Nini kifanyike kuwepo kwa single mother

Iziwari

Member
Jun 5, 2021
76
56
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wanawake wanao lea Watoto wenyewe katika jamii zetu. Sio kwamba ni sifa mbaya lahasha, bali ni moja ya mfumo unaoanza kuzoeleka na kufanywa kuwa kama ndio mfumo wa Maisha. Na nikisema wanalea wenyewe namaanisha bila kuwa na baba kama msimamizi.

Lengo kuu la kuandika kuhusu hili, ni kwa sababu tunahitaji suluhisho. Na suluhisho hili lina lengo la kama kupunguza au kuwezesha jambo hili kufanyika kwa njia ambayo haileti madhara katika jamii zetu.

Lakini kwanini tupunguze wanawake wanao lea Watoto wenyewe katika jamii zetu? au jambo hili ni kweli linaweza kuleta madhara kwa kipindi kijacho?

Na tunawezaje kupunguza swala hili au nini kifanyike?

Pia naweza kuuliza ni namna gani tunaweza kuinua mfumo wa kipato katika jamii zetu. Tukizingatia kuwa wakina dada hawa wanahitaji namna nzuri ya kujipatia kipato?

Maswali haya ndio ntajaribu kuyajibu kwa wale watakao endelea kusoma. Na hii ni kwasababu haya yote yana suluhisho rahisi sana kulinganisha na vile jinsi ulivokuwa unafikiria.

Kwa maana, wanawake wanao lea Watoto bila msaidizi katika jamii zetu ni wanawake wenye upendo na kujali Watoto wao sana.

Nimeshuhudia kwa wengi wakiwa wanapambana kujitengenezea kipato na wakiwa wanasomesha Watoto wao. Na kuhakikisha Watoto wanapata huduma na matibabu pale wanapopata tatizo lolote.

Wanawake hawa wakiwa katika hali ya kutafuta na kupambana Maisha. wamekutana na changamoto nyingi lakini wamekuwa wakitanguliza upendo kwa Watoto wao na kuzivuka changamoto.

Cha kwanza wanastahili pongezi na kwa kweli wanastahili sifa ya kuitwa Mama Afrika.

Umaskini umekuwa bado ni tatizo kubwa katika jamii zetu. Na tunakumbuka kuna Umaskini, ujinga, na maradhi. Kama maadui wakubwa watatu tunaopambana nao kwenye jamii zetu(J.k Nyerere).

Tukirudi kwenye mada kuu kwamba ni nini kifanyike ili kumkomboa mwanamke, mwenye jukumu la kulea Watoto wake bila msaidizi?

Tukianza na wanaume wanaoacha Watoto wao bila ya kujali wanaishije, na wanakuwa katika hali gani. Hili ni swala ambalo halimpendezi kabisa Mwenyezi Mungu. Na tukirudi kwenye swala la maadili hii ni picha kuu ya kuporomoka kwa maadili katika jamii zetu.

Na hii inapelekea hata Watoto wanaokuwa katika hali ya kumkosa baba, kuwa wapweke na kutaka kulipiza kisasi. Kitu ambacho kinaendelea kujenga jamii mbovu na yenye sifa mbaya.

Nini kifanyike kwanza kwa wakina baba?

Cha kwanza cha kufanya ni maandalizi. Maandalizi ya kuyapokea majukumu ambayo tayari yamesha kufikia.

Kumbuka Maisha hayapo ili kukimbia majumkumu. Bali Maisha yana mpa amani yule tu, ambae anajituma kuyatimiza majukumu yake.

Hakuna kinacho jificha apa, maana hata ulimwengu ukikupa nini cha kukufurahisha, kitaishia kuwa ni jukumu lingine lililoongezeka maishani mwako.

Mfano kuna mtu labla kafrahi sana kununua gari zuri kuliko mwenzake. Bila ya kujua kuwa gari linapoongezeka uzuri ndio pia na jukumu la kulitunza linaongezeka.

Kila kinachotokea maishani mwa mtu kama ni kitu kizuri sana. Iwe amepata udhamini wa Kwenda kusoma nje ya nchi au amepata safari ya Kwenda mbali. Yote haya ni majukumu na kama haupo tayari kuyafanya atayashindwa.

Hakuna jukumu baya au zuri.

