumia internet bila kikomo, speed ni nzuri hata kwa kifurushi cha chini cha elf 70 ambacho unaweza kudownload mb 1 (nasikia sikuhizi ni 2) kwa sekunde, ni speed nzuri hata videos utaangalia bila kukwama na hata kwenye kudownliad utaweza kudownload muvi hata ya gb 1 kwa takribani dakika 18 tu, kitu kizuri zaidi ni hakuna kikomo, hakuna mambo ya ukifikisha gb kadhaa speed inashuka,.makampuni mengi gharama za vifaa na kuletewa waya wa internet hadi kwako ni bure ikiwa utalipia bando la mwezi au miezi kadhaa.
changamoto ni kwmaba haipo kila sehemu dar na pia inabidi uwe mazingira ya nyumbani au ofisini ili kutumia wifi ya kifaa chao.
Kwa waliopo nje ya maeneo hayo au mikoani ttcl nao wana fibre sema nasikia ni gharama.
Kiukweli ni pigo kubwa, saizi wasanii wasahau kupata views nyingi kama zamani huko youtube, Internet ilikuwa silaha yetu kwa kuinua wasanii ila kwa hali hii jumna bovu limewaangukia