Nini hasa kinawapumbaza waajiriwa?

Nini hasa kinawapumbaza waajiriwa?

Kumwambia mtu ambaye ana mshahara duni kapumbazwa na ajira kwa sababu hajajenga nyumba ni kumtia chumvi katika donda lake la mshahara duni.

Sasa walimu na askari ni watu wa kuwalaumu kwa sababu hawajajenga?

Kwa mshahara gani wanaolipwa?

Angalau askari anachance ya kupata rushwa tofauti na mwalimu labda aendeshe bodaboda kuongeza kipato.Hakuna mwajira anawezajenga kwa mshahara nje ya rushwa.Mshahara wa mwajiriwa ni calculated kwa mtu mmoja tu.Wote wanaextended family mshahara hautoshi either wataiba muda au kupiga dill,rushwa,nk kumudu Maisha.
 
Angalau askari anachance ya kupata rushwa tofauti na mwalimu labda aendeshe bodaboda kuongeza kipato.Hakuna mwajira anawezajenga kwa mshahara nje ya rushwa.Mshahara wa mwajiriwa ni calculated kwa mtu mmoja tu.Wote wanaextended family mshahara hautoshi either wataiba muda au kupiga dill,rushwa,nk kumudu Maisha.
Sasa hapo utakuta mtu aliyeamua kuishi kwa uadilifu, bila kuchukua rushwa, kwa mshahara mdogo, na ndiyo maana hajaweza kujenga, analaumiwa kwa kutojenga.

Na aliyejikita kwenye kuchukua rushwa, akajenga jumba kubwa, wakati mshahara wake mdogo, anasifiwa.
 
Kama kijijini mwalimu anapewa nyumba bure, maji ya jumuiya ni sh 500 (kwa mwezi) na sh 1000 kwa mwezi kama umeingiza ndani (bei hiyo ni ya mwaka 2015), unapewa shamba bure, wanafunzi wanakusaidia kupanda, kupalilia, kuvuna na kukuletea nyumbani. Nauli hutumii kwa sababu nyumba inakuwa mita chache kutoka shuleni. Umeme haupo ni vibatari na taa tu. Na bado wanakijiji ukiishi nao vizuri wanakuwa wanakupa bure vitu vidogo kama kuku, mahindi nk
Halafu unakuta mtu anastaafu hana kitu! Sijui tunakwama wapi!
 
Kuajiriwa ni umasikini wa kujitakia!

Na ole wako uchukue mkopo saccos, utaichukia hiyo kazi nakwambia
 
Hakuna mwajira anaweza jenga kwa mshahara nje ya rushwa.Mshahara wa mwajiriwa ni calculated kwa mtu mmoja tu

Mkuu hapa naomba nipingane na wewe kabisa. Kwanza kabisa waajiriwa unaowazungumzia wewe ni wapi? Maana naona unachukulia kama waajiriwa wote ni sawa mfano waajiriwa kwenye mashirika ya kimataifa, taasisi nyeti za serikali, wakurugenzi, maafisa, madaktari, malecturer, TRA, mabenki nk wote hao kweli hawawezi kujenga?
Mfano walimu wengi siku hizi wanaofundisha shule za sekondari za binafsi, english medium, international school nk wanakula mishahara minono ambayo inawawezesha kujenga na kuishi maisha decent sana tu kinyume kabisa na matarajio yako. Pia siku hizi kuna SACCOS na benki zinawakopesha mpaka milioni 50 na zaidi kweli bado utasema muajiriwa hawezi kujenga?
 
Unakuta mtu ameajiriwa kila mwisho wa mwezi anapokea mshahara, kila katikati ya mwezi anapokea posho, anaishi kwenye nyumba za serikali.Umeme bure na Maji bure.

Amefanya kazi miaka yote na umebaki mwaka mmoja kustaafu, hana kiwanja wala nyumba alojenga kipindi cha ajira miaka yote Hata nyumba alonunua (maybe kujenga ni process)
Kipindi anatumia mshahara wake na posho zake kuwasaidia hamkumbuki tena...
Mnakuja kumjudge kipindi anastaff bila kujali pesa zake mlizitumiaje wakati yupo kazini.
Anyway.... Mlioajiriwa jijengeni kabla ya kuwahurumia wengine, wao ndio maadui wako wa kesho.
 
Mkuu hapa naomba nipingane na wewe kabisa. Kwanza kabisa waajiriwa unaowazungumzia wewe ni wapi? Maana naona unachukulia kama waajiriwa wote ni sawa mfano waajiriwa kwenye mashirika ya kimataifa, taasisi nyeti za serikali, wakurugenzi, maafisa, madaktari, malecturer, TRA, mabenki nk wote hao kweli hawawezi kujenga?
Mfano walimu wengi siku hizi wanaofundisha shule za sekondari za binafsi, english medium, international school nk wanakula mishahara minono ambayo inawawezesha kujenga na kuishi maisha decent sana tu kinyume kabisa na matarajio yako. Pia siku hizi kuna SACCOS na benki zinawakopesha mpaka milioni 50 na zaidi kweli bado utasema muajiriwa hawezi kujenga?
Hawa ambao awajaongezewa mishahara hadi miradi ikamilike sio hao wa daraja la juu.
 
Sasa hapo utakuta mtu aliyeamua kuishi kwa uadilifu, bila kuchukua rushwa, kwa mshahara mdogo, na ndiyo maana hajaweza kujenga, analaumiwa kwa kutojenga.

Na aliyejikita kwenye kuchukua rushwa, akajenga jumba kubwa, wakati mshahara wake mdogo, anasifiwa.
ukiwaweka waajiriwa kwenye kapu moja la uadilifu,wenye kukosa uwezo wa kujenga hawatakuwa askari na waalimu peke yao,hapo ndio utajua bado tz kwa ujumla wake haijafika popote.

kama mtu analipwa mil 1.5 na anajiona analipwa vizuri hili ni tatizo,tafuta sasa hawa wanaolipwa 1.5 mln ni wangapi nchini.

ndio maana mentle wangu kiduku lilo huwa analalamika kwamba hata huko barabarani anakutana na vifaa vimebeba watu ndani vikitembea,vimeandikwa vits,noah,toyota,carina nk[emoji1][emoji1][emoji1].anajiuliza inakuwaje watu wananunua hivyo??jibu ni kwamba ndio msuli wao umeishia hapo.
 
Back
Top Bottom