Wakina baba naombeni mnisikilize hapa. Hakuna jukumu baya au zuri. Kila jukumu limewekwa mbele yako kwa sababu Mungu anajua unaliweza.

Sa nyingine majukumu tunajitakia wenyewe. Na hapa wengi wetu ndio wanaanza kukasirika na akati ni kweli.Mfano, kuna watu wawili, mmoja alienda kununua mbuzi na mwingine akaenda kununua kuku. Alienunua mbuzi alijua kila siku ni kuhakikisha mbuzi anatoka nje kula majani. Na alie nunua kuku alijua ni kuwafungulia watoke nje wajitaftie. Wote walikuwa sawa lakini tunajifunza , walikuwa na maamuzi tofauti ya kuchagua mifugo kulinganisha na kile walichokiona kinawafaa.

Na tukirudi kwenye mada, mfano huu unatufundisha kufanya maamuzi ndani ya uwezo wetu. Kila mmoja anaruhusiwa kufanya maamuzi. Lakini maamuzi yeyote yalio nje ya uwezo wetu yanafananishwa na kujitoa muhanga.

Ni kama Kwenda benki kukopa milioni mia moja bila ya kujua jinsi utakavoirudisha. Ni maamuzi mazuri lakini pia utakuwa umefanya kujitoa muhanga bila ya kupiga mahesabu.

Tukianza kujifunza kwa namna yeyote ile. Inabidi tujifunze namna ya kufanya maamuzi. Na sana sana wakina baba ndio nawazungumzia hapa.

Kumbuka kuna umaskini, ujinga na maradhi.

Ujinga ni chanzo kikuu cha umaskini. Tukubali au tukatae hii ndio kweli.

Tukirudi kwenye mada ya maamuzi, chochote kinachotokana na maamuzi yako, kinatakiwa kuwa na elimu ndani yake. Narudia tena, mfululizo wa maamuzi yako yanatakiwa kutokana na elimu ulionayo kuhusu kile unachotaka kukifanyia maamuzi.Mfano Mtu mwenye uwezo wa kufuga kuku na kufanikiwa, ni yule mwenye elimu yote na uzoefu wa kutosha kuhusu ufugaji wa kuku.

Tumeshaondoka kwenye karne ya kufanya maamuzi bila ya kufikiria. Na neno fikiri kabla ya kutenda ndio neno la karne hii ya 21 ishirini na moja.

Elimu ndio chanzo pekee cha kupambana na ujinga.

Sio kwamba nasema watu wasio na elimu wote ni wajinga, lahasha. Namanisha kuwa, kuna njia nyingi za kujifunza vitu sasahivi.

Mfano unataka kujua kuhusu elimu ya uzazi utaipata haraka sana. Iwe ni Hospitali au kiliniki iliopo karibu na wewe. Au mtandaoni.

Tusijitoe ufahamu, maana kuitafuta elimu kuhusu kitu chochote unachotaka. Utaipata mtandaoni. Hii ndio karne pekee ambayo kila mtu ni msomi.

Kwaio usifikiri nazungumzia wasomi wengine Zaidi yako. Kama unajua kusoma basi jifunze kusikiliza na kufanya maamuzi sahihi.

Wakina baba wanahitajika kujua moja kwa moja jukumu walilo nalo; kabla hawajafanya maamuzi ya kupata Watoto bila maandalizi sahihi.

Na wale wababa ambao tayari wapo kwenye majukumu ya Watoto bila elimu sahihi. Basi ni vizuri wakaanza kujifunza jinsi gani ya kupambana na hayo majukumu.

Lakini pia, sababu za wanawake kuwa single mother zipo nyingi. Tofauti na hii sababu ya wanaume kukimbia majukumu.

Na sababu zingine zote za ziada sintazitaja hapa.

Jinsi gani ya kumkomboa single mother.

Nikisema single mother namaanisha mwanamke mwenye jukumu la baba na mama katika familia.

Basi tuanze na njia ya kwanza.

Tunajua kuwa umaskini ni adui wa kwanza wa haki. Na umaskini ni adui mkorofi sana, ukitaka kupigana nae hadi kumshinda inahitaji nguvu ya ziada(Elimu).

Nikisema nguvu, Tukumbuke kuwa umoja ni nguvu.

