Nini Maana ya "Tanga"?!

bullshark

Senior Member
Jan 28, 2018
132
119
.. Juzi natoka kazini, getini nikakutana na mlinzi. (ni mzee hivi kdg ameniambia eti ni mnyantuzu japo kabila hili silijui). Katika kutambulishana maana mimi ni mgeni hapa ofisini nikamjuza jina langu na mkoa nitokapo..... Yaani Tanga.. Naye hakukawia kuniuliza.... Nini maana ya Tanga?... Nikajiumauma pale... Lakini sikumpa jibu sahihi... Hivi Nauliza... Tanga ina maana yoyote zaidi ya Tanga la msiba au tanga la jahazi?! Au tanga ni kutangatanga yaani kuhangahika?
 
.. Juzi natoka kazini, getini nikakutana na mlinzi. (ni mzee hivi kdg ameniambia eti ni mnyantuzu japo kabila hili silijui). Katika kutambulishana maana mimi ni mgeni hapa ofisini nikamjuza jina langu na mkoa nitokapo..... Yaani Tanga.. Naye hakukawia kuniuliza.... Nini maana ya Tanga?... Nikajiumauma pale... Lakini sikumpa jibu sahihi... Hivi Nauliza... Tanga ina maana yoyote zaidi ya Tanga la msiba au tanga la jahazi?! Au tanga ni kutangatanga yaani kuhangahika?
Tanga ni kibondei
Maana yake ni shamba
 
Tanga inaweza maanisha lile shuka wanaloweka kwenye jahazi.

250px-Dhow_znz.jpg


Tanga pia inamaanisha kuzurura au kutembea sana au kutotulia sehemu moja, mfano mtu anaweza akasema bulshark kwa kutanga tanga tu hajambo, leo yupo jukwaa la michezo, kesho yupo jukwaa la siasa etc.

Tanga pia humaanisha nguo za ndani za kike, zina vikamba kama bikini lakini sio exactly bikini kwani nyuma zinakuwa pana kidogo.

Tanga pia humaanisha kundi la nyota.

source ya vingi wikipedia
Tanga - Wikipedia, kamusi elezo huru
 
Back
Top Bottom