Cha kwanza cha kufanya ni kutengeneza mifumo mingi na mizuri kwa ajili ya kusaidia Watoto. Kuwapa chakula, elimu, makazi na malazi. Tunafahamu vituo vya kulelea Watoto. Vimekuwepo kwa muda mrefu sana. Lakini vimekuwa kama sehemu ambazo za kujiuliza sana kabla ya mtu kumpeleka mtoto wake.Hasa kwa vijana wakike na wakiume wa miaka hii.

Na kwanini iwe ivo; Ni kutokana na jinsi ambavyo tumejitengenezea akilini mwetu. Hatuna elimu ya kutosha kuhusu vituo hivi. Sawa unaweza ukasema, Watoto wapo wengi, watatosha kwenye hivi vituo vilivyopo.

Au ukasema sintapenda mtoto wangu awepo kwenye vituo kama hivi. Na bado tutarudi kwenye swala zima la kutambua kitu kwa undani sio kwa hisia. Kwa sababu vituo hivi havipo kukusimanga kwamba wewe ni maskini. Bali vipo kukupunguzia jukumu kwa muda Fulani mpaka utakapo pata mwelekeo mzuri katika mapambano yako.

Ndio tunajua vituo hivi vya watoto, havipo vingi na pia vingine havina muonekano mzuri. Lakini izi ndio sehemu ambazo zikiboreshwa zitawasaidia sana wamama. Uboreshwaji wake uje na kauli mbiu mpya kwamba. Muhifadhi mtoto wako kwa kipindi Fulani mpaka utakapopata uwezo wa kumuendeleza mwenyewe.

Waliopo tayari kuanzisha hii wangewasaidia sana Watoto. Na wanaweza wakachangia mada hapo chini.

Kingine cha kufanya ili kuwakomboa wamama hawa.

Kutengeneza vituo vingi sana vya ujasiria mali. Mwanamke wa kiafrika anapata mafanikio yake pale ambapo anakuwa mjasiriamali. Kuna vikundi vingi vinajulikana vya kutengeneza sabuni, na vya ufugaji.

Lakini bado havijawa na mwendelezo mzuri kwa sababu watu bado hawafikirii kuviendeleza. Nikimaanisha sa nyingine vimekuwa vikundi vya kichoyo sana. Wamekuwa wakibania hela na kuchagua watu wao.

Kwaio kinachohitajika apa ni kuwa na vikundi vinavyoanzishwa na mashirika makubwa yenye pesa za kutosha. Maana watu ndio chanzo kikuu cha pesa, basi watu wapewe elimu ya kutumia wingi wao na umoja wao kama chanzo cha kujiongezea kipato.

Kila mtu ana Wazo la kupata mtaji, nini kifanyike.



Wazo linalohusu kupata mtaji ni wazo linalosumbua wajasiriamali wengi.Na ni Baada ya kupata elimu au wazo ndio unakuwa tayari kutafuta huo mtaji. Na Mtaji ni kweli unahitajika, maana lazima ,vifaa ,nauli , chakula mawasiliano, na mavazi vyote ni gharama hata kabla haujaanza kuchapa io kazi. Hii inapelekea watu kukata tamaa na kushindwa kuendelea katika mapambano yao ya kila siku. Vikundi vya kutoa mikopo vipo na tutaunga group moja la telegram kwa ajili ya wale wenye vituo vya Watoto na wale wenye vikundi vya kutoa mikopo. Yawezekana kila kitu kikawa kilishafanyiwa ufumbuzi sema watu wenyewe ndio hawana taarifa sahihi.Lakini nimekuja na taarifa sahihi kwamba unaweza ukaanza Maisha yako kwa upya tena kwa kupitia izo njia mbili nlizo shauri hapo.



Wengine mtaendelea kuchangia mawazo yenu baada ya haya yakwangu.



Angalizo.

hakikisha unatoa wazo la kusaidia.Maana Mungu amekupa akili kama zawadi na haujui imetoka wapi. Amekupa nguvu na uwezo wa kuiona leo kwa kusudi lake, ili na wewe uwe msaada kwa watu wote. Kwaio andika kitu chenye kuleta tija na kitakachofanya wakinamama hawa wapate suluhisho.
"you must forgive and forget for the sake of life".
 
Wasimbe huku usukumani wanazaraulika sana, hata kwenye uongoz wa kitongoji hawezi kupata msimbe. Masimbe ni mauza k tu, hata watoto kisimbe hutaniwa popote.
Kundi la wasomi ndo wanataka kulasimisha usimbe, lakn jamii inawaona wasimbe kama shimo la kutupa shahawa chafu.

Pumbavu zenu wasimbe wote except wajane.
 
Wasimbe huku usukumani wanazaraulika sana, hata kwenye uongoz wa kitongoji hawezi kupata msimbe. Masimbe ni mauza k tu, hata watoto kisimbe hutaniwa popote.
Kundi la wasomi ndo wanataka kulasimisha usimbe, lakn jamii inawaona wasimbe kama shimo la kutupa shahawa chafu.

Pumbavu zenu wasimbe wote except wajane.
Tena pumbavu haswaa
 
Wanasema kinga zinawasha, hazina ladha, hawataki kula pipi na maganda🤔

Mungu amekupa akili, unajua ukifanya mapenzi utapata mimba, ukipata mimba utazaa, ukizaa utalea.

Kama hutaki kuzaa, zuia mimba.

Ukishazaa lea mtoto usisumbue watu.
 
SINGO MAZA, SIKU ZOTE WANA JIONYESHA KWA WATU WANA UWEZO WA KUPAMBANA KULEA MTOTO/WATOTO WAO WENYEWE.

HAWELEZI UKWELI, JUU YA UGUMU WANAO UPITIA.KIASI KWAMBA WASICHANA WENGI WANAINGIA KWENYE MFUMO HUO WA MAISHA. WAKIJUA NI RAHISI RAHISI.
UKIISHAKUA SINGO MAZA, NDIO UNAJUA HATA HAWA WENGINE WANALEA WATOTO KWA MSAADA WA WAUME ZA WENGINE.CHUNGUZA!!
 
Wasimbe huku usukumani wanazaraulika sana, hata kwenye uongoz wa kitongoji hawezi kupata msimbe. Masimbe ni mauza k tu, hata watoto kisimbe hutaniwa popote.
Kundi la wasomi ndo wanataka kulasimisha usimbe, lakn jamii inawaona wasimbe kama shimo la kutupa shahawa chafu.

Pumbavu zenu wasimbe wote except wajane.
Si bure,kuna kitu ulifanywa
 
Hasa wakristo ndo wanaongoza yule wolper anaolewa ana watoto wawili tayari nandi aliolewa na mimba halafu baadae wanabariki ndoa ila hawa jamaa wasanii kweli
 
Hasa wakristo ndo wanaongoza yule wolper anaolewa ana watoto wawili tayari nandi aliolewa na mimba halafu baadae wanabariki ndoa ila hawa jamaa wasanii kweli
Ndoa kwa jamii ya sasa ni ndoa kwa kiasi fulani wolper hajakosea kalinda maslahi ya wanae hata nandy bora ndoa imefanyika basi kila la kheri ..

Tupend kuwaombea kheri ni hatua kubwa sana duniani.
 
Uzi wako unajikanyaga na kujicomplicate. Maana kuna sehemu unasema sio vibaya halafu mbele yake unasema tunafanyaje kusolve hili tatizo.

Mara tuwapongeze mara tuwasaidie wengine wasifike huku. So bado wewe binafsi una mgogoro wa ndani ya nafsi kushindwa kuelewa kama usingle mother ni tatizo katika jamii au ni baraka katika jamii.

Hebu jua unasimama wapi kwanza.
 
Uzi wako unajikanyaga na kujicomplicate. Maana kuna sehemu unasema sio vibaya halafu mbele yake unasema tunafanyaje kusolve hili tatizo.

Mara tuwapongeze mara tuwasaidie wengine wasifike huku. So bado wewe binafsi una mgogoro wa ndani ya nafsi kushindwa kuelewa kama usingle mother ni tatizo katika jamii au ni baraka katika jamii.

Hebu jua unasimama wapi kwanza.
mimi pia nimeona nisichangie chochote maana! mwenye uzi tayar yupo upande wa singo mama.
Naona anajarbu kuwasemea hapa .
Japo singo mama wengi wenye nimewahi kutana nao kiukweli mh!

me naamini ungeanza na mambo yanayopelekea usingo mama kwanza! me nakupa moja tu mengine watachangia wengine
FEMENISM
Hii movement inawafelisha sana hao singo mama.
Badala ya kuwakemea ninyi mnawasifia mnawapaisha nakuwaona wao ni victim katika hili. ila deep down wanajijua wao ndio wali orchestra mpango mzima mpaka mtoto kutokea.
 
mimi pia nimeona nisichangie chochote maana! mwenye uzi tayar yupo upande wa singo mama.
Naona anajarbu kuwasemea hapa .
Japo singo mama wengi wenye nimewahi kutana nao kiukweli mh!

me naamini ungeanza na mambo yanayopelekea usingo mama kwanza! me nakupa moja tu mengine watachangia wengine
FEMENISM
Hii movement inawafelisha sana hao singo mama.
Badala ya kuwakemea ninyi mnawasifia mnawapaisha nakuwaona wao ni victim katika hili. ila deep down wanajijua wao ndio wali orchestra mpango mzima mpaka mtoto kutokea.
Very true

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Usingle maza ni janga la dunia na one day tutazikumbuka ndoa sana japo inaweza kuwa too late.
Hawa watoto wanaozaliwa kwa single mothers tusitegemee waje wawe na ndoa bora huko mbele ni ngumu mno hasa single maza mwenyewe akiwa ni yule aliyeachika kwenye ndoa tena kwa vurugu zake binafsi.Nasema haya nikijua fika kuna single mothers wengine wamejiunda fikiria mtu kafiwa mme yupo na 30's afu anashindwa kuolewa utasema hajajitakia usingle mother?( Huyu alikuws kwenye ndoa mguu pande kifo cha mume kimemlainishia kuingia side iliyo ya wengi yaani ile ya kukataa ndoa hivyo anaona hapaswi kurudi kwenye ndoa maana anahisi kubanwa)

Wake za watu kadhaa wamewahi kutaka kuingia kwenye mahusiano na mimi ila wanadai niwajengee kijumba hata kama ni chumba na sebule ili waishi kivyao baada ya kuwaacha waume zao(walisema haya cos waliona nina uwezo wa kuwahudumia hata kama watakuwa nje ya ndoa zao) kwa utafiti wangu huo niliishia kusikitika na kukataa ukaribu nao maana tayari niligundua wanawake wengi fikra zao hazifikirii kesho ya ulimwengu bora ambao wao ni wajenzi muhimu hasa katika nyanja ya maadili , hii ilimaanisha wanatamani mfumo huu wa usingle maza unaoshika kasi sana japo kiundani ni mgumu kwa mwanamke si tu katika nyanja za kimaisha za kawaida bali hata za kidini haziwezi kuukubali.

Mimi ningeona fahari sana kama hawa single mothers wangejikita kuishi maisha ya kitaua yaani wamezikataa ndoa kwa sababu fulani maybe za uzinzi kwa waume zao lakini wameenda kutengeneza maisha yasiyouishi uzinzi , sasa mtu anamwacha mme wake afu anaenda kukaa single kila siku anazini ili apate mtaji na hata pesa ya kurun maisha.Hii ilikuwa na faida ipi sasa? Si heri angekomaa na ndoa yake tu?

Wanawake wajue wao wana jukumu kubwa la kulinda kizazi cha ulimwengu huu ,kikiwa kibaya maana yake dunia ijayo itakuwa yenye kusikitisha sana kimaadili haiyumkini hata mahusiano ya kijamii yatakuwa mabaya kiasi kwamba hata wao watayahisi maumivu waliyoyajenga kwa miaka mingi sana bila kujua watakapotuletea kizazi kisichojali.

Rai yangu kwa masingle mothers ,oleweni muishi maisha matakatifu yanayoandaa kizazi bora cha kesho na zaidi nawaasa acheni kupandikiza sumu mbaya kwa watoto wenu kwamba hakuna haja ya uwepo wa ndoa maana mnawaharibia wana wenu maisha ya baraka.Wewe kama yalikushinda mtie moyo mwanao wa kiume kwamba asiige maisha yako na aamini zaidi kwenye mipango ya Mungu hasa juu ya ndoa.
Mkumbushe kwamba anapaswa kuiga mazuri yako na ayakatae mabaya yako kwa vitendo tena mweleze bila kuona soni,nawe utabarikiwa.
 
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wanawake wanao lea Watoto wenyewe katika jamii zetu. Sio kwamba ni sifa mbaya lahasha, bali ni moja ya mfumo unaoanza kuzoeleka na kufanywa kuwa kama ndio mfumo wa Maisha. Na nikisema wanalea wenyewe namaanisha bila kuwa na baba kama msimamizi.

Lengo kuu la kuandika kuhusu hili, ni kwa sababu tunahitaji suluhisho. Na suluhisho hili lina lengo la kama kupunguza au kuwezesha jambo hili kufanyika kwa njia ambayo haileti madhara katika jamii zetu.

Lakini kwanini tupunguze wanawake wanao lea Watoto wenyewe katika jamii zetu? au jambo hili ni kweli linaweza kuleta madhara kwa kipindi kijacho?

Na tunawezaje kupunguza swala hili au nini kifanyike?

Pia naweza kuuliza ni namna gani tunaweza kuinua mfumo wa kipato katika jamii zetu. Tukizingatia kuwa wakina dada hawa wanahitaji namna nzuri ya kujipatia kipato?

Maswali haya ndio ntajaribu kuyajibu kwa wale watakao endelea kusoma. Na hii ni kwasababu haya yote yana suluhisho rahisi sana kulinganisha na vile jinsi ulivokuwa unafikiria.

Kwa maana, wanawake wanao lea Watoto bila msaidizi katika jamii zetu ni wanawake wenye upendo na kujali Watoto wao sana.

Nimeshuhudia kwa wengi wakiwa wanapambana kujitengenezea kipato na wakiwa wanasomesha Watoto wao. Na kuhakikisha Watoto wanapata huduma na matibabu pale wanapopata tatizo lolote.

Wanawake hawa wakiwa katika hali ya kutafuta na kupambana Maisha. wamekutana na changamoto nyingi lakini wamekuwa wakitanguliza upendo kwa Watoto wao na kuzivuka changamoto.

Cha kwanza wanastahili pongezi na kwa kweli wanastahili sifa ya kuitwa Mama Afrika.

Umaskini umekuwa bado ni tatizo kubwa katika jamii zetu. Na tunakumbuka kuna Umaskini, ujinga, na maradhi. Kama maadui wakubwa watatu tunaopambana nao kwenye jamii zetu(J.k Nyerere).

Tukirudi kwenye mada kuu kwamba ni nini kifanyike ili kumkomboa mwanamke, mwenye jukumu la kulea Watoto wake bila msaidizi?

Tukianza na wanaume wanaoacha Watoto wao bila ya kujali wanaishije, na wanakuwa katika hali gani. Hili ni swala ambalo halimpendezi kabisa Mwenyezi Mungu. Na tukirudi kwenye swala la maadili hii ni picha kuu ya kuporomoka kwa maadili katika jamii zetu.

Na hii inapelekea hata Watoto wanaokuwa katika hali ya kumkosa baba, kuwa wapweke na kutaka kulipiza kisasi. Kitu ambacho kinaendelea kujenga jamii mbovu na yenye sifa mbaya.

Nini kifanyike kwanza kwa wakina baba?

Cha kwanza cha kufanya ni maandalizi. Maandalizi ya kuyapokea majukumu ambayo tayari yamesha kufikia.

Kumbuka Maisha hayapo ili kukimbia majumkumu. Bali Maisha yana mpa amani yule tu, ambae anajituma kuyatimiza majukumu yake.

Hakuna kinacho jificha apa, maana hata ulimwengu ukikupa nini cha kukufurahisha, kitaishia kuwa ni jukumu lingine lililoongezeka maishani mwako.

Mfano kuna mtu labla kafrahi sana kununua gari zuri kuliko mwenzake. Bila ya kujua kuwa gari linapoongezeka uzuri ndio pia na jukumu la kulitunza linaongezeka.

Kila kinachotokea maishani mwa mtu kama ni kitu kizuri sana. Iwe amepata udhamini wa Kwenda kusoma nje ya nchi au amepata safari ya Kwenda mbali. Yote haya ni majukumu na kama haupo tayari kuyafanya atayashindwa.

Hakuna jukumu baya au zuri.

Wakina baba naombeni mnisikilize hapa. Hakuna jukumu baya au zuri. Kila jukumu limewekwa mbele yako kwa sababu Mungu anajua unaliweza.

Sa nyingine majukumu tunajitakia wenyewe. Na hapa wengi wetu ndio wanaanza kukasirika na akati ni kweli.Mfano, kuna watu wawili, mmoja alienda kununua mbuzi na mwingine akaenda kununua kuku. Alienunua mbuzi alijua kila siku ni kuhakikisha mbuzi anatoka nje kula majani. Na alie nunua kuku alijua ni kuwafungulia watoke nje wajitaftie. Wote walikuwa sawa lakini tunajifunza , walikuwa na maamuzi tofauti ya kuchagua mifugo kulinganisha na kile walichokiona kinawafaa.

Na tukirudi kwenye mada, mfano huu unatufundisha kufanya maamuzi ndani ya uwezo wetu. Kila mmoja anaruhusiwa kufanya maamuzi. Lakini maamuzi yeyote yalio nje ya uwezo wetu yanafananishwa na kujitoa muhanga.

Ni kama Kwenda benki kukopa milioni mia moja bila ya kujua jinsi utakavoirudisha. Ni maamuzi mazuri lakini pia utakuwa umefanya kujitoa muhanga bila ya kupiga mahesabu.

Tukianza kujifunza kwa namna yeyote ile. Inabidi tujifunze namna ya kufanya maamuzi. Na sana sana wakina baba ndio nawazungumzia hapa.

Kumbuka kuna umaskini, ujinga na maradhi.

Ujinga ni chanzo kikuu cha umaskini. Tukubali au tukatae hii ndio kweli.

Tukirudi kwenye mada ya maamuzi, chochote kinachotokana na maamuzi yako, kinatakiwa kuwa na elimu ndani yake. Narudia tena, mfululizo wa maamuzi yako yanatakiwa kutokana na elimu ulionayo kuhusu kile unachotaka kukifanyia maamuzi.Mfano Mtu mwenye uwezo wa kufuga kuku na kufanikiwa, ni yule mwenye elimu yote na uzoefu wa kutosha kuhusu ufugaji wa kuku.

Tumeshaondoka kwenye karne ya kufanya maamuzi bila ya kufikiria. Na neno fikiri kabla ya kutenda ndio neno la karne hii ya 21 ishirini na moja.

Elimu ndio chanzo pekee cha kupambana na ujinga.

Sio kwamba nasema watu wasio na elimu wote ni wajinga, lahasha. Namanisha kuwa, kuna njia nyingi za kujifunza vitu sasahivi.

Mfano unataka kujua kuhusu elimu ya uzazi utaipata haraka sana. Iwe ni Hospitali au kiliniki iliopo karibu na wewe. Au mtandaoni.

Tusijitoe ufahamu, maana kuitafuta elimu kuhusu kitu chochote unachotaka. Utaipata mtandaoni. Hii ndio karne pekee ambayo kila mtu ni msomi.

Kwaio usifikiri nazungumzia wasomi wengine Zaidi yako. Kama unajua kusoma basi jifunze kusikiliza na kufanya maamuzi sahihi.

Wakina baba wanahitajika kujua moja kwa moja jukumu walilo nalo; kabla hawajafanya maamuzi ya kupata Watoto bila maandalizi sahihi.

Na wale wababa ambao tayari wapo kwenye majukumu ya Watoto bila elimu sahihi. Basi ni vizuri wakaanza kujifunza jinsi gani ya kupambana na hayo majukumu.

Lakini pia, sababu za wanawake kuwa single mother zipo nyingi. Tofauti na hii sababu ya wanaume kukimbia majukumu.

Na sababu zingine zote za ziada sintazitaja hapa.

Jinsi gani ya kumkomboa single mother.

Nikisema single mother namaanisha mwanamke mwenye jukumu la baba na mama katika familia.

Basi tuanze na njia ya kwanza.

Tunajua kuwa umaskini ni adui wa kwanza wa haki. Na umaskini ni adui mkorofi sana, ukitaka kupigana nae hadi kumshinda inahitaji nguvu ya ziada(Elimu).

Nikisema nguvu, Tukumbuke kuwa umoja ni nguvu.

Cha kwanza cha kufanya ni kutengeneza mifumo mingi na mizuri kwa ajili ya kusaidia Watoto. Kuwapa chakula, elimu, makazi na malazi. Tunafahamu vituo vya kulelea Watoto. Vimekuwepo kwa muda mrefu sana. Lakini vimekuwa kama sehemu ambazo za kujiuliza sana kabla ya mtu kumpeleka mtoto wake.Hasa kwa vijana wakike na wakiume wa miaka hii.

Na kwanini iwe ivo; Ni kutokana na jinsi ambavyo tumejitengenezea akilini mwetu. Hatuna elimu ya kutosha kuhusu vituo hivi. Sawa unaweza ukasema, Watoto wapo wengi, watatosha kwenye hivi vituo vilivyopo.

Au ukasema sintapenda mtoto wangu awepo kwenye vituo kama hivi. Na bado tutarudi kwenye swala zima la kutambua kitu kwa undani sio kwa hisia. Kwa sababu vituo hivi havipo kukusimanga kwamba wewe ni maskini. Bali vipo kukupunguzia jukumu kwa muda Fulani mpaka utakapo pata mwelekeo mzuri katika mapambano yako.

Ndio tunajua vituo hivi vya watoto, havipo vingi na pia vingine havina muonekano mzuri. Lakini izi ndio sehemu ambazo zikiboreshwa zitawasaidia sana wamama. Uboreshwaji wake uje na kauli mbiu mpya kwamba. Muhifadhi mtoto wako kwa kipindi Fulani mpaka utakapopata uwezo wa kumuendeleza mwenyewe.

Waliopo tayari kuanzisha hii wangewasaidia sana Watoto. Na wanaweza wakachangia mada hapo chini.

Kingine cha kufanya ili kuwakomboa wamama hawa.

Kutengeneza vituo vingi sana vya ujasiria mali. Mwanamke wa kiafrika anapata mafanikio yake pale ambapo anakuwa mjasiriamali. Kuna vikundi vingi vinajulikana vya kutengeneza sabuni, na vya ufugaji.

Lakini bado havijawa na mwendelezo mzuri kwa sababu watu bado hawafikirii kuviendeleza. Nikimaanisha sa nyingine vimekuwa vikundi vya kichoyo sana. Wamekuwa wakibania hela na kuchagua watu wao.

Kwaio kinachohitajika apa ni kuwa na vikundi vinavyoanzishwa na mashirika makubwa yenye pesa za kutosha. Maana watu ndio chanzo kikuu cha pesa, basi watu wapewe elimu ya kutumia wingi wao na umoja wao kama chanzo cha kujiongezea kipato.

Kila mtu ana Wazo kuhusu mtaji nini kifanyike.



Wazo linalohusu kupata mtaji ni wazo linalosumbua wajasiriamali wengi.Na ni Baada ya kupata elimu au wazo na kuwa tayari kuchapa kazi. Na Mtaji ni kweli unahitajika, maana lazima ,vifaa ,nauli , chakula mawasiliano, na mavazi vyote ni gharama hata kabla haujaanza kuchapa io kazi. Hii inapelekea watu kukata tamaa na kushindwa kuendelea katika mapambano yao ya kila siku. Vikundi vya kutoa mikopo vipo na tutaunga group moja la telegram kwa ajili ya wale wenye vituo vya Watoto na wale wenye vikundi vya kutoa mikopo. Yawezekana kila kitu kikawa kilishafanyiwa ufumbuzi sema watu wenyewe ndio hawana taarifa sahihi.Lakini nimekuja na taarifa sahihi kwamba unaweza ukaanza Maisha yako kwa upya tena kwa kupitia izo njia mbili nlizo shauri hapo.



Wengine mtaendelea kuchangia mawazo yenu baada ya haya yakwangu.



Angalizo.

hakikisha unatoa wazo la kusaidia.Maana Mungu amekupa akili kama zawadi haujui imetoka wapi. Amekupa nguvu na uwezo wa kuiona leo kwa kusudi lake, ili na wewe uwe msaada kwa watu wote. Kwaio andika kitu chenye kuleta tija na kitakachofanya wakinamama hawa wapate suluhisho.
ukiweka mazingira mazuri hivi watakua hawaheshimu ndoa, si watajua wakiachika wanapata mtaji na kuna sehemu za kulea watoto, Hivyo wanaume watakua hawajali kuhusu kuacha na wanawake watakua na kiburi zaidi ya sasaiv.
 
Back
Top Bottom